Mfahamu vyema mnyama Tembo (Elephant )

Mfahamu vyema mnyama Tembo (Elephant )

Duuuu Wengine hata robo lita haifiki

mi natoaga kikombe kimoja cha kahawa kinajaa baada ya kula mihogo na karanga plus mdalasini na tangawizi weeee ni mmwago wa kutosha mpaka mdada akitoka zinamwagika kudadadeki
 
Mkuu huyo anakimbia kwa spidi gani nasikia ukigeuka ghafla anakula mzinga chini anadondoka hebu lete somo hapo
Spidi yake ni kilometers 40 kwa saa kuhusu kugeuka gafla hilo hawezi kutokana na kuwa na uzito mkubwa pamoja na umbo lake lakini ana uwezo mkubwa wa kukimbia kwenye milima
 
Mkuu niliwahi kusikia eti tembo nao wana weka matanga ya misiba akifiwa na wanazikana kama sisi na wanazikana maeneo gani hayo maalumu? na kwann wazikane? maana sisi binadamu hata Faru Ngabu tunazika tu
Ni kweli tembo huzikana na eneo walilozikia hukaa pale kwa siku kadhaa wakiomboleza kifo cha mwenzao na pia huweka hapo matawi ya miti na hudondosha chozi la huzuni wakimlilia mwenzao aliyefariki
 
Mkuu somo safi sana hili ,swali langu hivi hayo meno au mapembe yanatumika kwa shughuli gani kwa binadamu mpaka vimacho vidogo wanachanganyikiwa hivyo wakiona tembo wetu?
Hutumika kutengeneza daga pamoja na vitu vingine vya urembo ambavyo garama yake ni kubwa hasahasa katika nchi za kiarabu kama yemen ambayo biashara hii ya meno ya tembo ndo hufanyika
 
Shawahi kuona kwenye kitabu an albino elephant.Nlikuwa nauliza unamtofautishaje tembo wa Asia na wa Africa.
Tofauti ni kwamba tembo wa Africa ni wakubwa ukilinganisha na tembo wa Asia pia meno ya tembo wa Africa ni makubwa kuliko ya tembo wa Asia pia tembo wa Asia mara nyingi hutumika kama urembo mfano huwatumia katika kupamba harusi pamoja na kubeba mizigo lakini kwa Africa tembo wetu tunawatumia kwenye shughuli za kitalii na ndo maana huwezi ukawaona sehemu yoyote zaidi ya kwenye hifadhi
 
Daah safi sana hilo somo mkuu kila Wiki tupia ya mnyama mmoja mmoja tupate elimu adimu, hivi tembo anaweza kulala chini na nilikwenda Kule Manyara tukamuona kama alikua ana majimaji sikioni yanatoka polepole je nini yale maji au machozi ya hasira ??hebu nipe somo hapo mkuu
Ndiyo mkuu tembo ana aina kuu mbili ambazo huzitumia wakati wa kulala. Ya kwanza ni kwamba tembo anaweza kulala akiwa amesimama na hii ni kutokana na yeye kuwa na miguu kama meza ambayo humwezesha yeye kulala bila tatizo lolote akiwa amesimama na kwa kama umebahatika kutembea hifadhini nyakati za mchana utawaona tembo wakiwa wamesimama katikati ya miti mikubwa na wengiwao wanakuwa wamelala na njia ya pili ni kuwa tembo anaweza kulala chini ardhini lakini hutafuta sehemu yenye mwinuko kidogo kama kwenye kichuguu cha mchwa hapo ndo hulala na hufanya hivi kwa sababu kwenye tambarare hawezi kulala kwa sababu itakuwa vigumu kwake kuweza kuamka kutokana na uzito wake pamoja na umbile lake kubwa na ndio maana hupendelea zaidi kulala kwenye maeneo yenye mwinuko
 
Ni kweli tembo huzikana na eneo walilozikia hukaa pale kwa siku kadhaa wakiomboleza kifo cha mwenzao na pia huweka hapo matawi ya miti na hudondosha chozi la huzuni wakimlilia mwenzao aliyefariki

Daah huzuni sana kumbe hata hao wanajua msiba
 
Kwa kuongezea tembo ndiye mnyama pekee asiyeweza kuruka...
 
Back
Top Bottom