Meremeta & TANGOLD Revealed!

Meremeta & TANGOLD Revealed!

Rev. Kishoka wewe ni mchambuzi mzuri sana. Maswali uliyouliza hapo juu ni mazito sana ambayo Watanzania wana umuhimu mkubwa wa kusikia majibu yake. Ahsante sana.

nani atayajibu? nani? hata mkapa mwenyewe hawezi achia mbali hao wafuasi wao.
 
Uongo ulishindwa kuwasaidia kwa miaka yote waliyo kaa madarakani, wakaamua kuleta vitisho ambavyo navyo pia vimegwaya na sasa wameanza kutafunana ndani ya CCM kama Wanga.
Silaha yao ya mwisho ni Fedha, fedha ambayo kihistoria ilishindwa kulinda himaya zote tangu kale.
Kama Obama ameweza ingia White House kwa kuwa kuwaambia watu ukweli na kuusema uzandiki bila hofu, kwa nini sisi tushindwe?
Kama kuna hofu yeyote ya kushindwa, basi hofu hiyo inatokana na kuogopa vivuli vyetu wenyewe kuliko kuwaogopa CCM ambao wanajimaliza wenyewe kwa mtaji wa chuki na Uchoyo ulopindukia

Naamini kabisa kwamba CCM wanaiba na kurimbiza fedha wakiamini kwa dhati kwamba fedha itawasaidia kutawala milele. wasichojua ni udhaifu ambao fedha siku zote huuleta katikati ya kundi la wanasiasa na kuingiza ulegevu uzaao utepetevu.

Fedha hiyo hiyo wanayoiabudu itawateketeza wimo wao na mahali pao litabaki jivu tu.

Kabla ya mwaka 2010 tutashuhudia maanguko mengi ndani ya CCM.
 
Lakini waliochora mshiko wote si CCM kama chama, bali ni kakundi kadogo ka-wajanja ndani ya CCM na nje yake ambao walionaupenyo huu.

Sawa sawa, hapa tupo ukurasa mmoja mkuu.
 
Ndugu ma odita wanafunzi meremeta ni kampuni ya jeshi kama ni jeshi lazima fedha zake zitakuwa zilienda kununua silaha.sasa sijui mnataka kufanya auditing na hizo zilaha.na kama CCM haikuguswa katika suala la EPA mnataka kuisakama nini . huo ni uzushi eti ieleweke nani kawafadhili yote hayo ni udaku.Mfadhili wa ccm anaeleweka na ccm yenyewe.after all inaelekea watu wasahaulifu mbona hamsemi kuhusu zile harambe zilizofantwa kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi.Mana huwezi kujifanya kuchunguza suala kwa kubuni bora kunyamaza
 
Rev. Kishoka,

CCM walikuwa wanaendesha harambee ya kuchangisha pesa kibao kwa ajili ya uchaguzi. Hao mafisadi ndio walikuwa wanachangia kwa kiasi kikubwa.

Kwa siasa za TZ kuna uwezekano CCM kama chama hakikuhusika na wizi huo. Ingelikuwa huku kwa wenzetu kuhusika by association kungelitosha kabisa kuiweka CCM matatizoni, lakini kwa TZ haitoshi.

Muhimu case iko mahakamani, mimi ninachosubiri ni hivyo vimemo vya serikali au CCM kuhusika.

Kama ni kampeni ya nchi nzima, mbona hata CHADEMA pamoja na kutokuwa na matajiri wengi wa kukichangia bado waliweza kuzunguka nchi nzima? CCM hawakuwa na haja ya kuchota EPA ili kuendesha uchaguzi. Wao wanatumia kuwepo madaraka ili kupata pesa nyingi kwa hao matajiri. Kuruhusu matajiri kutumia mamilioni yao kwenye kampeni ni balaa kubwa kwa nchi. Hao hao matajiri ndio wanatuchagulia viongozi.

Kwa maoni yangu kuna watu ndani ya CCM walitumia huo uchaguzi ili kuchota pesa, pesa hizo zilizo nyingi hazikuenda kwenye uchaguzi, zilitumika kwenye mambo yao binafsi. Ili kujikinga wakamwaga kiasi kwenye CCM kama kununua kinga.

Huu ni muda wa kusubiri ili tuone nani atafikishwa mahakamani. Vigogo wakuu wa BOT wako ndani, hili ni jambo zuri, hao ndio waliidhinisha hizo pesa kutoka. Kama wana vimemo basi wavitoe.

Kuna mtu aliandika mbona naibu gavana hawamo? Uchunguzi wote kuanzia wa Makaburu mpaka E&Y haukuwahusisha hao manaibu gavana. Ulimhusisha Balali pamoja na hao watendaji. Labda naibu gavana na board nzima wangewajibishwa kwa kulazimishwa kujiuzulu kwa kushindwa kuzuia au kutambua wizi huo.
 
Mtanzania,

Hhela za Harambee hata ziwe ni za vibopa tosha haziwezi kuwa nyingi na kuweza tosheleza gharma za wagombea zaidi ya 300 wa Ubunge na Uwakilishi na ule wa Mgombea Uraisi na mgombea mwenza wake.
 
Ndugu ma odita wanafunzi meremeta ni kampuni ya jeshi kama ni jeshi lazima fedha zake zitakuwa zilienda kununua silaha.sasa sijui mnataka kufanya auditing na hizo zilaha.na kama CCM haikuguswa katika suala la EPA mnataka kuisakama nini . huo ni uzushi eti ieleweke nani kawafadhili yote hayo ni udaku.Mfadhili wa ccm anaeleweka na ccm yenyewe.after all inaelekea watu wasahaulifu mbona hamsemi kuhusu zile harambe zilizofantwa kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi.Mana huwezi kujifanya kuchunguza suala kwa kubuni bora kunyamaza

SaidSabke,

Uliwahi kusoma ripoti ya mkaguzi mkuu wa mahesabu Tanzania bwana Ludovick Utoh?

Kama hujawahi, basi hebu nikutonye. Jeshi na Wizara ya Ulinzi ni moja ya vitengo ambavyo mahesabu yake ni mabovu na hayajafanyiwa uhakiki wa ndani na wahasibu wa Jeshi. Kuna ufujaji mali na pesa wa hali ya juu katika Jeshi letu.

Nikirudi kwenye hoja yako, kama unadai eti tuliache Jeshi au kuwa tunachoongelea ni kubuni, kwa nini basi Jeshi lilienda kuomba mkopo kwa kampuni binafsi na si Serikali ya Tanzania? kama Jeshi ni tajiri na makini, iweje kampuni yake ya uchimbaji madini ifilisike?

Ni ujinga huu huu wa kusema eti tusiunganishe nukta au kuuliza maswali ambao unawafanya Watanzania waendelee kunyonywa na viongozi wao na wajanja wachache!

Kama hakuna ovu, kwa nii Waziri Mkuu alifukia chini ya uvungu suala la Meremeta huku ni fedha za walipa kodi zilitumika bila kufuata mkondo kamili wa bajeti na matumizi ya Serikali, Wizara na Idara zake? Je walishindwa nini JWTZ kuomba pesa hizi kwenye kikao cha bajeti cha 1997? kwa nini walikwenda upenuni kukopa kwa kaburu na mbaya zaidi kusajili kampuni Uingereza kwanza halafu waje miaka mitatu baadaye kusajili ndani ya nchi?

Je mwenzetu umemegewa kidogo? tuambiane ati kama mshiko na mugawo umeukumba!
 
hivi kiongozi, kama waziri mkuu anaruhusiwa kusema uongo, tena ndani ya bunge
 
CAG ashindwa kukagua hesabu za Meremeta na Tangold
ZITTO ASEMA NI LAZIMA ZIKAGULIWE

Na Ramadhan Semtawa


WINGU zito limegubika hesabu za mwaka 2007 za makampuni mawili nyeti ya Buhemba Goldmine (Meremeta) na Tangold baada ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kushindwa kukagua hesabu za kampuni hizo.

Kushindwa kwa CAG kukagua hesabu za Meremeta na Tangold kumekuja wakati tayari uendeshaji na mitaji ya makampuni hayo mawili, mojawapo ikiwa chini ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), ukigubikwa na utata huku watendaji wakipata kigugumizi kuzizungumzia na wakati fulani Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiapa kutozungumzia, hasa Meremeta.

Pinda alishawahi kubanwa bungeni kuhusu suala hilo, lakini akawataka wabunge kutojadili suala hilo, akieleza kuwa Meremeta inahusiana na masuala ya jeshi na hivyo haifai kujadiliwa kwenye chombo hicho.

Wakati kukiwa na wingu hilo, hali ya mashaka zaidi kuhusu Meremeta na Tangold imezidi kujitokeza mwaka huu ndani ya ripoti ya kwanza ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, inayoongozwa na mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Katika ripoti hiyo, ambayo imeingia kwa undani katika kuangalia mashirika yote 193 yanayomilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na yale ya ubia, hesabu za Meremeta hazijakaguliwa na CAG.

"Kuna uwezekano mkubwa kuwa thamani ya uwekezaji mitaji ya umma itakuwa ni kubwa zaidi kutokana na taasisi nyingine 51 ambazo zipo kwenye orodha ya msajili lakini hazijawasilisha hesabu zao za sasa zilizokaguliwa," inasema sehemu ya ripoti ya kamati.

"Vilevile kuna taasisi mpya ambazo hazikuwa zimekaguliwa hesabu zao pia, miongoni mwa taasisi hizo ni pamoja na kampuni ya Buhemba Goldmine (Meremeta) – TanGold.

"Kamati inaamini kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atahakikisha kuwa mashirika haya yanawasilisha hesabu zao kwa ukaguzi ili kuhakikisha mitaji ya umma haipotei au kutumika vibaya."

Akizungumza na Mwananchi kuhusu utata huo, Zitto alisema hesabu za mashirika hayo lazima zipelekwe kwa CAG kwa ajili ya ukaguzi.

Zitto alisema kamati itamwita msajili wa hazina aeleze uwekezaji wa serikali katika Meremeta na Tangold.

"Ni kweli CAG hajazikagua Meremeta na Tangold kwa sababu hazipeleka hesabu zao. Kamati imemuagiza CAG aikague Meremeta na pia itamwita msajili wa hazina aeleze uwekezaji wa serikali katika Meremeta na Tangold," alifafanua Zitto.

Kikatiba, CAG ana mamlaka ya kukagua hesabu zote za mamlaka za serikali kuu na mitaa na mashirika yote ya umma.

Habari zinadai kuwa ripoti ya Kamati ya Bomani iliyoundwa na rais kuangalia sekta ya madini na kutoa mapendekezo inaeleza kuwa ilishindwa kupata maelezo ya kutosha kuhusu uanzishwaji, umiliki na kufilisiwa kwa Meremeta na baadaye uanzishwaaji wa kampuni ya Tangold nje ya nchi. Inadaiwa kuwa Tangold ndiyo iliyorithishwa mgodi wa Buhemba.

Kwa mujibu wa ripoti ya CAG, ambayo Mwananchi inayo nakala yake, Meremeta na Tangold ni miongoni mwa mashirika 51 ambayo CAG alishindwa kukagua hesabu zake.

Ripoti hiyo ilifafanua zaidi kwamba, licha ya serikali kuwekeza mtaji wa sh 4.1 trilioni katika jumla ya mashirika 193, bado hesabu za baadhi ya mashirika hayo 51 zimejaa utata.

Katika jumla ya mashirika hayo, ripoti imebainisha mashirika 152 yanamilikiwa na serikali kwa kiwango cha hisa cha asilimia 100, ambayo ndiyo pekee yaliyokaguliwa na CAG.

"Mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30 2007, serikali iliwekeza kiasi cha Shilingi 4.1 trilioni katika jumla ya mashirika 193, Serikali ilikuwa na hisa asilimia 100 katika mashirika na taasisi 152, hizi ndizo zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali," inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Ripoti hiyo inaonyesha kwamba, katika jumla ya mashirika 9, serikali ilikuwa na hisa asilimia 50 au zaidi na katika mashirika 32 serikali ilikuwa na hisa chini ya asimilia 50.

Mchanganuo huo wa ripoti unaonyesha zaidi kwamba, kati ya mashirika 193 ya Umma, mashirika 48 ni ya kibiashara, taasisi 119 ni za huduma, mashirika 13 yako kwenye hatua mbalimbali za ubinafsishaji na mengine 13 yako kwenye ufilisi.

Ripoti hiyo, ambayo tayari imesisitiza umuhimu wa kubadilishwa kanuni za bunge kuipa nguvu kamati, inaonyesha kwamba mashirika yote ambayo serikali inashikilia hisa za asilimia 50 na chini ya hapo hayana usimamizi (oversight) wa kibunge.

"Hivyo kamati hii haikupata fursa ya kukagua hesabu zao na hatimaye kutokujua mtaji wa umma unaendeshwa namna gani," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Kuhusu gawio kwa serikali kutoka katika mashirika hayo, ripoti ilifafanua kwamba yaliweza kuchangia mapato serikalini.

Ripoti hiyo inaongeza kwamba gawio kutoka mashirika ya umma liliongezeka kutoka Sh12.2 bilioni mwaka 2005/2006 hadi kufikia Sh13.4 bilioni mwaka 2006/2007.

"Kwa ujumla, Mashirika ya Umma yalichangia serikalini makusanyo ya gawio na kiasi kingine cha michango ya jumla ya Sh26.05 bilioni ukilinganisha na Sh60.7 bilioni mwaka uliotangulia.

"Makusanyo haya ni pungufu ya zaidi ya asilimia 50 na ni faida ya chini ya 10% ya mtaji, uliowekezwa kwa mwaka mzima wa 2006/2007,"inafafanua.

Meremeta ni kampuni yenye uhusiano na JWTZ ambayo ilianzishwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kama moja ya kitegauchumi kusaidia jeshi kujiendesha.

Hata hivyo, kumekuwa na utata kuhusu uwekezaji wa serikali na kama bado iko chini ya Benki Kuu (BoT) huku kampuni ya Tangold nayo ikigubikwa na wingu kuhusiana na umiliki wa fedha zake zenye uhusiano na Meremeta.

Tayari, serikali imekuwa ikigoma kutoa ufafanuzi wa hilo ikisema Meremeta inahusu mambo ya Usalama wa Taifa, hivyo si rahisi kuanika utendaji wake hadharani. Hata hivyo, kumekuwa na maswali mengi kuhusu kauli hiyo kwani serikali imegoma kutoa taarifa bungeni, lakini miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo yaani British Law Association ni wageni, hivyo kuweza kujua siri za usalama wa taifa kuliko bunge.
 
Last edited by a moderator:
Tayari, serikali imekuwa ikigoma kutoa ufafanuzi wa hilo ikisema Meremeta inahusu mambo ya Usalama wa Taifa, hivyo si rahisi kuanika utendaji wake hadharani. Hata hivyo, kumekuwa na maswali mengi kuhusu kauli hiyo kwani serikali imegoma kutoa taarifa bungeni, lakini miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo yaani British Law Association ni wageni, hivyo kuweza kujua siri za usalama wa taifa kuliko bunge.

Mbona serikali ya JK wanatudanganya? Kwa nini Usalama wa taifa inakuwa ni kigezo pale tu wananchi wanapotaka kujua habari ambazo wafanyabiashara wa kigeni huzipata kirahisi?

Usalama wa Taifa unakuwepo vipi kwenye biashara halali ya madini?
 
Mmmhhhhhhhhhhhh na yeye ccm mbona hivyo....???
 
CAG ashindwa kukagua hesabu za Meremeta na Tangold
ZITTO ASEMA NI LAZIMA ZIKAGULIWE

Na Ramadhan Semtawa

WINGU zito limegubika hesabu za mwaka 2007 za makampuni mawili nyeti ya Buhemba Goldmine (Meremeta) na Tangold baada ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kushindwa kukagua hesabu za kampuni hizo.

Kushindwa kwa CAG kukagua hesabu za Meremeta na Tangold kumekuja wakati tayari uendeshaji na mitaji ya makampuni hayo mawili, mojawapo ikiwa chini ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ), ukigubikwa na utata huku watendaji wakipata kigugumizi kuzizungumzia na wakati fulani Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiapa kutozungumzia, hasa Meremeta.

Pinda alishawahi kubanwa bungeni kuhusu suala hilo, lakini akawataka wabunge kutojadili suala hilo, akieleza kuwa Meremeta inahusiana na masuala ya jeshi na hivyo haifai kujadiliwa kwenye chombo hicho.

Wakati kukiwa na wingu hilo, hali ya mashaka zaidi kuhusu Meremeta na Tangold imezidi kujitokeza mwaka huu ndani ya ripoti ya kwanza ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, inayoongozwa na mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.

Katika ripoti hiyo, ambayo imeingia kwa undani katika kuangalia mashirika yote 193 yanayomilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na yale ya ubia, hesabu za Meremeta hazijakaguliwa na CAG.

"Kuna uwezekano mkubwa kuwa thamani ya uwekezaji mitaji ya umma itakuwa ni kubwa zaidi kutokana na taasisi nyingine 51 ambazo zipo kwenye orodha ya msajili lakini hazijawasilisha hesabu zao za sasa zilizokaguliwa," inasema sehemu ya ripoti ya kamati.

"Vilevile kuna taasisi mpya ambazo hazikuwa zimekaguliwa hesabu zao pia, miongoni mwa taasisi hizo ni pamoja na kampuni ya Buhemba Goldmine (Meremeta) – TanGold.

"Kamati inaamini kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atahakikisha kuwa mashirika haya yanawasilisha hesabu zao kwa ukaguzi ili kuhakikisha mitaji ya umma haipotei au kutumika vibaya."

Akizungumza na Mwananchi kuhusu utata huo, Zitto alisema hesabu za mashirika hayo lazima zipelekwe kwa CAG kwa ajili ya ukaguzi.

Zitto alisema kamati itamwita msajili wa hazina aeleze uwekezaji wa serikali katika Meremeta na Tangold.

"Ni kweli CAG hajazikagua Meremeta na Tangold kwa sababu hazipeleka hesabu zao. Kamati imemuagiza CAG aikague Meremeta na pia itamwita msajili wa hazina aeleze uwekezaji wa serikali katika Meremeta na Tangold," alifafanua Zitto.

Kikatiba, CAG ana mamlaka ya kukagua hesabu zote za mamlaka za serikali kuu na mitaa na mashirika yote ya umma.

Habari zinadai kuwa ripoti ya Kamati ya Bomani iliyoundwa na rais kuangalia sekta ya madini na kutoa mapendekezo inaeleza kuwa ilishindwa kupata maelezo ya kutosha kuhusu uanzishwaji, umiliki na kufilisiwa kwa Meremeta na baadaye uanzishwaaji wa kampuni ya Tangold nje ya nchi. Inadaiwa kuwa Tangold ndiyo iliyorithishwa mgodi wa Buhemba.

Kwa mujibu wa ripoti ya CAG, ambayo Mwananchi inayo nakala yake, Meremeta na Tangold ni miongoni mwa mashirika 51 ambayo CAG alishindwa kukagua hesabu zake.

Ripoti hiyo ilifafanua zaidi kwamba, licha ya serikali kuwekeza mtaji wa sh 4.1 trilioni katika jumla ya mashirika 193, bado hesabu za baadhi ya mashirika hayo 51 zimejaa utata.

Katika jumla ya mashirika hayo, ripoti imebainisha mashirika 152 yanamilikiwa na serikali kwa kiwango cha hisa cha asilimia 100, ambayo ndiyo pekee yaliyokaguliwa na CAG.

"Mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30 2007, serikali iliwekeza kiasi cha Shilingi 4.1 trilioni katika jumla ya mashirika 193, Serikali ilikuwa na hisa asilimia 100 katika mashirika na taasisi 152, hizi ndizo zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali," inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Ripoti hiyo inaonyesha kwamba, katika jumla ya mashirika 9, serikali ilikuwa na hisa asilimia 50 au zaidi na katika mashirika 32 serikali ilikuwa na hisa chini ya asimilia 50.

Mchanganuo huo wa ripoti unaonyesha zaidi kwamba, kati ya mashirika 193 ya Umma, mashirika 48 ni ya kibiashara, taasisi 119 ni za huduma, mashirika 13 yako kwenye hatua mbalimbali za ubinafsishaji na mengine 13 yako kwenye ufilisi.

Ripoti hiyo, ambayo tayari imesisitiza umuhimu wa kubadilishwa kanuni za bunge kuipa nguvu kamati, inaonyesha kwamba mashirika yote ambayo serikali inashikilia hisa za asilimia 50 na chini ya hapo hayana usimamizi (oversight) wa kibunge.

"Hivyo kamati hii haikupata fursa ya kukagua hesabu zao na hatimaye kutokujua mtaji wa umma unaendeshwa namna gani," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Kuhusu gawio kwa serikali kutoka katika mashirika hayo, ripoti ilifafanua kwamba yaliweza kuchangia mapato serikalini.

Ripoti hiyo inaongeza kwamba gawio kutoka mashirika ya umma liliongezeka kutoka Sh12.2 bilioni mwaka 2005/2006 hadi kufikia Sh13.4 bilioni mwaka 2006/2007.

"Kwa ujumla, Mashirika ya Umma yalichangia serikalini makusanyo ya gawio na kiasi kingine cha michango ya jumla ya Sh26.05 bilioni ukilinganisha na Sh60.7 bilioni mwaka uliotangulia.

"mambo ya Usalama wa Taifa, hivyo si rahisi kuanika utendaji wake hadharani. Hata hivyo, kumekuwa na maswali mengi kuhusu kauli hiyo kwani serikali imegoma kutoa taarifa bungeni, lakini miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo yaani British Law Association ni wageni, hivyo kuweza kujua siri za usalama wa taifa kuliko bunge.
 
Makusanyo haya ni pungufu ya zaidi ya asilimia 50 na ni faida ya chini ya 10% ya mtaji, uliowekezwa kwa mwaka mzima wa 2006/2007,"inafafanua.


Meremeta ni kampuni yenye uhusiano na JWTZ ambayo ilianzishwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kama moja ya kitegauchumi kusaidia jeshi kujiendesha.

Hata hivyo, kumekuwa na utata kuhusu uwekezaji wa serikali na kama bado iko chini ya Benki Kuu (BoT) huku kampuni ya Tangold nayo ikigubikwa na wingu kuhusiana na umiliki wa fedha zake zenye uhusiano na Meremeta.

Tayari, serikali imekuwa ikigoma kutoa ufafanuzi wa hilo ikisema Meremeta inahusu mambo ya Usalama wa Taifa, hivyo si rahisi kuanika utendaji wake hadharani.
Hata hivyo, kumekuwa na maswali mengi kuhusu kauli hiyo kwani serikali imegoma kutoa taarifa bungeni, lakini miongoni mwa wanahisa wa kampuni hiyo yaani British Law Association ni wageni, hivyo kuweza kujua siri za usalama wa taifa kuliko bunge.
 
CAG is the judge, jury and executioner, Tangold and Meremeta are matters of national security.
 
SERIKALI imesisitiza kuwa haiwezi kuruhusu suala la kampuni ya Buhemba Goldmine (Meremeta), kujadiliwa hadharani kwa kuwa inahusu mambo ya usalama wa taifa, lakini ikaeleza kuwa suala la ukaguzi wa Mwananchi Gold linasubiri wakati mwafaka kwa kuwa kwa sasa inafilisiwa.

Kauli hiyo ilitolewa Bungeni jana na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari wakati akijibu swali la mbunge wa Karatu, Dk Willbrod Slaa, aliyetaka kujua sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Kauli hiyo pia imetolewa siku moja baada ya kuripotiwa kwa taarifa kuwa, Bunge limemwagiza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG), kuyakagua mashirika hayo tata yanayohusishwa na upotevu wa mabilioni ya fedha za walipakodi.

Swali hilo lilitakiwa kujibiwa Ijumaa iliyopita, lakini Spika Samuel Sitta aliliahirisha hadi jana.

Akitoa majibu ya serikali, Waziri Sumari alisema msimamo kuhusu Kampuni ya Meremeta ulishawekwa bayana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati wa kikao cha Bunge cha mwaka jana aliposema kuwa, suala hilo haliwezi kujadiliwa kwenye chombo hicho cha kutunga sheria kwa sababu linahusu usalama wa nchi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema yuko tayari kusulubiwa kuliko kuizungumzia Meremeta kwa kuwa inahusu usalama wa taifa.

Waziri Sumari alirejea kauli hiyo ya Pinda akitaka iheshimiwe na kwamba asingeweza kueleza chochote kuhusu Meremeta na badala yake angetoa majibu ya Kampuni ya Mwananchi Gold peke yake.

Hatua hiyo ya serikali kutangaza uamuzi huo inaonekana kwenda kinyume na Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya mwaka 2008 inayompa CAG, ambaye anawajibika kwa Bunge, mamlaka ya kufanya ukaguzi bila ya kuagizwa.

Sumari pia alisema: “Makampuni mengine yote yenye uhusiano na Maremeta kama alivyosema mheshimiwa waziri mkuu hayatajadiliwa hadharani na serikali haioni sababu ya kufanya ukaguzi."

Baada ya majibu hayo, Dk Slaa alisimama tena kuulizwa swali la nyongeza na kudai kuwa hakuwa amejibiwa chochote na wakati akiendelea kuuliza kuhusu Meremeta, Spika Sitta alisimama na kumzima.

“Mheshimiwa Dk Slaa, suala la Meremeta linahusu jeshi. Tulikaa kwenye Kamati ya Uongozi tukakubaliana kwamba suala hili lisizungumzwe hadharani. Waziri Mkuu alishalisema; nafikiri na wewe ulikuwepo, kwa hiyo sitakuruhusu kuuliza chochote kuhusu Meremeta. Uliza makampuni hayo mengine ya Mwananchi Tangold," alisema Spika Sitta na kuipa serikali ahueni.

Lakini Dk Slaa akajibu na kusema: “Siulizi Jeshi, nauliza wizi.” Lakini Sumari akamjibu kwa kusema: "Na wewe pia (Dk Slaa) tafuta hoja nyingine..."

Taarifa zinadai kuwa, Meremeta ni kampuni ambayo ilianzishwa ikimilikiwa kwa asilimia 50/50 baina ya serikali na kampuni ya Trinnex na kuna tuhuma kuwa Benki Kuu (BoT) ililipa zaidi ya Sh155 bilioni kupitia benki moja ya kigeni bila ya kufuata taratibu, kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi ya CAG ya kipindi kinachoishia Juni 30, 2006.

Kuhusu Mwananchi Gold, Sumari, alisema kwa sasa iko katika mchakato wa kufilisiwa.

Hata hivyo, alisema ni mapema mno kuzungumzia mchakato huo, bali alitaka wabunge, akiwemo Dk Slaa kuvuta subira na muda mwafaka utakapofika wataelezwa.

Mwishoni mwa wiki, CAG aliiambia Mwananchi kuwa amepata barua kutoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma inayomtaka azikague kampuni hizo tata, lakini akasema bado hajapanga ataanza lini kuzikagua.

Barua hiyo yenye kumbukumbu BC.50/155/06/98 inamtaka CAG afanye ukaguzi maalumu ili kubaini thamani ya mtaji na hisa za serikali katika makampuni hayo tata na pia aieleze kamati sababu za kampuni hizo kutokaguliwa.

Awali, Dk Slaa alimuuliza Waziri wa Fedha na Uchumi ni sababu gani za msingi zilizofanya kuchukua muda mrefu kuanza ukaguzi kwa kampuni hizo hata pale tuhuma hizo zilizopigiwa kelele na jamii na hata kamati mbalimbali zilizoundwa kuchunguza tuhuma hizo.

Katika swali hilo namba 76, Dk Slaa alisema kwa kuwa katika hotuba ya waziri mkuu kivuli kwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), aliyoitoa bungeni Juni, 2007, alieleza juu ya ubadhirifu mkubwa uliofanywa kwa kutumia makampuni ya Meremeta na Tangold.

Dk Slaa alifafanua kwamba ubadhirifu huo ulibainika kwenye Makampuni ya Mwananchi na Deep Green Finance Co, ambao kiasi kinachodaiwa kufanyiwa ufisadi ni zaidi ya Sh215 bilioni.

Alihoji: “Ni lini kampuni hizo zitafanyiwa ukaguzi maalumu kama ilivyofanyika kwa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ili kubaini ubadhirifu huo uliohusisha uhamisho wa fedha kutoka Benki Kuu (BoT) na vyombo vya umma kupitia NBC Corporate Branch DSM na Ned Bank ya Afrika Kusini.

Akizungumzia majibu hayo ya serikali, mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, Zitto Kabwe alisema serikali imepotoka.

Zitto alisema CAG anawajibika kwa bunge na si serikali kwa kuwa ndiyo inayokaguliwa.

"Serikali ndiyo inakaguliwa na CAG, huyo waziri kakosea kusema serikali haijaamua kufanya ukaguzi huo," alifafanua Zitto.

Zitto aliongeza kuwa kauli hiyo ya waziri ni sawa na kutangaza kujiingiza katika mgogoro na bunge kwa kuwa CAG anafanya kazi kwa niaba ya bunge.

Utata mkubwa uliopo Meremeta ambayo inamiliki mgodi wa dhahabu wa Buhemba, pamoja na tuhuma za ufisadi ni utata wa wanahisa.

Wakati serikali ikisema kampuni hiyo inahusu masuala ya ulinzi na usalama wa nchi, ndani yake kuna wanahisa ambao ni kampuni ya Uingereza ya British Law Associate.
 
Haki ya Mungu,kwa mawaziri kama hawa akina Sumari watz tuna kazi kweli kweli ya kufika!Mungu wabariki mawaziri wa JK na JK mwenyewe!lkn tunachojua ni kuwa Meremeta haipo jeshini na wala haijawahi kuwa kampuni-tanzu ya jeshi lolote nyumbani tz,na kibaya zaidi kampuni hii ilisajiliwa rasmi tarehe 1 januari,siku ambayo ni sikukuu duniani kote na waajiri wa serikali yeyote duniani huwa wapo majumbani mwao wakipumzika!
Mungu akuzidishie sana Rais JK na baraza lako la mawaziri-Amen!
 
Jamani mi nachoka na vi-nchi vyetu vya kiafrika.....yaani kweli karne hii bado watawala wanatuona hamnazo kiasi hiki? duh..eti usalama wa nchi wakati pesa za walipa kodi ndo zimetumika? Is there anything ambacho wabunge/wawakilishi wetu hawawezi ambiwa kwa sababu ni usalama wa nchi? What if..mtu akiiba billions zote za BOT..akasema ni usalama wa taifa..who will question?

Jamani hali inatisha kuliko tuvyofikiria....Its scary.......
 
Jamani ilishasema IGP Mwema kwamba:'kuna baadhi ya watu kama wataguswa/kupelekwa mahakamani,basi nchi itatikiswa' sasa which part of his statement don't we understand yet??????
 
Back
Top Bottom