Meremeta & TANGOLD Revealed!

Kuhani, kuna wakati unajenga hoja zinaingia kichwani lakini kuna wakati (kama huu) ambapo kuzipangua hoja zako ni rahisi kama kumchomolea mlevi.

Sheria zinaundwaje?
Jamii hujitungia sheria baada ya kuona haja au ulazima wa kufanya hivyo. Endapo kuna mahali fulani katika barabara ambapo panatokea ajali nyingi na baada ya uchunguzi ikaonekana ni kwa sababu ni karibu na shule na hakuna alama za kuvukia basi jamii inaweza kufanya maamuzi kadhaa, kuhamisha shule, kufunga barabara wakati watoto wanavuka n.k n.k Lakini jamii hiyo inapopima na kuona kuwa labda mahali hapa "panapaswa" kuwa na kivuko cha waendao kwa miguu.

Ni kutokana na kupasa huku basi wanaamua kuweka alama za kivuko cha miguu. Endapo pamoja na kivuko hicho madereva bado hawasimami na ajali zinaendelea pasipo tofauti kubwa kwa sababu hakuna adhabu yeyote ile, na kwa vile kwenye vitabu hakuna adhabu ya kwenda kasi, basi jamii au chombo husika kinaona inalazima "kutunga sheria" ya kutoa adhabu ya wanaoenda kasi n.k

Sasa, Usalama wa Taifa jinsi ulivyo sasa ni wazi una mapungufu, na mapungufu hayo si ya utendaji tu bali ni mfumo na sheria. Hivyo mwakilishi wa watu anapoonesha matatizo hayo na kupendekeza suluhisho hilo si kuota ndoto. Ni kulikabili tatizo. Kama hakuna sheria inayosema kuwa Usalama wa Taifa uangalie pia masuala yanayohusiana na uchumi n.k basi hatuwalaumu TISS bali sheria iliyowaunda.

Sasa tunaweza kukubali basi "sheria ndivyo ilivyo" au tukasema sheria zimetengenezwa na sisi wenyewe na ni sisi wenyewe tunapaswa kuzifanyia mabadiliko Hivyo tunapendekeza mabadiliko ya sheria ili kuipa nguvu taasisi hiyo. Sasa huu ni utaratibu wa nchi inayofuata sheria na Katiba.

Sasa "kupasa" huko tunakokuzungumzia kunatokana na haja (a need) na haja inatokana na hali halisi. Unapojaribu kuvuka mto unakuwa na maamuzi ya kutumia mitumbwi, kuogelea, au kujenga daraja. Haja inapoonekana kuwa daraja ni suluhisho bora na salama zaidi basi jamii inaona inapaswa kuwa na daraja na hivyo wanafanya mchakato wa kujenga daraja.

Unachoweza kunishawishi ni kusema kuwa TISS haihitaji mabadiliko yoyote, kuwa sheria iliyopo sasa inatosha kabisa na kuwa hakuna haja ya kuboresha kitu chochote na hivyo hakuna kinachopaswa kufanyika. Hiyo inaweza kuwa hoja.
 
kwanza, hao viongozi wanaoitwa mafisadi sio wana ccm hao. Ni mapandikizi ya upinzani ambao watatolewa muda si mrefu.

Sikujua Lowassa, Mkapa na Chenge ni mapandikizi ya upinzani. Kujiunga na JF kumenisaidia kujifunza mengi.
 

This was excellent. Academically, one could say you scored High Distinction, or A+
 
kwanza, hao viongozi wanaoitwa mafisadi sio wana ccm hao. Ni mapandikizi ya upinzani ambao watatolewa muda si mrefu.
Du, ndugu yangu Masaka sijui umeanzia kilabu la mataputapu ya namna gani aisee. Unasema viongozi mafisadi wa CCM ni mapandikizi ya upinzani kweli? Yaani hata Mkapa na Lowasa ni mapandikizi ya upinzani?.

Aisee itabidi upunguze hiyo dozi unayotumia, inakudhuru akili.
 

I hope you mean 2010!
 

Ndio maana kuna wachangiaji wengine wamesema huyu jamaa ni Schizo:

 
Masaka nenda taratibu siasa za kutishana zimepitwa na wakati. Juzi juzi tu umeomba msamaha hapa kwamba umeelewa kuwa chama chako cha CCM kimekuwa kinafanya makosa leo unasema CCM watu watawekwa ndani especially Zitto na Dr Slaa. taratibu kijana!
 

Samahani ndugu Major nadhani lugha uliyotumia si nzuri. Huo si mwendo wa JF
 

Wakuu hakuna mwenye jibu la kuhusu wakurugenzi wa usalama?
wa mkapa na JK?
 
jmushi... ungekuwa unasoma mada nyingi kuhusu Usalama wa Taifa ungepata majibu. Mambo haya yameshadiliwa vya kutosha. So, just google "Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa"... work a little bit to find answers my friend.
 
It was a question for everbody.
We work together towards a common GOAL...JUSTICE!
AREN'T WE?
Kwani niliuliza swali lenye kuhitaji majina mawili tu ya wakurugenzi wa usalama wa TAIFA wa awamu ya TATU NA NNE na si mambo ya mjadala!
Any ways nitafanya hivyo.
 
Samahani kama nitakuwa nimechelewa kidogo kutoa pongezi, ila ningependa kumpatia Mheshimiwa Zitto hongera na asante nyingi for spending his weekend working for wananchi, kama alivyotuahidi.

Kuna thread mbili zilikuwa zikizungumzia ama zikitafuta majibu ya kwanini wabunge wetu wana matumbo makubwa. Now I get the answer about SIRI ya ku-maintain weight nzuri, which is kutumia wikiendi efficiently kwa kujiandaa vizuri kwa wiki inayofuatia (matokeo yake unakuja na hoja fresh na zenye nguvu siku ya jumatatu), kama ndugu yetu Zitto alivyofanya, na sio ku-spend the weekend kwenye bia na kitimoto kama the majority of wawakilishi wetu wanavyofanya (matokeo yake ni kulala bungeni asubuhi na mapema siku ya jumatatu kwa sababu ya mafuta waliyokula wikiendi yanakuwa bado hayajawa digested vizuri).

Asante sana ndugu yetu Zitto kwa kuiweka hoja hii vizuri. Tanzania ingekuwa mbali sana kama tungekuwa na wachapa kazi kama 10 tu bungeni kama wewe.
 
Asante sana ndugu yetu Zitto kwa kuiweka hoja hii vizuri. Tanzania ingekuwa mbali sana kama tungekuwa na wachapa kazi kama 10 tu bungeni kama wewe.

Au hata mtu tano hivi.

Sasa hivi kuna wangapi, wawili watatu. Tungepata nondo nyingine kama tatu hivi, sisiemu wangekoma.

Duuh, kazi njema Zitto.
 

Nilishawahi kuzungumzia kuhusu bandari yetu ya Dar....Kama Muungwana angeacha kushamilia wawekezaji wa madini tu na kusahau mali asili isiyoisha ambayo ni bahari na kilimo leo tungekuwa mbali sana....mimi naamini tungeitumia port yetu ipasavyo,fedha ambazo zingepatikana hapo zingeweza kujenga barabara zote Tanzania bara.

Wazambia,Wazaire,Wamalawi,Warwanda na Waburundi wote wamechoshwa na urasimu unaoendelea hapo Dar Port hata sisi waTanzania wengi tu tunatumia Mombasa port.....Sidhani kama Muungwana kuwa halijui hili Zambia kujenga reli....kama sikosei wakati wa kampeni alinena sana mambo ya kuendeleza bandari yetu.

Cha ajabu alipochukua Ikulu,basi ametulia as if Ikulu ni holiday place...hakuna alichofanya zaidi ya kuwakumbatia kina Sinclair and co...hence smile isiyokauka.
 

Tumenyanyaswa (Walimnyanyasa marehemu Baba yangu) sana na hawa the so called "Usalama wa taifa" kwa kutaka kulinda Ideology za ujamaa ambazo hazijafika popotee.
 
Usalama si lolote si chochote.Wewe nenda ofisi yeyote ya RSO ucheke mwenyewe.UTAKUTA MAKABATI YA MAFAIL YA MAJINA YA WATU yamejazana hukooooooo,we??.Sisi tulikuwa tunawacheka kuwa wako tuition.Uliza Implementation sasa duuu ziro.

Yani aibu.
 

Asante mkuu...Nadhani sasa Kuhani atakuwa ameelewa! Taratibu tunaanza kuwekana sawa hapa..ingawa wengi bado wanachechemea ila tutafika tu.

Wembe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…