Meremeta 00:00:00. EXTRA

Status
Not open for further replies.
Raia Mwema - Muungwana ni Vitendo

Siri za Meremeta kwenye mtandao


Mwandishi wa Raia Mwema
Julai 29, 2009

bul2.gif
Serikali yatikisika, Usalama wa Taifa wafuatilia

bul2.gif
Nakala 100 za ripoti hiyo zaandaliwa


SAKATA la kampuni ya Meremeta Limited iliyochota Benki Kuu ya Tanzania Sh bilioni 155 na ambalo sasa serikali imetangaza kwamba inahusiana na mambo ya Usalama wa Taifa, limeingia katika hatua mpya, baada ya kuelezwa kwamba sasa ripoti kamili ya siri kuhusu ufisadi huo itaanikwa katika mtandao.

Taarifa zilizotolewa kwenye mitandao ya Mwanakijiji.com na jamiiforums.com

Mwanachama huyo, ambaye alikuwamo ndani ya serikali wakati wa mchakato wa uanzishwaji wa Meremeta, alielezea kutoridhishwa kwake na maelezo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kutaka aeleze kuhusu Meremeta; vinginevyo yeye na wenzake wataamua kufanya kazi hiyo ili kuhakikisha kuwa mjadala wa Meremeta unamalizwa.

Raia Mwema limefahamishwa kwamba tayari vyombo vya usalama vimeanza kufuatilia suala hilo na huenda kukatokea mtikisiko mkubwa serikalini baada ya kusomwa kwa ripoti hiyo.

Taarifa hizo ambazo zinaonekana kama kujichukulia majukumu mikononi, kundi la Watanzania hao limeamua kufichua siri ya "usalama wa taifa" inayohusisha kampuni hiyo ya Meremeta ambayo ilianzishwa kwa kazi ya ununuzi na uchimbaji dhahabu.

Kampuni hiyo, ambayo iliandikishwa Uingereza mwaka 1997 na baadaye kufilisiwa huko huko Uingereza mwaka 2006, imezua malumbano makali bungeni hivi karibuni baada ya baadhi ya wabunge kupinga matumizi mabaya ya fedha kuhusishwa na usalama wa taifa.

Ndani ya mtandao huo imeelezwa kwamba kufichuliwa kwa kampuni hiyo kunatarajiwa siku yoyote wiki hii baada ya uchunguzi wa muda mrefu na ukusanyaji wa taarifa mbalimbali ambao umefanywa na Watanzania hao katika ushirikiano wa aina ya pekee wakiwa wametawanyika sehemu nbalimbali duniani.

Akiandika katika mtandao wake, mwanachama huyo alimwambia hivi Waziri Mkuu:

"Kwa vile suala la usalama linahusu usalama wa Taifa letu na wanaoohoji ni wabunge wa Taifa hilo ambao ni wawakilishi wetu, basi hata kama suala la Meremeta haliwezi kuwekwa hadharani (kwa kurushwa kwenye Luninga) basi Bunge lifunge macho na masikio ya nje na Wabunge wote wawe briefed wazi na moja kwa moja kuhusu Meremeta, umiliki wake na uhusiano wake na jeshi na usalama wa Taifa.

"Na endapo wabunge wataridhika, basi, tutapenda kusikia kuwa wameridhika na maelezo hayo na kama wabunge wapige kura kama wasimamizi wa serikali kuamua kama habari hizo kweli zinatishia usalama wa Taifa na kama wananchi wanapaswa kuziona."

Maelezo ndani ya mtandao huo yameeleza kwamba tangu ombi hilo litolewe hakuna dalili yoyote ya serikali kuwa wazi juu ya Meremeta na kuwalazimu Watanzania hao kuunganisha nguvu zao na raslimali zao kufanya utafiti wa kina wa suala zima la Meremeta.

Kwa mujibu wa mmoja wa washiriki wa watafiti hao ambaye alikataa kutajwa jina lake kwa sababu ya utaratibu wao wa kutojitambulisha, "ripoti hii inakusudia kuchochea jitihada za kutafuta ukweli wote juu ya Meremeta kwa kufunua kwa kiasi kikubwa kile ambacho kilikuwa hakijulikani".

Sehemu ya ripoti hiyo, ambayo mwandishi ameweza kuiona, inagusa mambo mazito ambayo kwa hakika hakuna kiongozi wa kisiasa mwenye akili timamu ambaye angethubutu kuyaachilia hadharani hasa katika mazingira ya kisiasa katika Tanzania na katika maeneo ya maziwa makuu.

Sehemu ya ripoti hiyo inayohoji uhusiano kati ya Meremeta na Mgodi wa Buhemba inasomeka hivi "Kama Meremeta Ltd ni kampuni ya jeshi na Buhemba Gold Mine iko chini ya jeshi ni kwanini basi jeshi hilo hilo liingie mkataba na kampuni yake nyingine wakati vyote viko chini ya Mkuu mmoja na Wizara moja?"

Ripoti hiyo inaendelea kuelezea kwa kirefu juu ya kampuni moja ambayo ndiyo iliingia mkataba na serikali kuanzisha kampuni ya Meremeta. Kwa mujibu wa mdokezaji wetu "kampuni hiyo siyo Triennex ambayo imekuwa ikitajwa mara kwa mara". Hata tulipombana kuelezea ni kampuni gani basi iliyoingia mkataba huo na kwanini haijulikani, mdokezaji huyo alikataa akisema, "tafuta ripoti uisome mwenyewe".

Raia Mwema ilipotaka kujua jinsi ya kupata nakala ya ripoti hiyo aliambiwa kuwa haipatikani bure; kwani imegharimu jasho na muda mwingi wa wachunguzi wa timu hiyo na hivyo wanawapatia wale ambao watachangia kiasi chochote kuanzia dola 30 za Marekani (zaidi ya Sh 30,000) ili kufidia sehemu ya gharama hiyo.

"Tumetumia karibu mwezi mmoja kufanya kitu ambacho kilitakiwa kufanywa na wabunge wetu na watumishi wa serikali yetu; sisi si matajiri kama wao na hatuna raslimali kama za kwao, hivyo katika hali kama hii tunaomba mchango kidogo japo kufidia ile gharama tuliyoingia kwani kujua nako kuna gharama" alisema mdokezaji huyo ambaye alisema kuwa wameandaa nakala 100 tu ambazo hadi jana Jumanne karibu nusu ya nakala zilikuwa zimeshanunuliwa kabla ya kusambazwa.

Imefahamika kwamba baadhi ya watu ambao wanataka kuiona ripoti hiyo ni pamoja na wabunge kadhaa, wakuu wa taasisi za haki za binadamu na Watanzania wengine wa kawaida.

Raia Mwema limedokezwa kwamba, waandaaji wa ripoti hiyo wameshawahi kuandaa mambo mazito zaidi ya kimataifa, baadhi yakiwa na maslahi ya Taifa la Tanzania ikiwa ni pamoja na lile sakata la rada ambalo hadi leo halijapatiwa ufumbuzi na serikali.

Katika sakata la rada, kundi hilo la Watanzania lilifanikisha kuandika barua kwa wabunge wa Uingereza Norman Lamb na Claire Short kuhusu kashfa hiyo ya rada.

Sehemu ya barua hiyo ilisomwa kwenye Bunge la chini la Uingereza na Mbunge Lamb na kuchochea mjadala mkali juu ya Rada kiasi cha kusababisha siku chache baadaye Rais Jakaya Kikwete kulizungumzia suala hilo na kuahidi kuwa kama serikali itakuwa imedhulumiwa katika bei ya rada basi serikali "itaidai serikali ya Uingereza kwani kampuni ya BAE ni ya serikali".

Kashfa ya Meremeta imekuwa ikiisumbua serikali kwa muda mrefu sasa na imeshindwa kutekeleza mapendekezo ya Kamati ya Rais iliyoongozwa na Jaji Mstaafu Mark Bomani, ambayo ilipendekeza kukaguliwa kwa kampuni hiyo.

Taarifa ya awali ya wakaguzi waliokagua BoT, Juni 2006, ziliibua sakata hilo la Meremeta pamoja na kashfa nyingine lakini haikuweza kufahamika ripoti hiyo ya wakaguzi ilivyoyeyuka na kutoanikwa hadharani kabla ya wakaguzi wengine wa nje kuibua suala la EPA pekee miongoni mwa uchafu mwingi ndani ya BoT na serikalini.

Taarifa hiyo ya wakaguzi ilibainisha kwamba serikali ilitoa fedha hizo kiasi cha Sh. bilioni 155 kwa njia ya dhamana ya hazina ambayo inatakiwa kulipiwa riba ya asilimia 14.92 kila mwaka lakini hakukua na makubaliano yoyote rasmi kati ya Serikali na Meremeta hali inayoibua zaidi utata na kuonyesha hakuna njia yoyote ya kuweza kuzipata fedha hizo.

Imeeleza kwamba ripoti hiyo inafuatia kile ambacho kilichukuliwa kama tishio lililotolewa na mmoja wa wanachama wa mitandao hiyo kuhusu kuanika siri ya Meremeta.

SOURCE: Raia Mwema
 
Last edited by a moderator:
Kati ya vitu ambavyo sitakaa nijutie ni kujiunga JF. Kuna mengi sana yamefanya mfumo wa maisha yangu ukabadilika. Some members here have totally changed the way i was thinking and operating.
 
Kwa kweli JF imenibadilisha hata mimi kwa muda mfupi tu nimeona mahali penye nafasi ya wale wanaoipenda nchi yao Tanzania kuitetea, kuilinda na hata kujivunia. Wanaojifanya wanaipenda waUwT ni waongo, wanachofanya ni kulinda nafsi na maslahi fulani. Wengi wanafanya kazi ya kupaka marashi uozo ili usinuke. Wakisahau kuwa within a very short time marashi huzidiwa na harufu ya uozo inapenyeza tena hewani.
Abraham Lincolin alishadokeza, "you can cheat all the people at a time, but not all the people all the time"
Nawashukru sana wana-JF wote na haswa hawa waliojitoa kwa ajili ya taifa letu. Mungu awabariki na kuwaepusha na maadui popote pale walipo.
 
SteveD umenena,

Mkuu FP hapa sisi ndani ya JF tumebeba jukumu la viongozi wetu waliolala, na humu ndani ni sawa na ukumbi wa mikutano ambao wana JF ni wajumbe wanaowakilisha sehemu ya Watanzania wengi wakiwamo wale wa Mbagala na vijijini. Baada ya kuwaelimisha (si kama Ngurdoto) wana JF, moto wa mageuzi utaenea, kwa kuanzia utaona magazeti (mfano wa Raia Mwema leo) yatabeba hiyo ajenda (kama Richmond.radar, EPA etc) na baada ya hapo, pole pole kule kwetu Mgori ama Mhunze na kule Ndorwe Wanga wataanza kupata ujumbe pole pole na hapo mto wa mageuzi utakuwa umewashwa. Ni lazima jambo lipate mwanzo na huu ni mwanzo mzuri. Umejaribiwa na umefanikisha mengi mkuu, tusikate tamaa.


Haya kaka ninakubali, ngoja tuone...
 
Yap! but not to all of them. Kumbuka hapa Mbagala hakuna anayejali serikali imefanya nini na huko kijijini ndo kabisaaaaaaa!

Wengi tulio humu kwanza hata kura hatupigi! Wengi wasio na Internet connection ndo walitakiwa waelewe hiki kitu vizuri. Mwanakijiji amefanya kazi nzuri na team yake ila watakaoiona ni wachache, hasa walio mjini na wasiopiga kura.

Well done anyway!

FP
Hii ni kujidanganya, maana kama unajua history ya mafanikio ya vita ya ufisadi, yameanzia humu humu JF tena kwenye internet unayobeza na yakaiangusha serikali.
Mbona mnakuwa wepesi kusahau?
Subiri uje uone matokeo ndio utajua nguvu ya internet na JF kwa ujumla wake!

Watu 100 wanaweza kuwapeleka wapiga kura kuwa na sura kamili ya Viongozi wao. Bado uamini?
 
Sijajua vizuri kwa nini hii taarifa ya meremeta imekuwa confidential na ghali kama lengo ni kuufahamisha umma wawatanzania kuhusu huu uozo. Sishawishiki kwamba ni kuwalinda walio itoa kwani hata hizo nakala 100 zitasambazwa kwa njia moja au nyingine.


Mkuu sithani huelewi kuwa kuna gharama kubwa pamoja na kujitoa ndo kumefanikisha kupatikana kwa hii report. huu mchamgo ni kigodo sana kulinganisha na gharama halisi. hivyo sioni ubaya wa sisi kuchangia walau kidogo katika hili. Wao wamejitoa basi niwajibu wetu kuunga mkono
 
This is commendable work. keep it up. others have already warned that the fisadis and their agents will indeed seek to buy all copies and hide them from the public. I know you are smarter than that



mpa
 
MKJJ

Mwendo ndio huo

wakulipe hao...mambo ya bure bure hakuna

wakigoma kaa nazo mpaka wakulipe hao maana pesa za mengine wanazo sioni kwa nini washindwe kukulipa

thats the way to go

unajua wewe ni mwalimu mzuri; na wakomalie Bandari hadi wasalimu amri!
 
SteveD umenena,

Mkuu FP hapa sisi ndani ya JF tumebeba jukumu la viongozi wetu waliolala, na humu ndani ni sawa na ukumbi wa mikutano ambao wana JF ni wajumbe wanaowakilisha sehemu ya Watanzania wengi wakiwamo wale wa Mbagala na vijijini. Baada ya kuwaelimisha (si kama Ngurdoto) wana JF, moto wa mageuzi utaenea, kwa kuanzia utaona magazeti (mfano wa Raia Mwema leo) yatabeba hiyo ajenda (kama Richmond.radar, EPA etc) na baada ya hapo, pole pole kule kwetu Mgori ama Mhunze na kule Ndorwe Wanga wataanza kupata ujumbe pole pole na hapo mto wa mageuzi utakuwa umewashwa. Ni lazima jambo lipate mwanzo na huu ni mwanzo mzuri. Umejaribiwa na umefanikisha mengi mkuu, tusikate tamaa.

hapa umenena!
 
kazi nzuri mwanakjj.......lakini mbona hujanitaja kwenye shukrani?
 
We are officially sold out!!

Kazi nzuri wote mliochukua copy, ni kwa manufaa yetu waTz wote... Mbarikiwe sana jamani.... sasa kwa ufupi tunafahamu kuna askari mashujaa 100 ambao wapo "armed" na nyeti nzito tayari kwenda kufanya kazi ya kusaidia taifa la Tanzania..... safari njema na mapambano mema wakuu wote, tupo pamoja japo sio mstari wa mbele lakini mfahamu kuwa kuna mamilioni ya waTz nyuma yenu.....

aluta kontinyua........
 
We are officially sold
out!!

Hongera Mwanakijiji, we owe you !! Keep up the good work - historia itakukumbuka. Moto unaendelea kuwaka na ole wake atakayejaribu kutaka kuuzima - walililia moto na sasa heri uwachome. Pamoja na kwamba sikuweza kuwahi kupata nakala, itakua furaha ilioje kusikia vilio vyao - kwangu vitakuwa ni muziki unaoburudisha. A luta continua......
 
Hongera sana mkuu kwa hii kazi.Tanzania itaendelezwa na watu wenye moyo.
hizo nakala wasije wakanunua zote(WANA USALAMA WA TAIFA)maana ni uozo wa kupindukia
 
my my my!!! I wish the info ambayo nimeipata leo ningeipata kabla hatujamaliza. Nadhani sasa itabidi niendeleze kama kitabu rasmi maana...

Daymn.. kuna ombi la kutengeneza nakala nyingine 100. Kutokana na ufinyu wa muda.. hatutaweza kufanya hivyo; Kama kuna mtu anataka nakala tafadhali tuma mchango wako kwa njia zilizotajwa ili by early 2morrow morning (Thursday) tutaunganisha na wale wa mikoani ambao wao wanapata magazeti kesho. Halafu tutafanya nyongeza nyingine moja tu ku fill hizo oda.

Meanwhile, tutahakikisha sasa inatoka kama kitabu baadaya kuongezea mambo mapya ambayo ripoti imeyachokoza na data zimeanza kumiminika.

Asanteni kwa support yenu.
 
MKJJ

Mwendo ndio huo

wakulipe hao...mambo ya bure bure hakuna

wakigoma kaa nazo mpaka wakulipe hao maana pesa za mengine wanazo sioni kwa nini washindwe kukulipa

thats the way to go

- Haya niliyasema siku nyingi sana huko nyuma kwamba siasa sometimes iwe na biashara, maana hizo ndio zangu siku zote ninashukuru kwamba sasa mmenielewa, sasa uwe mwendo wa mdundo hot dataz na malipo ili kesho tuletewe zingine, lakini yale mambo unaleta dataz halafu unatukanwa na matusi juu, sasa yataisha kwa sababu ukitukana huku umeshalipa tayari ni vyema zaidi,

- One thing huwa ninawaheshimu sana Mchungaji Kishoka na Mkulu Mwanakijiji ni uwezo wao wa kusoma hali halisi na kujichimbia nayo as quick as possible, saafi sana hii ya kulipia dataz imenifurahisha sana na hii tabia idumu na JF idumu zaidi na mwendo huu huu wa mdundo mpaka kieleweke.

- Wiki nzima hii serikali inahaha na this thing, uuoooohhh! I love it yaani toka JF tuanze kumkoma nyani giladi, never like this thing before, Mwanakijiji again ubarikiwe tu na Mungu wa Mbinguni!, Huko serikali ni afadhali mrekebishe mambo badala ya kutafuta watu uchawi wakati wachawi ni nyinyi wenyewe huko ndani, mwananchi anawezaje kusioma hii kitu halafu akatoa kura kwa mafisadi?

Sasa kwa wale wateule 100 tuliotia ndani hii kitu dawa ni kufikishia wananchi wengi as much as we can, leo peke yake nimepasia wananchi karibu 150, viongozi tena wa juu 20, wa kati 30, na wananchi wa kawaida 100 ninategemea by mwisho wa wiki hii kuwafikia wananchi atleast 500 na the big picture ni kuwafikishia wananchi wengi vijijini yaani waalimu, manesi na madakitari, viongozi wa vijiji na hata machifu wetu, hakuna kulala pia natoa heshima za juu sana kwa gazeti la raia mwema I wish mngejua jinsi leo mlivyopigilia misumari hili jeneza la serikali na ile article, saafi sana! Mkulu Halisi ubarikiwe sana na Mungu wa mbinguni!

Respect.

Mungu Aibariki JF na A Luta Continua!

Field Marshall Es!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom