Kumekucha
Na sasa tumeizunguka Yeriko!
Si kwa nguvu ya majeshi
Au kwa utaalamu wa vita
Bali kwa barugumu ya mashujaa
Watangazo ukweli!
Wale wapigao panda bila kukoma
Wasimamao nje ya kuta za Yeriko
Ambako ndani yake ufisadi umesimama!
Na mashujaa walio ndani kama Rahabu
Na wao wataweka alama za kuupenda ukweli
Nao hawataangamia!
Hii basi ni mbiu
Mbiu ya mwanzo wa mwisho wa Yeriko ya leo
Ule unabii wa kuanguka kwa Yeriko
Utaanza kutimia; kwani ni masaa machache yajayo
Sauti za matarumbeta ya walioizunguka Yeriko yatapigwa
Na kuta ngumu zilizojengwa kwa miongo minne
Zitaanza kutikisika; Naam! Zitatikisika kama zile za Yeriko ya kale
Waambie! tumeizunguka Yeriko!
Ambako himaya ya ufisadi imejikita
Na utamaduni wa kifisadi unatawala!
Nayo Yeriko ya leo itaporomoka;
utawala wa kifisadi utakoma!
Kwa wale walioko ndan ya Kuta za Yeriko
"tokeni mkatengwe naye!"
Na. M. M. Mwanakijiji
Mkuu nimeskia asubuhi kwenye uchambuzi kuna kitu kimetolewa na Raia Mwema kama sikosei kina husu kijarida hiki mkuu jaribu kufuatilia wanaweza wakawa wametumbukiza nyongo tayari.
usiwe na wasiwasi!!!!! mwenye kukosa ndiyo keshakosa!
Ok shukrani kamanda ngoja niwajibike...
Ukiwa na maksai wanne ni muhimu kuwapa mahitaji yao muhimu ili kuwawezesha waendelee kukulimia mashamba yako. Usipofanya hivyo, msimu ujao utakupita na kuishia kupata kijunia kimoja cha mahindi au mchele kwa kutumia jembe la chapa jogoo badala ya plao!Babu yangu mwanakijiji, uchanguzi unakaribia, je hauoni ni haki ya kila mtanzania kujua nini serikari iliyokuwepo zaidi ya miaka 30 imekilea? watu tuchangie kwa kujitolea kwa kazi yako nzuri uliyoifanya ila wape haki kila mtanzania kujua nini kinaendelea. Maana kila mmoja wetu tunauwezo wa kubadilisha kainchi ketu cha Tanzania, iwe kwa njia ya kuchagua raisi na chama tawala au kujitoa muhanga wa ajili ya maendeleo ya kila mtu na watu masikini.
Naelewa unaitaji kurecover cost ila pia watanzania wangapi hasa wapiga kura wenye uwezo wa kubadirisha raisi wa nje wanaweza kuafford?
umenigusa roho yangu,Yeriko imebomoka!!!!Na sasa tumeizunguka Yeriko!
Si kwa nguvu ya majeshi
Au kwa utaalamu wa vita
Bali kwa barugumu ya mashujaa
Watangazo ukweli!
Wale wapigao panda bila kukoma
Wasimamao nje ya kuta za Yeriko
Ambako ndani yake ufisadi umesimama!
Na mashujaa walio ndani kama Rahabu
Na wao wataweka alama za kuupenda ukweli
Nao hawataangamia!
Hii basi ni mbiu
Mbiu ya mwanzo wa mwisho wa Yeriko ya leo
Ule unabii wa kuanguka kwa Yeriko
Utaanza kutimia; kwani ni masaa machache yajayo
Sauti za matarumbeta ya walioizunguka Yeriko yatapigwa
Na kuta ngumu zilizojengwa kwa miongo minne
Zitaanza kutikisika; Naam! Zitatikisika kama zile za Yeriko ya kale
Waambie! tumeizunguka Yeriko!
Ambako himaya ya ufisadi imejikita
Na utamaduni wa kifisadi unatawala!
Nayo Yeriko ya leo itaporomoka;
utawala wa kifisadi utakoma!
Kwa wale walioko ndan ya Kuta za Yeriko
"tokeni mkatengwe naye!"
Na. M. M. Mwanakijiji
Mwanakijiji,
Mimi dola 30 zangu ziko njiani (hewani) kuja kwako. Nataka niwe miongoni mwa wale wenye copy hii. Ikifikia hatua ya kuisambaza bure pale jangwani na mnazi mmoja, nitakuwa miongoni mwa paper nuts......IYWI
kazi njema.. it gonna be a long day.. ( saa tisa za usiku huku kijijini!)! Tanzania hii mmmh..