HIVI NIULIZE WAZIRI ANAPOSEMA 70% YA MINING CONCESSIONS ANA MAANA GANI KUWA 70% YA MINING RESOURCE UNDER CONTROL OF THE INDIGENOUS PEOPLE AU ANAMAANISHA NINI. KAMA 70% YA RASLIMALI MADINI ZINAZOCHIMBWA ZIPO CHINI YA WAZAWA NINA IMANI TUNGEKUWA MBALI SANA . LAKIN WAZIRI ANACHEZA NA AKILI ZA WATU TUNACHOTAKA NI SEHEMU YA MAPATO INACHUKULIWA NA WAZAWA NA SIO WATU SABIN KATIKA MIA WENYE UWEZO WA KUCHIMBA MADINI ANAYOCHIMBA TAJIRI 1 KUTOKA KUNDI LA 30% mUHONGO HIYO HESABU NI YA WAPI?
mkuu umenena halafu hawa wawekezaji uchwara kina mengi na wenzie mbona hawawekezi kwenye matayizo ya msingi kama mahospitali,vyuo vya utabibu wao nikutafuta mianya ya wizi tu Mengi mzalendo gani anatoa mshahara mbuzi kwa wafanyakzi wake yeye anaingiza billioni of money charity begin at home.Mengi bana.
Mengi akisema wazawa anamaanisha Bakhresa, Mengi, Dewji, Mufuruki,Rostam etc
Hivyo vitalu hata wakisema ruksa mtanzania kuwekeza mimi maundumula kitalu ntakipata wapi?
Hivi kwanini hatushupalii mambo ya msing ambayo yanaweza kutuletea tija sisi wananchi kama mambo yanayohusu elimu, afya bora kwa wakina mama wajawazito, uzazi wa mpango nk mambo ambayo nilitegemea mtu kama mengi ndio angeamua kuyavalia njuga.
Wewe unafanyia nipashe au redio one tunajua anakupa ugari huwezi kumpinga endelea na mzee wako.
Kama unatilia shaka mchango wa Dr. Mengi kwa jamii yetu ambayo inatambuliwa hata nje ya nchi basi lazima unamatatizo ya akili! gharama za kwenda kuwatibia wagonjwa wa moyo nje ya nchi unajua ni kiasi gani? kusomesha watoto mamia kwa maelfu unadhani ni kazi rahisi? hao wenye kutupa Condom na Vyandarua vyenye dawa za uzazi wa mpango na canser kwa msaada wa watu wamarekani in exchange of our Gold, Uranium, Tanzanite, Gas, Vipusa, TANESCO na wanajeshi wetu kutumiwa kubaka rasilimali za nchi jirani!"kwenye red "HIVI HUYU MZEE naomba mnikumbushe alisomeawapi hiyo PHD ? na ok hata kama anayo aliipatapata vipi ? kwakuwasaidia walemavu na kuwalisha maskini ? waliompahawakumuona SABODO? aliyeamua kuchimba visima 100 nchi nzima ? hebu huyu anayepiganiamaslahi ya watanznia atueleze ametoa mchongo gani katikakuwalinda tembo wetu kwanza !ametoaamchongo gani katika kuitangaza bandari ya dar es salaam ?.waongo mwisho wao ni aibu tu. huyu mzee si ndo yule aliyezaa watoto mapacha hivi karibuni akawapeleka nje ya nchi !?. usafi wa MENGI unatia shaka kabisa ...
zimwi likujualo halikuli likakwisha! hata kama mengi atakuwa na maslahi binasfi ukweli ni kwamba mchango wake kwa watanzania unaonekana moja kwa moja!Kutokana na upeo wako mdogo wakufikiri ndio unaona hvyo ila kwa wale tunao mfahamu Mengi tunajua anatetea maslahi ya watanzania juu ya umilikaji wa rasilimali za taifa.
Muhongo akitoka kwenye baraza jipya la mawaziri nakupa mke.[/QUOT
malizia vizuri mkuu, mke wako au unamtafutia?
Pex, Hope umewahi kumsikia Mkapa akilalamika kuwa wazungu walimdanganya kuwa akibinafsisha viwanda na mashirika ya umma wao wataingiza mitaji pamoja na technolojia! Mpaka anatoka amadarakani hakuona hayo yakifanyika bali aliona utoroshwaji mkubwa wa mitaji kwenda nje (Capital Flight). Wazungu hawaaminiki na hawakuwahi kuaminika maana hadi kwenye katiba yao wanasisitiza maslahi ya nchi yao lazima yawe mbele! states urgencies zote wanaziendesha kwa remote, TPDC sijui STAMICO wanategemea fedha za uendeshaji kutoka kwa hawa hawa wawekezaji! Huoni kuwa ni conflict of interest? kwanini tusiamini kuwa kuna watu wemepenyezwa kuhujumu TANESCO, TPDC, STAMICO, BOT, TRA nk?...Suala la muda tu...yote yatakuwa hadharani soon...Hii ni debate nzuri. Ila angalizo ni kuwa tusijadili watu tujadili hoja zao. Wote wawili hoja zao zina mashiko. Maana huwezi ukawa na sustainable development katika nchi pasipo kuwashirikisha wazawa katika kumiliki raslimali za nchi zilizopo, lakini pia katika dunia ya leo huwezi kujitosheleza kwa kila kitu pasipo kuwa na wawekezaji kutoka nje ambao watawekeza either ktk mtaji, utaalamu n.k. kikubwa ambacho tunapaswa kujadili ni namna gani haya makundi mawili yatashirikishwa na kusimamiwa katika kuvuna raslimali ya nchi kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa wananchi wote....
Kutokana na upeo wako mdogo wakufikiri ndio unaona hvyo ila kwa wale tunao mfahamu Mengi tunajua anatetea maslahi ya watanzania juu ya umilikaji wa rasilimali za taifa.
Mbali sana hiyo 2015. Jk akipiga reshuffle, jamaa atapigwa sub tu!!
Hiyo conflict of interest inayo attract interest za wananchi waliowengi inaubaya gani? wewe kama wewe Kasheshe hupendelei wananchi wamiliki Rasilimali zao Dhahabu na Gesi?...
Mkuu mjepo, jaribu kujiongeza japo kidogo tu, au wewe ni robot? wameformat brain yako?... nikweli kuwa huoni hatari kwa rasilimali zetu kumilikiwa na wageni?
Muhongo anawatetea watanzania? au unamaanisha Tanzania ilishauzwa na kuna wamiliki wapya wazungu so Prof. Muhongo anawatetea?...Funguka mkuu tukusome vema, epuka matumizi ya lugha za viashiria na mizunguko...Mengi mbinafsi , Mhongo hana shida kabisa ni mtetezi wa wa watanzania kabisa , ingia kwemye website ya Wizara angalia Leseni za Mengi utaziona zilivyo nyingi , eti anatudanganya kuwa ana leseni moja sasa tunaianika website mzione leseni atoe usanii wake asidhani watanzania wajinga, anapenda kujilimbikizia.
Mkuu mbona unapotoka? Mtu mchafu kama Muhongo atachafuliwa vipi wakati mchafu tayari? data zake za uongo, kuwanyima watanzania haki ya kumiliki rasilimali zao kwako si uchafu? kuukana uraia wake na baadae kurudi kama mamluki kwaajili ya kuwatumikia mabwana zake Ballali Style kwako si uchafu?...
Bado hujamsaidia hujatusaidia Mkuu, Tuwekee huo utaratibu maana kwenye taarifa ya mengi ameonyesha kuwa vitalu vya Gesi kuanzia kaskazini Tanga mpaka mtwara wenye leseni ni Wageni! Ndiyo maana akatoa angalizo kuwa USALAMA WA NCHI uko hatarini..Umewahi hata kusoma huo utaratibu wa kumilikiwa na wageni uko vipi? Hivi hao wageni watakuwa wanamiliki asilimia ngapi na asilimia ngapi itamilikiwa na serikali? Ukishakuwa obsessed na siasa ni tatizo kweli, you don't think!