Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Hivi Masha naye anaweza kuwa anaropoka mambo bila kutumia akili?

Huyu Masha naye ni mtetezi wa mafisadi. Huyu bwana mdogo naona anakerwa sana na mambo mazito kuhusu ufisadi uliofanywa na swahiba zake yanayoandikwa na magazeti mbali mbali ya Mengi. Huyu hastahili tena kuwemo katika baraza la mawaziri.
 
Katika yote,

Nimependa hii aliyosema hapa Mzee Mengi.

Kuna juhudi kubwa sana zinafanyika kuzima upinzani na kuzima wana harakati wa kupambana na ufisadi Tanzania. Ukweli utabaki pale pale, huu moto hakuna yeyote anayeweza kuuzima.

Hata wakiifunga mwanahalisi, wafukuze memba machachari JF (au waifunge JF kabisa), wafunge magazeti ya thisday na kulikoni (ya Mengi) bado tu kuna sehemu tutatokea na kuhakikisha mafisadi wanaoongozwa na Manji akifuatiwa na mwizi na mkoloni mwenye uraia wa utata (rostam azizi) wamefikishwa keko.

Naam, Watanzania tumeshasema sasa basi, kamwe wasidhani hii vita ni ya Mengi pekee au Slaa pekee au Zitto pekee. Watanzania ndani na nje ya nchi yetu tumechoka kuona viongozi mafisadi wenye uroho wa utajiri wa haraka haraka kama fisadi Mkapa, fisadi Chenge, fisadi Mramba, fisadi Yona na wengine mbali mbali wakiwa matajiri wa kupindukia kupitia migongo ya Watanzania wakati Watanzania walio wengi wakiendelea kuishi maisha ya dhiki kubwa. Tutapambana nao usiku na mchana. Tanzania isiyo na mafisadi inawezekana kabisa tumechoshwa kuona nchi yetu ambayo wiki ijayo itasherehekea miaka 47 ya uhuru wa Tanganyika ikiwa haipigi hatua zozote za kimaendeleo pamoja na mikopo na misaada chungu nzima toka nchi tajiri, mabenki ya kimataifa na rasilimali chungu nzima tulizokuwa nazo.
 
1.

2.

- Mkuu Bongolander, with all due respect eti hizo quotes mbili hapo juu zina uhusiano wowote with each other?

- Halafu eti Mzee Mengi sasa anakubalika na kuaminika ndani ya JF kwamba akisema ni ukweli? Since when? Kweli tukafukue hukumu zote alizowahi kuhukumiwa hapa JF ambazo ni mbaya kuliko hata hizi za Masha? Lakini this time anasema ukweli na ni lazima waziri wa ndani ajiuzulu maana anasema ukweli na anamsema yeye haiwezekani akawa anamsema mwingine, this is Mengi bwana you know he is telling the truth,

- Really? Yale tuliyoambiwa humu ndani ya Mengi kuiba hela za vilema na kukwepa kulipa kodi ya benzi sasa yameisha kwa vile huenda amegusa tunapopataka? Duhh! What a contradictoures!

Sasa Mengi is clean clean, lahaula lakwata!

Mkuu u-clean wa Mengi sidhani kama ni hoja hapa. Inawezekana yeye ni dirty kuliko hata hao waliopo serikalini. Aliyomsea mimi nayachukulia kama ni pre emptive strikes, may be anajua zaidi alichofanya na anaona mwelekeo ulipo unaweza kumfikia na yeye. Tofauti ni kuwa yeye hayuko serikalini moja kwa moja, nilikuwa najaribu kuzungumzia wale waliomo serikalini hasa vijana ambao tuliamini kama wanaweza kuwa msaada mkubwa kwenye kurekebisha mambo. Sasa inasikitisha kuona kuwa hawafanyi tuliyotarajia isipokuwa wanafanya kinyume, kumbambikia mtu kesi, kumbambikia mtu kodi ni siasa za kijinga sana, ndio maana kama ukiona post ya kwanza nilisema KAMA NI KWELI, kitu ambacho sitaki kuamini, na nimerecall events na kauli za siku chache zilizopita. KWa hiyo hapa siko in offense ya mtu fulani au defence ya mtu fulani.
 
- Mkuu u-clean wa Mengi sidhani kama ni hoja hapa. Inawezekana yeye ni dirty kuliko hata hao waliopo serikalini. Aliyomsea mimi nayachukulia kama ni pre emptive strikes, may be anajua zaidi alichofanya na anaona mwelekeo ulipo unaweza kumfikia na yeye. Tofauti ni kuwa yeye hayuko serikalini moja kwa moja, nilikuwa najaribu kuzungumzia wale waliomo serikalini hasa vijana ambao tuliamini kama wanaweza kuwa msaada mkubwa kwenye kurekebisha mambo. Sasa inasikitisha kuona kuwa hawafanyi tuliyotarajia isipokuwa wanafanya kinyume, kumbambikia mtu kesi, kumbambikia mtu kodi ni siasa za kijinga sana, ndio maana kama ukiona post ya kwanza nilisema KAMA NI KWELI, kitu ambacho sitaki kuamini, na nimerecall events na kauli za siku chache zilizopita. KWa hiyo hapa siko in offense ya mtu fulani au defence ya mtu fulani.

- Fair enough, "kama ni kweli".

- Mengi amesema tumemsikia sasa next ni zamu ya mawaziri vijana kujibu, maana lazima kuwa na due process yaani kusikiliza pande zote kwanza kwenye kesi kama hiii, najua kua atajibiwa very soon atakayejitokeza kwanza ndio nitatoa hukumu yangu, lakini so far bado nasubiri all the facts, lakini sizuii wengine kutoa hukumu.

Thanxs! & Later!
 
The way i look at it ni kwamba ccm ni lazima igawanyike kwa namna moja ama nyingine ili kuweza kuleta mabadiliko ya kweli kwa muda mfupi zaidi...So huu ni mwanzo tu....Ni muhimu sana kwa Taifa letu, kwasababu inapokuja kwenye kuwashughulikia mafisadi kiukweli na kuhatatrisha usalama wa maslahi yao ya muda mrefu na mfupi.....Basi mengi yatajitokeza. Mfano ni Mh Masha kwenda kuwatembelea watuhumiwa huko mahabusu Keko.

Mwalimu kwenye ile hotuba yake ya mwaka 1995 alipokuwa akilifananisha Taifa letu na nyumba wakati wa tetemeko...alisema kutatokea mtikisiko kuanzia kwenye paa hadi kwenye msingi kutakuwa na nyufa...Sasa kiukweli kuziba nyufa kama hizo si ni sawa na mapinduzi kabisa? Na jinsi jamii yetu ilivyo ni wazi kabisa tunahitaji mapinduzi kuanzia ngazi za chini kabisa ambazo ndiyo kama misingi ya jamii.

Nafikiri huu ni mwanzo tu wa "mtikisiko" ambao ni wazi hautakwepeka kwani ndio moja wapo ya njia madhubuti ya ku move forward bila kuwa na msuguano mkubwa zaidi.

Na kuhusu ndugu Mengi kwa kusema ukweli kwa maoni yangu yuko upande wa wazalendo hilo liko wazi kabisa na huyo waziri kijana ni lazima ajuwe hilo na si kuanza kusema eti ni mchafu, sasa huo uchafu wake ndio huo wanaotaka kumbambikia kesi ya kodi? Kwahiyo kabla ya Mkapa ama Yona ama Mramba kupanda mahakamani basi Mengi apande kwanza?

Kumbe ndiyo maana hao waheshimiwa walithubutu kuliangamiza taifa kwasababu kweli wanaamini sisi ni wajinga kabisa....Yani this is black lakini wao wanakulazimisha uone ni red.

We know they will try anything to protect themselves na kwasababu mambo ya mahakamani ni public sasa wale wenye kuwapa sapoti watuhumiwa hawawezi kujificha...Msije kushangaa Mkapa anatoa kauli ya kuwasapoti ama zile element za wale wanaomsikiliza ambao wamo kwenye serikali ya JK kuwasapoti watuhumiwa hao kama ilivyojitokeza kwa waziri Masha.

Hivyo basi kabla hatujaanza kunyanyua champagne na kupongezana...Ni budi tuwe makini sana wakati huu mgumu na muhimu sana kwa Taifa letu.
 
Bila jasho la damu kweli maendeleo ni ndoto
Katika dunia ya leo ukombozi uliobakia ni wa kiuchumi, na wakoloni wake wanahasira sana na hawako tayari kuachia watumwa wao(wananchi masikini) vita hii ni kubwa na nzito ni kweli wengi watakufa na wengi watafilisiwa.
Kaza buti Na Tumuombe Mungu.
Mapambano haya ni mazito ila ushindi ni lazima kwa jinsi yeyote ile.
Kwa wanao tishia wajue kuwa huu ni mwanzo, mapambano yanapamba moto, kwa wanaotishwa wajue wao ni mashujaa na mapambano ndio yanaanza.
 
It’s rotten, it can’t be repaired; it needs replacing. Kila unaposhika pameoza! Use by date ya serikali hii ya CCM ilipita kitambo lakini tunaendelea kuikumbatia tu!

We need a new beginning. To paraphrase Obama, let me say that we cannot continue to use the same CCM “leaders” over and over again and expect a different result.

Kama wananchi wa Mbeya Vijijini watachagua mtu wa CCM kuwawakilisha basi nitajua tumekuwa nchi ya vipofu. Utachaguaje samaki kwenye kapu lenye samaki wengi hivyo waliooza? Yako makapu mengine!

Labda JK anajitahidi kukarabati hili liserikali lake. Kwa maoni yangu, halikarabatiki. Ni la kubadilisha (kwa kura za wananchi).
 
Haya ya Reginald...
Hivi karibuni waziri mmoja kijana anayeongoza wizara nyeti alipendekeza nibambikiziwe kodi...

Alipendekeza, hajafanya, Ajakufanya Only kama atakuwa na mda! OOPS


MMKJJ Alas KLHNEWS
Vyanzo mbalimbali vimeihakikishia KLHN kuwa Waziri huyo ni yule mwenye dhamana ya Mambo ya Ndani ya nchi. Vyanzo hivyo toka kwenye Jumba letu Kuu vimeihakikishia KLHN kuwa siku za hivi karibuni Waziri huyo amekuwa akijikuta akitajwa na vyombo mbalimbali vya habari na vile vya udaku wa mtandaoni akihusishwa na tabia mbalimbali ambazo kwa mujibu wa Jumba hilo vinaiweka vibaya sura ya uongozi wa Taifa.

Hata MMKJJ hajathibitisha hii... Inaonekana hata "Jumba letu Kuu" wamekerwa 😱

Vuta nikuvute kati ya wenye mtandao ni kali kweli kweli!😀

Reginald nae ana-kamtandao kake ambacho naamini hata kwenye hilo "Jumba letu Kuu" wanafanya kazi 24/7 Kuona nani ni nani nao hawana mbavu huko!

Amani

😀😀🙂
 
Mhhh,

Mwenzangu, Nilihesabu kuwa wewe ni miongoni wa wale waliodai kuwa mimi naharibu hii forum? What happened? Nikiwa hapa nilikuwa naharibu forum, na nilipotoka ili nisiharibu forum, nikawa msaliti na mkosa mpango?

I hope hiki kitu unatania. Sijui lini nimewahi hata kudokeza kitu kama hicho. Umenichanganya ndugu yangu. Chochote kilichosemwa kikakufanya ufikiri hivyo utakuwa ulinisoma vingine kabisa. Halafu hata ningekuwa kweli nimedai hivyo sidhani kama mimi au, kwa kweli, yeyote yule humu ana uwezo wa kukukimbiza wewe hapa. Sio wewe yule ninaemjua. Ngoja niangalie kama ni yule yule, hebu nikuulize hivi: sasa kilichokurudisha ni nini hasa kama ulishatupisha ? Eennh, kilichokushinda kubaki huko huko ni nini hasa, si tulikutimua? 🙂
 
I hope hiki kitu unatania. Sijui lini nimewahi hata kudokeza kitu kama hicho. Umenichanganya ndugu yangu. Chochote kilichosemwa kikakufanya ufikiri hivyo utakuwa ulinisoma vingine kabisa. Halafu hata ningekuwa kweli nimedai hivyo sidhani kama mimi au, kwa kweli, yeyote yule humu ana uwezo wa kukukimbiza wewe hapa. Sio wewe yule ninaemjua. Ngoja niangalie kama ni yule yule, hebu nikuulize hivi: sasa kilichokurudisha ni nini hasa kama ulishatupisha ? Eennh, kilichokushinda kubaki huko huko ni nini hasa, si tulikutimua? 🙂

Unajua miongoni mwa makosa mengi aliyofanya Karl Rove, linalomsumbua zaidi ni lile la kufikiri kuwa yeye alikuwa bora kuliko watendakazi wengi wa Joji Kichaka. Alipoambiwa na Oneil, Powell na wengine wengi kuwa anaharibu chama cha Reps, yeye hakusikiliza ushauri uliopingana na principles zake za kutochukua wafungwa (take no prisoners).

Amekuja kugundua hayo ikiwa too late wakati Kichaka akiwa na approval rate kwenye toilet. Siasa za Kichaka na uongozi wake zimenifundisha mimi na baadhi ya rafiki zangu kuvuta pumzi (ule wimbo wa wakenya) kila baada ya muda na kusikiliza ushauri wa wengine. Nilitoka kupima ukweli wa madai yote yaliyotolewa dhidi yangu na kwa hakika naweza kusema zaidi kuwa madai hayo yamethibitika kuwa si ya kweli.

Nina hakika kabisa na ninachosema na sina haja ya kuanza kuleta maandishi yako hapa yaliyopita uliyosema kuwa ninachangia kuharibu hii forum (direct na kupitia wengine). Nimevuta pumzi na kutoa nafasi ya reality to kick in ili kujua kama nikitoka hapa hii forum itakuwa bora kuliko nilivyokuwa hapa.

Matokeo yake nimegundua kuwa yale yaliyoelekezwa dhidi yangu, ni yale yale yaliyoelekezwa baadaye kwa members wengine. Madai kuwa nilikuwa nina haribu hii forum yanaonekana yalikuwa na sababu nyingine zaidi ya kutaka kuboresha hii forum. Na kwa vile nina wajibu na kila sababu ya kuwa hapa kwa kadri muda wangu unavyoruhusu, basi nipo hapa mpaka pale nitakapoamua otherwise.

Jiandae tu kuwa na mimi hapa kwa muda mrefu sana. Na kwa vile mafisadi sasa wanaanza ugomvi na Mengi, ..... ladies and gents... start your engines
 
Huyu kijana analaumiwa kwa utumiaji mbaya sana wa madaraka yake.Kuna habari kuwa aliwahi kuwatolea bastola watu aliokuwa anakunywa nao bar huko mwanza jimboni kwake bila sababu yoyote ya msingi.
Tuamue kwa haki jamani,kama Mengi ana maovu yake wayaseme lakini kama wao wana maovu yao wayaache magazeti na TV zake zitangaze na wananchi wayajue.
Tukikumbuka last year Malima alimtuhumu Mengi kwa mambo ambayo si ya msingi eti kuwa anatumia vyombo vyake kuliko rais na waziri mkuu.Huu pia ulikuwa upumbavu,mbona Mama Lwakatare anatumia kutangaza kanisa lake hawasemi?
Mtu anapoanzisha chombo cha habari anakuwa na malengo yake ili mradi havunji sheria ya nchi.
Tutaendelea kuwachoma hata kama hawapendi.
 
Huyu Masha sasa anakoelekea tayari siko. Juzi tu walemevu wamemlaumu kwa kauli yake kwamba mauaji ya maalbino sio ishu kubwa sasa anaongea utata mwingine juu ya kauli zake, hii ni ishara tosha kwamba anafanya kazi kwa hisia binafsi bila kujali kutimiza wajibu wa kile anachotakiwa kukifanya.
 
Waziri atishia kuniua-Mengi


*Adai pia anasuka njama kumfilisi
*Chanzo ni msimamo kwa mafisadi

Na Peter Masangwa

MFANYABIASHARA mashuhuri nchini ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya IPP, Bw. Reginald Mengi amedai kutishiwa kifo na mtu aliyemtaja kuwa ni Waziri kijana katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete akihusisha vitisho hivyo na msimamo wake thabiti dhidi ya ufisadi nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana, Bw. Mengi alisema kuwa amekuwa akituhumiwa kuwa vyombo vyake vya habari vimekuwa mstari wa mbele katika kupiga vita ufisadi, jambo ambalo kwa maoni ya Waziri huyo kijana sio zuri kwa sababu linawanyanyasa baadhi ya watu.

''Nilitegemea Waziri huyo msomi angefahamu jinsi vyombo vya habari vinavyofanya kazi, kwani anayeamua nini kiandikwe na nini kisiandikwe ni mhariri wa gazeti ambaye taaluma yake ni uandishi wa habari na siyo mmiliki wa vyombo vya habari,'' alisisitiza Bw. Mengi.

Bw. Mengi alisema amekuwa akipokea ujumbe mfupi wa maandishi kwa njia ya simu kupitia namba 0768 373967 ambao umekuwa ukimlaumu moja kwa moja kuwa anatumia vyombo vyake vibaya kwa nia pia ya kujiandalia njia ili awanie Urais siku za usoni.

Uliusoma ujumbe huo ulioandikwa: ''Ni fadhali kunyofoa roho yako ipotee kuliko kuendelea kukuachia uchafue amani na utulivu wa nchi kwa TAMAA zako za kutaka Urais, Ugomvi wako na akina Manji hauwezi kutufanya watanzaniawote tuingie katika vita vya wenyewe kwa wenyewe uliofanya yanatosha, enough is enough, kaa tayari.''


Alisema Waziri huyo amekuwa akihusika katika njama pia nzito kwa kupendekeza katika vikao vya Serikali ili yeye (Bw. Mengi) apandishiwe kodi ili ashindwe kufanyabiashara na kufilisika kama alivyofanyiwa mfanyabiashara mmoja huko nchini Urusi.

Akitoa msimamo wake kuhusu vitisho hivyo, Bw. Mengi alisema wanaomfanyia hujuma hizo watambue kwamba hata kama watafanikiwa kuvinyamazisha vyombo vya habari kwa hujuma zozote na hata kama yeye hatakuwepo duniani, moto wa kupiga vita ufisadi uliokwishawashwa katika akili za wanajamii hauwezi kuzimika kamwe.

Bw. Mengi alithibitisha kuripoti vitisho hivyo kwenye Kituo cha Polisi cha Oysterbay na tayari uchunguzi umeanza kufanyika.

Aliusifu utawala wa Rais Kikwete kwa jinsi ulivyojipanga kuondoa tatizo la ufisadi nchini na kusema ni hatua ambazo zinapaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.

Akijibu swali kuhusu uhuru wa vyombo vya habari nchini, Bw. Mengi alisema kuwa kuna tofauti kubwa sana ukilinganisha na utawala wa Awamu ya Tatu kwani sasa wanahabari wamekuwa huru zaidi kujadili masuala ingawa hauwezi kupatikana uhuru wa moja kwa moja.

''Nampongeza Mzee Mwinyi kwani ndiye baba wa demokrasia ya habari nchini kwa kuruhusu kila mwenye uwezo wa kumiliki chombo cha habari kwani ni haki ya kila mtu kupata na kutoa habari,'' alisema.

Majira liliwasiliana kwa njia ya simu na mpelelezi wa kesi hiyo aliyeko kituo cha polisi Oysterbay ili kuzungumzia zaidi suala hilo lakini alieleza kuwa nje ya ofisi kikazi na kuahidi kulifanyia kazi suala hilo.


Habari ndiyo hiyo kutoka majira
 
Sasa wanataka kumwadapisha sio ahahaaaaaaaaaaaaa jamaa bwana.
Ila na yeye katoa maelezo mazuri na ujumbe mzuri kwao kuwa hata yeye wakimtoa kwenye ramani ya dunia moto huu dhidi ya ufisadi ndio kwanza unawaka.

Huyu waziri juzi pia si elenda kuwaona wakina mramba na yona rumande mhhhhhh ,mwenye conection jamani.Pia tukumbushane sehemu alizonufaika kwenye ufisadi.

Je alikuwa akimshauri muungwana kuwa IPP media anamwalibia muungwana au inawaalibia mafisadi?

Ninavyokumbuka huyu jamaa ni mhusika mkuu kwenye DEEP GREEN. Ila sina hakika kama ana connection na akina BPM na DY. Hata hivyo inawezekna ni maandalizi kwani hata yeye anaweza kuwa na taarifa kwamba naye ndiko anakoelekea. Mwenzio akinyolewa.... So alikuwa anaandaa kichwa kwa ajili ya kinyozi.
 
Nafikiri ni sahihi kama unapata habari kama alizopazta Mengi kutafuta namna ya kuzi expose. ukisha hakikisha kuwa ni kweli by expsosing the news wisely is the first stape ya kuzidhoofisha na kuzitafutia muafaka wa kudumu.

Sifikiri ni sahihi sana katika hali hiyo kuweka jina la mtuhumiwa moja kwa moja. Ni mapema.

Mtuhumiwa atakuwa amepata impact kuliko sisi ambao sio watuhumiwa.

Sisi ni kama tunapewa habari tu...

Then yeye Mengi anakuwa kwenye position ya kuobserve the move foward ...maana patakuwa na response!! ambayo itampa next stape..afanye nini au asifanye nini.

Lakini all in all hii ni bora kama hatua ya mwanzo kujaribu kumdhiti mtu anayetaka kwa siri kukufanyia jambo kama hilo. Strategically to expose the secret move publically.
 
Mengi acha udaku!

Kama ni kweli ongea kwa kujiamini!

Hata mimi naungana na wewe Kuhani...nilitegemea Mengi atoe maelezo ya kueleweka. Waziri fulani bin fulani na awe na evidence. Nafikiri pia Mzee Mengi anapenda "sifa" kitu kidogo tu keshaweka "Press Release" anatoa vitamko tamko. Tumemsikia lakini hatujaelewa anasema nini ...........! Au saa nyingine naona anakuwa amesahaulika kwa hiyo anatafuta "gia" ya kupamba magazeti at least tangia jana usiku yeye ndio ameshika hatamu ya mazungumzo! Mara SMS mara maneno...kwani wangapi wametishiwa kwa sms...mbona hawatoi press release?
 
Mengi m**ni na mnafiki tu.!

Mie nilishamchoka kuona upuuzi anoongea na mambo yake ya kila siku kutafuta sypmpathy kwa watanzania ndiyo yanayonikera sana. Inshort,Mkuu Mwanakijiji aacha ushabiki,Una uhakika gani kama ni MAsha na kwanini unamwandama masha?

Mkuu FMES tupo ukurasa mmoja.. Mie nina uhakika siyo masha sababu hausiki na mambo ya kodi.Labda kama kaanza ugomvi na malima Pili Mwambie Mengi akalipe deni alilokuwa anadaiwa ana NBC,yeye ni mmoja wawatu walioimaliza NBC
 
huyu kijana aliingia serikalini kwa ajenda ya ufisadi kumbe kaingia kipindi kibaya ndio maana ana hasira na anaropoka hovyoooo!!!!
 
Mimi naona nayumba tu kama wengine wanavyo yumba humu ndani kuhusu hii ishu.
Naweza kuamini kuwa wanao mtetea Masha wana masrahi naye binafsi.Kama ametuhumiwa kwa nini umtetee mwite aje au naye atoe utetezi wake.
Huyu Masha si ndo hata kule kwenye tunako jing'ata ulimi anatajwa tajwa sana kule ni kweli watakuwa wanamwonea?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom