Membe sio mmiliki wa Naf Beach Hotel

Membe sio mmiliki wa Naf Beach Hotel

Nafurahi kuona watu mkibishaba kuhusu mmiliki wa Naf beach.Mm nimewahi kufika kwenye hizo hotel tatu,NAF BLUE,NAF BEACH NA FAN CITY kwa kazi MAALUM ambayo siwezi iweka wazi kwa sababu za kiusalama.Nillikaa hapo kwenye hotel kwa zaidi ya wik mbili kutokana na kazi husika.
Naweza kusema kwa uhakika hotel za NAf blue na Fan city ni mali ya Sheb mix.
Hotel ya NAF BEACH ndo kizingumkuti;watu wanasema mara ya Sheb na wengine mara ya Membe.Sheb na familia yake ndo wanaonekana wamiliki wa NAF BEACH kwa 100%.Lkn kuna doc ambazo niliziona (siweze kuzisema) mh.Membe na vigogo wengine wakiwa copied.
Kwa ss kuna hotel nyingine mpya mbili zinazosemekana ni za Sheb zitafunguliwa siku yoyote.Moja ipo Lindi na nyingine Mtwara.

NB:Nashindwa kuweka hii habari na "supporting documents" vizuri kwa sababu za kiusalama.

Sasa si heri hata haya usingeyaandika
 
Mnanishangaza sana.Taarifa tulizonazo ni kwamba Shebby alijenga hoteli kwa mkopo wa Crdb na pato lake la udalali wa zao la korosho.

usipoteze muda na watu wanaoganga njaa kwa siasa za maji taka. anaesema NAF BEACH ni hotel ya Membe ni dhahiri hamjui Membe wala Shebby.
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!
Kawadanganye watoto wako!
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!

Picha bana!!
 
Peleka ujinga wako hapa nani unamfanya mtoto asiyejua uhusiano wa membe na huyo shebby wakati iko wazi biashara zote za membe shebby mix ndo msimazi au unataka tuweke na orodha ya biashara zake hapa, umechelewa kujisafisha bora ungepiga kimya.
Tunajua shebby mix ni mfanya biashara lakini hana uwezo wa kukopa mabilion ya kuwekeza katika biashara kubwa kama zile
Au ni lile duka la simu pale stand kuu ?
Au ni mazao na mbao?
Au nyara za serikali?
JIPANGE.

wewe unachekesha. unamjua vizuri Shebby? yaani Membe ahitaji msimamizi wa biashara zake amuweke Shebby?? hizo biashara ni za Shebby kama unasema ni za Membe weka ushahidi hapa.
 
Ile NAF ya baharini gharama zake ni mtaji mzima wa CRDB, ni lazima uwe fisadi ndo utamiki hotel kama hiyo,SHEBBY hana ubavu wa kumiliki hotel kama hiyo anauwezo wa kumiliki pikipiki , hat kile kiwanja cha karibu na maposeni kauza.

hotel substandard ile ndio ulinganishe na mtaji wa CRDB??? how much are they paying u??
 
Wakati Shebby ananunua hicho kiwanja cha naf beach hotel kwa Mkapa wa JAGAJU alimwambia ni kigogo Fulani ndiye mwenye kununua yeye ni mtu wa kati tu baada ya kutaja jina la kigogo huyo bwana ardhi mteule MAIBA ilifanya fasta kutransifer. Shebby alikiri kuwa yeye ni mtu wa kati tu.

aisee ni rahisi sana kuwa-fool wabongo!
 
Mbona unaongea kama ww ndo membe? Ulipokosea n pale uliposema, Hata kama n Ya kwake at least ana Toa ajira kwa wazawa. Kuliko mafisadi wanapeleka pesa Dubai . Maana yake n nn. Kingine mentality yangu sivyo inavoifikiria brother. I feel so proud nikiona mtz anajitahidi kuwekeza tz na kwingine, Nilikuwa najisikia fahar Sana nikikuta precision air O.R Tambo kabla haijaacha Safari zake huko.

acha kutetea usichokijua, Jenga hoja namtumbo

Shida ya watanzania hatujiamini wenyewe na hatuamini mwafrika mwenzetu akimiliki biashara kubwa. Tunapoona mswahili mwenzetu ana biashara yenye mafanikio, conclusion yetu ni kwamba hawezi kuwa mmiliki wake ...kwasbabau mtu mweusi hawezi kumiliki biashara. Ile hoteli ingekuwa inamilikiwa na Somji, hapo ndio tungeridhika ni ya kwake. Hii ndio mentality ya General....


Na hata kama for the sake of argument hiyo hoteli ingekuwa ni ya Membe, basi nampongeza maana walau yeye amewekeza nchini....hoteli ile inatoa ajira kwa watanzania, inatoa fursa za wauza maziwa, vinywaji na vyakula kupata soko na inalipa kodi nchini. Bora hivyo, kuliko akina Chenge na mafisadi wengine wanaoweka pesa zao Jersey, Dubai na kwingineko ambako wananchi haaambulii kitu...

That said, Nijuavyo mimi mmiliki wa hoteli ile ni mfanyabiashara mtanzania Bwana Shabani ambaye pamoja na hoteli hiyo anamiliki kampuni kubwa ya ujenzi kanda ya kusini. Bwana huyo pia ni Exporter wa Ufuta na korosho nchini Japan na kwingineko. Bwana Shabani biashara hakuanza leo, amemekuwa akifanya biashara kwa mafanikio makubwa kabla hata Membe hajawa Waziri mwaka 2001.
 
Basi NAF siyo na Shebby Mix ni Ya baba yako umefurahi sasa?
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!
Mkuu NAF ni Ya bana yako mkubwa sasa mmefurahi? Maana povu lawatoka kudiscuss watu
 
Back
Top Bottom