GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,593
- 108,963
Hilo eneo (Coco Beach) Hayati Magufuli alikataa kabisa kupewa Watu (hasa Matajiri) wawekeze hapo akisema kuwa paachwe wazi ili hata Masikini akina GENTAMYCINE tuwe tunakuja Kutembea, Kuogelea na Kupunga Upepo mwanana wa Baharini (wenye Afya) bila tatizo.
Cha Kushangaza na Kusikitisha tayari sehemu ya Eneo la Coco Beach ameshapewa Mwekezaji (Mfanyabiashara) maarufu Mmiliki wa Samaki Samaki na kuanza Kuzungushia kabisa na Mabati Eneo Kubwa tu ambalo huko nyuma lilikuwa likikaliwa na Sisi 'Beach Goers' tuliotukuka huku tukipunguza Mawazo ya Shida zetu za Kimaisha.
Na Wenye Akili tunajua huyu Mfanyabiashara Samaki Samaki nyuma yake kuna akina nani, anafanya Biashara gani nyingine ya Siri isiyotakiwa hivyo kupewa Kwake hilo eneo ni Kututhibitishia kuwa kile alichokikataa Hayati Magufuli sasa kinafanyika na Siku si nyingi Matajiri na Mafisadi watagawana Coco Beach yote na Masikini kuingia hapo kwa Hela au ukijua Kuogelea kama GENTAMYCINE unakuja huku maeneo ya Police Officers Mess unaogelea taratibu na kwa Mikogo huku ukielekea usawa wa Coco Beach na ukifika unatoka Majini unafanya yako na Maisha mengine yanaendelea.
Na nasikia hata Beach nyingine ya Sisi Masikini ya Kawe Beach nayo pia mnataka kuwapa Matajiri na Mmoja ni Rafiki wa Karibu wa Mtoto wa Kiongozi Mmoja Mstaafu ( ambaye Nyumba yake ya sasa inatizamana na Kawe Beach ) ili awekeze na pia muwafukuze Wavuvi walio Jirani nae kwa Kigezo cha kulinda Usalama wake.
Kwakuwa mmeamua taratibu kutunyang'anya Sisi Masikini akina GENTAMYCINE Beach zetu zote za Coco Beach na Kawe Beach tunaomba mtuombee kwa DP World watutafutie Beach mpya ili tuwe tunaenda huko kwani yawezekana hawa ndiyo wakawa na Uchungu wa Maisha Magumu ya Watanzania kuliko hata ilivyo kwa Viongozi Wetu ambao pia ni Watanzania Wenzetu.
Cha Kushangaza na Kusikitisha tayari sehemu ya Eneo la Coco Beach ameshapewa Mwekezaji (Mfanyabiashara) maarufu Mmiliki wa Samaki Samaki na kuanza Kuzungushia kabisa na Mabati Eneo Kubwa tu ambalo huko nyuma lilikuwa likikaliwa na Sisi 'Beach Goers' tuliotukuka huku tukipunguza Mawazo ya Shida zetu za Kimaisha.
Na Wenye Akili tunajua huyu Mfanyabiashara Samaki Samaki nyuma yake kuna akina nani, anafanya Biashara gani nyingine ya Siri isiyotakiwa hivyo kupewa Kwake hilo eneo ni Kututhibitishia kuwa kile alichokikataa Hayati Magufuli sasa kinafanyika na Siku si nyingi Matajiri na Mafisadi watagawana Coco Beach yote na Masikini kuingia hapo kwa Hela au ukijua Kuogelea kama GENTAMYCINE unakuja huku maeneo ya Police Officers Mess unaogelea taratibu na kwa Mikogo huku ukielekea usawa wa Coco Beach na ukifika unatoka Majini unafanya yako na Maisha mengine yanaendelea.
Na nasikia hata Beach nyingine ya Sisi Masikini ya Kawe Beach nayo pia mnataka kuwapa Matajiri na Mmoja ni Rafiki wa Karibu wa Mtoto wa Kiongozi Mmoja Mstaafu ( ambaye Nyumba yake ya sasa inatizamana na Kawe Beach ) ili awekeze na pia muwafukuze Wavuvi walio Jirani nae kwa Kigezo cha kulinda Usalama wake.
Kwakuwa mmeamua taratibu kutunyang'anya Sisi Masikini akina GENTAMYCINE Beach zetu zote za Coco Beach na Kawe Beach tunaomba mtuombee kwa DP World watutafutie Beach mpya ili tuwe tunaenda huko kwani yawezekana hawa ndiyo wakawa na Uchungu wa Maisha Magumu ya Watanzania kuliko hata ilivyo kwa Viongozi Wetu ambao pia ni Watanzania Wenzetu.