Kwanini Mmiliki wa Samaki Samaki kapewa Kuwekeza Coco Beach sasa ila Kipindi cha Hayati Magufuli hakupewa?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,593
108,963
Hilo eneo (Coco Beach) Hayati Magufuli alikataa kabisa kupewa Watu (hasa Matajiri) wawekeze hapo akisema kuwa paachwe wazi ili hata Masikini akina GENTAMYCINE tuwe tunakuja Kutembea, Kuogelea na Kupunga Upepo mwanana wa Baharini (wenye Afya) bila tatizo.

Cha Kushangaza na Kusikitisha tayari sehemu ya Eneo la Coco Beach ameshapewa Mwekezaji (Mfanyabiashara) maarufu Mmiliki wa Samaki Samaki na kuanza Kuzungushia kabisa na Mabati Eneo Kubwa tu ambalo huko nyuma lilikuwa likikaliwa na Sisi 'Beach Goers' tuliotukuka huku tukipunguza Mawazo ya Shida zetu za Kimaisha.

Na Wenye Akili tunajua huyu Mfanyabiashara Samaki Samaki nyuma yake kuna akina nani, anafanya Biashara gani nyingine ya Siri isiyotakiwa hivyo kupewa Kwake hilo eneo ni Kututhibitishia kuwa kile alichokikataa Hayati Magufuli sasa kinafanyika na Siku si nyingi Matajiri na Mafisadi watagawana Coco Beach yote na Masikini kuingia hapo kwa Hela au ukijua Kuogelea kama GENTAMYCINE unakuja huku maeneo ya Police Officers Mess unaogelea taratibu na kwa Mikogo huku ukielekea usawa wa Coco Beach na ukifika unatoka Majini unafanya yako na Maisha mengine yanaendelea.

Na nasikia hata Beach nyingine ya Sisi Masikini ya Kawe Beach nayo pia mnataka kuwapa Matajiri na Mmoja ni Rafiki wa Karibu wa Mtoto wa Kiongozi Mmoja Mstaafu ( ambaye Nyumba yake ya sasa inatizamana na Kawe Beach ) ili awekeze na pia muwafukuze Wavuvi walio Jirani nae kwa Kigezo cha kulinda Usalama wake.

Kwakuwa mmeamua taratibu kutunyang'anya Sisi Masikini akina GENTAMYCINE Beach zetu zote za Coco Beach na Kawe Beach tunaomba mtuombee kwa DP World watutafutie Beach mpya ili tuwe tunaenda huko kwani yawezekana hawa ndiyo wakawa na Uchungu wa Maisha Magumu ya Watanzania kuliko hata ilivyo kwa Viongozi Wetu ambao pia ni Watanzania Wenzetu.
 
Mama Africa na Jamaica kama wakiziuza itakuwa balaa sasa ,CARLITTLE si alipewa Beach Camp au wameuongezea nyingine?
Hawa jamaa wana roho Mbaya sana, lengo lao ni kuiuwa Wavuvi camp wameshindwa.

Wavuvi inafanyiwa figisu kama zote bila kujari kuna Watanzania wamepata ajira pale na wanaendesha maisha yao.

Kuna mwanangu mmoja alikuwa anabeba chuma tu mtaani bila faida, kalamba ajira pale ya baunsa anapiga pesa fresh sana tip za kumwaga kutoka kwa wateja, kapunguza kiwingu mtaani na yeye ni mtu sasa hivi.

Sasa hii mizaramo isiyokuwa na hata huruma yenyewe inajifikiria wao tu na familia zao shenzi type.
 
Mbona yule mtoto wa kiongozi nchi nzima ni yake nilienda Gairo nikaonyeshwa huu mlima ni wake umejaa madini,nikaenda Mahenge nikaambiwa huu msitu wote wanakijiji walihamisha ni kupisha hifadhi Siri umejaa madini tupu za chini ni wake anashirikiana na wa yuesi ei,Kila mkoa utasikia ili eneo ni lake,huyu mtu ni tajiri sana ee.
Bado kwenye malori story ni nyingi
 
Kumekucha; kama kawa, katika kupunguza stress za maisha, watu wamedamka na mashambulizi yao kwa kina jk wao!
Mwambie watafanya Siri Mambo yao ila GENTAMYCINE nina Uwezo mkubwa wa kujua Taarifa za Ndani na huwezi Ukanificha nikitaka kujua.

Iambie hiyo Familia ya huyo Fisadi na huyo Mwanae Fisadi Aliyeshindikana kwakuwa anaogopwa na walio Juu kuwa tunajua aliye nyuma ya huyo Samaki Samaki ni Wao na Yeye hapo Wamemtanguliza tu ili Kutuzuga tuliowazidi kwa Akili, Upeo na Maarifa.
 
Ulidhani Ridhiwani Kikwete aliwekwa wizara ya Ardhi kwa bahati Mbaya?

Ndio maana huyu mtoto huwezi kumuona anakwenda Umra Saudi Arabia anaweza akafia hukohuko kwa roho Mbaya aliyorithi kwa babake.

alipokuwa wizara ya ardhi lake oil imeongeza vituo vya mafuta vingi sana mijini kapata ardhi nyingi sana. na ardhi nyingi kahodhi huyu anamzidi Dp world
 
Back
Top Bottom