senator
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 1,924
- 68
Hili suala lilishafanyiwa uchunguzi na vyombo husika na ukweli umeshajulikana: Membe sio mmiliki wa NAF, FAN city, wala NAF blue Hotel.
NAF inasimama badala ya herufi za majina ya wototo wa mmiliki halali Shaibu Mohamed Juma. Watoto wanaounda NAF au FAN city ni Nadhir Abdul na Farid. Hotel hizo zilijengwa tangu enzi za utawala wa Mkapa kabla Membe hajawa Waziri. NAF beach ilichelewa kuanza kazi kwasababu ya kuchelewa kwa mkopo kutoka crdb uliombwa na mmiliki. Mkopo ulitoka mwakajuzi na hivyo hotel kuanza.
Ifahamike kwamba Chadema, takukuru, usalama wa Taifa, kamati ya maadili ya ccm na Cuf walishafanya uchunguzi juu ya hotel hii na wote wakaja na jibu moja: Membe hana biashara ya hoteli sehemu yeyote duniani. Wote wamejiridhisha kwamba upo uhusiano wa kawaida wa kirafiki kati ya bwana Shaibu Juma na familia ya Membe. Sawa na uhusiano uliopo kati ya mmiliki wa Serena hotel na Membe.
Uchunguzi wa mwisho na wakaribuni ni ule uliofanyika na mahasimu wa Membe ndani ya CCM. Huu nao haujamweka Membe kama mmiliki wa hotel lakini mahasimu hawa wameamua walazamishe kesi kwasababu hawana kesi. Wakati EPA Richmond Rada Tokomeza na Escrow vimekuwa vikiwasumbua mahasimu wa Membe, Membe amekuwa msafi Wakati wote.
Mahasimu hao pia wamekuwa wakitapatapa kwamba Membe kala ela za Ghadafi. Ni nchi gani duniani ambapo misaada au msamaha wa madeni unapitishiwa kwenye account ya waziri wa mambo ya nje? Kwa taarifa zilizo sahihi ni kwamba wanasheria waliotuingiza mkenge Escrow ndio wanaosambaza habari za uongo kwasababu Membe alikataa ombi lao la kuitambua kampuni ya MELt kuwa mmiliki halali wa fedha zilizopo TIB badala yake akatambua MEIS company kama ambavyo ilihainishwa na serikali ya Libya. Huwezi kumwingiza Membe mkenge hata siku moja na Tz tungepata viongozi wa aina ya Membe ambao wako makini na wametenganisha siasa na biashara tungekuwa mbali. Mbali sana.
Naona Mgonjwa umeongea facts ambazo wadau wamekuwa wapole kupingana na taarifa yako. Basi Nimekubali BCM hausiki na umiliki wa hizo hotel.