Membe sio mmiliki wa Naf Beach Hotel

Membe sio mmiliki wa Naf Beach Hotel

Hivi ni nani amekuambia hana uwezo? Uwoga wako wa kukopa ndo usifanye na wenzako wawe sawa na wewe. Hata Rombo Green view mmiliki alitolea ufafanuz ni mikopo. Anasema mwanzon ilianza ikiwa ndogo. Hata NAF ilianza Lodge ndogo ikiitwa NAF View, baadae sana ikajengwa NAF Beach na FAN City. Na hayo majina FAN au NAF ni kageuza majina matatu ya watoto wake huyo Shebby kama mdau alivyofafanua hapo juu!

Shebby kaanza gemu za kuhangaika na biashara pale Mtwara muda sana. Jamaa inaonekana anajua kufight!

Inawezekana Membe akawa na hisa labda kwa kuwa wako karibu au ni marafiki, hilo ni vigumu kuthibitisha, ila kusema Shebby hawez kukopa benki inashangaza, kwa nini asiweze? Ni mtu aliyeishi Mtwara muda na kuhangaika kibiashara, na wakat ule Mtwara viwanja na mapori ilikuwa ni bei ya kutupwa. Sasa kama alinunua kwa vision na baadae imekuwa value ni kubwa baada ya ugunduz wa gesi huoni ardhi imekuwa na thamani kubwa na hivyo ni rahisi kuwa na colateral ambazo ni rahisi kukopesheka benki? Eti Shebby hana uwezo wa kukopa, kwa nini? Kama wewe ni mwoga wenzako wanaweza?

Wakaz wa Mtwara nao ni wajanja sana siku hizi.

Watu kama Maarifa anamilik Safari Radio,Makonde Beach na Makonde Water. Bila kumsahau Mr Hamza kama sikosei anamiliki Pride FM, na hawa wote ni wazawa wa Mkoani Mtwara. Baada ya Wanamtwara kufunguka kifikra nao wako vizuri sawa na wakina Mfugale wa Iringa anaemiliki Ebony FM na Peacok Hotel au MAiro anaemiliki Hotel La Kairo Mwanza au mzawa wa Arusha/ Moshi anaemiliki Naura Springs. Exposure imewatoa matongotongo wanaMtwara, na bado Mahotel yanajengwa kwa wingi sana Mtwara kwa sasa. Wanamtwara na Watanzania wanawekeza sana tena sana. Naamini Mtwara soon itaipita hata miji mingine iliyotangulia. Sidhan kama Morogoro, Iringa, Dodoma na hata Mbya kuna hotel ya nyota4 sina hakika!

Duuunh, mnamuharibia mzee wa watu bure kwa kubwabwaja, hata kama sio yake utetezi wa aina hii ni bora ya kukaa kimya!!!!
 
Kwani ile hotel gharama yake ni kama bei gani. Na msimu wa korosho na ufuta mikoa ya kusini hukusanya billion ngapi? Hazifiki angalau 100? Na kwa mtu serious hawez kukusanya billion5 hadi 10? Ukikadiria kwa kutumia pro rata rate, billion 4 hadi 6 zinajenga hotel ile. Shebby naamini anaweza.

SIna ubishi na hilo lakini hoja yangu ni kuwa umefika wakati sasa wakulima wapewe au wajipe akili ya kujiongeza, maana wao miaka yote ni kulia tu, ni ajabu korosho walime wao hoteli ajenge dalali na wao wabaki kulalamika tu miaka nenda rudi, viongozi wajikite katika kuhakikisha wananchi wanakuwa na akili au elimu kama mtapenda kuiita hivyo.
 
Mnanishangaza sana.Taarifa tulizonazo ni kwamba Shebby alijenga hoteli kwa mkopo wa Crdb na pato lake la udalali wa zao la korosho.

Wewe Kiluvia usifanye watu hawana akili hoteli ni ya Membe ni zile pesa ni za Gadaffi hata bungeni aliulizwa akajikanyaga pesa hizo wamegawana na JK baada ya Gadaffi kufariki.
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!


Hadi mwezi wa Tano tutasikia mengi kweli..ila hii ingepingwa kwa ushahidi halisia kwa kuonyesha certificate of registration from Brela kuwa iko chini ya nani..otherewise maneno matupu na lisemwalo lipo...
 
habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa naf beach hotel iliyopo mkoani mtwara.kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.membe hajawahi kufanya biashara.kumhusisha membe na umiliki wa naf beach hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.hoteli ya naf beach ni mali ya shabaan maarufu kama shebby mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya membe na shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na membe katika umiliki wake.nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.nawasilisha!

umeulizwa??
 
Bwana Mapesa maswali yako ni mazuri sana. Niseme tu kwamba Membe hayuko responsible kuelezea maisha ya Shebby (Shaibu Mohamed Juma) na sidhani kama sisi hapa tupo responsible. Swali lililo mbele yetu ni je Membe anamiliki hotel Mtwara? Kuchunguza Shebby ni nani kihistoria hakujibu swali la msingi.

Ajabu tumedangamywa na kuaminishwa kwamba Shebby ni masikini huwezi kujenga hotel. Hata baada ya mmiliki kuongelea kupitia TV na radio historia yake na jinsi alivyopata utajiri wake. Lakini hao wanaotuaminisha hawana hesabu ya utajiri wa Sheby ambao unaweza kuwa wa urithi au umiliki wa maeneo mengi ya ufukweni ambayo kwa miaka ya karibuni yamenufaisha wakazi wa Mtwara.

Ifahamike Shebby ni dalali makubwa wa ununuzi wa korosho kutoka vyama vya ushirika kwenda kwa makampuni ya wahindi. Kinadhalia Udalali auhitaji mtaji na malipo yake ni makubwa nayapamoja. Kama Shebby anaweza kushinda mnada moja na akamchaji muhindi shilingi 10 kwa kila kilo aliyoshinda manake anapata billion moja kwenye tani laki moja. Hapo hajafanya organization ya transport kwa kilo kutoka mnadani hadi ghalani.

Shebby alikuwa mfanyabiashara wa simu kariakoo lakini mwanzoni mwa miaka ya 2000 alirudi kwao Mtwara mara baada ya kugundua kwamba udalali wa korosho unalipa. Akauza maduka yake ya simu aliyokuwa anamiliki kariakoo. Madalali wengine walioungana naye ni pamoja na bwana Salum Mkemi ambaye bado makazi yake ni Dar.

Shebby ni mfano wa kuigwa kwa vijana wanaodhani Dar ndio kila kitu. Shebby amekuwa akiiomba serikali iwawezeshe wanunuzi wa korosho wakizalendo kuuza korosho zao moja kwa moja inchi za nje. Tatizo, alijibiwa kwamba wahindi wamezuia kununua korosho kutoka kwenye nchi zinazolima pasipo kupitia makampuni yao ya India. Kila miezi kadhaa Shebby amekuwa akifanya mahojiano na TV akielezea jinsi alivyopata utajiri wake na ujumbe wake kwa vijana. Kwa kudhani Shebby huwezi kujenga hotel ni kudharau jitihada zake.

Tujifunze kupongeza na kutia nguvu vijana waliotoka jasho na wakafanikiwa. Tusiache wanasiasa watukatishe tamaa kwa kusema hatuwezi.

Good naration of story...but kuna kitu kinamiss kwenye majibu yako hasa ukiyasoma upya maswali yangu utaligundua hilo..thanks God umeeleza kuwa bwana SHEBBY ye ni DALALI, mtu ambaye anafanyabiashara bila mtaji, mtaji ni wateja wake.
 
Hili suala lilishafanyiwa uchunguzi na vyombo husika na ukweli umeshajulikana: Membe sio mmiliki wa NAF, FAN city, wala NAF blue Hotel.

NAF inasimama badala ya herufi za majina ya wototo wa mmiliki halali Shaibu Mohamed Juma. Watoto wanaounda NAF au FAN city ni Nadhir Abdul na Farid. Hotel hizo zilijengwa tangu enzi za utawala wa Mkapa kabla Membe hajawa Waziri. NAF beach ilichelewa kuanza kazi kwasababu ya kuchelewa kwa mkopo kutoka crdb uliombwa na mmiliki. Mkopo ulitoka mwakajuzi na hivyo hotel kuanza.

Ifahamike kwamba Chadema, takukuru, usalama wa Taifa, kamati ya maadili ya ccm na Cuf walishafanya uchunguzi juu ya hotel hii na wote wakaja na jibu moja: Membe hana biashara ya hoteli sehemu yeyote duniani. Wote wamejiridhisha kwamba upo uhusiano wa kawaida wa kirafiki kati ya bwana Shaibu Juma na familia ya Membe. Sawa na uhusiano uliopo kati ya mmiliki wa Serena hotel na Membe.

Uchunguzi wa mwisho na wakaribuni ni ule uliofanyika na mahasimu wa Membe ndani ya CCM. Huu nao haujamweka Membe kama mmiliki wa hotel lakini mahasimu hawa wameamua walazamishe kesi kwasababu hawana kesi. Wakati EPA Richmond Rada Tokomeza na Escrow vimekuwa vikiwasumbua mahasimu wa Membe, Membe amekuwa msafi Wakati wote.

Mahasimu hao pia wamekuwa wakitapatapa kwamba Membe kala ela za Ghadafi. Ni nchi gani duniani ambapo misaada au msamaha wa madeni unapitishiwa kwenye account ya waziri wa mambo ya nje? Kwa taarifa zilizo sahihi ni kwamba wanasheria waliotuingiza mkenge Escrow ndio wanaosambaza habari za uongo kwasababu Membe alikataa ombi lao la kuitambua kampuni ya MELt kuwa mmiliki halali wa fedha zilizopo TIB badala yake akatambua MEIS company kama ambavyo ilihainishwa na serikali ya Libya. Huwezi kumwingiza Membe mkenge hata siku moja na Tz tungepata viongozi wa aina ya Membe ambao wako makini na wametenganisha siasa na biashara tungekuwa mbali. Mbali sana.

MEIS wamefikia wapi na ujenzi wa kiwanda cha saruji Lindi?
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!

we ndio msemaji wa membe au shaabani?
 
Sasa si heri hata haya usingeyaandika

Kwa hiyo bado mnaamini Watz wa miaka ile bado wana uwezo ule ule wa kufikiri na kungamua? Hivi ninyi akija kiongozi yeyote mwenye mahela yake na kukuona una uwezo na uaminifu wa kusimamia mahela yake akawekeza kupitia kwako na akasisitiza usimtaje wewe utaikataa hiyo nyota ya jaha? Na bila shaka mtakuwa mmelishana viapo vikali na maandishi ya siri ambayo familia za kila pande zitakuwa nayo. Sasa wananchi hawawezi kuwaza nje ya sanduku kubaini ukweli? Uelewe mali zote zilizopatikana kifisadi zikawekezwa kwenye miradi na kusimamiwa na ndugu, wajomba na marafiki wananchi wanaelewa ni kwamba haujapatikana uongozi wa nchi wenye uwazi utashangaa yatakayoelezwa na wananchi. Na hata hivyo mtuhumiwa wa haya yupo ajijibie mwenyewe nyie amewatuma?
 
Alhaj camilius membe.jambazi anaejificha kwenye mgongo wa tezidume.
 
Habari watanzania wenzangu wapenda amani na maendeleo.Napenda kuchukua nafasi hii kutolea ufafanuzi suala la nani ni mmiliki wa Naf Beach Hotel iliyopo mkoani Mtwara.Kumekuwa na habari zikisambaa kwa muda mrefu sasa juu ya kuhusishwa kwa Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa katika umiliki wa hoteli hii ya nyota tano.

Ukweli ni kwamba Membe hajawahi kumiliki au kuwa sehemu ya umiliki wa hoteli hii.Membe hajawahi kufanya biashara.Kumhusisha Membe na umiliki wa Naf Beach Hotel ni kuchuma dhambi kwa muumba wa vyote duniani.Tusitumie siasa chafu kuchafua hata wasiohusika na mambo yanayozushwa mitaani.Hoteli ya Naf Beach ni mali ya Shabaan maarufu kama Shebby Mix aliyoijenga kwa mkopo kutoka Crdb.

Hakuna uhusiano wowote kati ya Membe na Shabaan iwe kiundugu,kiurafiki au kibiashara na ndio maana inakuwa sio afya kuleta mijadala inayosema uongo kuhusu hoteli hii isiyokuwa na jina lenye nasaba yoyote na Membe katika umiliki wake.Nasisitiza tujadili kweli na kuikataa uongo kwasababu itatuweka huru kifikra na kimaamuzi.Nawasilisha!


Ndugu yangu kama hujui kitu ni bora ukae kimya mimi nipo mtwara na ni mfanyakazi wa hii hotel bwana Membe Bernard ndo mmiliki halali wa hii hotel huyo unayemtaja kawekwa tu kama pambo
 
Back
Top Bottom