Peleka ujinga wako hapa nani unamfanya mtoto asiyejua uhusiano wa membe na huyo shebby wakati iko wazi biashara zote za membe shebby mix ndo msimazi au unataka tuweke na orodha ya biashara zake hapa, umechelewa kujisafisha bora ungepiga kimya.
Tunajua shebby mix ni mfanya biashara lakini hana uwezo wa kukopa mabilion ya kuwekeza katika biashara kubwa kama zile
Au ni lile duka la simu pale stand kuu ?
Au ni mazao na mbao?
Au nyara za serikali?
JIPANGE.
Hivi ni nani amekuambia hana uwezo? Uwoga wako wa kukopa ndo usifanye na wenzako wawe sawa na wewe. Hata Rombo Green view mmiliki alitolea ufafanuz ni mikopo. Anasema mwanzon ilianza ikiwa ndogo. Hata NAF ilianza Lodge ndogo ikiitwa NAF View, baadae sana ikajengwa NAF Beach na FAN City. Na hayo majina FAN au NAF ni kageuza majina matatu ya watoto wake huyo Shebby kama mdau alivyofafanua hapo juu!
Shebby kaanza gemu za kuhangaika na biashara pale Mtwara muda sana. Jamaa inaonekana anajua kufight!
Inawezekana Membe akawa na hisa labda kwa kuwa wako karibu au ni marafiki, hilo ni vigumu kuthibitisha, ila kusema Shebby hawez kukopa benki inashangaza, kwa nini asiweze? Ni mtu aliyeishi Mtwara muda na kuhangaika kibiashara, na wakat ule Mtwara viwanja na mapori ilikuwa ni bei ya kutupwa. Sasa kama alinunua kwa vision na baadae imekuwa value ni kubwa baada ya ugunduz wa gesi huoni ardhi imekuwa na thamani kubwa na hivyo ni rahisi kuwa na colateral ambazo ni rahisi kukopesheka benki? Eti Shebby hana uwezo wa kukopa, kwa nini? Kama wewe ni mwoga wenzako wanaweza?
Wakaz wa Mtwara nao ni wajanja sana siku hizi.
Watu kama Maarifa anamilik Safari Radio,Makonde Beach na Makonde Water. Bila kumsahau Mr Hamza kama sikosei anamiliki Pride FM, na hawa wote ni wazawa wa Mkoani Mtwara. Baada ya Wanamtwara kufunguka kifikra nao wako vizuri sawa na wakina Mfugale wa Iringa anaemiliki Ebony FM na Peacok Hotel au MAiro anaemiliki Hotel La Kairo Mwanza au mzawa wa Arusha/ Moshi anaemiliki Naura Springs. Exposure imewatoa matongotongo wanaMtwara, na bado Mahotel yanajengwa kwa wingi sana Mtwara kwa sasa. Wanamtwara na Watanzania wanawekeza sana tena sana. Naamini Mtwara soon itaipita hata miji mingine iliyotangulia. Sidhan kama Morogoro, Iringa, Dodoma na hata Mbya kuna hotel ya nyota4 sina hakika!