Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Andiko la Mdau wa kutoka Goba kuhusu watu wanaotaka kupora nyumba yao baada ya baba yao kupotea:
Usiku wa kuamkia leo Alhamisi Julai 6, 2023 kuna watu wamevamia katika nyumba yetu iliyopo Goba, Mtaa wa Kiburuni, Dar es Salaam na kuanza kuvunja sehemu ya nyumba, ikiwemo madirisha na milango, baada ya hapo wakamjeruhi ndugu yetu mmoja na kusema kuwa kama hatutahama kwenye nyumba hiyo watarejea kesho yake ambayo ni usiku wa kuamkia Ijumaa Julai 7, 2023.
Wahalifu hao walifika wakiwa makundi, wanne wakaingia ndani na wengine ambao sijui idadi yao walibaki nje, majirani wanasema kuwa walikuwa na silaha za moto ndio maana hata wao walisita kutoa msaada kwa haraka.
Walikuwa wanamtaka kiongozi wa familia ambaye alikuwa katika chumba kingine, wakati akifanya uharibifu huo wakamchukua ndugu yetu mmoja na kuanza kumpiga huku wakimtaka aseme alipo ndugu yetu ambaye ni mtoto wa kwanza wa mzee.
Alikataa kutii kile walichotaka na wakaendelea kumpiga hadi alipopata nafasi ya kuwatoroka na kwenda kuripoti Polisi.
Polisi walikuja baadaye wakakuta wahalifu wale ambao tunaamini wametumwa na aliyekuwa rafiki wa baba yetu kwa kuwa ndiye ambaye tuna mgogoro naye wa nyumba tunayoishi.
Kwa nini rafiki wa baba anahusishwa?
Anahusishwa kwa kuwa mshukiwa anayefahamka kwa jina la Thomas Daniel Kilumile, mzaliwa wa Iringa ambaye kwa sasa anaishi Mwanza, alikuwa ni kama ndugu kwetu wakati baba alipokuwa nasi.
Wawili hao walikuwa marafiki na hata kufikia hatua ya huyo rafiki yake kuwa anakuja kwenye nyumba yetu analala na kwa pamoja walikuwa wakimiliki kampuni.
Walikuwa wafanyabiashara walioshirikiana muda mrefu, ghafla Mwaka 2018 baba akiwa ametoka na gari kwenda kwenye mizunguko yake ya kawaida hakurudi tena mpaka leo.
Hatujui kama ni mzima au ameshakufa na hata gari lake pia halikuwahi kuonekana.
Rafiki wa baba aanza kudai nyumba
Baada ya baba kupotea, ndugu tukaanza kufuatilia madeni na biashara zake alizokuwa anafanya, hapo ndipo sokomoko likaanza, huyo Thimos akaja kudai kuwa nyumba tunayoishi ni mali yake na tunatakiwa kuhama.
Mgogoro ukaanzia hapo, tukamtaka aende Mahakamani ili haki ipatikane, hakufanya hivyo, aliishia kwenda Polisi na suala letu lilifika hadi Serikali za mtaa lakini hakukuwa na utatuzi uliopatikana.
Nyaraka za nyumba zinaonesha zina jina la baba yetu aliyepoteza lakini Kilumile alikuja na nyaraka anazodai ni za kiwanja na kuwa kile ni kiwanja chake.
Kinachoshangaza ni kuwa rafiki huyo wa baba hakuwahi kusema chochote kuhusu umiliki wake wa nyumba hiyo, na kwa kinachoendelea tunapata mashaka kupotea kwa baba na hiki kinachoendelea.
Vitisho
Mzee Kilumile alianza kutupa vitisho yeye na mwanaye ambaye ni Daniel Kilumile wakitutaka tuhame, shauri lilifika Kituo cha Polisi Goba, kwa kuwa alikosa ushahidi akawa ni kama ameshindwa kuendelea.
Nyumba hiyo ilianza kujengwa Mwaka 2011 na ikakamilika Mwaka 2014 ambapo ndipo familia ikahamia.
Mama yetu hayupo hapa anaishi Mwanza, aliwahi kusema rafiki wa baba anataka kutupora nyumba yetu kinyume cha sheria.
Kwa kuwa rafiki huyo wa baba mtoto wake ni mwanajeshi, amekuwa akidai kuwa lazima atatuhamisha na kwa mazingira yanayoonekana sasa inaonekana kuna vitu ambavyo anaweza kuhusika kwa kupotea kwa baba.
Tulitegemea pia baada ya baba kupotea angekuja kutuambia kuhusu biashara aliyokuwa akishirikiana na baba, tulipomuuliza hakuwa na majibu.
Usiku wa kuamkia leo Alhamisi Julai 6, 2023 kuna watu wamevamia katika nyumba yetu iliyopo Goba, Mtaa wa Kiburuni, Dar es Salaam na kuanza kuvunja sehemu ya nyumba, ikiwemo madirisha na milango, baada ya hapo wakamjeruhi ndugu yetu mmoja na kusema kuwa kama hatutahama kwenye nyumba hiyo watarejea kesho yake ambayo ni usiku wa kuamkia Ijumaa Julai 7, 2023.
Wahalifu hao walifika wakiwa makundi, wanne wakaingia ndani na wengine ambao sijui idadi yao walibaki nje, majirani wanasema kuwa walikuwa na silaha za moto ndio maana hata wao walisita kutoa msaada kwa haraka.
Walikuwa wanamtaka kiongozi wa familia ambaye alikuwa katika chumba kingine, wakati akifanya uharibifu huo wakamchukua ndugu yetu mmoja na kuanza kumpiga huku wakimtaka aseme alipo ndugu yetu ambaye ni mtoto wa kwanza wa mzee.
Alikataa kutii kile walichotaka na wakaendelea kumpiga hadi alipopata nafasi ya kuwatoroka na kwenda kuripoti Polisi.
Polisi walikuja baadaye wakakuta wahalifu wale ambao tunaamini wametumwa na aliyekuwa rafiki wa baba yetu kwa kuwa ndiye ambaye tuna mgogoro naye wa nyumba tunayoishi.
Kwa nini rafiki wa baba anahusishwa?
Anahusishwa kwa kuwa mshukiwa anayefahamka kwa jina la Thomas Daniel Kilumile, mzaliwa wa Iringa ambaye kwa sasa anaishi Mwanza, alikuwa ni kama ndugu kwetu wakati baba alipokuwa nasi.
Wawili hao walikuwa marafiki na hata kufikia hatua ya huyo rafiki yake kuwa anakuja kwenye nyumba yetu analala na kwa pamoja walikuwa wakimiliki kampuni.
Walikuwa wafanyabiashara walioshirikiana muda mrefu, ghafla Mwaka 2018 baba akiwa ametoka na gari kwenda kwenye mizunguko yake ya kawaida hakurudi tena mpaka leo.
Hatujui kama ni mzima au ameshakufa na hata gari lake pia halikuwahi kuonekana.
Rafiki wa baba aanza kudai nyumba
Baada ya baba kupotea, ndugu tukaanza kufuatilia madeni na biashara zake alizokuwa anafanya, hapo ndipo sokomoko likaanza, huyo Thimos akaja kudai kuwa nyumba tunayoishi ni mali yake na tunatakiwa kuhama.
Mgogoro ukaanzia hapo, tukamtaka aende Mahakamani ili haki ipatikane, hakufanya hivyo, aliishia kwenda Polisi na suala letu lilifika hadi Serikali za mtaa lakini hakukuwa na utatuzi uliopatikana.
Nyaraka za nyumba zinaonesha zina jina la baba yetu aliyepoteza lakini Kilumile alikuja na nyaraka anazodai ni za kiwanja na kuwa kile ni kiwanja chake.
Kinachoshangaza ni kuwa rafiki huyo wa baba hakuwahi kusema chochote kuhusu umiliki wake wa nyumba hiyo, na kwa kinachoendelea tunapata mashaka kupotea kwa baba na hiki kinachoendelea.
Vitisho
Mzee Kilumile alianza kutupa vitisho yeye na mwanaye ambaye ni Daniel Kilumile wakitutaka tuhame, shauri lilifika Kituo cha Polisi Goba, kwa kuwa alikosa ushahidi akawa ni kama ameshindwa kuendelea.
Nyumba hiyo ilianza kujengwa Mwaka 2011 na ikakamilika Mwaka 2014 ambapo ndipo familia ikahamia.
Mama yetu hayupo hapa anaishi Mwanza, aliwahi kusema rafiki wa baba anataka kutupora nyumba yetu kinyume cha sheria.
Kwa kuwa rafiki huyo wa baba mtoto wake ni mwanajeshi, amekuwa akidai kuwa lazima atatuhamisha na kwa mazingira yanayoonekana sasa inaonekana kuna vitu ambavyo anaweza kuhusika kwa kupotea kwa baba.
Tulitegemea pia baada ya baba kupotea angekuja kutuambia kuhusu biashara aliyokuwa akishirikiana na baba, tulipomuuliza hakuwa na majibu.