passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Wakuu habari za uzima?
Leo nilienda msibani kwa rafiki, mdogo wangu na jirani yangu wa muda kidogo.
Rafiki yangu huyu amefariki taarifa zikiwa zimeletwa Leo alfajiri saa kumi.
Kifo cha mdogo wangu huyu kimeniumiza sana, amezaliwa mwaka 2003 na alikuwa amemaliza UDSM mwaka jana na baada ya hapo baba yake ni kitengo kwenye usalama akamchukua mwaka huu tarehe 2/1/2024 ili akaanze kozi.
Kiukweli naumia sana, alikuwa bado kijana mdogo hajamaliza hata mwezi na alikuwa na ndoto nyingi, baba yake mzazi alileta taarifa kwa dada yake ambaye mdogo wangu huyu na rafiki amelelewa hapo kwamba amefariki.
Mama yake mkubwa alijaribu kuhoji lakini hakuambilia majibu zaidi ya kwamba walikuwa msituni kwenye mazoezi.
Binafsi sikuwahi kushuhudia kuagwa kwa namna hii kama niliyoiona leo, magari ya jeshi yalikuwa mengi sana, Hakuna mtu hata mmoja aliyeonekana na simu hapa kuchukua tukio hili. Sijui ni mambo ya jeshi au laah.
Baba yake alikuwa ametulia muda mwingi huku akizungukwa na wanajeshi. Daah amelala mdogo wangu huyu na jirani pia.
Baada ya kuagwa kwa mwili, mazishi yanafanyika Bukoba kwao.
16/1/2024
Pumzike kwa Amani.
Leo nilienda msibani kwa rafiki, mdogo wangu na jirani yangu wa muda kidogo.
Rafiki yangu huyu amefariki taarifa zikiwa zimeletwa Leo alfajiri saa kumi.
Kifo cha mdogo wangu huyu kimeniumiza sana, amezaliwa mwaka 2003 na alikuwa amemaliza UDSM mwaka jana na baada ya hapo baba yake ni kitengo kwenye usalama akamchukua mwaka huu tarehe 2/1/2024 ili akaanze kozi.
Kiukweli naumia sana, alikuwa bado kijana mdogo hajamaliza hata mwezi na alikuwa na ndoto nyingi, baba yake mzazi alileta taarifa kwa dada yake ambaye mdogo wangu huyu na rafiki amelelewa hapo kwamba amefariki.
Mama yake mkubwa alijaribu kuhoji lakini hakuambilia majibu zaidi ya kwamba walikuwa msituni kwenye mazoezi.
Binafsi sikuwahi kushuhudia kuagwa kwa namna hii kama niliyoiona leo, magari ya jeshi yalikuwa mengi sana, Hakuna mtu hata mmoja aliyeonekana na simu hapa kuchukua tukio hili. Sijui ni mambo ya jeshi au laah.
Baba yake alikuwa ametulia muda mwingi huku akizungukwa na wanajeshi. Daah amelala mdogo wangu huyu na jirani pia.
Baada ya kuagwa kwa mwili, mazishi yanafanyika Bukoba kwao.
16/1/2024
Pumzike kwa Amani.