Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

sio zaman hata sasa leaving unapata kama kawaida maana huwa inatoka kabla hata yakufnya mtihan
Kwa hiyo Ndalichako ana majibu lakini kaamua kukuaa kimya? sasa hao anawatishiaga kuwa watakiona cha moto huyu RC hayumo kwenye kundi hilo?
 
KWA HILI KADANGANYA AU KADANYANYIKA..NECTA HUWA HAITOI DIVISION ZERO CERTIFICATE..TUNAMUOMBA MH GWAJIMA AKIONYESHE HICHO CHETI.
Hii Vita ya madawa ya kulevya nimeamini sio ndogo kama hadi viongozi wa dini wanamfokea makonda kwa njia zote za uongo au ukweli za haramu au tukufu .Makonda kakanyaga waya wa umeme wa msongo mkubwa wa umeme kugusa madawa ya kulevya. pole makonda drug lords kama ilivyo America kusini they are sticking back Na hawatapumzika hadi uondoke.Cha msingi umetuamsha kujua who is who katika hii biashara ya madawa ya kulevya kujua nani ni muuuzaji au mnunuzi au mtumiaji au protocol officer au mchunga au sheikh au afisa au ni bodyguard au ni mwanaharakati au ni mwanasheria au ni mtetezi wa wahusika wa dawa za kulevya.Makonda umeturahizishia kazi come what may to you .you have done your part
 
sijawahi kuona cv kama hii, hakuna kilichoniinspire kama ufaita wake

wallah amefaiti kinoma maana naamini wenzake waliofeli naye aidha ni wachunga ng'ombe, wamachinga, wachimbaji madini wadogowadogo, n.k. kwa ujumla wahangaikaji au walala hoi

yeye ni salute kwenda mbele, na naamini hata akitolewa ukuu wa mkoa lazima atatoboa tundu jingine tu, hafi kizembe huyu mtu, amini usiamini.

ni nadra kupata watu wa hivi, ukimletea gozigozi anakupoteza, si mtu wa mchezomchezo
 
Nyie mpo kwenye payroll ya Daudi, mwambieni aende Clouds na vyeti vyake akamalize hizi kelele. Simple.
 
Na hapo ndipo watz tulipofungwa akili zetu,tunafuata mkumbo tu,div 0 na cheti wapi na wapi?
Alipata leaving hata kwenye graduation alikuwepo na mashada alivaa. Cheti ambacho hakupata ni cha masomo (Academic certificate)
 
Maisha ya watetezi wa wahusika wa madawa ya kulevya ni ya kusikitisha sana. Hivi huyo Gwajima yeye kielimu yukoje, kaishia kiwango gani ama sivyo naogopa tusije kupoteza mda wetu mzuri kuwajadiri watu wasiojitosheleza
Anhaa PhD
 
Kosa lingine Makonda anashindwa kuelewa anadhani anapambana na Gwajima as individual. Gwajima ni institution, ana waumini wengi sana. Lakini kuna watu wengi sana wako kinyume na Makonda wako serikalini, wengine ni watumishi, wengine ni wanasiasa, tena ambao wanajua details zote za mhusika. kwa hiyo wanachofanya kwa kuwa hawana uwezo wa kusema wao wenyewe, wanapeleka kwa Gwajima anapasua pwaaaaaaaaaaaaaaaah.
Hahaha, watu walikosa pa kukimbilia maana mwana mfalme alisema mkoa wake now wamepata.

Niliumia sana alipomdhalilisha yule mama k/ndoni, sijui alikuaje kwa watoto majirani wananchi na wafanyakazi wenzake.

Sent from my TECNO-Y3 using JamiiForums mobile app
 
Hakika mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,siku ya jana wengi tumesikia audio ya mchungaji wa kanisa la ufufuo na uzima ndugu Josephat Gwajima ikiwa imelenga kujibu mashambulizi dhidi ya mkuu wa mkoa mh Paul makonda,katika sakata linalotuhumu u halali wa elimu aliyonayo mkuu huyu wa mkoa.
Moja ya vitu vilivyotamkwa na kiongozi huyu wa dini ni kuwa anamiliki vyeti vyote vya mh Paul makonda kile alichoPata division zero na hicho chakugushi.
Mchungaji Gwajima kwa kauli hii ya kumiliki cheti cha mtu mwenye division zero inaalalisha uongo maradufu kwani,kuanzia nnchi hii imepata uhuru NECTA haijawahi kutengeneza cheti cha mtu aliyepata sifuri,Ni aibu kwa mtumishi wa Mungu tena mwenye wafuasi wengi kiasi chako kutumia madhabahu kuongea uongo.mh gwajima huenda akawa napoint dhidi ya elimu ya makonda ila ameitamka kwa kukurupuka,mh Gwajima zungumza kwa kutulia,bado tutatega sikio kukusikiliza na wala hatutakupuza..
Kwani statement of results/result slip kwa kiswahili inaitwaje vile?!!Au cheti ni lazima kiwe certificate lakini hata hiyo result slip ni certificate na hata cheti cha hospitali pia maana kinakuwa certified na Dr nadhani, vinginevyo pharmacy wasingetuuzia dawa.Bado Gwajima yuko sahihi.
 
Ahya sasa inaonekana wengi wa wachingiaji hapa wa/tumemaliza kwanzia miaka ya 2005.
Baadhi ya watoa maoni wanasema kabla ya 2005 vyeti vya wahitimu waliopata zero vilikua vikitolewa.
 
Kumbe jamaa anatokwa povu kuwa tumejazana tu mjini bila shughuli eti turudi kijijini tukalime dengu na soya kuliko kuuza leso,, alaaa kumbe na yeye alikimbia uvuvi wa changu na kambale emb toka mjini kavue bwana!! Haiwezekani mtu unakaa tu mjini wakati umeukimbia uvuvi huko mwanza!!
 
Patatokea danadana tu za maneno na vitendo. Patasemwa tu kubadilishwa majina ya wakuu hao. Lakini,ukweli wa vyeti vyao vya kidato cha nne utawatafuna milele.

Wote ni wasemaji wazuri. Wote ni watu wa kujitamba,kujivuna na kuonesha mambo yao mazuri na mabaya ya wa upande wa pili. Wote ni wapenda media na attention. Lakini,kwenye vyeti na majina,wanafunga breki. Hawafurukuti hata kwa ukuti

Wana kila nafasi,wasiwasi na sababu za kuonesha vyeti vyao vya kidato cha nne vyenye ukakasi usemwao. Lakini,hakika nawaambia,vyeti vyao ni siri yao. Wapo na wataendelea kuwepo kama upepo!

Mwafaaaa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
PAUL MAKONDA: Majina yake halisi ni Daudi Albert Bashite. Alianza darasa la kwanza mwaka 1988 katika shule ya msingi Koromije akitumia majina ya Daudi Albert Bashite. Mwaka 1991 alifeli darasa la 4, akarudia. Mwaka 1992 alifeli tena na hivyo akahamishiwa Mwanza mjini, ili aweze kusoma na kupata masomo ya jioni (tuition).

Mtu aliyefail darasa la nne miaka ile alikuwa anaitwa ''tutusa mzungu wa reli''. Unafail standard 4 mara mbili?? Kweli!??
 
Back
Top Bottom