Mchumba wa Dk. Slaa aibua tuhuma nzito

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
  • Adai kuna mpango wa kumuua mumewe kwa sumu, uchawi

MWANDISHI WETU | Kulikoni | Sep 21, 2012

attachment.php


MCHUMBA wa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Mandeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, Josephine Mushumbusi, ametoa madai mazito kwa vyombo vya dola akidai kuwapo kwa mpango wa kumdhuru mumewe.

Josephine amekataa kuingia undani wa madai hayo, pamoja na kukiri kuyaweka katika mtandao kupitia ukurasa wake wa Facebook, kwa maelezo kuwa yuko nje ya nchi kwa sasa.

Madai hayo yanataja baadhi ya watu wazito ndani ya serikali, ambao wanadaiwa kuwa katika mpango huo, lakini baadhi ya wanaotajwa kutokuwapo kiunganishi na tuhuma husika.

Katika madai yake, mama huyo machachari, ameandika kwamba kumekuwa na vikao vya watu ndani ya serikali vyenye lengo la kutaka kummaliza Dk. Slaa, kwa njia yoyote ile.

“Wanaamini kwamba Slaa ndiye mzizi katika Chadema na anaweza kuiangusha CCM 2015. wameona mazingira ya kuchakachua 2015 ni magumu sana,” anaeleza.

Anaendelea kwa kudai kwamba njia pekee ambayo imebakia ni kuwaondoa wagombea ambao ni tishio na wenye ushawishi wa kuhamishia wanasiasa wengine walio CCM kwenda Chadema.

Katika madai yake hayo, Josephine amewataja watu ambao wamekuwa wakitajwa mara kwa mara wakihusishwa na matukio ya utesaji kukiwa na jina moja jipya. Majina tunayahifadhi kwa sasa.

Kama hadithi ama sinema, madai hayo yanawataja watu mbalimbali walioathiriwa na matukio yanayoituhumu serikali kuhusika.

Katika hali ya kutatanisha, Josephine anahusisha madai ya kuwapo hata ushirikina ambao utatumika kumdhuru Dk. Slaa.

“Kwenye kikao chao cha kidhalimu, mmoja wao akapendekeza matumizi ya ama uchawi au sumu inayoua taratibu. Huyu aliyependekeza anahofia kuwa njia yoyote itakayofanana na nyingine italeta kelele na dunia nzima itagundua. Anajaribu kuwashawishi wenziwe waachane na hiyo, isipokuwa watumie njia hizi mbili mbadala; sumu au uchawi,” anaeleza Josephine na kuendelea;

“Jamaa wanamiliki wachawi wengi sana na wachawi hawa wako makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile linalotumika kulinda viongozi na huwa linafanya kazi kila wiki mara moja. Kundi hilo liko kwenye payroll ya serikali.

Anaendelea: “Kundi la pili ni lile la wachawi waliotaka kumuua .... (anataja jina la kiongozi) kipindi fulani. Kundi hili liko katika mazungumzo na ... (anataja kiongozi) kwa ajili hiyo.”

Imeelezwa na mama huyo kwamba mkakati huo unapangwa kutekelezwa baada ya Dk. Slaa kurejea kutoka nje ya nchi.

Katika madai yake hayo, Josephine anataja hadi namba za gari ambalo linaelezwa kutumika katika mkakati huo unaofanana na sinema ya Kinigeria.

Mbali ya Dk. Slaa, mama huyo anadai kwamba kuna mpango wa kuwadhuru wabunge ambao wanaamini hawahongeki kifedha.

Hata hivyo, viongozi mbalimbali wa serikali na watu mbalimbali, wameelezea tuhuma hizo kama njia ya kumchota akili Dk. Slaa ili kumuondoa katika hoja za msingi na hata kumtisha asirejee nchini na hazina ukweli wowote.

“Hizi tuhuma zinachanganya sana maana inaonekana baadhi ya wanaotajwa ni wale wale wanaotajwa katika tuhuma nyingine na hii inaonesha kwamba ni madai ya kupikwa na watu wenye nia ya kutaka kummchezea akili Dk. Slaa na pengine kumfanya asiaminike katika jamii,” anaeleza kiongozi mmoja mstaafu serikalini.

Habari zimethibitisha kwamba vyombo vya dola vimeanza kufuatilia kwa karibu taarifa hizo na huenda ikatolewa taarifa rasmi hivi karibuni, pamoja na kutokuwapo kiongozi aliyekuwa tayari kuzungumzia tuhuma hizo.
 

Attachments

  • mama-slaa.jpg
    mama-slaa.jpg
    53.6 KB · Views: 4,772
Kama wapo na tunawaona waliotishwa kwa namna hiyohiyo inayoelezwa na huyo anaeitwa mchumba wa Dr. Slaa. Wakatishwa na kudhuriwa. Serikali kupitia vyombo vyake uchunguzi ikasema madai hayo ni uzushi tu! Walotishwa na kujitetea wakadhurika kweli, kwa nini mwenye akili asione ukweli wa madai ya huyu mama?
 
Mchumba .......... Anasema mume wake........???!!!!!! yupo nje ya nchi aki4marisha chama. huyu mama na mchumba wake wana kiwanda cha kutung uongo
 
This is very serious, na sijui kwanini kwa nje serikali haiamini uchawi, ndani ni watumiaji wazuri sana wa uchawi. Waweke wazi ili watu wapunguze kuuana, anayetuhumiwa kwa uchawi ashtakiwe badala ya wananchi kumkata mapanga!
 
Mimi naona Slaa akae uhamishoni, akiendesha chama remotely, with advanced technology it is possible (hotuba za conference calls etc) aje tu wakati wa uchaguzi. This people kwa kweli wameamua!
 
..magazeti mengine bwana.

..kwenye heading wanasema Josephine ni mchumba.

..kwenye sub heading wanam-refer Slaa kama mume.

..binafsi nikishaona makosa kama hayo huwa sijisumbui kusoma habari nzima.
 
Kweli CCM wameshikwa pabaya sana wanafikiria kuua tu kwa sasa...sera zimegoma!!wakiua ndio watazidisha hasira kwa vijana wooote wapenzi wa Dr Slaa na CDM kwa ujumla!ndio mtaharibu kabisaaa....mtakosa ubunge hadi hamtaamini hata kama urais mkichakachua,haitasaidia maana wabunge wengi sanaa watakuwa vijana wa CDM,huko bungeni hakutakalika!!
 
Ni mke wake au mchumba wake?
HALAFU, HIVI BADO WATU WANAAMINI USHIRIKINA? .... THATS STUPID!!
Walishafunga ndoa lakini nashangaa gazeti bado linamwita 'mchumba wake'.
Mkuu wewe huamini kama kuna ushirikina? Sisemi kama unaamini katika ushirikina bali nauliza unaamini ushirikina upo?
 
  • Adai kuna mpango wa kumuua mumewe kwa sumu,
    uchawi

MWANDISHI WETU | Kulikoni | Sep 21, 2012

attachment.php


[FONT=courier
new]MCHUMBA wa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Mandeleo
(Chadema), Dk. Willibrod Slaa, Josephine Mushumbusi, ametoa madai mazito
kwa vyombo vya dola akidai kuwapo kwa mpango wa kumdhuru mumewe.

Josephine amekataa kuingia undani wa madai hayo, pamoja na kukiri
kuyaweka katika mtandao kupitia ukurasa wake wa Facebook, kwa maelezo
kuwa yuko nje ya nchi kwa sasa.

Madai hayo yanataja baadhi ya watu wazito ndani ya serikali, ambao
wanadaiwa kuwa katika mpango huo, lakini baadhi ya wanaotajwa kutokuwapo
kiunganishi na tuhuma husika.

Katika madai yake, mama huyo machachari, ameandika kwamba kumekuwa na
vikao vya watu ndani ya serikali vyenye lengo la kutaka kummaliza Dk.
Slaa, kwa njia yoyote ile.

“Wanaamini kwamba Slaa ndiye mzizi katika Chadema na anaweza kuiangusha
CCM 2015. wameona mazingira ya kuchakachua 2015 ni magumu sana,”
anaeleza.

Anaendelea kwa kudai kwamba njia pekee ambayo imebakia ni kuwaondoa
wagombea ambao ni tishio na wenye ushawishi wa kuhamishia wanasiasa
wengine walio CCM kwenda Chadema.

Katika madai yake hayo, Josephine amewataja watu ambao wamekuwa
wakitajwa mara kwa mara wakihusishwa na matukio ya utesaji kukiwa na
jina moja jipya. Majina tunayahifadhi kwa sasa.

Kama hadithi ama sinema, madai hayo yanawataja watu mbalimbali
walioathiriwa na matukio yanayoituhumu serikali kuhusika.

Katika hali ya kutatanisha, Josephine anahusisha madai ya kuwapo hata
ushirikina ambao utatumika kumdhuru Dk. Slaa.

“Kwenye kikao chao cha kidhalimu, mmoja wao akapendekeza matumizi ya ama
uchawi au sumu inayoua taratibu. Huyu aliyependekeza anahofia kuwa njia
yoyote itakayofanana na nyingine italeta kelele na dunia nzima
itagundua. Anajaribu kuwashawishi wenziwe waachane na hiyo, isipokuwa
watumie njia hizi mbili mbadala; sumu au uchawi,” anaeleza Josephine na
kuendelea;

“Jamaa wanamiliki wachawi wengi sana na wachawi hawa wako makundi
mawili. Kundi la kwanza ni lile linalotumika kulinda viongozi na huwa
linafanya kazi kila wiki mara moja. Kundi hilo liko kwenye payroll ya
serikali.

Anaendelea: “Kundi la pili ni lile la wachawi waliotaka kumuua ....
(anataja jina la kiongozi) kipindi fulani. Kundi hili liko katika
mazungumzo na ... (anataja kiongozi) kwa ajili hiyo.”

Imeelezwa na mama huyo kwamba mkakati huo unapangwa kutekelezwa baada ya
Dk. Slaa kurejea kutoka nje ya nchi.

Katika madai yake hayo, Josephine anataja hadi namba za gari ambalo
linaelezwa kutumika katika mkakati huo unaofanana na sinema ya
Kinigeria.

Mbali ya Dk. Slaa, mama huyo anadai kwamba kuna mpango wa kuwadhuru
wabunge ambao wanaamini hawahongeki kifedha.

Hata hivyo, viongozi mbalimbali wa serikali na watu mbalimbali,
wameelezea tuhuma hizo kama njia ya kumchota akili Dk. Slaa ili
kumuondoa katika hoja za msingi na hata kumtisha asirejee nchini na
hazina ukweli wowote.

“Hizi tuhuma zinachanganya sana maana inaonekana baadhi ya wanaotajwa ni
wale wale wanaotajwa katika tuhuma nyingine na hii inaonesha kwamba ni
madai ya kupikwa na watu wenye nia ya kutaka kummchezea akili Dk. Slaa
na pengine kumfanya asiaminike katika jamii,” anaeleza kiongozi mmoja
mstaafu serikalini.

Habari zimethibitisha kwamba vyombo vya dola vimeanza kufuatilia kwa
karibu taarifa hizo na huenda ikatolewa taarifa rasmi hivi karibuni,
pamoja na kutokuwapo kiongozi aliyekuwa tayari kuzungumzia tuhuma
hizo.
[/FONT]

Hivi nani atamuua huyu babu wakati kaishajichokea? nonsense!
 
hizi habari zililetwa humu mara nne na zikaondolewa,sasa imekuja upya ikiwa ndani ya gazeti sijui hawa mods kama wataitoa au watafanya nini,tunatazama kwa karibu
 
Mod Naomba upige BAN gazeti la KULIKONI maana watu humu walikula BAN
si kawaida

PLEASE MOD DO THE NEEDFUL BAN KULIKONI NIMEREPORT
report-40b.png
 
hizi habari zililetwa humu mara nne na zikaondolewa,sasa imekuja upya ikiwa ndani ya gazeti sijui hawa mods kama wataitoa au watafanya nini,tunatazama kwa karibu

Inakera sana hii tabia ya ku copy na ku paste ...let's try to be creative walau kidogo basi
 
Mazinguzi tu haya, mpaka leo wachumba wakati weshazalishana....?
Basi watazeekea uchumbani.....!!
 
Back
Top Bottom