Dk. Slaa, Mwambukusi na Mdude kufikishwa mahakamani Mbeya

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Philipo Mwakilima ambaye ni Wakili wa Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyangali amesema kuwa taarifa alizopewa na maafisa wa Jeshi la Polisi ni kuwa wateja wao ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya uhaini pamoja Dk. Slaa wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani Mkoani Mbeya hii leo Agosti 16, 2023.

Ameyasema hayo akizungumza na Watetezi tv ilipofanya nae mahojiano kujua nini kinaendelea dhidi ya watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi kwa zaidi ya saa 48.

Ikumbukwe watuhumiwa hao Mdude na Mwambukusi walikamatwa kwa pamoja mkoani Morogoro huku Dk. Slaa akikamatwa kwa wakati tofauti lakini wote wakidaiwa kukabiliwa na tuhuma za uhaini.

Hata hivyo baadhi ya wadau ambao ni Watetezi wa Haki za Binadamu ikiwemo Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) pamoja na Jukwaa la Katiba Tanzania wamepaza sauti wakitaka watuhumiwa hao kuachiwa bila mashariti au kufikishwa mahakamani.

Jana ilibuka taarifa kutoka kwa Wakili wa Dk. Slaa kuwa hafahamu mteja wake alipo ikiwa ni baada ya kushindwa kumuona kwenye kwenye kituo cha Polisi Osterbay jijini Dar es salaam.

Lakini itakumbukwa kukamatwa kwao kulikuja ikiwa ni muda mchache baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camilius Wambura kutoa tamko mbele ya Wanahabari akudai kuna watu wana njama ya kutaka kuiangusha Serikali akisisitiza kuwa hatua zitachukuliwa dhidi yao huku akiwataka wananchi kuwapuuza watu hao aliodai kuwa wanaandaa maandamano yasiyo na ukomo.

Source: Watetezi TV
 
Mob psychology iliwadanganya hapo wako wenyewe tu. Huwezi kutamka hadharani kwamba at extreme utapindua serikali ilio chaguliwa na wananchi, hiyo kauli ni nzito na ni uhaini. Hata raisi akiwa mpole kiasi gani lazima achukue hatua.
 
Mob psychology iliwadanganya hapo wako wenyewe tu......huwezi kutamka hadharani kwamba at extreme utagundua serikali ilio chaguliwa na wananchi, hiyo kauli ni nzito na ni uhaini.
aise hiyo kitu mbaya sana unajitosa kufanya ujinga bila kuangalia athari zake baadae sasa wanapata shida wenyewe mbowe na lissu wako wanakula bia na kuwachora tu
 
Philipo Mwakilima ambaye ni Wakili wa Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyangali amesema kuwa taarifa alizopewa na maafisa wa Jeshi la Polisi ni kuwa wateja wao ambao wanatuhumiwa kwa makosa ya uhaini pamoja Dk. Slaa wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani Mkoani Mbeya hii leo Agosti 16, 2023.

Ameyasema hayo akizungumza na Watetezi tv ilipofanya nae mahojiano kujua nini kinaendelea dhidi ya watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi kwa zaidi ya saa 48.

Ikumbukwe watuhumiwa hao Mdude na Mwambukusi walikamatwa kwa pamoja mkoani Morogoro huku Dk. Slaa akikamatwa kwa wakati tofauti lakini wote wakidaiwa kukabiliwa na tuhuma za uhaini.

Hata hivyo baadhi ya wadau ambao ni Watetezi wa Haki za Binadamu ikiwemo Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) pamoja na Jukwaa la Katiba Tanzania wamepaza sauti wakitaka watuhumiwa hao kuachiwa bila mashariti au kufikishwa mahakamani.

Jana ilibuka taarifa kutoka kwa Wakili wa Dk. Slaa kuwa hafahamu mteja wake alipo ikiwa ni baada ya kushindwa kumuona kwenye kwenye kituo cha Polisi Osterbay jijini Dar es salaam.

Lakini itakumbukwa kukamatwa kwao kulikuja ikiwa ni muda mchache baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camilius Wambura kutoa tamko mbele ya Wanahabari akudai kuna watu wana njama ya kutaka kuiangusha Serikali akisisitiza kuwa hatua zitachukuliwa dhidi yao huku akiwataka wananchi kuwapuuza watu hao aliodai kuwa wanaandaa maandamano yasiyo na ukomo.

Source: Watetezi TV
Wanapo sema kuchoma moto vituo via polisi na ofisi za ccm uoni kuwa nihaki yao kufichwa moja kwa moja
 
aise hiyo kitu mbaya sana unajitosa kufanya ujinga bila kuangalia athari zake baadae sasa wanapata shida wenyewe mbowe na lissu wako wanakula bia na kuwachora tu
Mbowe aliteseka peke yake miezi 9 jela bila msada huyu alikua ubalozini anaenjoyi maisha kwahiyo ni zamu yake, mdude yeye ni kama nzi hufuata uvundo tu.
 
Back
Top Bottom