Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Chama cha Kulinda na Kutetea Haki za Walimu Tanzania (CHAKUHAWATA) kimejibu tuhuma kuwa kuna baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho wanafuja fedha za michango ya Wanachama kwa kugawana zaidi ya Tsh. Milioni 400.
Kufahamu zaidi kilichosemwa kuhusu tuhuma hizo, soma hapa - CHAKUHAWATA wawageuza Walimu upatu, wagawana milioni tsh milioni 400
Makamu Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea na Kulinda Haki za Walimu Tanzania (Chakuhawata), Ashery Kisogoro Ntayomba amezungumza na JamiiForums na kusema hakuna ukweli kuhusu tuhuma hizo na kuwa zinafanywa na watu wasiowatakia mema.
Amesema “Ninachoweza kujibu kwa ufupi ni kuwa habari hiyo ya viongozi wa Kitaifa wamegawana zaidi ya Milioni 400 na madai kuwa wanagawana mgawanyo wa fedha za michango Tsh. 3000 kwa Tsh. 2000, hicho kitu hakipo.
“Ukitaka nitoe au upate taarifa zaidi au maelezo ya tuhuma hizo basi aliyeleta mada naye alete ushahidi.”
Ameongeza “Mapato na matumizi ya taasisi zote Duniani zinapaswa kuwa wazi, taarifa zipo na tunazipeleka kwa msajili ili tuweze kutambulika.”
Alipoulizwa madai kuwa kuna Wanachama wao ambao wamekuwa wakikatwa mara mbili kuchangia michango kwao na kwenye chama walichokuwa awali, amesema “Madai ya kukatwa mara mbili labda ungesema hilo linafanyika kwa Wanachama wetu wa wapi, lakini changamoto hiyo ilikuwepo kwa Wanachama kadhaa lakini kwa sasa haipo.”
Kufahamu zaidi kilichosemwa kuhusu tuhuma hizo, soma hapa - CHAKUHAWATA wawageuza Walimu upatu, wagawana milioni tsh milioni 400
Makamu Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Kutetea na Kulinda Haki za Walimu Tanzania (Chakuhawata), Ashery Kisogoro Ntayomba amezungumza na JamiiForums na kusema hakuna ukweli kuhusu tuhuma hizo na kuwa zinafanywa na watu wasiowatakia mema.
Amesema “Ninachoweza kujibu kwa ufupi ni kuwa habari hiyo ya viongozi wa Kitaifa wamegawana zaidi ya Milioni 400 na madai kuwa wanagawana mgawanyo wa fedha za michango Tsh. 3000 kwa Tsh. 2000, hicho kitu hakipo.
“Ukitaka nitoe au upate taarifa zaidi au maelezo ya tuhuma hizo basi aliyeleta mada naye alete ushahidi.”
Ameongeza “Mapato na matumizi ya taasisi zote Duniani zinapaswa kuwa wazi, taarifa zipo na tunazipeleka kwa msajili ili tuweze kutambulika.”
Alipoulizwa madai kuwa kuna Wanachama wao ambao wamekuwa wakikatwa mara mbili kuchangia michango kwao na kwenye chama walichokuwa awali, amesema “Madai ya kukatwa mara mbili labda ungesema hilo linafanyika kwa Wanachama wetu wa wapi, lakini changamoto hiyo ilikuwepo kwa Wanachama kadhaa lakini kwa sasa haipo.”