Mchele wa plastic; Clouds Fm yaiumbua TFDA

Mchele wa plastic; Clouds Fm yaiumbua TFDA

My Take;
TFDA badala ya kukaa ofisini mnapulizwa kiyoyozi kwa nini msikimbie hapo mikocheni kwenye studio za clouds fm mkachukue sample yao mkaipime pia.



Kwa jinsi walivyo, basi wataanza kuhangaika na Clouds badala ya aliyeingiza mchele
 
Vipimo vya mchele na vitu vya muhimu hawafuatilii ila lisu anapelekwa fasta mpimeni na ngwajima madawa hivyo ndo vya muhimu na bandarini wapo mchele umepita wapi au mnaangalia vibali vya mzigo mzigo hauangaliwi nashauri wanahabari wafuatilie mpaka wamjue aliekagua huo mzigo ukaingia nchini msifumbe macho wauwaji hawa majipu sugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo kipimo kimekuwa too cheap yaani kuudundisha chini ukadunda kama kitenesi ndo kusema ni plastic, kwanini wasijaribu kuuchoma moto km utayeyuka na kuwa ujiuji hapo sawa. Hiyo ya kudundisha chini ni local sana

Kuuchoma moto sio local? Wewe ulifikiria hilo la kuangalia kama unaweza kudunda kabla ya kusikia? Huoni hicho kipimo cha kudunda kinaonesha hata material yaliyotumika yaweza kuwa rubber/ mpira ila watu wanaita tu plastiki na ikawa ni ugunduzi zaidi wa design ya mchele huo? Kwa mchele wa kawaida, tonge la wali likibwagwa chini lazima lisambae na wala sio kudunda. Kwani plastiki zote ziko sawa na zinayeyuka zikichomwa au kuwekwa kwenye joto kali? Kwa taarifa yako kuna teknolojia ya masufuria ambayo yana layer ya plastiki kwa ndani (ya aina yake sio kama plastic bag) na yanapika kwa kutumia joto kali sana na ile plastiki haiyeyuki. Kwenye engines za magari kuna rubber kibao na joto ni kali sana wakati zinafanya kazi lakini haziyeyuki.
 
Mbona wameshatoa elimu ukitaka kuujua huo mchele kama wa plastic au sio.unachukua mchele weka kwenye maji ukiona unaelea bc kuna walakini na ukiona unazama jua uko sawa.2 wanasema chukua jiko kama la mkaa halafu tia huo mchele ikiwa plastic utaona unavyoyeyuka na ukiwa sio utaona pia.3 chukua mchele weka ktk sufuria bila maji halafu angalia ukipata moto unakuaje.wengi wetu tunaamini ukidunda ndo plastic kumbe sivyo.mchele asili ya ni uwanga kwa hio automatic utakuwa unakamatana kwa hio sio hoja kusema ukodunda ndio plastic.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Napendekeza kipimo kingine, wajaribu kuangalia je mtu akila huo wali wa aina hiyo ya mchele akienda haja kubwa, inakuwaje? kama ya mbuzi au ya kuku? je na yenyewe itadunda au la kutokana na digestion?

Pia mchele huo na ule wa kawaida ikimwagiwa acid matokeo yake yanakuwaje?
 
Kulitakiwa kuwe na njia nyingine ya kupima mchele wa plastic zaidi ya kuudundisha.
Unaeza uchoma kwenye moto utatoa harufu ya plastic na kuwaka mda mrefu but wa kawaida hauwaki na ukichoma una harufu ya wali

sending using jamiiforum makinikia
 
Kwanza lazima tujue maana ya plastiki? Na je, kuna aina ngapi za plastiki? Halafu tujue mechanism gani inafanya kitu kidunde.
Kiongozi, kabla ya kutaka kuleta shule kuuubwa hapa, jua LISEMWALO LIPO. Usiumize kichwa kwa kujaribu kujitutumua kuwa unauelewa mpana wa masuala COMPLEX ilihali hili jambo ni sawa na 3+3 tu.

Zile package za unga, let say NGANO ya Azam, ni plastic au udongo? Je, umewahi ona ile clip inayoonesha jamaa wanatumia 'nyuzi' za kusukia sandarusi hizo kutengeneza mchele??? Mchele huo utaitwaje?
 
Back
Top Bottom