Mchekeshaji Nyanda Kabundi fanya haya

BIG Africa

Member
Oct 15, 2022
84
116
Screenshot_20240313-001813_1.jpg


Habari zenu.

Iko hivi nadhani kwa kila mmoja wetu anamfahamu mchekeshaji aliyeibuka siku za hivi karibuni anayeitwa Nyanda Kabundi.

Iko hivi mchekeshaji huyu nataka nimshauri kitu kimoja. Atafute watu sahihi wa kumsimamia nyuma yake.

Ninamuona ana kipaji kikubwa lakini kuna marekebisho anatakiwa ayafanye.

Kwanza apate Meneja mzuri ambaye atamsimamia katika kazi yake ikiwemo kumshauri mambo gani afanye na mambo gani asifanye.

Kwa mfano Nyanda Kabundi amekuwa akitangaza bidhaa ya kampuni za nguo za ndani za watoto wadogo katika namna ambayo siyo ya kuvutia.

Yaani anaongea tu haraka haraka akiwa anatangaza hiyo bidhaa hiyo.

Mtu mwingine akiona hivyo anaweza asipeleke tangazo kwake kwasababu hatumii lugha ya mvuto katika kutangaza bidhaa.

Atazame wachekeshaji wengine kama wakina joti wanavyotangaza bidhaa za makampuni.

Wanatangaza vizuri. Kingine Nyanda Kabundi aanzishe TV yake online mfano aiite NYANDA TV AU KABUNDI TV.

Hii pia itamsaidia kupata matangazo ya kibiashara Kwa wingi. Kiufupi Nyanda Kabundi anahitaji msaada mkubwa wa kisimamizi kwani yeye ni kijana anayetoka usukumani katika familia za wafugaji ambapo nahisi hakupata elimu ya kutosha.

Ni hayo tu.
 
Hujaibua kipaji chake wakati hajatoka,sasa kashasikika unatoa ushauri
 
Back
Top Bottom