Chama cha siasa au kikundi chochote kile kinachojengwa kwa misingi ya Hasira, chuki, na uzushi hakiwezi kuishi. ACT-Tanzania ni genege la watu wenye chuki na majeraha ya kufukuzwa kwenye vyama vyao. matamko yao, mikakati yao na kila aina vitendo vyao vimejaa hasira na chuki binafsi na watu.
Leo Habibu Mchange ametoa tamko la ajabu sana kupata kutolewa eti anajitetea kutokana na kauli ya sebastian ya yeye kushiriki kulipua Chopa ya Dr Slaa.
ACT-Tanzania kwa matamko haya ya ajabu yanaendeleza riwaya ya kwanza ya matusi binafsi kwenye ulimwengu wa siasa. Siasa haijawahi kuwa ni personal attack hata siku moja, ni sera kwa sera. Ukiwa umejeruhiwa kisiasa jiponye majeraha, cool down, think, focus, tafuta ushauri nasaha kabla hujarukia treni jipya na kuanza kuuliza linakokwenda.
Matamko ya Habibu Mchange ni ya kutunga, uzushi, na yanaonyesha wazi matumizi mabaya ya fedha za kodi za watanzania kutoka serikali-ACT via CCM.
Siamini hata siku mmoja kiumbe yeyote kuanza kupiga kelele baada ya kupewa talaka. Wote leo wanaoisakama Chadema walipiga magoti kuomba wabaki, waling'ang'ania, na wengi wapo mahakani kutaka kubaki ndani ya Chadema. Hii yote inadhirihirisha wazi wanachuki mbaya sana kwa uchungu wa kutemwa na gari maridhiwa.
Mchange tunaomba uende polisi, ukaisaidie ili riwaya yako iweze kufanyiwa kazi. Unapotoa tuhuma za kuuliwa watu huku unajua na umekaa nazo ni kukiuka sheria za nchi, uhai wa mwanadamu ni muhimu kuliko kitu chochote hauchezewi na hatuwezi kukubali mtu kuuchezea.
Waliokufa na kuuwawa chini ya ulinzi wa polisi na wana CCM ni ndugu zetu. Mwangosi ameuwawa na jeshi la polisi hadharani, Mauji ya Arusha polisi walifyatua risasi hadharani, na raia walikufa na kadhaa kujeruhiwa, Ndago aliuwawa raia na wana CCM mchana kweupe.
Huwezi kuleta mzaha kwenye maisha ya watu.