Mchange awashambulia viongozi wa CHADEMA

Mchange awashambulia viongozi wa CHADEMA

Kuhusu dada yake Lissu aulizwe Kitila Mkumbo si ndio alikuwa mkuu wa kugawa viti maalum na alishakiri mara kibao hapa? Huenda aliweka ukabila ndio maana anampa huyo kama ni kweli maana Mchange huaminiki hata kidogo .....leo kaulizia maswali na waandishi kuishia kutukana tu......
Duu kumbe ndo maana yule mwenyekiti Bawacha alikimbia.
 
Pasco mbona hujataja bahasha za kutosha? Maana navyojua wapo watu kwa umaarufu wao wakiita waandishi wao wenyewe hawataki kukosa kwa vile wanajua kuna habari nzito. Lakini Mchange kweli anaweza kuwakalisha waandishi makini kumsikiliza bila vibahasha? Labda uniambie ni waandishi wa Global P.
Sent from my iPad using JamiiForums
Mkuu Chakaza, kwanza asante!. Habari ni bure!, bahasha za khaki ni by the way tuu!, ziwepo, zisiwepo, bado habari kama ni habari itasimama tuu!. Lengo la bahasha ni logistics

Ila pia kwa habari hii, kwa jinsi nilivyoisoma!, narudia tuu ile kumbu kumbu yangu kuwa, kuwa ...sio mtu lazima mpaka aokote makopo!.

Thanks.

Pasco.
 
Pasco inakuaje mtu kama wewe unaungana na hawa political failures with cheap politics in this stiff political competition? Au these guys are your type?
Mtu ambaye mpaka sasa anafanya kazi ya ccm ni kijana asiyeaminika maana ccm haina maana yeyote sasa zaidi ya kukaba kila ambacho kinaweza msaidia mtanzania.
Mkuu LOMAYANN, asante. Ni njaa tuu!, if you can't beat them, join them!.

Thanks.

Pasco
 
Mmm huyu ni mlamba viatu vya zitto basi!

Hizi siasa zina mambo mengi sana.
Watu ukiwakuta majukwaani mishipa na jasho imewatoka unaweza kusema ni watu kweli na wana machungu na nchi.

Lakini wanayoyafanya wakiwa huko faragha yanatisha sana.

Jamaa kanitia hofu iliyonipelekea kukiogopa hiki chama hadi naogopa hata kukiandika hapa na katu sitokiandika popote pale make nahisi nitaota matendo yao ndotoni.

Natoa wito kwa watanzania wapenda amani. Heri nusu shari kuliko shari kamili.

Na zimwi likujualo halikuli likakwisha. Bora kuendelea kubaki na mkoloni mweusi kuliko hawa wapaka poda.
 
Chama cha siasa au kikundi chochote kile kinachojengwa kwa misingi ya Hasira, chuki, na uzushi hakiwezi kuishi. ACT-Tanzania ni genege la watu wenye chuki na majeraha ya kufukuzwa kwenye vyama vyao. matamko yao, mikakati yao na kila aina vitendo vyao vimejaa hasira na chuki binafsi na watu.

Leo Habibu Mchange ametoa tamko la ajabu sana kupata kutolewa eti anajitetea kutokana na kauli ya sebastian ya yeye kushiriki kulipua Chopa ya Dr Slaa.

ACT-Tanzania kwa matamko haya ya ajabu yanaendeleza riwaya ya kwanza ya matusi binafsi kwenye ulimwengu wa siasa. Siasa haijawahi kuwa ni personal attack hata siku moja, ni sera kwa sera. Ukiwa umejeruhiwa kisiasa jiponye majeraha, cool down, think, focus, tafuta ushauri nasaha kabla hujarukia treni jipya na kuanza kuuliza linakokwenda.
Matamko ya Habibu Mchange ni ya kutunga, uzushi, na yanaonyesha wazi matumizi mabaya ya fedha za kodi za watanzania kutoka serikali-ACT via CCM.

Siamini hata siku mmoja kiumbe yeyote kuanza kupiga kelele baada ya kupewa talaka. Wote leo wanaoisakama Chadema walipiga magoti kuomba wabaki, waling'ang'ania, na wengi wapo mahakani kutaka kubaki ndani ya Chadema. Hii yote inadhirihirisha wazi wanachuki mbaya sana kwa uchungu wa kutemwa na gari maridhiwa.

Mchange tunaomba uende polisi, ukaisaidie ili riwaya yako iweze kufanyiwa kazi. Unapotoa tuhuma za kuuliwa watu huku unajua na umekaa nazo ni kukiuka sheria za nchi, uhai wa mwanadamu ni muhimu kuliko kitu chochote hauchezewi na hatuwezi kukubali mtu kuuchezea.

Waliokufa na kuuwawa chini ya ulinzi wa polisi na wana CCM ni ndugu zetu. Mwangosi ameuwawa na jeshi la polisi hadharani, Mauji ya Arusha polisi walifyatua risasi hadharani, na raia walikufa na kadhaa kujeruhiwa, Ndago aliuwawa raia na wana CCM mchana kweupe.

Huwezi kuleta mzaha kwenye maisha ya watu.
 
HABIBU MCHANGE AKANA TUHUMA ZA KUHUSIKA NA ULIPUAJI WA HELKOPTA ILIYOWABEBA MNYIKA NA SLAA.

Leo mchana katika mkutano wake na waandishi wa habari,Mchange amewashambulia waziwazi viongozi wakuu wa chama cha demokrasia na maendeleo na kuwatuhumu kuhiska na mauaji ya aliyekua mbunge wa CHADEMA Tarime,marehemu Chacha Wangwe,kisha kumkana mtu aliyehusika na mauaji hayo Deus Mallya,wakati alikuwa mjumbe katika kamati iliyokuwa chini ya John Mnyika,na rafiki wa Mnyika lakini Mnyika kumkana hajawai hata kumuona.

Kisha kawataja Lissu,Mbowe na Slaa kuajiri vijana na kuwalipa kuwatesa vijana wanaoonyesha kuiunga mkono CCM katika kampeni mbalimbali za chama,hasa kwa kumwagia watu tindikali.

Pia amesema Lissu ni mbinafsi na fisadi aliyedhurumu fedha za miradi ya mazingira,na kujenga nyumba ya ghorofa Tegeta,Mbowe anahujumu mamilioni ya CHADEMA,na Slaa akihujumu fedha za chama kulipia mkopo wa NSSF.
===================================



Mchange ni nani ?
 
Chama cha siasa au kikundi chochote kile kinachojengwa kwa misingi ya Hasira, chuki, na uzushi hakiwezi kuishi. ACT-Tanzania ni genege la watu wenye chuki na majeraha ya kufukuzwa kwenye vyama vyao. matamko yao, mikakati yao na kila aina vitendo vyao vimejaa hasira na chuki binafsi na watu.

Leo Habibu Mchange ametoa tamko la ajabu sana kupata kutolewa eti anajitetea kutokana na kauli ya sebastian ya yeye kushiriki kulipua Chopa ya Dr Slaa.

ACT-Tanzania kwa matamko haya ya ajabu yanaendeleza riwaya ya kwanza ya matusi binafsi kwenye ulimwengu wa siasa. Siasa haijawahi kuwa ni personal attack hata siku moja, ni sera kwa sera. Ukiwa umejeruhiwa kisiasa jiponye majeraha, cool down, think, focus, tafuta ushauri nasaha kabla hujarukia treni jipya na kuanza kuuliza linakokwenda.
Matamko ya Habibu Mchange ni ya kutunga, uzushi, na yanaonyesha wazi matumizi mabaya ya fedha za kodi za watanzania kutoka serikali-ACT via CCM.

Siamini hata siku mmoja kiumbe yeyote kuanza kupiga kelele baada ya kupewa talaka. Wote leo wanaoisakama Chadema walipiga magoti kuomba wabaki, waling'ang'ania, na wengi wapo mahakani kutaka kubaki ndani ya Chadema. Hii yote inadhirihirisha wazi wanachuki mbaya sana kwa uchungu wa kutemwa na gari maridhiwa.

Mchange tunaomba uende polisi, ukaisaidie ili riwaya yako iweze kufanyiwa kazi. Unapotoa tuhuma za kuuliwa watu huku unajua na umekaa nazo ni kukiuka sheria za nchi, uhai wa mwanadamu ni muhimu kuliko kitu chochote hauchezewi na hatuwezi kukubali mtu kuuchezea.

Waliokufa na kuuwawa chini ya ulinzi wa polisi na wana CCM ni ndugu zetu. Mwangosi ameuwawa na jeshi la polisi hadharani, Mauji ya Arusha polisi walifyatua risasi hadharani, na raia walikufa na kadhaa kujeruhiwa, Ndago aliuwawa raia na wana CCM mchana kweupe.

Huwezi kuleta mzaha kwenye maisha ya watu.

Kaka acha kutoa povu. Hayo yote aliyoyasema Mchange wengine tunayajua siku nyingi. Mnyika ndio maana alishindwa kumaaliza Chuo kwa sababu ya laana ya damu za watu. Haiingii kichwani kijana asiyekua na elimu yoyot katika karne hii anakabidhiwa majukumu mengi katika Chama wakati vijana wasomi wapo. Ni mbulula tu kama wewe unayeweza kuwaaminisha watu kuwa viongozi wa Chadema siyo wauaji.

Eti ndege iliyombeba Babu Slaa na Mnyika ilitaka kulipuliwa!! This is no sense!! What is so special in them? Kama ukiwataka hao huhitaji hata kusubiri ndege yao.

Damu za watu alioshiriki kuwaua Mnyika zitamfuata popote. Huwezi kuwa unashiriki kuua watu halafu wewe ubaki salama.

Chadema nje ya siasa za mauaji hawana lolote. Kila mtu anajua jinsi wanavyohangaika kila siku ili wamuue Zzk.
 
Haya na nyie nendeni mahakamani kama mmesingiziwa mlimuua Chacha wangwe.
Soma hapa.

Dunia Nzima inajua kwamba watu hawa wameshiriki kikamilifu kumuondoa DUNIANI aliyekuwa makamu mwenyekiti wa chama CHACHA ZAKAYO WANGWE, Hii haina ubishi kwamba, MBOWE, SLAA na MNYIKA walijaribu mara kadhaa kutaka kumuua CHACHA WANGWE kwa kutumia sumu na kushindwa mpaka walipofanikiwa kumuua kwa ajali ya kutengeneza tarehe 28.7.2008 wakimtumia kijana ambaye Dunia nzima inamjua.
Wewe mjinga waambie hao waume wako (serikali ya magamba) wawakamate wakina mbowe na mnyika kwa mauwaji pambaf
 
Ni bora ndugu mchange ameweka wazi kuhusu namna CHADEMA wanavyotekeleza mauaji na ugaidi nchi hii, katika harakati za kueneza chama chao.

Mchange amesahau kumtaja Igondu Ramadhani, mtumishi wa ikulu aliyemteka na kumtesa Ulimboka nae alikuwa chadema.
 
Back
Top Bottom