define kwanza maana ya uchochezi maana ndo Lugha ya Magamba then Niambie kwanini Rc Mulongo asiunganishwe ktk hii kesi? Weka uchama pembeni buku 7 isikufanye huna utu.
Uchochezi ni hali ya kushinikiza haidha mtu au kundi la watu kufanya tukio lisilo kubaliwa na jamii au lililo kemewa na sheria. Lema baada ya kumaliza mazungumzo na wanafunzi akampigia simu Mkuu wa mkoa, kumbuka mkuu wa mkoa ndie m/kiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, alipaswa kuwepo eneo la tukio kutekeleza majukumu yake, lakini Lema hakuwa na nafasi yeyote kwenye eneo la tukio, sasa alikuwa akifanya nini kwenye hali kama ile? ndio maana amekamatwa ili polisi wachunguze ajenda ya Lema na wale wanafunzi wala hawajamuonea, pia polisi hawajazuiwa na sheria kumkamata mtu kwa kigezo cha wakati, muda wowote na mahala popote wakitakiwa kukamata, wao ukamata.
Mkuu wa mkoa hapaswi kuhusishwa na hii kesi kwa maana ya kukamatwa, la hasha, ila atahusishwa kutoa ushaidi wa mambo kama kupigiwa simu na Lema na aliyoelezwa, kujeruhiwa baada ya kurushiwa kitu chenye ncha kali, na mambo ya namna hii. Katika hali ya utomvu wa nidhamu aliyo nayo Lema na tendo la yeye kuwa eneo la tukio, lazima itaaminika kuwa kwa namna moja hama nyingine ameshiriki kushinikiza jambo ili.
Wote hapa tunajua historia za wana harakati na wakombozi kote duniani zilivyokuwa zikifanywa, zilikuwa zenye kusisimua na zenye mashiko, hawakuwa wakitumia vitisho wala jazba, na zaidi ya yote, hawakuwa wakitumia matusi kujenga hoja zao. Walitumia nguvu yao ya ushawishi tena inayo kubalika kuleta vuguvugu la mabadiliko na hawakuwa wakisababisha machafuko kwa namna yeyote ile, na ndio maana walikuwa wakiuawa wao huku wafuasi wao wakiwa salama kabisa, sio hawa CHADEMA.
Sasa hawa CHADEMA na huyu bwana mdogo Lema wako kundi gani? waleta mabadiliko? sifa hizo hawana, binafsi nawaona kama majangili wa amani iliyopo, kama wanaubiri nguvu ya umma leo basi wamechelewa, maana nguvu ya umma ni maneno yaliyopo kwenye neno "DEMOKRASIA", kutoka kwa Abraham Linkolin, CCM wamekuwa wakilitumia ili neno nguvu ya umma kwa vitendo, kwa kuleta mfumo wa kupiga kura hapa nchini.
"HAKUNA NGUVU NYINGINE YEYOTE YA UMMA INAYOZIDI KUPIGA KURA."