Ni ujinga kujitolea nafsi zetu kuondoa maadui
umasikini, ujinga, maradhi, na dhuluma
(ufisadi) na ukandamizaji wa demokrasia kwa kutumia silaha ya woga,
wasiwasi, mashaka, ubinafsi na hisia hasi
zote za namna hiyo. Hisia hizi hazijawahi
kutumika kama silaha na kuleta ushindi zaidi
ya kumjenga adui na hata kujikuta
akisujudiwa na kutumikiwa. Hisia hasi sio kinga
wala sio silaha popote!
Uko ushahidi kuthibitisha kuwa maadui hao
wa nne waliogunduliwa tangu enzi ya
kuasisiwa taifa hili wana rutubishwa,
kudumishwa na kuendelezwa na nguvu ya
hisia zetu ambazo ni hasi kiutu na
kibinadamu. Nguvu ambayo anaizalisha askari
yuleyule aliye vitani kupambana na maadui
hao wa maendeleo, afya na ustawi wa jamii.
Utu ni utambuzi uliopevuka dhidi ya mkondo
wa hisia hasi. Rasilimali Utu ni uwezo wa
kumomonyoa ubinafsi wa hisia hasi na kusitiri
heshima, imani, upendo na matumaini ambazo
ni nguzo kuu za maadili ya ubinadamu dhidi ya
unyama au Utu hasi. Hivyo werevu wa kina
dhidi ya hisia hizi angamizi kwa Utu ndio
unaotafsiriwa kama kuerevuka na kueleimika
Kiutu (emotional intelligence: EI); ni kufuta
ujinga Kiutu. Hii ni tofauti na werevu wa kiakili
(intelligence quotient: IQ)
Kutoelimika juu ya dhana nzima ya Utu na
sheria za mfumo mzima wa hisia hasi kwenye
ustawi wa jamii, ni ujinga wa Kiutu unaozidi
ujinga wa kiakili katika nafasi hiyohiyo. Ukweli
lema analeta uchochezi na ni mtu hatari kwa taifa letu..kama kuna watu wanafikiri lema ni shujaa basii wamepotea.sizazi kama mtu mwenye akili anaweza kuchochea fujo badala ya kutafuta suluisho la tatizo..POLENI IAA.Tusiruhusu wanasiasa kuingilia hata mambo yasiyowahusu.