Mbunge Lema akamatwa na Polisi!

Mbunge Lema akamatwa na Polisi!

Katika kufuatilia yaliyojiri kwa Mhe. Lema, kuna vitu kadhaa ninashindwa kuvielewa. Kosa la Lema linalosisitizwa liko katika muktadha wa kuwachochea wanachuo wa IAA-Arusha.
1. Mkuu wa Mkoa akatoa amri ya Mhe. Lema kujisalimisha Polisi. Kwanini amri hiyo isitolewe na RPC? Na kama kwa RPC ni sahihi, je DC dhidi ya OCD inaweza kuwa sahihi pia?

2. Kwanini Polisi wamekwenda kuchukua vitu kadhaa vya Mhe. Lema wakati wanajua havina ushirikiano wa moja kwa moja na makosa wanayomtuhumu?
Jamani, kweli watanzania ni wasahaulifu. Mnasahau kuwa huyu bwana alikuwa jambazi la kutupwa, wakisachi kwa uhakika wanaweza kupata mabaki ya kazi hiyo, si unajua polisi wasivyo na dogo
 
Hivi wewe mbulumundu unataka kuwapangia polisi kazi au?
Ni jukumu la polisi kuchukua nyaraka zozote zinazoweza kutumika kama ushahidi mahakamani.
Vitu kama laptops na simu vinatunza kumbu kumbu nyingi tu, kuanzia mawasiliano yako na magaidi wengine hadi video za kichochezi.
Pia ni rahisi kunasa mipango yoyote inayoweza kuwa imepangwa kufanyika. Subiri tamko la polisi utasikia mengi
Halfu nikukumbushe tu kuwa mkuu wa mkoa ndio mkuu wa kamati ya ulizni na usala wa mkoa, anamuwakilisha Rais kwenye mkoa hivyo katika mkoa wa ASrusha mkuu wa mkoa ndio mkubwa ki protocol kuliko wote hapo mkoani, na huyo Lema ni mbunge tu kama nasari

Chris, kukaa uingereza kusikufanye uwe mvivu wa kufikiri na mwepesi wa kuporomosha matusi kwa watanzania wenzako. Ukijiheshimu, utaheshimiwa.

Kwene ku-uingeresa povali vahehe, vabena na vadzungwa volufu. Lakini avayago vagaya maligo ni khidada ngita dza-nyavako.
 
Jamani, kweli watanzania ni wasahaulifu. Mnasahau kuwa huyu bwana alikuwa jambazi la kutupwa, wakisachi kwa uhakika wanaweza kupata mabaki ya kazi hiyo, si unajua polisi wasivyo na dogo

Sasa, Mkuu wa Mkoa anapataje amri ya kumtaka aende Polisi?

Hivi kwa fikra zako hata kama alikuwa mwizi (japokuwa siafiki sana) mabaki ya tabia ya wizi utayakuta kwenye laptop au ipad?

Kwanini nisiwe na fikra nyingine kuwa wanataka kujua ushahidi wa Lema dhidi ya Pinda na dhidi ya Kikwete?
 
Chris, kukaa uingereza kusikufanye uwe mvivu wa kufikiri na mwepesi wa kuporomosha matusi kwa watanzania wenzako. Ukijiheshimu, utaheshimiwa.

Kwene ku-uingeresa povali vahehe, vabena na vadzungwa volufu. Lakini avayago vagaya maligo ni khidada ngita dza-nyavako.

Chris ni wa kumuonea huruma ,............... inasemekana ni mgonjwa!!!!!
 
mnabishania jina,sisi muuaji tunaye selo na tutampeleka jela siku si nyingi

M 23 unachefua! sijui unatumia sehemu gani ya Ubongo? Ujue sio wasomaji wote humu wana ushabiki wa vyama kama wewe ulivyo. Unadevalue JF kwa interventions zisizo tumia akili
 
mimi polisi huwa nawashangaa kweli hivi kwanini hawatumia akili zao wanatumia akili za kisiasa? alaf wakishindwa wanaonekana wao mtori huyo aliyewaagiza ambaye hana taaluma yeyote ya usalama anabakia bila kuzomewa? nashauri mwenyekiti wa kamati ya usalama asaidie mambo yanapowashinda kamanda wa mkoa na wa wilaya na siyo hasara na uhasama na umbumbumbu wa mtu mmoja uwasumbue na kusababisha watu kupoteza imani na nyinyina dhana ya polisi jamii inakosekana na watu sasa wanachukulia sheria mikononi sasa
 
kweli Mheshimiwa lema anawa.jambi.sha mwaka huu mtaona. hata mmkamate mtamwachia tu nasema kama imeandikwa hakuna wa kupingana naye lazima iwe tu
Kwa akilizi zake zilivyo ndogo, Mh. Lema ni mtu hatari kwa usalama wa watu. Huwezi jua ni kitu gani atafanya sekunde chache zijazo.
 
ktk ujambazi wake aliumiza wengi sasa haya ni matunda,ayakubari tu.
Kwa hiyo mbakaji hukumu yake ni kubaka watoto wake.?Kweli logic ya gamba zero. Pia ujambazi nani ana hakika nao?CCM wajinga kweli, mmemzika Babu sambeke kama Mungu
 
mkuu cyo kosa lao wanatekeleza maagizo ya mwenyekiti wa kamati ya usalama ya mkoa ambaye naye anatekeleza maagizo ya aliyemchagua.kumbuka according to rule#1 boss is always right na polisi ni kosa kugomea order ya mkuu

nakubaliana na wewe; wanatekeleza maagizo ya m/kiti kwa nia ya kutisha wananchi waogope kuunga mkono CHADEMA. Aliyetoa maagizo ajue kuwa vitisho hivyo vinazidi kuwatia nguvu wananchi ambao wamechoka maisha duni kila nyanja kuanzia hospitali, shule nk.
 
Inaelekea unajua mengi, hebu tuorodheshee matukio angalau 10 tu ya hatari aliyoyafanya Mhe. Lema toka mwaka jana hadi mwaka huu. Kama haitoshi ongeza matatu aliyofanya mwezi wa Machi tu; ambayo unafikiri yanahatarisha amani na usalama wa watu.
Mkuu ccm imekabidhiwa kwa jeshi la polisi na TISS.
 
Ndiyo maana tunasema jeshi la aina yoyote including POLISSM wanatakiwa wasiwe washabiki wa vyama. Hapa wanatekeleza maagizo. Ila Lema hamatamuweza, wala mbunge mwingine wa CDM anayetetea maslahi ya watanzania. Mh. Lema usiwe na shaka, wanakutafuta kwa udi na uvumba ila hawatakupata. Wanajisumbua bure. Kisa Mkuu wa Mkoa asiyejua wajibu wake ana aliyeteuliwa na CHAMA CHAKE. Sasa subiri hizo nafasi zitakuwa zinajazwa kwa usaili. Tupeni mbal vilaza.
 
Hivi wewe mbulumundu unataka kuwapangia polisi kazi au?
Ni jukumu la polisi kuchukua nyaraka zozote zinazoweza kutumika kama ushahidi mahakamani.
Vitu kama laptops na simu vinatunza kumbu kumbu nyingi tu, kuanzia mawasiliano yako na magaidi wengine hadi video za kichochezi.
Pia ni rahisi kunasa mipango yoyote inayoweza kuwa imepangwa kufanyika. Subiri tamko la polisi utasikia mengi
Halfu nikukumbushe tu kuwa mkuu wa mkoa ndio mkuu wa kamati ya ulizni na usala wa mkoa, anamuwakilisha Rais kwenye mkoa hivyo katika mkoa wa ASrusha mkuu wa mkoa ndio mkubwa ki protocol kuliko wote hapo mkoani, na huyo Lema ni mbunge tu kama nasari
Njaa zinakusumbua mno! Umezingirwa mno na tongotongo za magamba kila sehemu ya mwili wako. Haki imefichika rohoni mwako. Huna jipya hadi unatia kinyaa! Naona kila wakati unashindia hapa JF ili magamba wakufanyie fadhila ya walau mlo mmoja kwa siku huko uliko. Shame on you!! Huna faida yoyote katika Tanzania ya leo!!
 
Jamani, kweli watanzania ni wasahaulifu. Mnasahau kuwa huyu bwana alikuwa jambazi la kutupwa, wakisachi kwa uhakika wanaweza kupata mabaki ya kazi hiyo, si unajua polisi wasivyo na dogo

Kwahiyo mabaki ya wizi wanayatafuta kwenye laptop, simu na flash disc walivyo ondoka navyo? mkuu ushahidi wa Lema noma... afu sidhani kama atakuwa mjinga kwamba alikuwa hana digital backup ya hizo info on line. Mtafuta mtaharibu computer mtaiwekea software za kunasa mawasiliano yake, lakini ipo nguvu ya Mungu mtashindwa na kulegea na ukweli utasimama!
 
In a minute nitarusha video niliyo record kipindi MheshLema tangu anazingiwa nyumbani kwake mpaka mpaka amefikishwa kituoni centra;,nimerekodi kwa peni.kalamu.
 
In a minute nitarusha video niliyo record kipindi MheshLema tangu anazingiwa nyumbani kwake mpaka mpaka amefikishwa kituoni centra;,nimerekodi kwa peni.kalamu.

Aisee. Kumbe? Kwa post hyo leo utalipwa buku 3..
 
In a minute nitarusha video niliyo record kipindi MheshLema tangu anazingiwa nyumbani kwake mpaka mpaka amefikishwa kituoni centra;,nimerekodi kwa peni.kalamu.

Eh! si ungerusha tu, kwani lazima useme "in a minute". Haya sasa zimepita kumi!
 
Jamani, kweli watanzania ni wasahaulifu. Mnasahau kuwa huyu bwana alikuwa jambazi la kutupwa, wakisachi kwa uhakika wanaweza kupata mabaki ya kazi hiyo, si unajua polisi wasivyo na dogo

He, kweli e? mimi ndiyo kwanza naskia kwako. Kama ndiyo hivyo basi hatuna jeshi la polisi Tanzania, kama wewe kibwengo wa namanditi unajua huyu jamaa ni jambazi inamaana polisi wameshindwa kufanya kazi yao!
 
Back
Top Bottom