Mbunge Lema akamatwa na Polisi!

Mbunge Lema akamatwa na Polisi!

Mkuu siku zote serikali zilizo madarakani ndizo chanzo cha matatizo. Sidahni kama hiyo ni issue ya kupeleka polisi hata kupekuwa nymbani kwa kamanda Lema. Kwa namna hii, CDM itaendelea kujulikana na kujikita mioyoni mwa watu bila gharama ya kuwafikia. Zote hizi ni baraka za Mungu. Watu wanaona na dunia inaangalia.
Na kwa mpango huo nashukuru wanatusaidia uchaguzi uwe mwepesi kwa CDM maana watu wanazidi kuwa na hasira juu ya vitendo vya unyanyasaji kama huo.
 
Kosa lake ni wanachuo kumzomea mkuu wa mkoa, then, hasira RPC kuzimzlizia kwa kamanda
 
Hata kule alikukimbilia Idd Amin?

Enzi za Idd Amin hakukuwa na ICC ndo maana hakurudishwa Uganda. Na Kikwete aelewe fika kuwa hawa wazungu wanaomsapoti kwa sasa wote watahamia CHADEMA ikishinda uchaguzi 2015 na kuchagiza nchi itakayomficha kumrudisha haraka. Kwa jinsi hali ilivyo sasa mambo madogo kama haya ndio yanazidisha chuki dhidi ya CCM, kila kitu kimeonekana hapo. Mwisho wa siku mkuu wa mkoa anaamuru mbunge akamatwe, anaamuru chuo kifungwe kwa kuwa wamemzomea, mambo gani hayo. Msifikiri CHADEMA wameturoga watanzania, upumbavu wenu maCCM na kutokuwa na ubinadamu ndio vinafanya tukimbilie kutafuta ukombozi CDM maana uonevu huu wa waziwazi kama wa ibilisi haukubaliki
 
Baada ya mabishano ya muda mrefu nyumbani kwa kada huyu na Mbunge wa Arusha mjini na uvamizi onevu wa Polisi wakati huu wa usiku; Mh. Lema amekubali kukamatwa na amechukuliwa na gari la polisi wakati huu na kupelekwa kituo kikuu cha polisi Arusha yaani Central Polisi.

Wananchi wengi wamejitokeza ku-support mbunge wao na huenda Asubuhi wananchi wakawa wengi zaidi.

Scene two ni hali itakavyokuwa huko polisi.

Updates
Sasa wamefika CLocktower anasindikizwa na msululu wa magari ya makada waliojitokeza ku-support kuelekea kituo cha polisi.

Baada ya kumfikisha Lema Central police Arusha amesachiwa na kuingizwa ndani. Kamanda Lema alikuwa ameambatana na magari ya makamanda waliomsindikiza ili kushuhudia kinachojili hapo kituoni.

Hivi sasa polisi wamewafukuza makamanda wote hapo kituoni na kuwaambia hawatakiwi kuonekana hapo. Makamanda wameondoka kwa amani na kwenda kupaki Safari hoteli wakisubiriana kupata mwongozo.

03:41am
Wamekutana pembeni ya kituo cha polisi na wamekubaliana kuwa watawanyike wakalale hadi kesho asubuhi watajuzwa kinachoendelea. Hivyo, Lema yupo ndani na wananchi waliomsindikiza wametawanyika kwenda kulala. Tutaonana asubuhi kwa yale yatakayojiri.

11:15am
Kwa sasa Lema bado yuko ndani na bado hajahojiwa. Kwa sasa anasubiriwa Mwanasheria wake ili ahojiwe. Mpaka sasa hakuna tamko lolote juu ya sababu za kukamatwa kwake. Baada ya kuhojiwa huenda mwanasheria wake atasema kilichojiri. Watu waharuhusiwi kukaa au kusimaa vikundi vikundi eneo la polisi.


Earlier by Emanzi:

Ni kamanda wa Jeshi gani au Kikosi gani???
 
Lema amekamatwa kwa chuki za Kisisa; anayemtesa Lema na Wapiga kura wa jiji la Arusha si mwingine ni yule mama aliyeshindwa na Lema na aliyekataliwa na wapiga kura. Nasema hivyo kwa sababu toka huyu mama baada ya kufail kihalali watawala wa nchi hii wamekuwa hawana amani. Naamini yule mama alikuwa tayari ametengewa nafasi nzuri tu kwenye serikali hi isiyo sikivu na inayoamini kuongoza nchi kwa kutumia vyomba vya dola. Kufail ubunge kukawa ni pigo kwa mama yule aliyekuwa mgombea na kipenzi cha watawala,waliotaka awe karibu nao bungeni na kwenye baraza la mawaziri. Umma ukishasema hapana ebu uheshimiwe kwa maamuzi yake kuendelea kumtenda ndivyo sivyo kipenzi chao ( LEMA) ni kuendelea kuzipoteza kura hata ifikapo 2015.
 
Yawezekana wanataka kumtengenezea ushahidi wa uongo kwenye simu, ipad na laptop waliyochukua. Au wanataka kufuta sms iliyotumwa na mkuu wa mkoa? Tutaona mengi ya kuudhi ili tuwe na hasira ya kutosha tutakapoamua.

Watakua wanataka kufuta sms ya mkuu wa mkoa
 
Umekosa nini we Lema,
kuvamiwa usiku bila staha?
Mwenye kustahili haya,
si wewe si wewe Lema, ni Magesa!
Ndugu yangu haya yote ni mashinikizo. Walijua kabisa kama hawatamkamata siku au usiku wa alhamis basi wasingetimiza lengo lao la kumlaza rumande (lock up) wikiendi nzima bila dhamana, kwa kuwa siku ya ijumaa ni sikukuu ya muungano wa tanzania na jumamosi na jumapili watasema ni wikiendi mahakama hazifanyi kazi. Kwa hiyo watakaa naye wikiendi nzima hapo kituo cha polisi kwa kisingizio hicho, kuwa asubiri kufikishwa mahakamani siku ya jumatatu ambako ndiko atapata dhamana. Kosa lenyewe wanajua linadhaminika labda ndo wambambikizie kosa la ugaidi ili asipewe dhamana na hivyo kumpotezea muda tu.
 
Haya maigizo hadi Jumatatu ndio Mh. Lema atpewa dhamana baada ya hapo makamanda wataongoza maadamano makubwa ya wana-CDM hadi viwanja vya NMC Unga Ltd, kisha chama kitatoa TAMKO KALI.
 
Kwa sasa Lema anajisaidia haja kubwa kwenye ndoo,nita rusha video yake na kuwajuza kila tukio humu ndani lumande

Asee nikuwa sijui kumbe mahabusu kunatumika ndoo! Kweli wewe mzoefu! Enhee ndo ya plasiki ama ya chuma
 
Tayari uongozi wa chama mkoa chini ya katibu wa mkoa wameshaongea na RCO, muda si mfupi kamanda Lema atachukuliwa maelezo, ndiyo taratibu zingine zitafuata ikiwa ni pamoja na dhamana.

Nchi hii nidhamu ya uongozi imepotea kabisa, haiingii akilini RC anafanya kazi ya siasa. Huu wote ni mwendelezo wa siasa chafu za ccm na mawakala wake.

Jamani mkiangalia ile video ya pale IAA lazima ujiulize sababu ya Lema kukamatwa ni nini? Magesa anaonekana ana shinikizo pia nyuma yake.

Haya ni matumizi mabaya ya madaraka

Hii ni hujuma tu inafanywa na magamba ili watu wa Arusha wajitokeze mtaani na polisi watumie huo mwanya kuanzisha fujo. Fujo zikianza watoe kisingizio kuwa Arusha hamna amani hivyo uchaguzi uliotangazwa na tume ya uchaguzi usimamishwe.
Napenda kutoa mwito kwa watu wa Arusha kuwa makini na hili. Hii ni move ya magamba na watatumia kila njia ili uchaguzi usifanyike. Kama fujo hazitatokea kwa kumkamata Lema basi wataanzisha fujo kwenye mikutano ya kampeni.

Tukumbuke pia mkuu wa mkoa alisema mauaji ya huyo mwanafunzi yanahusishwa na siasa. Huenda Magamba walifanya hayo mauaji karibu na nyumbani kwa Lema wakijua kuwa wanafunzi wakireact lazima Lema ajitokeze hivyo watamuhusisha na vurugu na kumkamata ambapo fujo kubwa zitatokea na hivyo uchaguzi utasimamishwa. Angalia maneno ya mkuu wa mkoa kuthibitisha hili, “Baada ya kuletewa taarifa za tukio hili na Mbunge Lema, niliondoka na kwenda kuwasikiliza wanachuo lakini tayari nilijua mazingira yalikuwa yamebadilishwa".
 
Hii yote no matokeo ya kupeana vyeo kiswahiba....huyu mkuu wa mkoa ni mbumbumbu wa kutupwa! Ametengeneza uhasama kwenye kitu kilichohitaji a minute common sense! Kulikuwa na haja ya yote haya? Km ameshindwa ku-control wanachuo tu sidhani hata family yake anaiweza.....seuze mkoa! (Mind u this come from a pro CCM)

:angry:nchi haitawaliwi na TISSI kweli?wanajf tafakarini.:angry:
 
Lema is a hero na atabaki hero hii issue ya lema si ndio kama ya ile ya mh mnyika kipindi udsm alipotuumiwa kua yupo nyuma ya mgomo wa wanafunzi mungu ambariki mkuu wa kanda ya kaskazini
 
Kilichobaki kwa uongozi wa CDM mkoa wa Arusha ni kutangaza mgogoro na Mkuu wa mkoa hichi Kimlongo,tena mgogoro usio na ukomo mpaka hapo aliemleta hapo aondoke.hivi kweli huyu anaweza kujifanya ndo mmiliki wa ARUSHA nanyi wana wa Arusha mnakubali tu?kimsingi imeniudhi sana na kunisikitisha kwa kitendo cha kuamua kumvamia Lema kwake,hata kwa watoto najua imewaumiza kisaikolojia,huu ni unyama.Nawashauri watu wa Arusha wanaopinga uonevu,dhuluma na unyanyasaji,wote wanaopinga unyama huu,suluhisho ni KUTANGAZA MGOGORO USIO NA UKOMO NA MAGESA MULONGO.Ni kumzomea kila apitapo,ni kumwandika vibaya kila mahali,kutokumsikiliza kila asemapo.na kufanya maandamano makubwa ya kupinga vitendo vyake.
 
hivi huyu kamanda wa jeshi gani na kikosi gani??? Kwanza hawajamkuta na vigrunedi? Vibomu? Ak 47? Manake si CHA DEMU huyu? Kile chama cha maga idi
 
Aluta continua, safari ya mafanikio haina mtelemko hata kidogo, walio mstari wa mbele wanaonekana wanaumizwa lakini mateso yao siyo bure na Mungu hataacha mateso haya kudumu kwa muda mrefu, TULIKOTOKA ni mbali tunakokwenda karibu, labada mtuuue wote only two years have left kwa utawala huu dhalimu kuendelea kukandamiza haki katika nchi hii! Namuomba Mungu kuwa atupe ujasiri zaidi katika kipindi hiki kifupi cha mpito, tunapo anza kukata tamaa ndipo mwisho unakaribia, asiwepo wa kurudi nyuma ila tuongezeke mastari wa mbele! "If God is for us who can be against us"
Kamanda Lema ninakuombea Bwana hatakuacha kazi yako ni njema! Peoplesssssssssssssssss!
 
There are currently 3630 users browsing this thread. (178 members and 3452 guests)
  • hii number ya guests inanitisha, serikali nzima imehamia JF!
 
Back
Top Bottom