Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,988
spika makinda aungana na familia ya marehemu naibu waziri sumari
on Friday, January 20, 2012
Spika wa Bunge Mh. Anne Makinda akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya aliyekuwa Mbunge wa Arumeru na Naibu Waziri wa Fedha, marehemu Jeremia Sumari, wakati alipofika nyumbani kwa marehemu Tang Bovu jijini Dar es Salaam leo Januari 19, 2012, kwa ajili ya kutoa pole kufuatia kifo cha mbunge huyo kilichotokea usiku wa kuamkia jana Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa Picha na Owen David
Kama huyu Owen David aliyeandika hii habari ndie yule wa bunge, na hajui kwamba marehemu Mh. Sumari alikuwa mbunge tu na hakuwa naibu waziri wa fedha kama anavyomuelezea hapo, nadhani kuna watu wanapewa majukumu ambayo hawakustahili kuyapata.
Inawezekanaje mtumishi wa bunge hawajui mawaziri wa fedha, ama hajui nyadhifa za wabunge zaidi ya ubunge? na sitarajii mtu yeyote ambaye yuko kwenye sekta ya habari afanye kosa kama hilo hata kama si muajiriwa wa bunge.