Angel Msoffe
JF-Expert Member
- Jun 21, 2011
- 6,781
- 1,657
HAPO SASA? Ubunge wenyewe hajauhalalisha kaongezewa na unaibu waziri, KATIBA MPYA INAHITAJIKA HARAKA SANAHuyu ni Mbunge elect.........hakuapishwa, lakini alipewa unaibu waziri!!!
HAPO SASA? Ubunge wenyewe hajauhalalisha kaongezewa na unaibu waziri, KATIBA MPYA INAHITAJIKA HARAKA SANAHuyu ni Mbunge elect.........hakuapishwa, lakini alipewa unaibu waziri!!!
"Mmiliki" halisi wa Jimbo hili ni Lowasa akisaidiwa na Mzee Jackson Kaaya. Unaiona shughuli ilivyo pevu. Hapa kumsukuma mlevi hakupo. CHADEMA ilipata kura hizi Igunga baada ya "mmiliki" wa Jimbo lile, RA, kususa.
Hakuna wa kudumu -dunia mapito. Ngoja wanaoutamani ubunge wajipange kwa kuanzia kwa kalimanzira. Ole wao. Tupokezane vijiti hivyo
Mwanakijiji tujulishe kama unafahamu kuhusu mbunge kutokuapishwa mara baada ya uchaguzi na kutokuhudhuria vikao mfululizo,sheria zinasemaje?
Ni MBUNGE. Ibara ya 68 ya KATIBA ya JMT inasema hivo. Anaishia tu kumchagua Spika. Ili aendelee na kazi zingine za kibunge inabidi aape kwanza. Ibara ya 71(1) inaainisha mambo yatakayomfanya mtu asiendelee kuwa mbunge. La kuapa halimo.
Wakuu naona bado ni tetesi... Maana kila nikimpigia mtu wa karibu nae hakuna hata mmoja mwenye taarifa za msiba wake ila wanadhibitisha kuwa alikuwa kalazwa MOI. Ebu mwenye tarifa za uhakika atujuze kwa undani zaidi
"Mmiliki" halisi wa Jimbo hili ni Lowasa akisaidiwa na Mzee Jackson Kaaya. Unaiona shughuli ilivyo pevu. Hapa kumsukuma mlevi hakupo. CHADEMA ilipata kura hizi Igunga baada ya "mmiliki" wa Jimbo lile, RA, kususa.
Hivi sheria ikoje mbunge akifa kabla ya kuapishwa? Kunakuwa na by-election au vipi?
Mbunge anatangazwa kuwa ni Mbunge na Msimamiwi wa Uchaguzi wa Jimbo baada ya matokeo yote kukamilishwa. Anapotangazwa pale kuwa "kwa mamlaka .... namtangaza Ndg. x,y kuwa ni Mbunge wa jimbo z" mtu huyo anakuwa Mbunge. Lakini kisahihi zaidi anakuwa Mbunge Mteule kwa maana ya kwamba amechaguliwa na wananchi na tayari ametangazwa kuwa ni mbunge.
Hata hivyo, ili aweze kuanza kutekeleza wajibu wake kama Mbunge ni lazime ale kiapo cha uaminifu - Uaminifu kwa Jamhuri ya Muungano na Katiba. Kazi pekee ambayo ataifanya kabla ya kiapo hicho ni kumchagua Spika kwani Spika anachaguliwa kwanza na wabunge wateule halafu anaapishwa nao na kisha yeye anakuja kuwaapisha wabunge kiapo cha uaminifu.
Hivyo, Sumari alikuwa ni Mbunge- Mbunge Mteule to be precise. Alikuwa na haki nyingine zote za Mbunge na kulipwa mshahara wake kama mbunge na mafao mengine ya kibunge ukiondoa yale ambayo yanatokana na mahudhurio.
Cdm = Nassary Ccm = E. Kaaya.
Kama Spika hatakuwa na taarifa ya kutokuwepo kwake. Mzee Sumari ilifahamika ni mgonjwa na pengine ilijulikana hatapona. Katiba yetu ina mapungufu mengi tu. Inataja ugonjwa wa AKILI tu ndio unaomwondolea mtu sifa ya kuwa Mbunge ibara ya 67( 2)(b).kuna kile kifungu cha kutohudhuria mikutano mitatu mfululizo.... nadhan kikatiba Sumari si mbunge (existence???)
"Mmiliki" halisi wa Jimbo hili ni Lowasa akisaidiwa na Mzee Jackson Kaaya. Unaiona shughuli ilivyo pevu. Hapa kumsukuma mlevi hakupo. CHADEMA ilipata kura hizi Igunga baada ya "mmiliki" wa Jimbo lile, RA, kususa.