Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis Kigwangalla ,ni kiongozi mchapakazi sana kuanzia jimboni mwake na anahisimamia vizuri serkalini pale inapokesea lakin kwa hili linaloendelea katika Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Nzega mkoani Tabora tayari kumemjadili Dk Kigwangalla katika vikao vyake vya Kamati za Usalama na Maadili na Kamati ya Siasa, kuhusu kile kinachodaiwa kuwa ni utovu wa nidhamu wa mbunge huyo ni dalili mbaya za kumpoteza katika harakati zake za kuwasaidia wananchi.
Kupitia mitandao hiyo Dk Kigangwalla aliandika: "Nimepokea taarifa kuwa madiwani walioungana na wananchi wa Nzega pamoja na mimi kupinga uamuzi wa Baraza la Madiwani kuzigawa pesa kwenye Kata wameadhibiwa na Kamati ya Siasa ya Chama Wilaya ya Nzega, bila kusikilizwa na ilhali miongoni mwa ‘mahakimu' hawa ni watu waliokuwa wakilalamikiwa na madiwani na wananchi. "Mbunge huyo aliongeza: "Nimepewa taarifa kuwa mapendekezo ya adhabu dhidi yangu kutoka wilayani kwenda vikao vya juu, ...tena bila kusikilizwa maana nilitoa udhuru, ni kuwa ninyang'anywe kadi ya uanachama wa CCM. Nimeshangazwa sana na kusikitishwa na jinsi chama kinavyoendeshwa Nzega."Mbunge huyo alisema anaamini viongozi wakuu wa CCM wanafuatilia kwa karibu suala hilo na watachukua hatua stahiki, huku akisema hatahudhuria tena kikao chochote cha CCM wilayani humo.
"Kama chama hiki kimefika huku, kwamba kuna watu wana nguvu kuliko chama, kwamba wachache wanaweza kuwaonea wengine kwa kuwa wana vyeo na mamlaka ya kufanya hivyo na hakuna wa kuingilia kati na kusema ‘no', basi sina haja ya kuendelea kupambana," aliongeza.
Aliendelea: "Nimechoka, sintokata rufaa wala sintolalamika tena. Watekeleze hukumu hiyo. Sintojitetea na sintohudhuria kikao chochote kile kuanzia sasa, nimechoka kupambana na watu wenye nguvu, nimechoka. Ni bora kuwa mnyonge, lakini ukabaki na uhai, uzima, heshima na furaha yako".
"" NAMSHAURI MBUNGE HUYU MACHACHARI NA MPENDA HAKI NA MAENDELEO KWA WANANCHI WAKE ASOME ALAMA ZA NYAKATI NA AFANYE MAAMUZI SAHIHI YA KUJIUNGA NA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) SABABU HUKO NDIO KUNA WAPIGANIA HAKI ZA WANANCHI NA WAPENDA MAENDELEO.