Mbunge Hamis Kigwangalla hatarini kuvuliwa uanachama CCM

Mbunge Hamis Kigwangalla hatarini kuvuliwa uanachama CCM

Source: Facebook page ya Dr. H.K.

Hamisi Kigwangalla

Nimepokea taarifa kuwa Madiwani walioungana na wananchi wa Nzega pamoja na mimi kupinga uamuzi wa Baraza la Madiwani kuzigawa pesa kwenye Kata wameadhibiwa na Kamati ya Siasa ya Chama Wilaya ya Nzega, bila kusikilizwa na ilhali miongoni mwa 'mahakimu' hawa ni watu waliokuwa wakilalamikiwa na madiwani na wananchi.

Nimepewa taarifa kuwa mapendekezo ya adhabu dhidi yangu kutoka wilayani kwenda vikao vya juu, ...tena bila kusikilizwa maana nilitoa udhuru, ni kuwa ninyang'anywe kadi ya uanachama wa CCM! Nimeshangazwa sana na kusikitishwa na jinsi Chama kinavyoendeshwa Nzega.

Ninaamini Viongozi wakuu wa Chama wanafuatilia kwa ukaribu na watachukua hatua stahiki. Kama chama hiki kimefika huku, kwamba kuna watu wana nguvu kuliko Chama, kwamba wachache wanaweza kuwaonea wengine kwa kuwa wana vyeo na mamlaka ya kufanya hivyo, na hakuna wa kuingilia kati na kusema 'no', basi sina haja ya kuendelea kupambana. Nimechoka, sintokata rufaa wala sintolalamika tena! Watekeleze hukumu hiyo.

Sintojitetea na sintohudhuria kikao chochote kile kuanzia sasa. Nimechoka kupambana na watu wenye nguvu, nimechoka. Ni bora kuwa mnyonge lakini ukabaki na uhai, uzima, heshima na furaha yako
 
Kutoka kitabu uso ya mbunge wa Nzega:

Nimepokea taarifa kuwa Madiwani walioungana na wananchi wa Nzega pamoja na mimi kupinga uamuzi wa Baraza la Madiwani kuzigawa pesa kwenye Kata wameadhibiwa na Kamati ya Siasa ya Chama Wilaya ya Nzega, bila kusikilizwa na ilhali miongoni mwa 'mahakimu' hawa ni watu waliokuwa wakilalamikiwa na madiwani na wananchi. Nimepewa taarifa kuwa mapendekezo ya adhabu dhidi yangu kutoka wilayani kwenda vikao vya juu, ...tena bila kusikilizwa maana nilitoa udhuru, ni kuwa ninyang'anywe kadi ya uanachama wa CCM! Nimeshangazwa sana na kusikitishwa na jinsi Chama kinavyoendeshwa Nzega. Ninaamini Viongozi wakuu wa Chama wanafuatilia kwa ukaribu na watachukua hatua stahiki. Kama chama hiki kimefika huku, kwamba kuna watu wana nguvu kuliko Chama, kwamba wachache wanaweza kuwaonea wengine kwa kuwa wana vyeo na mamlaka ya kufanya hivyo, na hakuna wa kuingilia kati na kusema 'no', basi sina haja ya kuendelea kupambana. Nimechoka, sintokata rufaa wala sintolalamika tena! Watekeleze hukumu hiyo. Sintojitetea na sintohudhuria kikao chochote kile kuanzia sasa. Nimechoka kupambana na watu wenye nguvu, nimechoka. Ni bora kuwa mnyonge lakini ukabaki na uhai, uzima, heshima na furaha yako.

Mimi ni Mfanyakazi wa H/shauri ya nzega huyu jamaa ni muongo na mpotoshaji Magamba wamemshughulikia kwakua alisema CCM ni Mzigo na Madiwani aw CCM nzg ni Mizigo ya Mavi,na 2010 wana nzega mjini mlifanya maamuzi sahihi kumpa kura Dk slaa Urais,ubunge mkanipa mm,udiwani Cuf hiki chama ni Mzigo.Hamna cha haki na hii kauli viongozi wetu walimtaka aseme haya alipokuja kuomba CDM na CUF wamsaidie kuandaa mkutano wa hadhara na yakifanywa maandamano mpaka kwa DC Baada ya Full council kupiga chini miradi alioleta akitaka ifanywe.Labda niwaeleze kwa ufupi.

Makamanda huyu gamba asipotoshe na Kutafuta Huruma,alileta miradi Yake Magamba wenzie wakamkatalia,na Mgogoro huu ni 2bn za mgodi Anaataka kuzilamba kwa kuanzisha miradi ya kuagiza Catappilar na Gari ya kuchimba visima kupitia kampuni Yake,Madiwani wakamgomea,Akaleta wazo la kuanzisha Benki ili kukopesha wananchi akaipa Jina Benki ya wananchi we nzg ,,Madiwani wakamkatalia wakadai hata wakianzisha Benki kwa Huo Maji bado itasismamiwa na Taratibu za kibenki na RIBA itakua sawa na Benki zingine wakamgomea . Hapa nzg huyu jamaa wanavutana na Bashe na Yule msomali anaangalia makosa ya huyu jamaa,Inasemekana Huko kwao Magambani alipoleta hoja ya Benki,Catappilar ,Gari la kuchimba kisima na kutembelea Ziara ya mafunzo Yule Msomali akawapiga shule Madiwani juu ya hii miradi akawaambia Ilani Yao haijatekelezeka na 2015 ktk kata zenu Hamna,zahanati,nyumba za waalim,maabara,Madawati,barabara,na mwaka huu shule msingi ya Mwisho kitaifa imetokea nzg,na mwanafunzi wa Mwisho katoka nzg pelekeni hizi fedha kuetekeleza Ilani ya uchaguzi hii miradi haina maslahi Benki haitawasaidia.na ili kuanzisha Benki ya aina hii lazima wananchi wanunue hisa Je mko tayari?na haya magari na Catappilar mbunge anaigiza kwa kampuni Yake wakstuka na kukubaliana na hoja hizo.

Pia kuna ishue ingineKigwa alitaka kupiga Dili Yake kupitia RIBA waliopata kwa kuziweka fedha Benki hizo 2bn Mkurugenzi akagomaMadiwani inasemekana walitaka kupitisha mradi Benki,Catappilar,na gari kuchimba Visima,na ziara ya kutembea Dodoma,Kilimanjaro,na Njombe ambayo ingetumia zaidi ya 80m. Sasa baadae wakambadilikia Wakasema hii miradi haina maslahi kwa Watu,fedha za ziara zitumike kulipa Motisha wauguzi na waalimu wanafanya kazi vijijini sana(Remote area) halafu hizo pesa 2bn ziende kujenga Nyumba za waalim,zahanati,na kuweka Umeme aw Solar ktk mashule na kuchimba Visima,Haya makatapila,na gari la kuchimba Visima yakija hapa yataleta Ufisadi na ukiritimba na hakuna wataalam wa kuyasimamia.Pia haiwezekani Kampuni ya Mbunge itumike kuagiza.

Swala Benki itaendeshwa kwa misingi na sheria za Fedha zinazosimamiwa na BOT na RIBA haitakuwa nafuu,hakuna wataalam,wananchi Kama kukopesha Council inatenga Kila mwaka asilimia 10 za Mapato zinakopeshwa hazirudishwi,na wananchi pia wananchi wanatakiwa kuchangia hii itatuletea Ufisadi Huko mbele,tulishindwa kusimamia Mabilioni ya JK itakua Benki?Baada ya Madiwani kubadilika jamaa akaandaa mkutano aw hadhara na Maandamano ktk Huo mkutano aliomba Nguvu ya Umma viongozi wetu wakampa Masharti jamaa atakubaliana basi mkutano ukafanyika yeye Ana agenda zake na Makamanda agenda kuishugulikia CCM ,akatangaza chama Mzigo,Madiwani Mizigo ya Mavi isiyokuwa waliomuunga mkono Madiwani watatu,maandamano na mnajua sisi makamanda maandamano ni Kama Maji Akapewa mabango kumshughulikia Katibu aw CCM,mwenyekiti wa CCM kuwa wote Mizigo wanamsaidia Bashe.

Hapa alishika Sharubu za Chama chake kwa kuwasifia wananchi kumnyima Kura Jk 2010 na pia kuwaita madiwani Mizigo ya Mavi na mwenyekiti aw CCM nzg na Katibu kuwa hawafai,jamaa wakamshughulikia inasemekana wameamua kumchukua Kadi Yao, Ila huyu jamaa is mkweli hata kidogo Aliwahi kuwaambia wananchi tunaenda kufunga mgodi aw resolute Watu wakaandamana kufika badala ya Kwenda resolute akaenda kufunga mgodi aw Mzawa sehemu inaitwa ISUNGA,akampiga kesi iPo Mahakama ya hapa nzg,Jamaa aliwakopa wananchi Pamba akawapa mbegu feki angalau sasa hivi wamekuja Wafanyabiashara aw shinyanga Anaitwa GAKI ndo kidogo amewaokoa wananchi aw hapa anawalipa kwa Wakati na jamaa kutoka singida,huyu jamaa aliwatapeli wananchi akawacheleweshea malipo na kwa halii hii hapa makamanda mabadiliko yamekaribia jamaa kavurunda sana hapa nzg,na sisi CDM na CUF tumekubalina tunamtumia yeye kuimaliza CCM,viongozi wenzie hapa wanaamini jamaa ni mtu wa JK na Mama Salma alivopata ubunge,alivomuondoa Mkurugenzi aliegoma kupiga nae Dili Jk kuja mkutano wa hadhara jamaa akasema huyu DED hafai aondoke Dhaifu nae kamuondoa.

Makamanda hapa huyu jamaa msaniii anatafuta Huruma
 
Chochea kuni, chochea kuni, washa moto wa mafarakano katika Chama Cha Mizigo!
 
ccm yenyewe imechoka hivyo afu imvue uanachama dokta vitumbua...!? thubutu yao..
 
ni CHADEMA tu ndo haichokagi!

Mimi nilitegemea ni mtu kama Shonza au Mwampamba ambao wameingia huko juzi juzi tu ndo walalamike kwasababu hawaijui CCM vizuri, lakini inapotokea mtu kama huyu Said Bagaile ambaye yupo huko miaka mingi kujifanya ndio anakijua CCM leo! Lazima atakuwa na matatizo ya Ubongo. Ina maana yooote tunayozungumzaga humu kuhusu hicho chama cha Mizigo, yeye antena ya akili yake ilikuwa haiyakamati tu?
 
Swaga zetu Mhs Hamisi hawezi hama kirahisi, anabanwa na deni
2billion toka MaCCM!!
Amemaliza kulipa??
 
Last edited by a moderator:
yaani pesa ziende katani zikatafunwe,ccm majanga jamani,wao wanawaza jinsi ya kutafuna tu sio mae deleo kwa vizazi vijazo,
pambana nao kigwangala,hao ni mafisadi wenzio ukoo wenu wa ccm kila mtu ni fisadi.
 
Hahahaaaaa! Kwikwiiiiii! Huhuhuuuu! Huyu jamaa aliye weka hii post nadhani ni mganga wa kienyeji kama mchawi, yaan huu ni wakati wa kulilia kubaki ccm badala ya kumshukuru mungu kwa kumwondoa kwenye dimbwi la majanga. Ccm hatariiiii, weka mbali na watoto.

Kigwangalla wewe ni msomi tena daktari wa binadamu sasa mbona una lia lia badala ya kuchukua hatua? Achia ngazi ukafanye kazi ulio somea siasa itakufanya ufe kwa stress kutokana na majungu. Chama chako kimesha fariki labda ulikuwa hujui wewe tu kuwa mtumbwi ulisha zama zamani. Kila mtu anajinasua ajiokoe mwenyewe sasa nani atakusaidia kaka kigwangalla? Unaodhani watakusaidia nao wana lalama kila siku majukwaani, sasa who can help u my brother?
 
tangu alipotoswa uwaziri wa afya hata ule wa kutokea benchi , kama kadata vile !
 
Chochea kuni, chochea kuni, chochea moto wa mafarakano katika Chama Cha Mizigo! Napata raha katika roho!
 
Hii habari itakuwa ni ya uongo, maana sisi hatuna migogoro ndani ya chama chetu.
 
Hamisi yuko sahihi this time around, hayo mapendekezo ya kuanzia bank pamoja na hiyo construction company yana tija zaidi ya kuzitapanya hizo pesa kwenye kata, hao wanaotaka zitapanywe wanataka wakazile hizo pesa.

Shime shime. Operation Pamoja Daima iende nzega kumsaidia Hamisi katika hilo.
 
Hii habari itakuwa ni ya uongo, maana sisi hatuna migogoro ndani ya chama chetu.

wewe gamba wewe usiwafanye watu ni vipofu na ni viziwi! Wewe kwako moto unawaka na moshi unafuka halafu uanasema hakuna moto??? Ila ndo tatizo lenu watu wa chama cha mashetani hamsikii wala hamuoni! Kwishney
 
Mbunge wa Nzega (CCM), Dk Hamis Kigwangalla ,ni kiongozi mchapakazi sana kuanzia jimboni mwake na anahisimamia vizuri serkalini pale inapokesea lakin kwa hili linaloendelea katika Uongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Nzega mkoani Tabora tayari kumemjadili Dk Kigwangalla katika vikao vyake vya Kamati za Usalama na Maadili na Kamati ya Siasa, kuhusu kile kinachodaiwa kuwa ni utovu wa nidhamu wa mbunge huyo ni dalili mbaya za kumpoteza katika harakati zake za kuwasaidia wananchi.
Kupitia mitandao hiyo Dk Kigangwalla aliandika: “Nimepokea taarifa kuwa madiwani walioungana na wananchi wa Nzega pamoja na mimi kupinga uamuzi wa Baraza la Madiwani kuzigawa pesa kwenye Kata wameadhibiwa na Kamati ya Siasa ya Chama Wilaya ya Nzega, bila kusikilizwa na ilhali miongoni mwa ‘mahakimu’ hawa ni watu waliokuwa wakilalamikiwa na madiwani na wananchi. “
Mbunge huyo aliongeza: “Nimepewa taarifa kuwa mapendekezo ya adhabu dhidi yangu kutoka wilayani kwenda vikao vya juu, ...tena bila kusikilizwa maana nilitoa udhuru, ni kuwa ninyang’anywe kadi ya uanachama wa CCM. Nimeshangazwa sana na kusikitishwa na jinsi chama kinavyoendeshwa Nzega.”Mbunge huyo alisema anaamini viongozi wakuu wa CCM wanafuatilia kwa karibu suala hilo na watachukua hatua stahiki, huku akisema hatahudhuria tena kikao chochote cha CCM wilayani humo.

“Kama chama hiki kimefika huku, kwamba kuna watu wana nguvu kuliko chama, kwamba wachache wanaweza kuwaonea wengine kwa kuwa wana vyeo na mamlaka ya kufanya hivyo na hakuna wa kuingilia kati na kusema ‘no’, basi sina haja ya kuendelea kupambana,” aliongeza.

Aliendelea: “Nimechoka, sintokata rufaa wala sintolalamika tena. Watekeleze hukumu hiyo. Sintojitetea na sintohudhuria kikao chochote kile kuanzia sasa, nimechoka kupambana na watu wenye nguvu, nimechoka. Ni bora kuwa mnyonge, lakini ukabaki na uhai, uzima, heshima na furaha yako”
.
"" NAMSHAURI MBUNGE HUYU MACHACHARI NA MPENDA HAKI NA MAENDELEO KWA WANANCHI WAKE ASOME ALAMA ZA NYAKATI NA AFANYE MAAMUZI SAHIHI YA KUJIUNGA NA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) SABABU HUKO NDIO KUNA WAPIGANIA HAKI ZA WANANCHI NA WAPENDA MAENDELEO.
 

Attachments

  • kigwangala+clip.jpg
    kigwangala+clip.jpg
    20.5 KB · Views: 286
Hamisi yuko sahihi this time around, hayo mapendekezo ya kuanzia bank pamoja na hiyo construction company yana tija zaidi ya kuzitapanya hizo pesa kwenye kata, hao wanaotaka zitapanywe wanataka wakazile hizo pesa.

Shime shime. Operation Pamoja Daima iende nzega kumsaidia Hamisi katika hilo.

hatuna muda wa kusaidia magamba sisi zaidi ya kuyang'oa na kuayweka pembeni,yaani ukamwongezee silaha adui yako?? Acha afe kivyake na piiiipoz itapita kiulainiii,si mlitufanyia uhuni igunga?? Ngoja sasa!
 
Back
Top Bottom