Mbunge Abood alaani vikali ukatili uliofanywa dhidi ya mama mjasiliamali

Oct 8, 2023
37
17
MBUNGE WA JIMBO LA MOROGORO MJINI ALAANI VIKALI UKATILI ULIOFANYWA DHIDI YA MAMA MJASILIAMALI.

Mhe. Abdulaziz M. Abood Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini mapema hii leo amefika wodini Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro alipolazwa Mama Bi Aziza Juma Mjasiliamali ndogondogo mara baada ya kushushiwa kichapo kikali na wanaosadikika kuwa ni Mgambo wa Manispaa ya Morogoro

Mhe Mbunge ameeleza masikitiko yake makubwa na kulaani Vikali kitendo hicho cha Ukatili kilichofanywa dhidi ya huyo mama ambaye anaangaika kupata chochote kwa ajili ya familia yake, aidha ameahidi kulisimamia ili haki yake ipatikane sheria ichukuwe mkondo wake dhidi ya wahusika na hata kuzuia matukio ya kikatili kama hayo kutokea tena katika Jimbo la Morogoro Mjini sambamba na hilo Mhe. Mbunge amelipa gharama zake za Matibabu.

Vilevile Mhe. Mbunge akiwa Hospitalini hapo amefika wodini walipolazwa Majeruhi wengi waliochalangwa mapanga na kikundi kinachosadikika kuwa ni panya road Kata ya Lukobe, sambamba na kugharamia matibabu yao uku akilaani kitendo hicho na kuomba mamlaka husika kuhakikisha Usalama wa Wananchi unawekewa jicho la ukaribu zaidi.
IMG-20231115-WA1183.jpg
 
Hii inawapa nguvu wakiona wanajeshi wanapiga, Polisi wanapiga, Waalimu wanapiga na hata viongozi wengine tumeona wanapiga viboko watu

Sasa hii ya kupiga mmeichukua kwa mkoloni na mkaiweka kisheria zaidi
Mmekataa kuacha kuchapa watoto sasa itabidi mkatae yote
Hakuna utetezi wa upande mmoja
Wajeda waache mara moja na sheria ipitishwe kwa wote la sivyo huko Mali Asili mtauwawa kwa kipogo pia

Hizi ni Baraka za serikali na msibishe maana hakuna mtu anaweza kuvunja sheria hivyo
 
Pole sana Mhanga, adhabu isiishie kwa mgambo tu iende mpaka kwa maboss wao wote
 
Halafu utasikia jitu limevimbiwa maharage huko linaimba SISIEMU namba wani na limevaa kofia na tisheti ya rangi za kijani/njano. Ni muendelezo wa yaleyale maonevu ya kila siku kama yule mama aliyefungwa miaka 22 kwa kukutwa na mshikaki wa nyama ya swala wakati yule bosi wa ATCL aliyeisababishia serikali hasara ya billion 71 kafungwa miaka 5 tu. Hii ni kwa sababu ya mfumo wa hiki chama chakavu.
 
Wajeda waache mara moja na sheria ipitishwe kwa wote la sivyo huko Mali Asili mtauwawa kwa kipogo pia

Hizi ni Baraka za serikali na msibishe maana hakuna mtu anaweza kuvunja sheria hivyo
Hii inatokana na serikali yenye watendaji na viongozi fake wasio na ubunifu katika kutenda kazi zao, nguvu zaidi akili robo
 
Back
Top Bottom