Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Tafiti: Nafikiri quartz ameshakupa list, endelea na hesabu zako, then njoo na conclusion.

Kuhusu kujua mahusiano uliyoyataja, nilikuwa najua kuwa Lilian Mbowe ni mtoto wa mzee Mtei. Ila kwamba Grace amewahi kuwa girl friend wa Freeman hiyo kwa kweli nilikuwa sijui na sidhani kama ni muhimu nijue. Tukiamua kufuatilia nani alikuwa girl friend wa nani itatuchosha mno na haitatusaidia katika kutafuta mustkabali wa nchi kama ulivyosema. Kama ni utafiti, huu wa kutafiti ma-girl friend na ma-boy friend wa watu hauna manufaa japokuwa unaweza kuwa ni utafti pia!

Kuhusu kwamba kwa kuwa Mbowe wana uhusiano na Mtei basi atakuwa alipewa tu hayo madaraka, mimi siamini hivyo maana kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA, mwenyekiti huchaguliwa na Mkutano Mkuu wa CHADEMA wenye wajumbe zaidi ya 1000. Sasa kama Mtei aliwashawishi wote hawa au wote ni ndugu zake Mtei, kwa kweli sina jibu. Ninachojua kwa fika ni kwamba Bwana Mbowe alichaguliwa kwa kura na kwa kweli mpaka sasa ameimudu kazi yake vizuri. Hata hapa kwenye forum kwamba tunaijadili CHADEMA na sio TLP, NLD, PPT au chama kingine cha upinzani ni matunda ya Mbowe. Ninajua pia kwamba katika ahadi zake Kikwete aliahidi kuona CHADEMA inakufa come 2010 kama NCCR ilivyokufa! Hiyo inaashiria jinsi joto la CHADEMA linavyoogopwa na utawala. Kazi yangu kama mwanachama mwaminifu wa CHADEMA ni kuchangia katika kuona kuwa ndoto za Kikwete hazitimii.

Next time nitaeleza msingi wa undugu huo kama mwanachama tu wa CHADEMA na wala sio msimamo wa CHADEMA. This needs time and I will come back soon.
 
DR.WHO.
UTAUA NDUGU YANGU. Chairman katoroka, vipi Mnyika? nae ndio maana kawa mtoro kumbe anaiga kwa mwenyekiti?

poleni mwanasiasa chama cha wajinga.
tuambie hiyo flexibility uliyowadanganya wanaforum au umekuwa kama Jasusi kwa uongo/
 
Ndugu yangu chinga, labda nikwambie tu kuwa kuingia kwangu CHADEMA sio ajali. Nimeingia nikijua nitachokifanya kwa mapenzi yangu na akili zangu zote. Kila mtu akijiunga katika chama cha siasa ana malengo yake. Malengo yangu ya kuingia siasa siku zote sio kutafuta cheo au chakula kama unavyofikiria. Kama ni kazi niliyo nayo inatosha na ninaipenda sana.

Nipo katika siasa na katika CHADEMA nikiamini kile CHADEMA inafuata na muhimu zaidi CHADEMA inanipa jukwaa la kutoa mawazo yangu ya kisiasa katika kuchangia maendeleo ya nchi yangu. Kwa hiyo kwamba mimi na Mnyika tunashika pembe ni mawazo ya ki-ccm. Ni katika ccm mnakoamini kuwa kukaa katika chama cha siasa lazima upate cheo. Nasisitiza umuhimu wa chama cha siasa kwangu ni kunipatia jukwaa la kutoa mawazo yangu sio vinginevyo.

Yakitokea mengineyo ni by the way. Kwa sasa hivi in so far as Tanzania is concerned, CHADEMA ndicho chama kinachoweza kunipatia hilo jukwaa na sijaona chama kingine.

Mwisho, achana na kuita watu wanashika pepmbe. Hizo ni dharau na sio vizuri watu wazima kudharauliana. Nakushauri tena jaribu mara zote ku-focus katika hoja badala ya pua za watu. Itakusaidia sana sio katika forum hii bali katika mahusiano na watu pia. Halafu achana na kujifanya unanijua sana. Hatupo hapa kuonesha nani anamjua nani. Kuna watu wengi wanawajua watu humu ndani, lakini hapa ni hoja tu.

Tuliamua kutumia pen names ili tukate issue na sio vinginevyo. Kama unanijua hiyo sio hoja hapa. Wengine pia wananijua nami nawajua, But so what!?
 
Chinga,
Muongo ni wewe.Hapa tunafahamishana na kuelimishana. Sio kusutana kama ulivyo wewe. Lakini karibuni uongo wako utakutokea puani!
 
Chinga,
Starehe za burudani hua zinavuta sana!.. mimi binadamu na nadhani ktk maelezo yangu umepata moja la maana.

Sasa hivi umeanza kutupa mavitu!...haya ndiyo maswala hizo habari za Chifupa hazina uzito, isipokuwa uzito upo hapa kwenye haya mawe unayorusha. Hizi ndizo hoja ambazo hata sisi akina yakhe zinatupa mwanga na kuanza kujiuuliza Mhhhhh!.... what's going on?

Natumaini Freeman mwenyewe ataweza kutupa ukweli maanake hapa sasa inachanganya. Wengi wentu tupo huku majuu na tunafahamu huu ni wakati wa mitihani, kila umjuaye yuko busy ile mbaya inakuwaje mwenyekiti wetu awe Bongo?...

Hilo la Family businesi ni another issue ambayo tunahitaji majibu kama kweli Chadema ni chama cha wananchi.

Sasa Chinga upo ktk right direction...
 
Mwanasiasa,
Asante kwa hili la kumtaka Chinga aachane na kujifanya anawajua watu sana. Mimi keshanishikilia kwenye kundi anakotoka Nyirabu ingawa mimi hata kule Tarime sijawahi kufika.

Tumulike issues na kutoa hoja si kujifanya tunajua huyu na yule. Kama ningetaka kujulikana si ningeandika jina langu halisi kama alivyofanya Mwalimu Moshi?
 
chinga,
kwa jinsi watu wanavyokupinga inaonyesha dhahiri watu wamechoshwa na propaganda za ccm na wanataka mabadiliko, unaweza kuona wewe ndio unawakilisha wana ccm humu na mawazo yako ni yale yale. na hatari zaidi hata serikalini wamejaa watu kama wewe,ndio maana tunaletewa mikataba ya aibu kama ya Richmond na IPTL, unategemea maendeleo tutapata lini?

kwa taarifa yako wimbi la vijana wanaojiunga na chadema hivi sasa ni moto wa kuotea mbali, na mfano unaona jisni mwanasiasa anavokujibu hoja zako kisayansi.
 
Quarz
Ukifuatilia maelezo au maswali ya chinga, sidhani kama ina uhusiano sana na mashambulizi kutoka ccm. Na yeye kuna mahali fulani kakataa. I may agree with him on that.

Badala yake inaonekana ana usongo fulani na Chadema au Freeman. He is free on that as well.
 
Quarz.
Mwanasiasa hakuna chama alichobakiza, hapo kaja mara moja bado yuko safarini.

kama napingwa huoni hoja zinaibuka mbali mbali? za kina Grace kwelu n.k
hao vijana wanaokuja huko wana shule? au wakija huko mnawatorosha shule kama kwa Mnyika?

Mnyika kabla ya chadema alikuwa na maendeleo na moyo wa shule kuja masikani ya wajinga naye kajibweteka.

Mrudishe mwenyekiti wako shuleni, then uje kwangu,
unasema mimi mwana ccm naomba unitajie ni kadi namba ngapi ninamiliki?

ukweli unazidi kudhihiri kama ni chama au NGO au saccos na sasa imekuja kujulikana kuwa ni business ya familia fulani.
 
chinga,
wewe unawivu na akina ndesamburo na mbowe,
hawa wamekuwa na pesa zao kabla hata hawajaingia kwenye siasa, na unajua kuna watu kama sisi hatufuati pesa kwenye siasa au chama, bali tunachakalika na maisha kama kawaida, kuingia kwenye siasa ni ile tu kutoridhika na jinsi mambo yanavyokwenda.

sasa watu kama wewe mnaotafuta chakula kupitia siasa kazi mnayo, maana ndio mnatumika kama vibarua,
wewe unamsakama mnyika aende shule wakati mwenzako ni msomi wa chuokikuu sasa unataka shule gani hiyo kama sio mzushi wewe.

tena mnyika kwa style yake ya usomaji na kushiriki na mambo ya jamii ndivyo haswa elimu inavyotakiwa, unatumia moja kwa moja kile ulichojifunza,
mimi ningependa kufahamu wewe elimu yako ikoje ili tukulinganishe na mnyika.

invicible,
hawa jamaa, kwa kujua uwezo wa mbowe kujenga hoja, wakaamua kumkimbiza mapema kwa personal attack na kushusha hadhi ya forum
pia sielewi kwanini mtu kama personal problem na mtu fulani aje kuzihamishia mahali kama hapa, it make no sense to me.
 
Naam Nashukuru mjumbe ulieniletea list ya viongozi, nadhani haijakamilika manake kwa mfano sijaona mwenyekiti bara. Lakini nashukuru kwa efforts.

Sasa mheshimiwa mwanasiasa naona unaendeleza political manipulation yako kwa kuja na superficial answers. Nimekuuliza kama ulikuwa unajua hawa niliowataja.

I will let you off on Mbowe/Lilian partnership, vipi kuhusu Lucy Owenya na Grace Kihwelu kuna na mahusiano ya kidugu kabisa na Mzee Ndesamburo?

Ulikuwa unajua hii au umejua sasa?

Hivi huoni tatizo kama kiongozi wa mkoa mmoja nyeti wa CHADEMA kuwa na mtoto wake wa kumzaa,yeye mwenyewe na ex mkwewe wote kuwa wabunge?

Hata mwinyi anaesemwa sana alisubiri kwanza alipoondoka ndio watoto wameanza kuja. Naam na hapa nijibu hii hoja kwa jinsi ninavyoiona.

Mwinyi watoto wake wamekuja long afterwards baada ya baba kuondoka tena ni wa kugombea na kuchaguliwa majimboni/bungeni na wabunge. Ikiwa hoja ya mwanasiasa kwamba haoni tatizo kama Mbowe kuwa ni mkwe wa ex chairman, kwa vile alichaguliwa na wajumbe zaidi ya 1000 wa chadema, hili ni tatizo kwa watoto wa mzee Mwinyi?

Do you really expect Mzee Ndesamburo akitaka lake na Mzee Mtei wajumbe wakataka vinginevyo halafu wazee hawa washindwe?

Samuel Sitta imeshajibiwa...leteni list nami nilete lakini nina mashaka sana na Ndesamburo na watoto wake walivyoprivatise CHADEMA Moshi/K'njaro....

will be back...
 
Mwanasiasa.

Hoja za ma girl friend au personal issue ziko huko chadema, mbona hukukemea watu waliposema Chifupa alikuwa wa fulani na fulani?au kujua msimamo wa rais mtarajiwa juu ya hisia zake dhidi ya ukimwi ni personal issues?

Conservatives walimjadili sana Cameron na tabia yake ya kuvuta bangi siku za nyuma na akakiri kuwa yaliyopita, jee ilikuwa ni personal issues? Lazima tujue maadili ya Mbowe unless hamko serious.

Platform la siasa hata Mrema alikupa pale TLP, lakini ulipoona hakuna kitu ulikimbia, tizama umemaliza vyama vingapi? nadhani umebakiza NLD ya mzee Makaidi tu, jeee huko kote ulikuwa unatafuta paltform au masilahi?

Najua kiswahili kinakusumbua uliza kwa waswahili nini mshika mapembe si matusi ni msemo tu ndugu yangu siwezi kukutukana hapa tunaelimishana.
Asante kwa ushauri wako lakini ungeanza kumshauri Mwenyekiti wako kuacha utoro, ukabila, umajimbo,udini n.k.

Jasusi.

Acha jazba tunashindana kwa hoja na nimekushinda kwa hoja haya mengine hayana maana.
uliongopa Ahmed Rajab yuko London. nikakwambia MUONGO WEYE, jamaa kafukuzwa na ukweli umedhihiri,sasa donge la nini?
 
freeman mbowe kabla ya kuwa mwenyekiti wa chadema alikuwa ni mbunge wa hai, je aliteuliwa na mtei/ndesamburo kushika hiyo nafasi?

ndesambiro mwenyewe ni mbunge wa kuchaguliwa moshi mjini, je ameteuliwa na mtei au alijeteua mwenyewe kushika hiyo nafasi?

wiillbroad slaa ni mbunge wa kuchaguliwa, je aliteuliwa na mtei?
hawa watu kama umeshawahi kuwasikia kwenye majukwaa wakiongea utajua kuwa kinacho waweka kwenye hizo nafasi ni uwezo wao wa kujenga hoja na si undugu kama unavyodai.
 
its getting more interesting as time goes by

na hivi huko Bongo hakuna Umeme

Personally mimi sio mpenzi wa ounch and judy politics lakini hii haimaanishi kuwa viongozi wawe immune kuwa discussed kwa sababu japo kuna watu amabo watabisha lakini leo au kesho huyu FREEMAN MBOWE na CHADEMA wanaweza kuchaguliwa kuwa watawala Tanzania sasa ni vizuri tukawajua hawa jamaa na mambo ambayo wanayoamini

N ahili la uhusiano wa kimapenzi nadhani ni private matters lakini katika jamaiii yetu watu hawalioni hilo na kwa sababu hiyo basi mimi pia nisingependa kuongozwa na mtu ambaye anadeal na ma CRIMINALS ( i will keep this private kwa sababu dossier ya ku back up hili ninayo na sidhani kama humu ni mahala kuliweka ) for simple reasons its not how i operate. Hii haimaanishi kuwa halina wanayofanya hivyo ambao wako serikalini
 
Kwa kweli Watanzania tuna safari ndefu tena sana

Haya kama watanzania wote tulivyo wasomi na wasio wasomi, badala ya kujadili mada tunajadili watu, badala ya kujadili sera tunajadili mahusiano ya watu.

Tangia BCS Times nilikuwa naona hiki kijuwe kama sehemu ya kujadili matatizo na namna ya kuyatafutia ufumbuzi lakini naona tumepoteza mwelekeo.

Chadema iwe NGO, au chama cha siasa, CCM iwe chama cha taifa, jambo muhimu ni je tunaweza kupiga hatua kwa kupitia sehemu hizo kuondokana na maadui watatu wa maendeleo.

Nadhani hamna mtu aliyelazimisha au anayelazimishwa kujiunga na aidha CHADEMA au CCM au chama cho chote kingine bali ni mapenzi ya mtu baada ya kusikiliza na kukubali anachosikia na kuona. Yes, Chadema inaweza kuwa chama chenye chimbuko au kuongozwa na watu kutoka Kaskazini au familia moja, wanaojiunga nacho wanafanya hivyo kwa mapenzi yao. Swala la kujiuliza je undugu au ukaskazini unaolalamikiwa umezuia shughuli za chama au za wabunge na madiwani wa chama kufanya kazi zao, jibu ni hapana.

nadhani tunachofanya hapa pamoja na elimu yetu ni kuwakosea haki waTanganyika na wanachama wa vyama husika kusema eti chama cha siasi ni mradi wa kibiashara wa familia. Nadhani Tanzania tulivyo na ubinafsi kama chama hiki na vyama vingine vingekuwa miradi ya biashara ya familia fulani, sidhani kama wangewachagua wabunge na madiwani kutoka kwenye hivyo vyama.

Ndugu Tafiti, nashukuru sana kwa utafiti wako, fanya hivyo pia kwa wabunge wa kuteuliwa na kuchaguliwa wa vyama vingine hususani CCM kwa sababu ndicho kina wabunge wengi bungeni wa kuchaguliwa na kuteuliwa, halafu angalia pia nafasi za kuteuliwa. Baada ya hivyo leta ulinganisho hapa na wanaforum watajadili na kufikia uamuzi.

Kitu kingine ambacho kimeniacha hou kwenye mada hii ni kitendo cha wanaforum kuamua/kupima maendeleo ya mtu bila kutuambia vipengele walivyotumia. Ni aibu kubwa kwa mtu mwenye akili makini kutoa misemo kama "..alikuwa na maendeleo au anazingatia maendeleo lakini sasa hivi hana maendeleo.." Kila mtu ana maana yake ya maendeleo, na kila mtu anajua yaliyomuhimu kwake kufikia maendeleo anayotoka. Kama hatumpendi mtu au kikundi cha mtu tusitumie kigezo hicho kuwaamulia wengine maendeleo yao.

Kuna valid question ambazo tungependa kujua majibu yake lakini nandhani mfumo tunaotumia wa muulizaji kuuliza na kupendekeza majibu hapo hapo, ni vigumu sana hata kwa Mwendawazimu kujibu maswali kama hayo.

Jambo lingine ni tabia ya watu kuibuka na hoja mpya kabla ya kujibu utata unajitokeza kwenye hoja alizotoa awali. Haitoshi kusema mtu ni mwizi halafu polisi anakuambia nadhani siyo mwizi, wewe badala ya kumweleza polisi huyu ni mwizi kwa sababu hizi na zile, unaibuka na kusema ni mbakaji, ukiambiwa siyo mbakaji badala ya kutetea hoja na vielelezo vyako uanibuka na kusema ni msemaukweli. Kumbe kule BCS Times tulikuwa na vichwa vilivyokwenda shule kweli na tulikuwa serious.

Mzee ES, Sam,Mkandara, et al turudishe ile HESHIMA ambayo iliwafanya mpaka wa USALAMA wakeshe hapa kwani kulikuwa na hoja zenye maana na nzito, hoja ziliwafanya mpaka baadhi ya watu wa usalama wasaliti wakubwa wao na kuingia hapa kumwaga mambo.
 
@Chinga

Hivi huko Southampton University hawana cha kufundisha huko zaidi ya upupu?


Unajua jumapili ya leo nimejifunza mengi sana humu
 
dr who,
kwenu nyinyi watanzania au wabongo kama mnavyojiita, criminal ni yule mtu anaeiba kuku, LAKINI MTU AKIIBA BILIONI MBILI HUYO HAITWI CRIMINAL BALI NI MJANJA NA ANAENDELEA KUTESA,
lakini mtu akiiba kuku, mtatia mafuta ya taa na kumchoma moto.
HATA WALE WALIOLIINGIZA TAIFA KWENYE MKATABA WA IPTL AMBAO TUMELIPA KWAMIAKA KUMI KILA MWEZI ZAIDI YA BILINI 30,HAO KWA TANZANIA SIO CRIMINALS BALI NI VIONGOZI HODARI NDIO MAANA MPAKA LEO WANAENDELEA KUSAINI MIKATABA MINGINE KAMA YA RICHMOND.
 
Quarz.

pole sana usihamaki. naomba majibu ya maswali niliyokuuliza huko nyuma?
siwezi kuwa na wivu wa utajiri wa Mbowe, dada zetu wangapi wamekufa kwa ukimwi pale Mbowe club? ana wauza dada zetu kwa wazungu, huo si utajiri kwangu.

ukinichafua zaidi nitakupa hata file la Benki kuu kuungua, ila umesema tusiende kwenye personal issues,

hakuna anayepinga Alex Massawe (A.M INVESTMENT 1988) nI TAJIRI.
lakini wengi wetu ukisikia utajiri ule ulivyopatikana kwa mtu kama mimi (mmachinga) bora nishinde nazurura barabarani kuzaa bidhaa,

najua kuna watu wa maeneo ya kaskazini ambao huaga kwao, lazima arudi kwao akiwa tajiri hata kwa kutoa roho ya mtu.

Quarz.

Baada ya Alex Massawe kushikiriwa na polisi, jee umeona kuna Benki nyingine imevamiwa?

sina wivu na utajiri usio na source za kueleweka.
 
Q
Naomba usome jibu langu hapo juu kisha utanielewa.

Unajua kwa nini CUF hawawi discussed humu? kwa sababu hawana potential ya kuchukua nchi lakini CHADEMA wanayo na kwa sababu ya mambo kama ya IPTL na RICHMOND ndio maana we have high expectation toka kwa CHADEMA lakini sisi wengine huwa hatufuati tu mkumbo ndio maana tunauliza maswali na kudiscuss issues ambazo kusema kweli CHADEMA wamekubali kuziweka sawa na zingine wamezi dodge sasa haiwezekana wao kuwalaumu wenzao CCM kuwa ma sleaze wakati wenyewe nao wanafanya Sleaze
 
Sasa Ni Mbowe Ndio Aliwauwa Kwa Ukimwi Hao Dada Zako?

Au Ni Kutokana Na Serikali Ya Ccm Kushindwa Kutatua Tatizo La Ajira Na Kusababisha Hao Dada Zako Kujiuza Kwa Hao Wazungu Walioletwa Na Hiyo Serikali

Club Billcanas Ni Club Nzuri Sana, Hata Mimi Niko Huku Majuu Miaka Mingi Bado Sijaona Club Nzuri Kama Ya Billcanas,

Tatizo La Ukimwi Halina Uhusiano Na Club Billcanas, Hilo Ni Tatizo Kwa Afrika Nzima , Kuanzia Afrika Kusini Mpaka Nigeria:
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom