Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
mTz

Nafikiri kwa sababu watu hawataki kusema, hiki ni chama cha wavuta bangi?
 
Mzee Es

heshima yako; WAPUKI ni chama cha wavuta bangi, i.e. Chinga alimfananisha na David Cameron alipokubali kwamba alivuta bangi. therefore there is no way ni lazima kiwe chama cha wavuta bangi kilichokuwa Kibaha.
 
Mzee Quarz nashukuru kwa maelezo yako...
Umenikumbusha Sumaye alivyosema (akiwaambia wafanyabiashara) "ukitaka mambo yako yakunyookee jiunge na CCM."

Nasikia Mzee Ndesa TRA washamshindwa kwani yeye huwalipa kodi yao yote halali na hata baadhi ya maofisa wanapotaka rushwa ili wampunguzie, yeye hukataa!
 
Hili la kuunda chama ambacho kitakubalika kitaifa ni gumu sana - kwa sababu tusisahau hata mwalimu alisema opposition itatokana na CCM yenyewe kumeguka. (opposition within CCM) and this is a fact that the majority of CCM supporters are people in rural areas and benefitted in one way or the other in whatever they do today.

NDIO SABABU BAADA YA SOME FACTS AMBAZO ZIMETOKEA HAPA KWENYE FORUM I THINK CHADEMA IS TOO CLOSE TO FAMILY BUSINESS

Kwa hiyo kazi bado ni kubwa.
 
Ndabita,

Ningeomba sana ujaribu kuangalia hoja hizi kwa makini zaidi kwani itakuwa tunacheza karata hapa.

hakuna sehemu nimesema kwamba majina ya vyma ndio hitimisho la malengo yao...Nooway , naelewa hilo na Liberal party ya Australia sijasema wao ni Progressive ama Socialist.

Isipokuwa elewa kwamba unaposema kuwa Chadema wameweza kuwa karibu na Conservative kwa kupitia IDU kwa malengo yaliyo sawa hapo, nadhani utakuwa umeposha ama kutufunga kamba.

Na sababu ya kusema hivi nafahamu kwamba Chadema wamedai kuwa wao hawana malengo ya Ubepari /Mhadharia (kati-kati Kulia) at the same time wanafunga ndoa na Conservative ambao ni Mhadharia...(Kati Kulia), mbali kabisa na huo Uanachama wa IDU.

This is a question!...
Ni sawa na mtu aulize kwa nini CCM wamefunga ndoa na chama tawala cha Korea (WPK).

Hapa unahitaji kuelewa mapana ya swali hilo na sio sababu za kuwa wanachama wa Socialist International na kutoa mifano ya vyama vinginevyo. WPK wanajulikana kwa ukiukaji wa haki za binadamu na wana malengo tofauti sana na baadhi ya vyama vya Kisocialist.

Kifupi swali ni uhusiano kati ya CCM na WPK kwa kuzingatia ubaya wa hawa WPK...Na swala hapa ni hao WPK sio Usocialist ama unachama wa SI - Kwa hiyo chukua mfano huu na uweke kule kwa Chadema na Conservative.
Hoja inakuja kuwa Conservative wa Uingereza na Ujarumani ni vyama ambavyo vilishiriki kikamilifu na bado vinaendelea kutunyanyasa waafrika.

Ukisoma hoja za wengi humu zinawagusa moja kwa moja na matukio ya South Afrika na hata hotuba kama za Botha hawa watu walizikumbatia.
Hawa jamaa walikuwa Conservative kwa maana ya kutnza na kuhifadhi mila zao kama - Wazungu. Mila ambazo zinapingana kabisa na zetu na sisi tunapokuwa Conservative lazima tuwe na malengo ya kuhifadhi yaliyo yetu. UAFRIKA ama Niseme UTANZANIA. Sasa hapa msiwe kama wale wafuga ng'ombe wa kizungu ambao hawana malengo ya kuuza nyama hizo Ulaya bali kubadilisha kabisa mila na tamaduni zetu sisi zifanane na hizo za wazungu.

Mimi binafsi napenda sana kusikia nyie ni Conservative kwa malengo yaleyale lakini wahusika ni Watanzania/waafrika pia sio kuiga yao na kuyalenda ndani mwetu kuondoa kabisa hifadhi ya Mila na Tamaduni zetu ambazo hazina Udini wala Ukabila.

Mwisho, ndugu yangu historia itakuonyesha kuwa vyama vingi vya Conservative vilianzishwa chini ya misingi ya kidini - Kikristu. Na sababu kubwa mbili moja wapo ikiwa kwamba nchi yingi za Ulaya ziliweza kujikomboa (kupata Uhuru wao) kupitia dini hii. Na ya pili ni kwamba Wakristu wengi walishiriki ktk mbinu za kuupinga Usocialist ambao ulikuwa ukipiga vita DINI na UBINAFSI ktk utawala wa nchi.

Hivi majuzi tu ndipo Conservative wanaanza kujitoa ktk udini na kuendesha siasa zao kwa misingi nje ya dini (soko huria na mtu binafsi kumiliki mali). Hata hivyo Ukitazama kwa undani zaidi utaona kuwa kila swala linalohusiana na imani ya dini (kikristu) huwa linapingwa sana na mara nyingi halikubaliki ktk misingi ya Conservative hasa hawa wa Ulaya.

Kwa lugha hii tunaweza kusema hata Waarabu wenye siasa kali wanajiita Conservative kwa maana yao na sio hiyo ya Ulaya. Hii ndiyo mila na Utamaduni wao.

Je, sisi tunapojiita Conservative tuna malengo yapi maana historia yao na yetu hazifanani kabisa. Na vipi tunafunga ndoa na mtu ambaye hatukubaliani kimsingi.
 
KICHUGUU.
wenyewe wapo na hawajasema data zimepotoshwa au umekuwa msemaji wao?

pili.
hata mtu akituma post mia wewe una umia nini? au unataka tulipe? tuko tayari kulipa.

tatu.
unachefuka na mada hizi nani kakulazimisha kusoma? usichokipenda wewe wenzako wanakipenda, na unachokipenda wewe, wenzako tunaona upuuzi. Ukisema wewe huli nguruwe wapo wanaokula. unaumia nini?

nne.
Mada binafsi kwani wewe katika huo mchango wako wa taifa huwa hutaji watu?

Tano.
hivi wewe ni judge wa kutuamulia topik hii inafaa au haifai? nani kakupa uwezo huo? acha udikteta.
 
Both Mbowe and Mwansiasa have dodged my questions...mwanasiasa said i should give him couple of hours but its now over 12 with no answer from him and i hope he is not trying to get notes from JJ who i believe should stick to wring his essays and sort out his grammar as well

If this goes on for another week then its gonna get nasty that it already is
 
DUA,ES.
wote mmekosa endeleni kutafuta maana ya WAPUKI au mtumie PM mzee Mbowe atawafahamisha.
 
KICHUGUU.
wenyewe wapo na hawajasema data zimepotoshwa au umekuwa msemaji wao?
pili.
hata mtu akituma post mia wewe una umia nini? au unataka tulipe? tuko tayari
kulipa.
tatu.
unachefuka na mada hizi nani kakulazimisha kusoma? usichokipenda wewe wenzako wanakipenda, na unachokipenda wewe, wenzako tunaona upuuzi.
Ukisema wewe huli nguruwe wapo wanaokula. unaumia nini?
nne.
Mada binafsi kwani wewe katika huo mchango wako wa taifa huwa hutaji watu?
Tano.
hivi wewe ni judge wa kutuamulia topik hii inafaa au haifai? nani kakupa uwezo huo? acha udikteta.

Mzee Chinga Samahani kama nimekuudhi binafsi kwa sababu naona unanishambulia binafsi vile vile. Maoni yangu ilikuwa ni kwamba topic hii imekosa uelekea kwa sababu baada ya kuwe nimesoma posts zote tangu mwanzo nimekuwa napata mielekeo tofauti tofauti.

Kwa vile nategema kutumia forum kama hii kupata taarifa ambazo hazipatikani magazetini, sikufurahishwa kuona kuwa watu wanaandika taarifa ambazo siyo sahihi bali kwa ushabiki tu kwa vile baadaye imeonekana taarifa hizo zikikanushwa. Hebu jaribu mwenyewe kurudia posts zote ujionee mwenyewe.

In any case, nakuona umewaka moto sana kama vile nimekuingilia katika riziki yako; hapana mzee nakuomba sana radhi na wala usipoteze muda wako kunijibu kwa vile utakuwa unazidi kutoka nje ya mada yako bure tu; wewe chukulia tu kuwa mimi nilikosea njia hapakuwa mahala pangu.
 
KICHUGUU
taarifa gani imekanushwa so far?
Niko kwenye riziki gani ndugu yangu? jee hizi taarifa uliwahi kuzipata magazetini i.e WAPUKI?
kazi njema mheshimiwa.
mie namsubiri Mbowe mzee wa mlima kilimanjaro sio kichuguu.
 
Chinga, nilikuomba usinijibu labda sikuongezea kuwa usiniulize chochote..

Kuhusu swali lako nitatoa mfano mmoja tu kuwa kuna mtu alisema kuwa Mbowe aliwekwa Benki Kuu na baba mkwe wake Edwin Mtei.
Halafu mtu mwingine akaipinga hiyo.

Binafsi nimefuatilia na kuona kuwa siyo kweli kwa sababu ifuatayo hapa chini.

Mtei alikuwa Gavana wa kwanza Tanzania kuanzia 1966 mara baada pesa ya east africa yenye tundu kutoweka wakati huo waziri wa fedha akiwa Amil Jamal. Baada ya hapo alikuwa katibu mkuu wa wizara ya fedha na baadaye waziri wa fedha, kazi aliyomaliza 1979. Baada ya hapo hakuwahi kuwa serikalini tena. Magavana walimrithi ni kama ifuatavyo: Kuanzia 1974-1989 alikuwa Charles Nyirabu, akifuatiwa na Gilman Rutihinda mwaka 1989-1993 ambaye baada ya kifo chake alipokewa na Idris Rashid hadi mwaka 1998 na kumwachia Daudi Balali anayeshikilia hadi sasa.

Ukiweka timeline hiyo ya Mtei kama Gavana wa benki kuu, Katibu Mkuu, hadi Waziri wa Fedha, hakuna nafasi ya yeye kumpachika Mbowe pale benki kuu kwa vile kwanza sidhani kuwa tayari Mbowe alikuwa ameshaoa binti yake kama ilivyosemekana hapa. Mbowe aliyezaliwa mwaka 1961 wakati huo alikuwa ni mtoto mdogo. Kati ya 1966-70 hivi wakati Mtei akiwa Gavana wa BOT, Mbowe alikuwa na umri kati ya miaka 5 hadi 9, halafu kati ya mwaka 1970-1979 wakti akiwa katibu mkuu na waziri wa fedha, Mbowe alikuwa na miaka kati 10 na 18 tu. Asingekuwa amemaliza form 6 na JKT na kumwoa binti wa Mtei na hivyo kuwekwa Benki kuu pale na Mtei. Ndiyo maana nikaona kuwa hapa watu hawasemi ukweli.

Nimeunganisha hapa pesa zote zilizotokea Tanzania katika kipindi cha Mtei na magavana waliozisaini. Mtei alisaini zile za kwanza tu ambazo wengine wenu hamjawahi kuziona, na nyingine chache sana alizosaiani kama waziri wa fedha kwa muda mfupi wa mwaka mmoja na nusu hivi.

Baada ya maelezo hayo, tafadhali nakuomba Chinga usinijubu chochote kwa vile sijauliza kitu na wala usiniulize chochote. Wewe endela na mjadala wako.

Kichuguu cha Jangwani
Shilingikumi1977-1985.jpg
Shilingikumi1972-1977.jpg
ShilingiIshirini1966-1971.jpg
 
Wapuki.......... very interesting, but are U sure of your allegations?

FD
 
Chinga
Mzee Es

Unajua katika ukurasa wa saba suala zima la Elimu nimelielezea kinaga ubaga na upeo wa Mbowe kuwa shule aliyonayo kwa sasa ni kubwa muno hana muda wa kupoteza sana na shule.

Tatizo lilionikwaza nimekuta chinga akikimbia na kurusha risasi bila kuwa na targeti. Inaonekana tangia aanzishe hii story ambayo iliitwa udaku(makandara), Mimi nikaongezea catunio gazeti la mtanzania(Ziro) inaonekana kweli kabisa hajaweza kutulia au kujenga akili yake vizuri amekuwa mtu wa kutanga tanga mpaka amefikia hatua ya kwenda mpaka kibaha. na pia ameonekana kwenda mpaka Hai na kusahau kuwa alikuwa ametoa jibu kuwa suala lake halikuwa na maana yoyote kwa sababu ktk mjadala mzima mpaka sasa hatuna tena chifupa. Kwa ujumla either ibadilishwe na kiwekwe kitu kingine au irekebishwe na kuondoa Chifupa(Tegemeo la CCM)


Generally mada yenyewe inaelekea sasa inamshinda nguvu na kuelekezwa kuonyesha Mbowe alivyobabu kubwa. Hawezi kulinganishwa na kasi mpya hali mpya na Nguvu mpya (udaku mwingine).
 
Dr WHO: swali gani hatujajibu bado? May be hukuridhika na majibu, lakini maswali mengi tumejitahidi kuyajibu. Anyway, remind me which ones have not been answered.
 
Tafiti: Usihangaike kutafuta Makamu Mwenyekiti Bara. Alikuwa ni Kaburu ambao CCM wameshamchukua. Hatujachagua mwingine bado. Lakini Kaburu alikuwa wa Kigoma na sidhani kama alikuwa na mahusiano na akina Mtei.

On a serious note, naanza kuwa na wasiwasi kuwa hizi mada za CHADEMA zina lengo la kututoa ku-focus kwenye kujadili matatizo ya nchi yaliyosabishwa na uongozi dhaifu wa CCM. Maisha bora imegeuka kuwa kitendawili, maisha yanazidi kuwa magumu kwa mwananchi wa kawaida kila kukicha huku viongozi wakijineemesha kwa mikataba feki ya Richmond n.k.

Mkiendelea kutuuliza CHADEMA muwe pia mnatupa majibu ya umeme tapatikana lini, rushwa mtaanza lini kupambana nayo na lini wananchi wataanza kupata maisha bora kama mlivyoaidi.
 
WACHA: wacha wewe, hata kama upeo wako wa kufikiri ni mkubwa huna haki ya kutudharau sisi wenye upeo mdogo. Actually, kwa kutudharau sisi wenye upeo mdogo kinyume chake kinakuwa ni kweli.

Jaribu kuelewa inclination ya mchangiaji vizuri kabla ya kujibu hoja. Kuna wachangiaji ambao bila kutoa katusi mchango wake haujakamilika. Mimi sio miongoni mwao. Kwa hivyo unaponijibu kwa kuweka na vitusi unakuwa umelenga silaha pasipokwenyewe.

Chinga: nilishakushauri ndugu yangu achana na habari zangu binafsi. Nani kakwambia nipo Southampton. Mahala nilipo mimi hapakuhusu. Wewe komalia hoja yangu tu. Umeonesha jinsi ulivyo kwa kusema kuwa kozi ninayesomea ni zile za kibwege.

Huna haki ya kuchagulia watu kozi gani ni bwege na ipi sio bwege. Wewe sio muajiri wangu.
 
Kakindomaster

I expected more from page seven on education but you left a lot of questions to be answered by mbowe – is this correct?
 
Kwako Dua

Ushauri wangu kama anataka degree(moja inamtosha kulingana na upeo wake) tayari anauwezo wa kuitwa mtu aliyesoma.

naomba kuwasilisha
 
Kakindomaster


Hoja 2: Elimu

(a)Si wote wana elimu ya kidato cha sita. Hapa siongelei mambo ya kufaulu au kushindwa. Kuendana na record kutoka source nilizotaja hapo mwanzo ni kwamba Freeman Mbowe ana Stashahada ya Elimu. Mpaka sasa hivi sijafanikiwa kupata majibu kamili kutoka NECTA kama Mbowe alisomea hiyo stashahada baada ya Form Four au Form six, kwani wale wa miaka ya nyuma mtakumbuka kwenda kusomea ualimu uliweza kufanya baada ya kidato cha nne au cha sita. Pia kwa sasa siwezi kutaja shule na chuo alichosomea kwani sijathibitisha kutoka kwa mamla husika au shule.
Nadhani Mbowe mwenyewe ndiye anaweza kuondoa utata huu wakati tunasubiri NECTA watumwagie vitu.

b) Huwezi kulinganisha uelewa wa Mbowe na Chifupa, hata mtu mwenye akili makini hawezi kumlinganisha mtu aliyewahi kuajiriwa na Bank na mtu ambaye hakuweza kuajiri na vyombo vya Uandishi wa habari pamoja na Diploma yake uandishi wa habari (sijui kutoka chuo gani). Ijapokuwa ni fani tofauti lakini ukijaribu kulinganisha sidhani kuna mlinganyo.

c) Kuhusu mbowe kusomea shahada mbili kutoka vyuo tofauti hilo siyo swala geni hata kidogo. Usilinganishe Tanzania ambako mtu huwezi kufanya shada mbili kutoka vyuo tofauti, mfano Open University na Mlimani. Binafsi nikiwa nafanya shahada yangu nje, nilikuwa nafanya vyuo viwili tofauti katika miji tofauti, kuna kitu kinaitwa "interdisciplinary studies". hapa vyuo vina makubaliano na vyuo vingine ili kusimamia program ambazo hazipo chuoni kwao, lakini ni sehemu ya degree ya mwanafunzi. mfano mimi nilipata degree kutoka UK na Canada wakati muda wote nilikuwa kwenye chuo kimoja isipokuwa mara chache kama kwenye defense ya thesis.

d) Pia kumbuka Mbowe hasomi program za kawaida ambazo mimi na wewe tunaweza kusoma, tumeambiwa program zimetengenzwa mahsusi kwa ajili yake. Kwa hiyo course load inaweza kuwa tofauti kabisa na course work ya wanafunzi wa kawaida.

d)Kuhusu kutajwa Hull tu nadhani, kwenye gazeti habari ilisema rpogram moja imetengenezwa kwa kushirikisha vyuo vya Uingereza, japani na Marekani, haikusema kuwa atasomea kwenye vyuo vitatu. Naomba mwenye hile habari kwenye archieve zake aiweke tena hapa.
>>Nadhani Mbowe pia anaweza kujitokeza kuclarify mambo zaidi

e)Ndugu yangu nani alikuambia elimu inategema umri. Nyerere (rip) aliwahi kusema elimu haina mwisho wakati anaanzisha Elimu ya Watu wazima. Kama watu wangefuata umri kwenda shule basi tusingekuwa na maprofesa kwani hamna mtu anayepata huo uprofesa kwa sababu ana umri mdogo bali wanazotea bila kujali alianza akiwa na mwaka mmoja au hamsini.
Pia mtu mwenye majukumu ya kisiasa kama mbowe au kiongozi mwingine hawezi kufuata syllabus ya kawaida, pita dunia nzima na utaona huu ukweli.

Yaani wewe badala ya kumshauri Chifupa hata angalau ajiunge na open University tena wamtengenezee program maalum kwa ajili yake (kuenddana na habari za kimtandao hana sifa za kujiunga na University kama kweli alipata Division 0 kidato cha sita).


The quote above from page seven as you said
Unajua katika ukurasa wa saba suala zima la Elimu nimelielezea kinaga ubaga na upeo wa Mbowe kuwa shule aliyonayo kwa sasa ni kubwa muno hana muda wa kupoteza sana na shule.

Now as I said above you seem to mislead us, fundamental questions should wait for Mbowe? am I wrong?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom