Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Dr Who,
unafahamu malengo ya freeman kujiunga humu ilikuwa ni kujibu hizi hoja,lakini kutokana na jinsi hoja zenyewe zilivyojengwa itakuwa vigumu kupata majibu sahihi na matokeo yake tunabaki kuongelea habari za vijiweni.
 
Al-jazeera.
hakuna ofisi yeyote ambayo imahudumia jamii isiwe na equal opportunities policy,complaints procedure na Confidentiality. nenda hata Conservative,

hata taratibu za usajili wa chama cha siasa hazina room ya ukabila,undugu au udini.
kama Chadema kilisajiliwa kwa misingi hiyo basi itakuwa ni makosa.

Maendeleo ya Mnyika hayawezi kupatikana kwa kuhudhuria makongamano bila kwenda shule na hakuna maendeleo bila elimu.

WANABODI.

mbowe kwenye maelezo yake binafsi wakati anagombea urais kuna sehemu alidai ana masters degree toka U.K.

sasa imekuwaje anakuja kusoma tena undergraduate? mzee Kulikoni tuambie kulikoni?
 
Quarz.

kuna nchi duniani haina ukimwi? jee kisa ni ajira?

pale Bilicannas alikuwa ana wauza na halafu anachukua kamisheni kubwa sana yeye,kazi wafanye wengine yeye awatoze kamisheni. kwa mtaji huu hatufai kutuongoza.
 
chinga,
hilo swali ilitakiwa ujiulize wewe kwanza, na jibu lake ungepata kuwa billcanas haina uuhusiano wowote na ukimwi

kuna clubs kubwa kabisa marekani na kuna changudoa wengi zaidi kuliko billcanas lakini idadi ya ukimwi tanzania ni kubwa kuliko marekani.
 
Kwa kweli Watanzania tuna safari ndefu tena sana

Safari yetu ni ndefu. Ila kinachonitisha mimi ni huko tuendako. It seems any one can twist us(with our phds, masters, bachelors, etc) in any direction and we will follow.

Tunaonekana tumesoma; ila kuelimika...mhh!....
 
WACHA.

Hatari hiyo utaua.

Mtoto wa Iron lady alikamatwa akishiriki katika njama za kutaka kupindua nchi.
Huyo mwanasiasa msamehe, hata phd anayofanya nikikwambia utashangaa ni zile kozi za kibwegeee.
 
Form Vi For President - No Way
Quote:
Originally Posted by mwanasiasa
Wacha: unataka kusema kuwa kiongozi lazima awe na elimu kubwa ndio ajali elimu? Hii ni hesabu ya wapi? Kuna viongozi wengi duniani ambao elimu zao zilikuwa za kawaida na bado walifanya maajabu katika maendeleo ya elimu na kinyume chake pia ni kweli. Mfano mzuri ni nyumbani TZ; Mzee Mwinyi alinyanyua sana elimu ya juu.

Ni kipindi chake ndipo idadi ya wanafunzi iliongezeka katika vyuo vya elimu ya juu na kipindi chake pia vyuo vikuu vilingezeka. Lakini alipokuja Mkapa akakubaliana na mapendekezo ya IMF na dadake WB kuwa nchi kama Tanzania ilikuwa haitaji elimu ya juu. Wakamshauri awekeze tu katika elimu ya msingi. Ni katika kipindi hiki tulishuhudia elimu ya juu ikiminywa na vyuo vya serikali viliishi kwa shida na vingine vilibaki kaputi kabisa. Sasa nani ana elimu kubwa kati ya Mwinyi na Mkapa?

Ndio nilisema hapo juu kuwa mantiki ya hoja zako bado naitafuta. Labda nitaipata kadiri ninavyosoma post zako.

Halafu tusipotoshe mambo. Pamoja na kwamba naunga mkono kina JJ kwenda shule, sio kweli kwamba kina JJ hawana elimu ya kutosha. Form Six ni elimu kubwa bado kwa kiwango cha wanasiasa wa Tanzania.

Wanahesabika wenye Form Six hata katika rank za uongozi wa kisiasa wa nchi yetu. Kabla sijaendelea, naomba unitajia kiwango cha elimu alicho nacho Katibu Mkuu wa CCM Makamba.

Hatuwezi kuwa na kiongozi wa nchi ambaye ni form VI period.

Unafahamu ukisikia watu wanasema Bush hakusoma, John Major hakusoma, sio kwamba shule hawakwenda kabisa – walikwenda lakini kichwani hamna lolote (ndio hivyo hivyo tena) uelewaji wao wa masuala ni mdogo. Pia kuna msemo elimu haina mwisho, ndio kusema kila siku unajifunza na hii ni tabia tu. Kama wewe hukwenda shule sawa sawa tabia ya kusoma na kujifunza huiwezi ndio kitu ninachoongelea. (samaki mkunje angali mbichi)

Tatizo ambalo naliona kwa mwenyekiti wako ni pale anapotaka watanzania wamkubali kwamba naye amesoma ili apate cheo. Lakini ukweli utabaki pale pale hiyo degree itakuwa uchwara. Huhitaji hesabu kulijua hili.


Ukiangalia chadema sasa hivi kwa maelezo yako uelewaji wenu ni finyu ndio sababu mnaingia kichwa kichwa tu na Conservative Party siasa za chama hiki zinaeleweka fika tangu enzi hizo na mara ya mwisho natumaini unamkumbuka vizuri Iron Lady kama walivyokuwa wanamuita. Kumbuka vile vile mkutano wake na nchi za Jumuiya ya madola kule Zambia kabla Zimbabwe haijapata uhuru wa bendera. Kuelewa haya huhitaji kupiga hesabu.

Chama kinachokuwa bega kwa bega na Conservative ambao kila siku hawapendi maendeleo ya mtu mweusi na vile vile wanakampeni chafu ya kuwazuia waafrika kwenda UK, lakini wao kuja kwenye nchi zetu ni sawa na halali yao kutuibia na kujichana. Uliza mtoto wa Iron Lady baada ya uhuru wa South Afrika kwa nini aliamua kuhamia kule? Hadi pale matatizo yalipomsibu. Sasa hizo ndio sera za Chadema kutaka kuturudisha kule ambako tulikataa miaka ya nyuma. Conservative ni chama cha wenye nacho na nyinyi kwa ukosefu wa kuelewa mambo (mambumbumbu wengi) ndio sababu mnakumbatia mshiko bila kufahamu maana yake. Ndio sababu nilikuuliza wasomi katika Chadema ni kina nani?

Maana siwafahamu? Wewe unapindua kibao na kuniuliza suala la Makamba na CCM pamoja na uozo wao, waulize wakupe majibu, mie sio msemaji wao na vile vile sina sababu ya kushabikia Chadema ati kwa sababu kuna uozo CCM, vile vile nao wana wasomi ambao ni pungufu katika uelewaji wao na hili halihitaji kupiga hesabu yeyote kulielewa. Siwezi kuruka mkoja kukanyaga m*

Wewe ndio unataka nijiunge na Chadema hivyo inabidi ujieleze sawasawa ili niweze kujua kulikoni, lakini kwa kutoelewa kwenu mambo siwezi kujiunga wala kuwapa support.

Hao CCM unaowaogopa tutawaondoa lakini si kwa kupitia Chadema waliooza.

Ulitaka maswali rahisi hata hayo rahisi unajichanganya. Mmeanzisha chama lazima kiwe makini kwani usanii kama wa CCM hatuutaki, lakini nyie mnaojiunga na Conservative Party ni moto wa kuotea mbali.

Wacha
 
lakini still namsifu kwa kujiunga at least ameonyesha courage ambayo wanasiasa wengi hawana

Lakini tatizo langu ni pale yeye na timu yake walivyo dodge maswali yangu

wanasahu kuwa kura yangu moja inaweza kuwaingiza ikulu
 
Mzee Quarz...
"...hawa wamekuwa na pesa zao kabla hata hawajaingia kwenye siasa,
na unajua kuna watu kama sisi hatufuati pesa kwenye siasa au chama, bali tunachakalika na maisha kama kawaida, kuingia kwenye siasa ni ile tu kutoridhika na jinsi mambo yanavyokwenda."

Kauli yako imefanya nijiulize watu kama kina Dewji au Manji sijui wao wako kundi gani katika kujiingiza katika siasa!
 
Eti wazee wa London, vipi jana huko tunasikia kulikuwa na Uhuru Day Party, nasikia haiyo party ilihuduhuriwa na viongozi wa bongo hebu wazee huko tupeni!
 
Unajua mimi nilifikiri mwanasiasa ni Freeman lakini mpaka pale Freeman alipojoin humu nika noticce grammar lakini hili la mwanasiasa kuwa anafanay PHD ndio nalisoma sasa hivi kweli wewe expert wa mambo ya watu lakini haionekani kam Southampton University wanafundisha propaganda hivyo naamini hiii itakuwa ina run in the family bwana Chinga

haya at least naweza kumsikiliza na kuzungumza na huyu mwanasiasa kuliko JJ
 
Mzee Quarz...
Kauli yako imefanya nijiulize watu kama kina Dewji au Manji sijui wao wako kundi gani katika kujiingiza katika siasa!
hili si swali rahisi kulijibu mwanagenzi, watu wanamalengo tofauti, ila moja wazi ni kuwa wapo wanaotumia nafasi ya siasa ili waweze kurahisisha biasha zao ,mfano kusafiri nje ya nchi kwa urahisi na kufanya biashara kwa kukwepakwepa kulipa kodi, hawa ni oportunist.

na watu kama hawa mara nyingi watajiunga na chama kilichoko madarani na kujiweka kariabu na watawala(mf RA na D).

lakini ukiona mfanyabiashara yuko kwenye chama cha upinzani inatakiwa ujiuluze tena marambili,maana kwa tanzania ukiwa kwenye upinzani basi wewe na biashara zako unaziweka kwenye risk, na utawekewa watu maalum wa TRA kukufatilia wewe tu na kila hatua unayopiga

yamewakuta wengi pale bongo wakati wa mrema, na sasa wote wamerudi ccm na biashara zao zinaendelea vizuri.
 
chinga,
kwa taarifa chadema imejitolea kusomesha wanafunzi waliokosa mikopo vyuoni, hiyo habari mbona haukuileta?
 
VIPI Mnyika?
pia ninao vijana 10 wamekosa mikopo nipitie wapi?unasema mnasomesha mbona haipo kwenye website yenu?
nisaidie kuhusu hawa vijana 10.
 
Qaurz.
TRA KUNA WACHAGA WATUPU.
safi sana,
ni nani amewaweka hao wachaga hapo, ni freeman mbowe au ndesamburo?

sasa unahamia tra, endelea bwana, huko tra mimi siwajui kabisa!
chinga tukubaliane kitu kimoja wewe umeathiriwa zaidi na mitazamo ya kikabila,kidini na chuki zisizo za msingi.
maendeleo binafsi yanaletwa na juhudi za mtu binafsi na kukubali kurisk hata maisha wakati mwingine, hakuna mteremko katika maisha,

vinginevyo utabaki kujadili watu na magirfriend na familia zao, jali kwanza mambo yako, pili jali mambo ya jamii inayokuzunguka na fanya mambo ya maana. kwaheri kwa leo.
 
Quarz.
siwezi ku-risk kuwa jambazi. samahani sana.
 
Topic hii haina tofauti kabisa na topic iliyokuwa imeanzishwa na Nungwi ikiwa na title ya "Mzumbe (LSE) na UDSM nani zaidi;" maudhui yake ni sawa kabisa. Zote zinazungumza mtu au watu fulani binafsi na kuahidi kuwachimba zaidi kutafuta data au mafaili yao na kuyaweka hadharani.

Kinachoniudhi binafasi kwenye mijadala ya namna hii ni jinsi isivyokuwa na mwelekeo, na hasa pale maelezo binafsi ya watu wanaozungumzwa yanapopotoshwa na hizo "data" au "mafaili". Vile vile, utashangaa mtu mmoja anaandika posts tano kwa mpigo zote zikiwa na maudhui hayo hayo hayo bila kupanua mjadala kuelekea kwenye maswala ya kitaifa.

Wazee walisema kuwa "Great Minds Discuss Ideas; Average Minds Discuss Events; Small Minds Discuss People."
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom