Mbowe atolewa nje ya bunge

Mbowe atolewa nje ya bunge

Kwa ndugai siwezi kushangaa, maana yeye hafuati kanuni bali ni jazba na chuki kwa kwenda mbele! Allah amwangazie yale yanayostahili!
 
Miongozo ya dini haina nafasi bungeni mkuu. Mle wenyewe walijitungia kanuni, ingawa ndugai hawezi kuzitafsiri.

Kwani hijabu ni ile kanzu au ni kile kitambaa cha kichwani hadi shingoni au ni vyote kwa pamoja? In that regard, amevuliwa nini? Sikuwa na nafasi ya kuangalia vipindi vya bunge. Naona leo nimemiss kweli kweli. Kuanzia KUB kuondolewa bungeni hadi wengine kuvulia hijabu!!! Mmh!

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Haya mengine tena, msinikumbushe yale ya igunga....
yule mkuu wa wilaya ya Igunga hakuvuliwa hijabu na wala hakuwa akivaa hilo vazi la heshima ila alikuwa akijifunga ka kitambaa kichwani.Hata hivyo hakakuvuliwa ila alikadondosha alipofumaniwa akifanya vikao haramu.
 
Mkuu ishu ilianza jana wakti muswada wa sheria ya kuundwa kwa Bunge la katiba unawekwa mezani tayari kwa wabunge kuchangia. Kama ilivyo kawaida msemaji wa kambi ya upinzai Tundu Lissu alisoma hotuba yake ilieleza wazi jinsi ambavyo mabadiliko ya sheria hiyo ilivyokua imejaa mapungufu. Kwanza kamati ya sheria ya bunge haikuwashirikisha wazanzibar katika kupata maoni ya wadau na kwa ushahidi ni kwamba Tundu Lissu mwenyewe alikuwepo pamoja na Mnyika John John na hakuna hata safari moja waliyoifanya kwenda Zanzibar. Hali hiyo iliwafanya wabunge wote wa Cuf na wale wa NCCR kuungana kupinga hoja ya kuendelea na majadiliano hayo na hatimaye kwa ubabe wa Naibu spika Job Ndugai muswada uliendelea kuchangiwa na wabunge lakini ni wale tu wa CCM kwani wabunge wote wa upinzani ukimtoa Mrema walisusia kikao na kuondoka baada ya naibu spika kutojibu hoja zao. Kikao cha leo asubuhi kilivyoanza ilifika zamu ya kuendelea kuchangi ndipo mkosamali na mbunge mmoja wa CUF walipoomba mwongozo wa spika kutaka bunge lisijadili muswada huo hadi wadau kutoka pande zote mbili watakapotoa maoni hali iliyolazima kupiga kura kwa mbunge mmoja mmoja lakini hata hivyo kwa uchache wa wapinzani hawakufanikiwa kufikisha idadi inayokidhi kanuni za bunge,baada ya hapo ndipo mh. Mbowe aliposimama kuomba mwongozo wa Kiti kuhuji uhalali wa kuendelea kuchangia muswada huo wakati mapungufu yake ni mengi na hata kura zilizopigwa hazikuhesabiwa kwa haki lakini naibu spika alimkatalia na ndipo wabunge wote wa upinzani walipoungana (ukimtoa Mrema) na kukataa kukandamizwa na naibu spika hali iliyoleta tafrani hadi askari kulazimika kumtoa nje Mbowe na wabunge wengine. Hata hivyo wabunge wote wa upinzani walitoka nje na kuwaacha wale wa CCM wakiendelea kuchangia.
 
Ndugai ni janga la Taifa jamani ,haiwezekani kila ukikaa kwenye kiti ,mambo yanakuwa hivyo!!!!.

hekima jamani ,hekima si jambo la mzaha lahitaji neema ya MUNGU.
 
Nadhani ni ishara ya wazi ya tatizo la uongozi wa Naibu Spika Huyo kwa kushindwa kusimamia na kujibu hoja chokochoko za Upinzani ambazo zipo katika mabunge yote Duniani yenye vyama vingi!

Sidhani kama Mh huyu anajua kuwa ni kipimo kibaya kinachomshusha hadhi yake?

Mkuu huyu Naibu Spika ana matatizo makubwa na ni mtu wa mipasho mwanzo mwisho, kwann akikalia kiti karibu kila siku kunakuwa na hali hii? rubbish
 
tanzania kwa sasa maadui wapo 5 namba 1 ni UJINGA 2 Maradhi 3 umaskini 4 CCM 5 Job Ndugai kama naibu spika

Umemsahau Savimbi mwenye ushahidi wa ugaidi atakaoutoa mbinguni.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Harafu watu wengi sana humu ndani wanaongea, Ndugai hajielewi, hajielewi, inamaana hamjuai kama jamaa hajielewi mpaka mnapoteza mda wenu kuhoji Kama Ndugai anajielewa.

Kama mtu anashindwa kujua idadi ya watoto wake, huyo anajielewa kweli? msinitanie.
 
Huyu spika anaendesha bunge kibabe hajui sheria huyu hongera mh mboe kumdindia polisi njaaa hao na huyo gamba
Hata kama mtu hajui sheria lakini hata ile aibu ya kibinadamu ya kuiita 1+1=22 haoni shida, aibu kweli!

 
Ndugai yupo kichama wala sio mtanzania achunguzwe uraia wake kukaa katikati ya nchi sio hoja ya kusema ni mzawa huyu.weeeeeeeeeee nduga weeeeeeeee ushindwe na ulegee kwa jina la yesu
 
Si mliipigia debe ccm mpaka misikitini, haya ndiyo madhara yake, mapigo yanaanza kuonekana hapahapa duniani.
Hakuna mwenye haki ya kudhalilisha dini ya Mwenyezi Mungu..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom