Mbowe atolewa nje ya bunge

Mbowe atolewa nje ya bunge

Dhambi mbaya ni "WOGA" Mbowe haishi kwa Ndugai amatetea maslahi ya Wananchi wote
 
Fundisho kubwa kwa Watanzania wanaopenda uhuru wa mijadala ya bunge, bila kubagua itikadi za kisiasa. Hakuna tija KUJAZA CHAMA KIMOJA BUNGENI.
 
Kiongozi mzuri husikiliza hoja na kutoa maamuzi. Alichofanya Ndugai hata mzee wa kijijini asiye na elimu hatafanya. Aibu yake na hata kwa Taifa.
 
mmh bunge letu linakaribia kuwa kama lile la urusi.ni misuguano kwa kwenda mbele.tunachosubiri sasa ni kuona wakichapana makonde!
 
Kunatofauti gani kati ya mbowe na watoto wa sekondari walioko shuleni make anafanya vituko na kutia aibu bungeni.
 
Kila mmoja wetu mwenye nia njema naTanzania anapaswa kusimama kidete kuhakikisha tunapata katiba bora kwa maslahi ya Watanzania wote. Tusiwaachie wabunge wa CDM, CUF na NCCR peke yao hapana. Tanzania ni yetu sote na wala si mali ya ccm, hakuna mwenye haki miliki na Tanzania awe ccm au chama kingine chochote. Katiba ya leo itaamua hatima ya miaka mingi ijayo ya kizazi hiki na watoto, wajukuu, vitukuu na hata vilembwe na vilembwekeze.
Chama cha Mapinduzi hakiwezi kutuamulia katiba ya Tanzania kwanza hawana nia ya dhati kwani nia yao ni kuimarisha utawala wao wa ki-ccm, tusikubali.
Kwa haya yanayotokea bungeni ni ushahidi tosha kwamba ccm hawana nia ya kuwa na katiba inayozingatia maslahi ya watanzania wote. Kila mmoja ana haki ya kusikilizwa na pale inapoonekana kuna kasoro zirekebishwe, kama wenzetu wa Zanzibar hawakushirikishwa washirikishwe tena vya kutosha kwani haraka ni ya nini? Na je tunakimbilia wapi na kwa maslahi ya nani zaidi yetu sisi wananchi? Zanzibar ni nchi mshirika wa Muungano anapaswa kuwa na haki sawa na Tanzania bara(Tanganyika)Hakuna aliye bora zaidi katika hili si Bara wala Zanzibar.
Rai yangu ni kuwataka kila mwenye nia njema na taifa hili azinduke, aamke, aamue hatima ya Tanzania na vizazi vijavyo.
 
Mbowe alidhani hupo kwenye kampen ambapo huwa anaropoka hadi mishipa ya shingo inamsimama kama kakabwa na vibaka.toa nje kilaza huyo kanuni za bunge lazima ziheshimiwe asilete udj wake
 
Hivi bungeni kama kila mbunge akijiona hana haki na kuamua kusimama kuongea na akiambiwa aache na Spika agome............kweli kutakuwa na Bunge?

Siku tegemea mtu kama Mbowe anaweza kufanya aliyofanya

Kuna haja ya CDM kuangalia upya strategies zao za kisiasa................hizi siasa zenye elements za ubabe na vurugu itafikia mahali wataonekana kama kundi la vurugu

Mjadala hauhusu vyama tatizo lako unadhani wakati wote wanapigania chama...hata hivyo tuliowachagua tunawaelewa
 
Iwonder huyu mrema anaongea nini..kapiga kula ya sio mswada usitolewe bungeni sa hvi anasema tulekebishe katiba ya zamani ituvushe kwenye uchaguzi 2013..hawa viongozi vipi?

Waliopiga kura ya "Siyo" ndiyo waliokuwa wakitaka majadiliano yaendelee!
 
Ujinga wa kukandamiza upinzani na kuwafanya kama watoto wadogo ndio una sababisha yote hayo.
Ukijaaliwa kuwa na elimu na kupata uelewa mabavu unaweka kando.Mbowe bora arudi Dar aje kusimamia kiosk chake cha Billicanas masuala ya siasa aweke kando.
 
Walichagua wavuta bangi waitegemea nini chama kimejaa wavuta bangi haya ni matokeo yake,
chadema karibia kila mtu anavuta haya ndiyo matokeo yake.
 
Nalikumbuka bunge la kina Dr. Slaa na Hamadi Rashid chini ya Spika Samwel Sitta.
Hamad Rashid alikuwa CCM-B tatizo lingetoka wapi? CCM mnachemka sana kila kona uchochoro.
 
Ukijaaliwa kuwa na elimu na kupata uelewa mabavu unaweka kando.Mbowe bora arudi Dar aje kusimamia kiosk chake cha Billicanas masuala ya siasa aweke kando.
Mbowe amezoea kutumia nguvu kuzuia watu kuingia ukumbini pale dar kwenye bar yake anadhani kila sehemu nguvu tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom