Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

chadema mbio zote leo ndio mmefikia hapa? Watanzania mtawaambia nini?
 
Kwa takriban siku tatu sasa kuna uvumi mwingi sana kuhusu Lowasa kuhamia CHADEMA.
Binafsi katika mizunguko yangu kila ninapokuta mazungumzo nimejaribu kupata maoni ya watu kuhusu uamuzi huo.
Kimsingi watu hawapingi sana Lowasa Kuhamia CHADEMA, ila wanachopinga ni Lowasa kugombea kupitia CHADEMA.
Kwa uhakika, endapo Lowasa atagombea kupitia CHADEMA, watu wengi watachoma moto kadi za CHADEMA, wengine hawataenda kupiga kura. Mimi ni mmojawapo wa watu hao.

Wananchi wamejiandaa kisaikolojia kuwa chaguo lao ni Dr. Slaa, vinginevyo jiandaeni kufa kifo cha mende.
Na ikitokea mnampitisha Lowasa, natamani bunge lijalo chadema liwe na wabunge watano tu bungeni, maana mmelewa sifa, mnajiona mnajua kuliko wananchi waliowafikisha hapo mlipo. Mwaka 2010 nilisafiri kilomita 700 mpaka Dar ili kupiga kura ili tuu niwapigie CHADEMA. Mwaka huu mkifanya upuuzi huo hata kama kituo kiko mlango wa pili sitaenda.

Msitufanye sisi mazuzu.
 
Ila ba ndugu sishangaii. Kama walimpokea Ndg Alcardo Ntagazwa mbunge wa wakat ule alivyoondolewa ktk kura za maon na wana CCM akahamia CHADEMA. Hvyo wanapnga kishngo upande
 
Ccm wamegeuka washauri wa ukawa na chadema haya ni maajabu sawa na paka kumshauri panya
 
tunaihitaji mabadiliko yakimfumo.... lowasa ana nyota Kali sana, mbali ya nyota hakuna alie kuja na ushahidi unaomuhusisha Lowasa moja kwa moja na ufisadi...angalau angeburuzwa court ningeamini...

List of Shame iliyosomwa Mwembe Yanga na Dkt Slaa itafaa kuitwa jina gani maana ndio iliyotuaminisha Lowassa ni Fisadi wakati hakuwa amepelekwa mahakamani? Mkiingia kichwa kichwa kwenye huu mtego mtajikuta mnakosoa wenyewe yale mliyoaminisha Jamii na jamii ikawaamini. MKAPA na Jakaya watakuwa si Mafisadi kama mtatumia hiyo hoja. Akina Nape wapo active sana msidhani ulingoni mko peke yenu mnapigana na Punching bag Shauri yenu!!
 
Mandokwa I will support Dr.Slaa.Sitakubaliana na upuuzi kama huo.Na CDM inajitafutia kifo cha ghafla.Mawili either ifutike kwa kumkaribisha Lowassa au Ibaki kwa kumkataa Lowassa.

Na hapo maccm lazima washeherekee kifo rasmi cha CDM.

Nitamshangaa Dr.Slaa akiendelea kukaa CDM,siyo tu ni kumdhalilisha bali watakuwa wametudhalilish watanzania tuliokuwa tunaiona CDM kama mkombozi wa Taifa.Hatuwezi kusema tunapiga vita vya rushwa na.ufisadi halafu tunamkatibisha fisadi.

Nitamshangaa Tundu Lissu aliyepiga vita vya rushwa leo akae meza moja na aliyewadhulumu watanzania maskini haki zao za msingi kwa kujilimbikizia mali yeye na familia yake.

Nitamshangaa Mbowe kwa kudhani watanzania ni wapumbavu.

Waamue CDM ifutike wabaki na Lowassa au wabaki na watanzania wa kawaida pamoja na Chama.

Dr. Slaa anatosha kabisa

Kama Lowassa akija poa, akaribishwe.. na aje kuteuliwa ubunge apewe uwaziri apige kazi
 
Slaa ndio mgombea wa ukawa jamani ila nafurahi watu wanavyoumiza kichwa juu ya ukawa inafurahisha sana ile dhana ya tunamjua haipo tena

labda nayeye kama ametishia kuhama chama lakini wala haisaidi tena wala haamna cha kutueleza juu ya hili na unafiki wenu mfiche msimfiche hatuitaji tena unafiki wenu ,ndo maana mumejificha unasubili wate watakao kosa nafasi ccm mkaokote,
 
magamba yanasambaratika.Majambazi wa rasilimali zetu yanajinyea
 
Dk. Slaa ndo mgombea uraisi sahihi kwa upinzani

Lowassa aje kuwa mwanachama tu.

Wanachama huku site wamegawanyika sana, hii ishu itapasua chama
 
tetesi wapi ameambiwa na mtei kama hataki aondoke ,
wewe unaweza kubisha kwenye saccoss ya mtu na mkwe wake ,masikini SLAA amekaa kimia ,unacheza na njaa ni mbaya?


Hapa nitapingana na wewe kukaa kimya kwa Dr.Slaa sidhani kama ni kukubaliana na matakwa ya Mwenyekiti wake.

Ila nitamshangaa asipoondoka CDM,kwani anauwezo wa kutosha kuishi bila kuwa kiongozi wa chama chochote.
 
Nimenasa mpango mzito wa siri wa kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi mwaka huu kiulainii bila kutumia nguvu kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na Urais. Mpango wenyewe umeanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2011 kwa mamluki wengi kupandikizwa chadema kuanzia ngazi ya mtaa mpaka taifa; Nawahakikishia kuwa CCM itashinda kata nyingi na majimbo mengi bila kupingwa baada ya mamluki kujitoa pindi watakapokuwa wamepitishwa na NEC; Katika nafac ya urais ndugu Magufuli anatarajia kushinda kiulaini baada ya mgombea wa chadema ambae anatarajiwa kuwa Lowasa kujitoa katika mbio hizo baada ya kuwa nae ameshapitishwa na Tume ya uchaguzi. Lowasa ni sehemu ya mpango huo wa kuhakikisha ccm inashinda kiulaini huwezi mtenganisha lowasa na ccm na Kikwete

Ulikuwa wapi miaka yote hiyo bila kutaarifu namna mipango ingekuwa hadi kuenguliwa kwa-EL mbona ulikaa kimya
 
Kwa hiyo slaaa atakatwaaa? hata mimi nasema akatwe tu lowasa akija maana hakuna namna ingine.
 
EMMY
UMEANZA KUTAPATAPA SASA NA BADO MPAKA ROHO ZIWATOKE NYA....MBAF..

**mwakani serekali ya mseto!!
maana mtagoma kuachia nyumba nyeupe!!
 

Ndugu wanajamii,
Nimesoma kwa tahadhali sana maandiko juu ya kumkaribisha Lowasa Chadema ambayo yamemnukuu Mr.Mbowe na wabunge kadhaa ndani ya chama. Binafsi nimestushwa kwani sifikirii kama chama kitatueleza nini wafuasi wa dr.slaa juu ya posibility kwamba atakuwa replaced na lowasa....

Natahadhalisha kwamba maamuzi yakifikia huko then tufanye referendum ndani ya chama kujua upepo unaendaje. Haiwezekani mtu akatwe ccm asababishe kukatwa kwa mlezi tegemeo wa chama. pia natahadhalisha isije ikawa ni gabachovu wa ccm kaja kama mtengwa kumbe ni longterm plan yao kutuvuruga.

Msiseme sijasema.

acha hizo propaganda za kitoto, hivi nyie maiti wa lumumba mbona hamjui propaganda, hivi kama wewe ni mwanachama wa cdm hujui ukweli wa kinachoendelea ndani ya chama chako si uulize viongozi wako wa tawi -wilaya -mkoa -taifa, huku unakuja kuleta upuuzi wako
 
Viongozi CHADEMA msipuuze sauti za watu.... watu wanatoa ushauri wanatukanwa...

CHADEMA fanyeni utafiti kdg

Ni sawa Lowsa aingie CDM asaidie ushindi lakini sio kugombea... kama Rais

Dk. Slaa ndo anafaa
 
Mr. Emmy.... Hongera.............. Wanaopinga waje waseme... Je Lowassa akitoa, watafanyaje?

Hata mm naliona angalizo la mleta mada. Huu mchezo wanaotaka kuucheza cdm utawagharimu na wala wasiamini. Sio mara moja au 2 wagombea wacdm wamekuwa wakijitoa dk za mwisho kisa hongo. Nimesikitishwa sana na cdm. Ni kweli haina viongozi wake mpaka wangoje toka ccm? Nashauri wawapokee lakini wasiwape nafasi yoyote ya ugombea kwenye uchaguzi huu mpaka uchaguzi upite.
 
Thread nyingi wote nyie huwa mnachangia kama wana CCM lakini cha ajabu eti thread hii mnajifanya wana CHADEMA acheni unafiki nyie CHADEMA itabaki kuwa imara kama ilivyo Lowasa aingie au ata asipoingia.

Inajadiliwa tetesi za Lowassa kuhamia Chadema sio history au itikadi ya Mchangiaji, wengine tupo huru kukosoa au kuunga mkono hoja au tukio lolote kwetu siasa sio ushabiki wa Mpira. Rejea comments zangu ujiridhishe pia kuwa kwako kila jambo la viongozi wako kuliunga mkono hakuwasaidii sana viongozi labda kama agenda yako ni kujipendekeza au kujituma au kutumwa otherwise muwe mnasema thread hii ni ya watu wa itikadi fulani hutatuona baadhi yetu
 
Back
Top Bottom