Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

yaani CDM wana muomba Lowassa ajiunge nao hii ajabu kweli bora yeye ndiyo angeomba basi.
 
Miye nilidhani wewe ni mwanachama wa cdm kumbe ni m-ccm. Pikipiki usoila yakuwashani?
 
mbona mnaweweseka sana!! viongozi wanajua nini wanachofanya, na siku zote siasa hazina uadui wa kudumu. Mi ninachotaka kwa sasa ni ccm itoke tu, siangalii ni njia gani itakayotumika, kufika hapo,
 
Karibu Sana UKAWA lowasa nilitamani siku moja itokee hivi sasa ukawa lazima tuchukue inchi pamoja Sana lowasa
 
mkuu na nukuu,"kwangu taifa ni bora kuriko chama ,maana chama cha weza kufa lakini si taifa langu.' mwishp wa kununu, mungu akuzidishie hekima na wewe ni mtanznaia wa kweli,na watu wote waige kutoka kwako,hii docrine yako ni zaidi ya kuwa na phd ya shule,

kwanini nasema hivyo ni kati ya mln 48 za watz wenye mtizamo wa utaifa kama wako ni kama mln 5, wengine vyama kwanza saccoss za babu ,njomba, kabila letu na shangazi kwanza zaidi ya utaifa,


Asante.Tulishindwa kumwelewa JKN alipotuambia huyu tuliyenaye bado mtoto,tulapumbazwa na fedha zilizomwagwa kwa wajumbe na baadhi ya watanzania kumpigia debe sana.

Leo tunakaribisha yale yale tuliyokatazwa.Tuachane na madiwani,wabunge,na wagombea wote wa urais watakaowek peaa ili kununua uongozi.Tujiulize akisha pata uongozi analipaje?

Leo tunadeni kubwa lisiloweza kulipika na mkopo.huo umeishia kulipa madeni ya kupata uongozi.Tumeona Kura za NDIYOOOOOOO zisizosaidia Taifa zikipigwa bungeni wala kuwa na tija kwa Taifa sababu ya woga wa kukatwa pale ubunge utakapo koma.Wabunge wetu wanahongwa vijisent ili waweze kupitisha hata miswada isiyo na tija kwa Taifa ukiangalia 90% ya wabunge wameingia kwa kununua nafasi hizo.

Jamani tuseme basi sasa.
 
Chadema mkomboz wa taifa, ukitubu na kuacha utasamehewa.. Karibu kamanda
 
Karibu Lowassa utuambie wote waliyohusika na Richmond najua ulikuwa kafara. Ili mambo yaende
 
Inawezekana mtoto wa mmiliki danguro kubwa la kwanza Tanzania then Tanganyika akawa msafi kweli?No,haiwezekani kwa kuwa huyu ni mtu aliyezaliwa kwenye uovu uliopindukia na dhambi ya baba yake bado inamtafuna.What does this imply,ni kwamba kumtegemea Mbowe awe mtu msafi kwa lolote ni kama kutaka kuchuma embe kwenye Mchungwa,jambo lisilowezana kabisa.Kwangu kwa Mbowe lolote linawezekana.
Sasa ni dhihiri kuwa CHADEMA iko kwenye mikakati mizito ya kumshawishi au kuafikiana na Edward Lowassa ili aweze kuhama CCM na kujiunga CHADEMA na hapo hapo apewe nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA.
Nikiwa kama mshambuzi wa mambo ya siasa humu JF, mtanzania mpenda maendeleo na mpenzi wa CHADEMA jambo hili limenishtua na kunisikitisha sana.

Tayari Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amenukuliwa na magazeti kadhaa ya leo akisema, Lowassa anakaribishwa CHADEMA na hana tatizo lolote, na hapo hapo baadhi ya wabunge na viongozi wa juu wa CHADEMA wamenukuliwa ama wakiunga mkono ujio au kumumunya maneno kuhusu hilo.

Mpaka sasa sijui, ni nini kimewaingia viongozi wa CHADEMA kuanza kukubali jambo hili. Nini msukumo wao?
Ni nani asiyemjua Lowassa? Huyu ni mwanasiasa mchafu, ambaye amewekeza muda, pesa na watu wake wengi sana katika siasa ili afanikiwe tu kuwa rais wa Tanzania.

CHADEMA bado tu humjajifunza kutokana na makosa? Yuko wapi Samweli Sitta, John Shibuda nk?
Mtaacha lini kusubiri makapi ya CCM ili kuyapokea na kuwapa nafasi za ugombea katika uchaguzi?

Hivi mnajua kwanini watanzania wengi waliwapenda na kuwaamini?
Hivi agenda ya kupambana na Ufisadi hamhitaki tena?

Hivi viongozi wa CHADEMA mnatambua siasa itaendelea tu hata baada ya October 25?
Hivi mnajua kwanini watanzania walitoa maisha yao hata kufa kuona CHADEMA inasonga mbele?

Inakuwaje muwe na mawazo ya kupata madaraka tu kiujanjaujanja kwa kutumia mtaji wa Fisadi Lowassa hata kwa gharama ya kuuza Identity yenu ya kisiasa na agenda zenu?
Hivi mnajua athari za kisiasa baada ya October kama mkimpokea Lowassa sasa?
Hivi CHADEMA itakuwaje kisiasa kama Lowassa atagombea kwa tiketi ya CHADEMA na akafanikiwa kushinda au bahati mbaya akashindwa?

Hivi CHADEMA mnajua Lowassa ana malengo gani na huo urais?
Hivi mnajua kwa nini CCM kwa gharama kubwa kabisa ilihakikisha Lowassa hapewi nafasi ya kugombea?

Hivi hamjiamini kuwa nyie wenyewe mnaweza pasipo msaada wa makapi ya CCM?
CHADEMA mnawezaje kuacha mbachao kwa msala upitao?

CHADEMA NI NANI ALIYEWALOGA?
 
Nimenasa mpango mzito wa siri wa kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi mwaka huu kiulainii bila kutumia nguvu kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na Urais. Mpango wenyewe umeanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2011 kwa mamluki wengi kupandikizwa chadema kuanzia ngazi ya mtaa mpaka taifa; Nawahakikishia kuwa CCM itashinda kata nyingi na majimbo mengi bila kupingwa baada ya mamluki kujitoa pindi watakapokuwa wamepitishwa na NEC; Katika nafac ya urais ndugu Magufuli anatarajia kushinda kiulaini baada ya mgombea wa chadema ambae anatarajiwa kuwa Lowasa kujitoa katika mbio hizo baada ya kuwa nae ameshapitishwa na Tume ya uchaguzi. Lowasa ni sehemu ya mpango huo wa kuhakikisha ccm inashinda kiulaini huwezi mtenganisha lowasa na ccm na Kikwete
 
Jipange tena mkuu.. Upo kama waandishi wa Yale magazeti yanayoandika bikira ya flank ilitolewa na flani. Nenda halafu uje tena
 
Sasa ni dhihiri kuwa CHADEMA iko kwenye mikakati mizito ya kumshawishi au kuafikiana na Edward Lowassa ili aweze kuhama CCM na kujiunga CHADEMA na hapo hapo apewe nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA.
Nikiwa kama mshambuzi wa mambo ya siasa humu JF, mtanzania mpenda maendeleo na mpenzi wa CHADEMA jambo hili limenishtua na kunisikitisha sana.

Tayari Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amenukuliwa na magazeti kadhaa ya leo akisema, Lowassa anakaribishwa CHADEMA na hana tatizo lolote, na hapo hapo baadhi ya wabunge na viongozi wa juu wa CHADEMA wamenukuliwa ama wakiunga mkono ujio au kumumunya maneno kuhusu hilo.

Mpaka sasa sijui, ni nini kimewaingia viongozi wa CHADEMA kuanza kukubali jambo hili. Nini msukumo wao?
Ni nani asiyemjua Lowassa? Huyu ni mwanasiasa mchafu, ambaye amewekeza muda, pesa na watu wake wengi sana katika siasa ili afanikiwe tu kuwa rais wa Tanzania.

CHADEMA bado tu humjajifunza kutokana na makosa? Yuko wapi Samweli Sitta, John Shibuda nk?
Mtaacha lini kusubiri makapi ya CCM ili kuyapokea na kuwapa nafasi za ugombea katika uchaguzi?

Hivi mnajua kwanini watanzania wengi waliwapenda na kuwaamini?
Hivi agenda ya kupambana na Ufisadi hamhitaki tena?

Hivi viongozi wa CHADEMA mnatambua siasa itaendelea tu hata baada ya October 25?
Hivi mnajua kwanini watanzania walitoa maisha yao hata kufa kuona CHADEMA inasonga mbele?

Inakuwaje muwe na mawazo ya kupata madaraka tu kiujanjaujanja kwa kutumia mtaji wa Fisadi Lowassa hata kwa gharama ya kuuza Identity yenu ya kisiasa na agenda zenu?
Hivi mnajua athari za kisiasa baada ya October kama mkimpokea Lowassa sasa?
Hivi CHADEMA itakuwaje kisiasa kama Lowassa atagombea kwa tiketi ya CHADEMA na akafanikiwa kushinda au bahati mbaya akashindwa?

Hivi CHADEMA mnajua Lowassa ana malengo gani na huo urais?
Hivi mnajua kwa nini CCM kwa gharama kubwa kabisa ilihakikisha Lowassa hapewi nafasi ya kugombea?

Hivi hamjiamini kuwa nyie wenyewe mnaweza pasipo msaada wa makapi ya CCM?
CHADEMA mnawezaje kuacha mbachao kwa msala upitao?

CHADEMA NI NANI ALIYEWALOGA?

Kama mtaendelea kumwamini Mbowe basi mmepotea,Mara kumi mngempigania Dr Slaa awe Mwenyekiti kipindi kile,Nimesikia mambo mengi machafu kuhusu huyu jamaa,kwamba hata kwenye ESCROW pia alishiriki kupiga ila sikutaka kuamini,ila kwa kumsafisha Lowassa sasa kumenifanya niamini niliyoyasikia,jamaa ni mjanja mjanja tu hana lolote.
 
cha ajabu wanao ponda wote ni ccm tuna juana humu na hizo ID zenu,tangu lini mkawa na mapenzi na chadema mpaka mnajifanya mna huruma eti cdm itapotea kwa vile lowassa ana tia maguu cdm rasmi kesho mwanza.
 
Back
Top Bottom