Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Mbowe amkaribisha rasmi Lowassa CHADEMA

Nimenasa mpango mzito wa siri wa kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi mwaka huu kiulainii bila kutumia nguvu kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na Urais. Mpango wenyewe umeanza kutekelezwa kuanzia mwaka 2011 kwa mamluki wengi kupandikizwa chadema kuanzia ngazi ya mtaa mpaka taifa; Nawahakikishia kuwa CCM itashinda kata nyingi na majimbo mengi bila kupingwa baada ya mamluki kujitoa pindi watakapokuwa wamepitishwa na NEC; Katika nafac ya urais ndugu Magufuli anatarajia kushinda kiulaini baada ya mgombea wa chadema ambae anatarajiwa kuwa Lowasa kujitoa katika mbio hizo baada ya kuwa nae ameshapitishwa na Tume ya uchaguzi. Lowasa ni sehemu ya mpango huo wa kuhakikisha ccm inashinda kiulaini huwezi mtenganisha lowasa na ccm na Kikwete

Naona unapenda sana ukawa lakini hupendi lowassa awe mgombea wake. Usiwe na hofu kwa kuwa kamwe hataingia ukawa.
 
hisia zako !
kuna tofauti kati ya hisia na uhalisia.
 
BAVICHA wepesi sana sasa hivi hawna nguvu maana wanamsubiri mkuu wa SACCOS awape go ahead! Low Assa!!!
 
utakuwa siasa umezianza leo, acha kuishi kwa hisia, umejuache kama mgombea wa ukawa ni lowasa? au unaweweseka baada ya kutokuwa na uhakika kama ENL atabaki ama la? unajuwa jamaaa kaumizwa kiais gani? unajuwa kwa nn ni magufuri na si membe au lowasa? unajuwa kilichotokea dodoma mpaka akapatikana magufuri? usipende kutengeneza habari usizokuwa na taarifa nazo ongea na watu wenye taarifa rasmi.
 
Mabandiko kama haya hayapaswi kuwepo mahala kama hapa
 
Sasa ni dhihiri kuwa CHADEMA iko kwenye mikakati mizito ya kumshawishi au kuafikiana na Edward Lowassa ili aweze kuhama CCM na kujiunga CHADEMA na hapo hapo apewe nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA.
Nikiwa kama mshambuzi wa mambo ya siasa humu JF, mtanzania mpenda maendeleo na mpenzi wa CHADEMA jambo hili limenishtua na kunisikitisha sana.

Tayari Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amenukuliwa na magazeti kadhaa ya leo akisema, Lowassa anakaribishwa CHADEMA na hana tatizo lolote, na hapo hapo baadhi ya wabunge na viongozi wa juu wa CHADEMA wamenukuliwa ama wakiunga mkono ujio au kumumunya maneno kuhusu hilo.

Mpaka sasa sijui, ni nini kimewaingia viongozi wa CHADEMA kuanza kukubali jambo hili. Nini msukumo wao?
Ni nani asiyemjua Lowassa? Huyu ni mwanasiasa mchafu, ambaye amewekeza muda, pesa na watu wake wengi sana katika siasa ili afanikiwe tu kuwa rais wa Tanzania.

CHADEMA bado tu humjajifunza kutokana na makosa? Yuko wapi Samweli Sitta, John Shibuda nk?
Mtaacha lini kusubiri makapi ya CCM ili kuyapokea na kuwapa nafasi za ugombea katika uchaguzi?

Hivi mnajua kwanini watanzania wengi waliwapenda na kuwaamini?
Hivi agenda ya kupambana na Ufisadi hamhitaki tena?

Hivi viongozi wa CHADEMA mnatambua siasa itaendelea tu hata baada ya October 25?
Hivi mnajua kwanini watanzania walitoa maisha yao hata kufa kuona CHADEMA inasonga mbele?

Inakuwaje muwe na mawazo ya kupata madaraka tu kiujanjaujanja kwa kutumia mtaji wa Fisadi Lowassa hata kwa gharama ya kuuza Identity yenu ya kisiasa na agenda zenu?
Hivi mnajua athari za kisiasa baada ya October kama mkimpokea Lowassa sasa?
Hivi CHADEMA itakuwaje kisiasa kama Lowassa atagombea kwa tiketi ya CHADEMA na akafanikiwa kushinda au bahati mbaya akashindwa?

Hivi CHADEMA mnajua Lowassa ana malengo gani na huo urais?
Hivi mnajua kwa nini CCM kwa gharama kubwa kabisa ilihakikisha Lowassa hapewi nafasi ya kugombea?

Hivi hamjiamini kuwa nyie wenyewe mnaweza pasipo msaada wa makapi ya CCM?
CHADEMA mnawezaje kuacha mbachao kwa msala upitao?

CHADEMA NI NANI ALIYEWALOGA?
 
Wewe hata matamshi yako yanaonyesha sio kamanda ni Gamba la mamba.

Nlikuwa namchukia sana lowasa hasa makundi yake yanayomzunguka huwezi kumtofautisha lowasa, rostam,chenge,karamagi na manyang'au wengine wenye uchu na rasilimali za nchi hii ...na mtambue ugumu wa kumuuza huyo jamaa kwenye majukwaa
 
Itakuwa ni unafki dhahiri..huyuhuyu fisadi namba 1 bora nipgie kura pombe maguful

Hahahahaaa
Eti fisadi lol
Ukiulizwa kaiba nini hujui....umekaririshwa tu mkuu.

Mfano Kama Lowassa akiwa rais na waziri Mkuuu akawa Slaa, Spika Lipumba, na mawaziri unawajua unadhani atapata mafasi ya kuiba hapo?
Itamlazimu kutenda kazi.

Btw we hamia kwa magufuli tu ni haki yako mkuu
 

Ndugu wanajamii,
Nimesoma kwa tahadhali sana maandiko juu ya kumkaribisha Lowasa Chadema ambayo yamemnukuu Mr.Mbowe na wabunge kadhaa ndani ya chama. Binafsi nimestushwa kwani sifikirii kama chama kitatueleza nini wafuasi wa dr.slaa juu ya posibility kwamba atakuwa replaced na lowasa....

Natahadhalisha kwamba maamuzi yakifikia huko then tufanye referendum ndani ya chama kujua upepo unaendaje. Haiwezekani mtu akatwe ccm asababishe kukatwa kwa mlezi tegemeo wa chama. pia natahadhalisha isije ikawa ni gabachovu wa ccm kaja kama mtengwa kumbe ni longterm plan yao kutuvuruga.

Msiseme sijasema.
 
Mbona mnjamba jamba na mambo ya ukawa,magamba punguzeni presha dawa iwaingie.Mambo ya ukawa yanawahusu nini?
 
Uko sahihi mkuu....akija itamlazimu kunana na beat tu hata km hataki.

Kwanza jamaa ni mtendaji mzuri...Kuliko wanaofumbia Escrow
 
Back
Top Bottom