Mbona watu wengi wanapenda kuhama usiku tu?

Sababu kuu ni 2.

1. Imani ya kishirikina na mila za kurithi.
Hapa huamini ukihamia sehemu mpya mchana kweupe utakuja kuishi maisha magumu (pesa hutoiona). Pia wachawi watakufanyia jambo baya.

2. Aibu itokanayo na kumiliki vitu vichache na vikuu kuu.

Kuna mhaya mmoja tulisoma naye Lindi sekondari. Yeye shule ikifungwa huondoka shule kwa kutoroka tu. Hata kama wewe ni rafiki yake hawezi kukuaga. Imani za kishirikina na mila potofu hupelekea hizi tabia za kiwendawazimu. Mimi nimepanga nyumba zaidi ya tatu.

Na karibu zote nilihamia muda wa mchana kasoro moja tu ndio nilihamia usiku kwakuwa nilichelewa kumaliza kuhamishia vitu vyote maana nilikuwa nabeba mwenyewe tu na mashkaji wakinisaidia. Nilianza mchana nikamaliza usiku
 
Mimi sijui kwa kweli lakini haya mambo haya, yanaanzia mbali sana, tena sana na hatimae watu tunakuja kuyarithi bila kujua chanzo chake!!

Hebu twende taratibu, tusianzie mbali sana bali tuanzie zama za Nyerere!!

Mtu unahama zako Mapipa kwenda makazi mapya Manzese!!! Je, wangapi walikuwa na uwezo wa kukodi magari ya kuhamisha mizigo yao, na hayo magari yenyewe yalikuwa wapi?!

Lemme guess, njia ya haraka kwa akina sie ni kubeba mavyombo na magodoro yetu ya sufu sisi wenyewe, labda na kwa msaada wa majirani tuliokuwa tunaishi nao kwa wema!!!

Sasa unaanzaje kutembea na misufuria ya enzi za Nyerere mchana kweupe na mbuzi wanapiga misele mitaani??! Kumbuka misufuria ya enzi za Nyerere ilikuwaga myeusiii iliyobonyea bonyea!!!!

Mashuka ya enzi za Nyerere yalikuwa taabu tupu manake hata sabuni za kufulia ilikuwa anasa!! Na hapa tukumbushane tu kwamba magodoro ya enzi za Nyerere yalikuwa yanaitwa Matandiko!!

Sasa kwanini nisisubiri giza linafanyie hifadhi ndipo nianze kufungasha mamizigo yangu kama Mkimbizi kumbe nahamia makazi mapya?!
 
Mkuu kama huachi milango na madirisha ya nyumba yako wazi ili kila mtu achungulie kilichomo, utagundua tu kwa nini watu wanahama usiku.
 
wiki moja nyuma nilihama mchana kweupeeee!
watu wakanishangaa, sioni sababu za kujificha gizani
 
Kunasababu zaid ya moja. Baadh ni
Uvhafu uliopitiriza, kunguni n.k
Scurity. Mchana nirahis kujikaribishia vibaka
Iman za kishirikina. Pia watu ni washirikina balaa unakuta mikia ya punda na meno ya simba si rahis kusafirisha mchana.
Kasumba. Pia watu wengi hufanya kimazoea unakuta hana sababu yyote ya kumpereka usiku ila anafanya hivo bas tu alizoea.
Mm kipind ninapanga sikuwai kuhama usiku. Acha mazoea, acha ushirikina na uchafu kama sofa limechoka waweza badilisha.
 
Mimi sijui kwa kweli lakini haya mambo haya, yanaanzia mbali sana, tena sana na hatimae watu tunakuja kuyarithi bila kujua chanzo chake!!

Hebu twende taratibu, tusianzie mbali sana bali tuanzie zama za Nyerere!!

Mtu unahama zako Mapipa kwenda makazi mapya Manzese!!! Je, wangapi walikuwa na uwezo wa kukodi magari ya kuhamisha mizigo yao, na hayo magari yenyewe yalikuwa wapi?!

Lemme guess, njia ya haraka kwa akina sie ni kubeba mavyombo na magodoro yetu ya sufu sisi wenyewe, labda na kwa msaada wa majirani tuliokuwa tunaishi nao kwa wema!!!

Sasa unaanzaje kutembea na misufuria ya enzi za Nyerere mchana kweupe na mbuzi wanapiga misele mitaani??! Kumbuka misufuria ya enzi za Nyerere ilikuwaga myeusiii iliyobonyea bonyea!!!!

Mashuka ya enzi za Nyerere yalikuwa taabu tupu manake hata sabuni za kufulia ilikuwa anasa!! Na hapa tukumbushane tu kwamba magodoro ya enzi za Nyerere yalikuwa yanaitwa Matandiko!!

Sasa kwanini nisisubiri giza linafanyie hifadhi ndipo nianze kufungasha mamizigo yangu kama Mkimbizi kumbe nahamia makazi mapya?!
Sad indeed
 
Wakuu,

Nina hoja fupi hapa, hivi mbona wakazi wengi wa Dar es salaam na miji mingine wanapenda kuhama usiku usiku tu? Mtu anatoka Keko anahamia Mbagala lazima atahamisha vitu usiku tu. Hivi kunani hapa? Wanaficha nini? Kwanini wasihame mchana au asubuhi?

Wakuu karibuni hapa mtujuze
Vitu anavyomiliki ni changamoto, godoro lina ramani ya dunia na ramani nyingine ambazo hazitambuliki
 
Back
Top Bottom