Mbinu za kuchukua namba ya Simu katika Mazingira Magumu

Gentlemen_

JF-Expert Member
Nov 24, 2019
3,563
10,549
Wazee wa kupambania Kombe
Huwa mnatumia Njia gani kuomba/kuchukua namba za simu katika Mazingira MAGUMU na HATARISHI?

Umafia:

Part 1>
Nilikuwa nipo katika Daladala watu wengi vibaya mno, nikatupia jicho pembeni nikaona KIFAA kimetulia kinachezea simu. Nikajiuliza hapa namba nabebaje? Kuangalia nje bado vituo viwili nishuke.

Kuchek katika wallet business card binafsi zimeisha zimebaki za Ofisini (Michoresho) nikaona hii hapana kuitoa.

Nikajipapasa huku na kule bahati nzuri nilibahatisha kipande cha TICKET ya Bus la mkoani, na katika ile ticket kuna namba yangu ya SIMU, sikujiuliza mara mbili wakati nashuka nikamshtua yule mrembo kwa kumgusa begani then ile ticket nikaipitisha kwa chini kama vile alikuwa kaiangusha then nikamkazia machoni huku nikimuonyesha ishara ya NIPIGIE. Mie nikashuka zangu huyo Home nikatulia.

Zikapita kama siku 5 kimya, nikaona hapa Mkeka umechanika siku ya 6 jioni nipo viti virefu nashangaa namba ngeni kupokea ni yule Manzi akajitambulisha pale then the rest is history.😋

Kuna wengine wanatumia mpaka Hela kuandika namba (Karatasi hakuna) mtu anachukua noti ya elf 10 anachora namba yake anamkabidhi mrembo.
 
Part 2:
Nilikuwa Samaki Samaki pale Mlimani City.

Napiga maji, ghafla nikaona Chuma kikali sijapata kuona aisee ubaya alikuwa na Boyfriend/Mume wake.

Basi nikamlia timing wakati wa kwenda Washroom nimfate huko huko (Mazingira ya pale kwa upande wa Washroom kuna Distance kubwa).

Basi kweli bhana Manzi akajipindua kuelekea Washroom na mimi nikaunga Tela, tulivyokunja kona tu ya kuingia corridor la choooni nikamshtua, akasimama nikamwomba namba akasema yeye ameisahau kama vipi nimpe yangu, basi akanipa simu yake nimuandikie Namba yangu..

Kumbe nyuma Bwana ake anakuja na yeye tyr kashanipa simu yake ndio niandike namba nashangaa Manzi kageuka chap kakimbilia choo cha wanawake. Mie nikawa nimesimama tu sielewi nini kinaendelea ila kwa kuwa nimesoma CUBA sikugeuka ila nikapiga jicho kwenye kioo (Reflection) nikaona mjuba anakuja ila bahati nzuri na yeye alikuwa anatembea huku anachat so hakuona tukio la mbele.

Sasa simu ninayo ya yule Manzi namrudishiaje??.. 🤣

Na jamaa kumbe alikuja kumsubir kule kule kwenye Corridor la Washroom ili arudi naye.

Mie nikajipindua Choo cha kiume kama Kawaida nikazuga zuga pale, Dem akatoka akanipa ishara ya nitulie huko huko.

Basi jamaa akarudi naye Mpaka walipokuwa wamekaa. Mie nikatoka baadae kurudi ktk meza yangu, nikamuita mhudumu mmoja hivi (Best yangu) nikamwambia nenda pale idondoshe hii simu miguuni (Mapajani) kwa yule Dada pale then uje kuna Zawadi yako hapa..

Mhudumu hakusita, alifanya hivyo na yule Dada aliiokota simu yake then.. tukaendelea kuwasiliana pale pale...

Huyu aliniletea shida sana.. mpaka nikawa naishi kama Mwizi.
 
Part 2:
Nilikuwa Samaki Samaki pale Mlimani City.

Napiga maji, ghafla nikaona Chuma kikali sijapata kuona aisee ubaya alikuwa na Boyfriend/Mume wake.

Basi nikamlia timing wakati wa kwenda Washroom nimfate huko huko (Mazingira ya pale kwa upande wa Washroom kuna Distance kubwa).

Basi kweli bhana Manzi akajipindua kuelekea Washroom na mimi nikaunga Tela, tulivyokunja kona tu ya kuingia corridor la choooni nikamshtua, akasimama nikamwomba namba akasema yeye ameisahau kama vipi nimpe yangu, basi akanipa simu yake nimuandikie Namba yangu..

Kumbe nyuma Bwana ake anakuja na yeye tyr kashanipa simu yake ndio niandike namba nashangaa Manzi kageuka chap kakimbilia choo cha wanawake. Mie nikawa nimesimama tu sielewi nini kinaendelea ila kwa kuwa nimesoma CUBA sikugeuka ila nikapiga jicho kwenye kioo (Reflection) nikaona mjuba anakuja ila bahati nzuri na yeye alikuwa anatembea huku anachat so hakuona tukio la mbele.

Sasa simu ninayo ya yule Manzi namrudishiaje??.. 🤣

Na jamaa kumbe alikuja kumsubir kule kule kwenye Corridor la Washroom ili arudi naye.

Mie nikajipindua Choo cha kiume kama Kawaida nikazuga zuga pale, Dem akatoka akanipa ishara ya nitulie huko huko.

Basi jamaa akarudi naye Mpaka walipokuwa wamekaa. Mie nikatoka baadae kurudi ktk meza yangu, nikamuita mhudumu mmoja hivi (Best yangu) nikamwambia nenda pale idondoshe hii simu miguuni (Mapajani) kwa yule Dada pale then uje kuna Zawadi yako hapa..

Mhudumu hakusita, alifanya hivyo na yule Dada aliiokota simu yake then.. tukaendelea kuwasiliana pale pale...

Huyu aliniletea shida sana.. mpaka nikawa naishi kama Mwizi.
Hapa umetupiga mkuu
 
Part 2 mkuu
Part 2 aisee ni kisa kirefu kidogo..

Ila huyo Manzi baada ya kuwasiliana siku mbili tatu niligundua kuwa ni Mke wa Mtu na ametoka kufunga ndoa recently na aliyemuoa sio yule aliekuwa nae pale.

Yaan story ni ndefu ila ile Ndoa sina hakika kama ipo au La.. ila mie ndio nikawa Suspect namba moja, nilibadiri kuanzia namba yangu ya simu, Mpaka Makazi niliyokuwa naishi.
 
Back
Top Bottom