Mbinu gani ya kudai Boss alipe Mishahara

Mbinu gani ya kudai Boss alipe Mishahara

sergio 5

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2017
Posts
9,851
Reaction score
11,438
Nimejishikiza katika kaajira flani private sasa boss watu wanadai ndiyo michezo yake wafanyakazi wakifanya kazi miezi kadhaa huwa anataka kuzurulumu.

Mwezi mmoja ili muondoke then alete wengine nao wakifanya anawadhurumu .

Trend huwa ipo ivyo Leo tumekaa kupanga jinsi gani Tu deal na BOSS ila hatujapata muafaka mwenye madini mazuri apo atusaidie ilikuwa tarehe 26.

Lakini Hadi Leo hakuna kitu akiulizwa BLA BLA KIBAO

1776272730327.png
 
1. Fanya kazi kwa kiwango ambacho ataona tija yako kiasi aone ugumu kuku replace.

2. Dai mkataba

3. Chukua advance Kwa kujifanya unamatatizo. Yaani kabla mwezi haujafika kati mkope

Mostly ya kaz za namna hii zinakuwa ni zile za kutumia nguvu na ujuz kidogo.
Unskilled labour.

Hata ujitutumue vipi. Boss hawez kuona faida yako. Yeye anaangalia kazi yake. Na akikufukuza leo. Kesho anakuja mtu anakuwa trained siku 2 na anafanya kazi kama unayofanya ww na pengo halionekani.

Kama wanao mkataba ni rahis kumdai.

Ila Kama hamna.
Mchomeni kwenye ngazi za juu boss wenu...
-Siku muite kikao na akiongea mmrekodi saut yake chochote atakachowaambia.
-kama kuna kitabu cha registry kiibeni na muwe nacho nyinyi maana ndio ushahidi wenu.
-Nenden wilayani (sio Polisi)
Na katoeni malalamiko yenu kule.
(wakuu wa Wilaya wataruka nayo fasta sana, wanatafuta kick kama hizo).

NB: Kitabu cha mahudhurio ndio uchahidi wenu wa kuwa mliingia kufanya kazi kwake muda flan na kutok muda flani.
 
Ukifika mwisho wa mwezi hajakupa stahiki yako
Acha kazi
Dai mshahara
Mimi mambo ya kujitolea ndo nilipiga marufuku ndugu zangu woote
Bora nikupe mtaji ugungue banda la chips
Sasa mahi km hakuna wa kukupa mtaji je? Watu wanajitolea lwa kukosa replacement ya hiyo kitu.
 
Yalinikuta boc hakunipa mshahara miez 5 zaidi posho ten ten za hapa na pale end the day nilichomfanyia never hawez nisahau kwenye maisha yake na saiv anawalipa watu vizur
 
Mimi mambo ya kujitolea ndo nilipiga marufuku ndugu zangu woote
Masai Dada nakuunga mkono kwenye hili. Siku hizi kuna majambazi bila huruma yanatangaza nafasi za kujitolea... mdogo wangu nilimpa mtaji alime vitunguu na ndani ya miaka mitano kajenga jumba la maana.
 
Sasa mtu anajitolea miaka n miaka
Bora ufunguue banda la kuuza matunda
Trust me
Kujitolea bure hupati hata nauli ni ukoloni kuliko wa mtu mweupe
Hii kitu ni kweli, ila sasa hakuna mtaji wa kufungua banda la Matunda.
Lol
 
Yalinikuta boc hakunipa mshahara miez 5 zaidi posho ten ten za hapa na pale end the day nilichomfanyia never hawez nisahau kwenye maisha yake na saiv anawalipa watu vizur
Tuhadithie, ilikuajee?
 
Sasa mtu anajitolea miaka n miaka
Bora ufunguue banda la kuuza matunda
Trust me
Kujitolea bure hupati hata nauli ni ukoloni kuliko wa mtu mweupe
Mimi nilishawahi kujitolea miaka 2 ila lengo langu ilikuwa kujifunza biashara kama anayofanya boss ili nikiondoka nikafungue. Nilipiga kazi kama kichaa. Nilikuwa sichagui kazi. Hadi mke wake akinituma kazi nafanya na niko tayari muda wowote. Mshahara siulizi wao ndo huwa wanajishtukia ikiwa imepita hata miezi mitatu. Nilichokuwa ninazingatia ni kuwahudumia wateja kwa viwango vya juu na kuhakikisha hawamfikii boss. Siku ilipofika nikipiga mahesabu ya mshahara na commissions ambazo sijalipwa ni kama 20m. Boss akawa analeta viswahili ila sikuleta tafrani yoyote... kilichotokea ni mimi kuhama na kufungua the same business kisha kuhama na wateja kama 90%. Ilikuwa ni mtikisiko mkubwa.
 
Nenda ofisi ya idara ya kazi iliyopo kwenye mkoa wako husika
Peleka malalamiko yako hapo kwa maafisa kazi mwajiri wako atashughulikiwa.
 
ofisi ya idara ya kazi ipo chini ya wizara ya kazi inashughulika na utekelezaji wa sheria za kazi na kusimamia haki za wafanyakazi na kupokea malalamiko yote ya kazi na kuyatafutia suluhu
Ukifika ofisini mwajiri wako ataitwa na swala lenu litatuliwa kisheria
 
Back
Top Bottom