Mbingu saba, siri na nguvu ya namba saba

Mbingu saba, siri na nguvu ya namba saba

Nani aligundua namba? Lengo lake lilikuwa ni nini? Huo upekee wa namba 7 yeye aliuzungumziaje kwa wakati huo pindi amegundua namba? Kama biblia na misaafu mingine ya dini imeelezea upekee wa namba 7, je, Mungu alikusudia kuifanya namba 7 kuwa ya kipekee? Lakini naamini mungu hakutufundisha kuhesabu ila kuhesabu kuliletwa na wanadamu, tena kumbukumbu zangu zinasema wa Misri ndio waligundua namba. Ntarudi kuuliza maswali mengine baadae!
Juu ya namba saba si lazima tumshirikishe huyo Mungu wa kwenye vitabu. Kwanza tuijue na huyo Mungu atajifunua kwetu mwenyewe.
 
Viwanja vya Saba saba, Maadhimisho ya saba saba, Saba saba hotel enzi hizo bakurutu murua pande za chuga, kuna Seven eleven hotel (huyu yy sijui vipi) nayo ipo chuga.
Kaka.ufafanuzi tafadhali.
Hapana sio somo jepesi kihivyo, mazingira ya Tanzania mwezi wa saba ndo kiangazi murua kufanya sherehe. Kuna nchi zingine mwezi huo hata haina lolote. Hii namba saba inayozungumzwa hapa iko kispiritual, sasa tunauhitaji kiaje inahusika na kiaje inatenda kazi.
 
Kwahiyo kitu kilichokuja kuondoa kiza ndo kinanguvu kwamaana kabla ya kuumbwa palikua kiza na mwangaza ukaja kuondoa kiza!!sasa asili yetu jibu lake bado inakua siri yake muumba kwamaana ukisema asili yetu ni kiza sasa je kuna kati yetu kabla ya kuzaliwa alitambua kua yupo kizani ama kwenye mwanga?
Kiza ni pasi uhai, sa kuna kuna kujitambua hata kabla ya kuzaliwa?
 
Kwahiyo kitu kilichokuja kuondoa kiza ndo kinanguvu kwamaana kabla ya kuumbwa palikua kiza na mwangaza ukaja kuondoa kiza!!sasa asili yetu jibu lake bado inakua siri yake muumba kwamaana ukisema asili yetu ni kiza sasa je kuna kati yetu kabla ya kuzaliwa alitambua kua yupo kizani ama kwenye mwanga?
Yeah kwa dhana ile ile ya kiza kiza (mwanzo wa kutojua jambo) kuna mengi huyajajua /hatujayajua bado hasa yale ya ulimwengu wa roho ama ulimwengu wa kiza
 
Kwanza dini hapa uwe tu mfano wa kuthibitishwa hoja, kisiwe ni kigezo cha hoja tutajifunga wenyewe ktk mjadala hata kweli ya saba hatutaipata.
uko vizuri sana
 
Saba ni utukufu na mamlaka ya kiroho, sita ni binadamu katika ulimwengu wa roho, binadamu asiye mkamilifu, ila akiwa juu ya mamlaka nyingine zote kidunia, huyu aliumbwa siku ya sita, ufahamu wake unagotea hapo
Kwahiyo anapotaka kudadisi nini kilitokea siku ya saba inayosemekana Mungu akapumzika ndipo inapokuja dhana nzima ya mpinga Kristo na Freemasons kwenye namba 666
Mshana najua una akili sana!
 
Inaonyesha hii namba saba ina siri kubwa iliyojificha nyuma yake. Katika utafiti mdogo usio rasmi nilioufanya, ukiachana na mambo ya hizi dini za jahazi, hata maisha kabla yalikuwa yanaienzi hii namba kwa namna moja au nyingine. Mf. kuna usemi au tahadhari katika makabila mengi iliyokuwa inatolewa kwa mtu anayetaka kuoa kwamba asioe ukoo fulani kwa vile huo ukoo/nyumba ni mlango wa SABA. Ikiwa na maana ni mkosi.
 
Yeah kwa dhana ile ile ya kiza kiza (mwanzo wa kutojua jambo) kuna mengi huyajajua /hatujayajua bado hasa yale ya ulimwengu wa roho ama ulimwengu wa kiza
Saaa hoja yako yakusema asili yetu kiza iko wapi? Kwamaana hujazaliwa unatambua je kua ulikua kizani? Hapo ndo kwenye utata
 
Kiza ni pasi uhai, sa kuna kuna kujitambua hata kabla ya kuzaliwa?
Ndo swali la msingi unajitambuaje kabla hujazaliwa kujua kua ulikua kizani? Na je kabla ya uumbwaji ulimwengu palikua kiza je uliwahi kuuliza mwangaza ulikua wapi? Mpaka ikaja kuuondoa kiza? Ni vitu ambavyo vilikuepo sasa kusema asili yetu ni kiza kwahiyo kabla yakuzaliwa kwetu tulishajitambua kua tulikua kizani!! Haileti maana kabisa hii ni siri yake muumba wetu!!
 
Inaonyesha hii namba saba ina siri kubwa iliyojificha nyuma yake. Katika utafiti mdogo usio rasmi nilioufanya, ukiachana na mambo ya hizi dini za jahazi, hata maisha kabla yalikuwa yanaienzi hii namba kwa namna moja au nyingine. Mf. kuna usemi au tahadhari katika makabila mengi iliyokuwa inatolewa kwa mtu anayetaka kuoa kwamba asioe ukoo fulani kwa vile huo ukoo/nyumba ni mlango wa SABA. Ikiwa na maana ni mkosi.
Hakuna dini ya majahazi ndugu kwavile unahukumu kutoa neno kwa njia ilioletwa khabary njema basi kulikua hakuna haja yakuumbwa makabila na rangi tofauty ni kwasababu tufahamiane mungu ni mkubwa kuweza kufanya haya!! Sasa haijalishi habary njema imekuja kwa njia gani ilimradi imetufikia vizury! Huna haja yakubeza!!
 
Saaa hoja yako yakusema asili yetu kiza iko wapi? Kwamaana hujazaliwa unatambua je kua ulikua kizani? Hapo ndo kwenye utata
Ukiwa hujazaliwa ndio kiza chenyewe...kiza ni dhana pana sana kuliko tunavyofikiri ndio maana kuna usemi usemao usilolijua ni sawa na usiku wa kiza,, kwahiyo kutambua jambo kujua jambo kuangaziwa jambo ni nuru na kinyume chake ni kiza
Ukisoma Buddhism kuna kitu kinaitwa enlightenment yaani kuangaziwa,, kuangaziwa ni hali ya kutoka kwenye kiza cha ufahamu
 
Back
Top Bottom