Mbeya vijijini: Kampeni, uchaguzi na yatokanayo

Hizi habari za SISIEMU kotofautiana kutokana na mgombea wao ni kwa mujibu wa habari iliyoko katika gazeti la Mtanzania Daima. Soma hapa chini:

CCM sasa ngoma nzito Mbeya Vijijini
• Wabunge wake wagawanyika


na Mwandishi Wetu
ZIKIWA zimebaki siku tano kabla ya kuanza kampeni za uchaguzi mdogo Mbeya Vijijini, hali ya kisiasa ndani na nje ya vyama vinavyoshiriki kwenye uchaguzi huo inaonyesha kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kipo katika wakati ngumu wa kuendelea kushikilia kiti hicho kilichokuwa chini ya mbunge wake, marehemu Richard Nyaulawa.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima, unaonyesha kuwa moja ya mambo yanayoiweka CCM katika nafasi ngumu kwenye uchaguzi huo ni mgombea wake, Mchungaji Luckson Mwanjale, kutoungwa mkono na wabunge wa mkoa huo kutokana na tofauti za makundi yaliyokuwapo mwaka 2005 wakati wa mchakato wa kusaka mgombea urais.

Mmoja wa wabunge wa mkoa huo aliyezungumza na Tanzania Daima kwa sharti la kutotajwa, alisema Mchungaji Mwanjale alikuwa mwana mtandao asilia, hivyo hakumuunga mkono Profesa Mark Mwandosya (kutoka Mbeya) aliyewania kiti hicho na kushindwa na Rais Jakaya Kikwete.

Makundi hayo ndiyo yanayoendelea kuutafuna Mkoa wa Mbeya na ndiyo sababu ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba kushindwa kufika mkoani Mbeya katika ziara yake ya hivi karibuni aliyoishia mkoani Iringa, baadaye Dodoma na Arusha.

Wakati Makamba akiwa mkoani Iringa, iliwahi kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa CCM Mbeya hawamtaki Makamba mkoani humo, taarifa ambayo hata hivyo baadaye ilikanushwa na chama hicho tawala.

Ukiachia mpasuko huo, habari zaidi zinadai kuwa mgombea huyo hana sifa za kutosha kuungwa mkono na wananchi wa jimbo hilo kutokana na elimu yake, ikilinganishwa na wagombea waliopitishwa na vyama vingine vya CHADEMA na CUF.

“Mwanjale alishaomba kuteuliwa kuwania ubunge katika jimbo hilo kupitia CCM mara tatu na mara zote alishindwa kutokana na kuzidiwa sifa na wagombea wenzake kama alivyozidiwa na marehemu Nyaulawa katika uteuzi wa ubunge, mwaka 2005, sasa safari hii sifa hizo amezipata wapi?” alisema mchambuzi huyo wa siasa ambaye hakupenda jina lake litajwe.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanailezea hali hiyo kuwa inaweza kumwathiri mgombea huyo na chama chake, kwa kuwa wananchi wanaweza kuhofia kumchagua kwa sababu alishathibitika kuzidiwa sifa na wagombea waliopita.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, aliripotiwa na waandishi wa habari Jumapili iliyopita, akikiri kuwa Mwanjale alishaomba kuteuliwa kuwania kiti hicho katika chaguzi zilizopita lakini hakupitishwa kwa madai kuwa alikuwa hajakomaa kisiasa.

Chiligati alisema CCM imempitisha mgombea huyo baada ya kuona sasa amekomaa na kudhihirisha uvumilivu na ustahimilivu mkubwa wa kisiasa, kwani angeweza kukimbilia upinzani.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wanauona msimamo huo wa CCM kumtetea mgombea wake, kuwa unakiweka chama hicho kikongwe nchini katika mazingira hatarishi kwenye uchaguzi huo.

Wanaona kuwa itawawia vigumu wananchi kuamini kwa haraka ukomavu wa mgombea huyo katika kipindi cha kampeni, hasa ikizingatiwa kuwa hakuungwa mkono na chama chake huko nyuma.

“Hii inaweza kusababisha wananchi kuamua kutafuta chaguo lililo bora kutoka vyama vingine,” alisema mmoja wa wataalamu hao.

Baadhi yao wanakitafsiri kitendo cha CCM kumpitisha mgombea huyo kuwa kimechangiwa na kukosa mgombea mwingine mwenye umaarufu kati ya waliojitokeza, baada ya kuepuka kumpitisha, Jenerali Mstaafu Robert Mboma, kutokana na kushambuliwa tangu awali.

Mwanjale (58), Katibu wa CCM jimboni humo na mchungaji wa dhehebu la Uinjilisiti, mwenye stashahada ya ufundi, anaonekana kuwa dhaifu mbele ya mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Shambwee Shitambala, ambaye kitaaluma ni wakili, na mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Daudi Mponzi, ambaye ni Mhandisi wa Mawasiliano.

Aidha, katika miaka ya hivi karibuni, CCM inaonekana kupungukiwa wanasiasa wenye mvuto na uwezo wa kulitawala jukwaa la kisiasa katika mikutano ya kampeni zake, hasa baada ya gwiji lake la kampeni, Makamu Mwenyekiti Mstaafu, John Malecela, kutopenda kushiriki kwenye kampeni kama ilivyokuwa Tarime, ambapo CCM ilimteua kuwa mmoja wa wapiga debe wake, lakini hakushiriki.

Uamuzi wa CCM kupanga kumtumia Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, katika uzinduzi wa kampeni zake, unadaiwa kuwa unaweza kutia doa kampeni hizo, kutokana na tuhuma nyingi za ufisadi kudaiwa kuwa zilianzia katika awamu yake.

Kwa upande mwingine, umaarufu wa CCM katika jimbo hilo na Mkoa wa Mbeya kwa ujumla unaonekana kupungua, hasa ikizingatiwa kuwa Rais Kikwete, alipofanya ziara mkoani humo, msafara wake uliripotiwa kutupiwa mawe na wananchi wanaodaiwa kuwa na hasira na kutotekelezwa kwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania.

CCM inatarajiwa kuzindua kampeni zake Januari 4, mwaka 2009.
 
Sidhani kama elimu inaweza kuwa sababu ya wana SISIEMU wengine kutomuunga mkono mgombea wao. Kuna wabunge wengi tu tena wa SISIEMU ambao wamefikia elimu ya sekondari. Hii ni kwa mujibu wa CV za wabunge kwenye website ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa hiyo site kuna mtu kama Chitalilo wa Buchosa hakumaliza sekondari. Mohamedi Abdallah wa CCM Pangani hakumaliza chuo, na wengine wengi ambao bado nakusanya majina yao pamoja na wasifu wao.
Sasa iweje leo hii waweke visingizio hivyo vya elimu wakati wengine wameishia sekondari au ualimu? Mwenye CV ya huyo mgombea wa SISIEMU naomba aiweke hapa ili tuone kama kuna ukweli wowote ule kuhusu elimu yake.
 
Date::12/29/2008
Chadema yaenguliwa uchaguzi Mbeya vijijini
Na Brandy Nelson na Peter Edson
Mwananchi Newspaper

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeenguliwa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Mbeya Vijijini baada ya mgombea wake, Sabwee Shitambala kuondolewa katika orodha ya wagombea kutokana na Tume ya Uchaguzi kukubali pingamizi dhidi yake lililowekwa na vyama viwili.

Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na kusainiwa na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi jimboni hapo, Juliana Malange mgombea huyo wa Chadema hataruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo ulioandaliwa kuziba pengo lililoachwa na Mbunge Richard Nyaulawa aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

"Kutokana na pingamizi lililowekwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) maombi yao yamezingatiwa na hivyo mgombea wa Chadema hataweza kuendelea na kampeni zozote za uchaguzi," inaeleza sehemu ya barua hiyo.

Uongozi wa Chadema mkoani Mbeya ulithibitisha kupokea barua yenye maamuzi hayo na kusema kuwa wanatarajia kukaa kikao baadaye jana usiku ili kujua hatima ya chama chao.

Mamia ya mashabiki wa Chadema waliokuwa wamejikusanya katika ofisi za msimamizi wa uchaguzi walionekana kujikusanya katika makundi baada ya uamuzi huo kutolewa, wengi wakiilaani hatua hiyo ya tume ya uchaguzi.

Katibu mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa alisema amesikitishwa na uamuzi huo kwa kuwa umekifanya chama hicho pamoja na wadau wengine kupoteza imani na usimamizi unaoendelea katika mchakato wa kumpata mbunge atakayerithi kiti cha Marehemu Nyaulawa.

Alisema tayari wameshapata taarifa za pingamizi dhidi ya mgombea wao kwamba limetupiliwa mbali na lile la CUF na CCM kukubalika jambo ambalo alisema limezua utata ndani ya chama chake.

"Tunajiandaa kukata rufaa ndani ya masaa 48 yajayo ili tuweze kupata haki yetu ya msingi dhidi ya mgombea wetu ambaye tunaamini kuwa alikuwa na vigezo vyote vtya kushiriki kwenye uchaguzi," alisema Dk. Slaa.


"Mimi sipo Mbeya ila tumepewa taarifa kuwa ombi letu limetupiliwa mbali, wenzetu wa CCM na CUF wamekubaliwa... jambo hili limetufanya tupoteze imani," aliongeza.

Taarifa dhidi ya pingamizi ya mgombea wa chama hicho ziliwakilishwa kwa msimamizi huyo wa uchaguzi jimboni hapo zikieleza kuwa Shitambala alikwenda kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya mahakama ya wilaya, kitendo ambacho kimeelezwa kuwa ni kinyume cha sheria.

Juzi Shitambala aliwekewa pingamizi na vyama vya CUF na CCM. Chadema ilimwekea pingamizi mgombea wa CCM kwa madai kuwa alisema uongo kuhusu mahali alipozaliwa.

Vuta nikuvute hiyo ilitokea katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo ambako CUF na CCM walidai kuwa mgombea wa Chadema aliapa kinyume na taratibu za uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasilisha fomu ya pingamizi hilo, mjumbe wa tume ya uchaguzi ya CUF, Hussein Mmasi alisema chama chake kiliamua kumwekea pingamizi Shitambala kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya Mahakama ya Wilaya.

Madai hayo ndio pia yaliyoifanya CCM kumwekea pingamizi mgombea huyo.

Wakati huohuo, CUF imesema kuwa kinazitambua mbinu zinazotumiwa na CCM katika kuhakikisha kinapata ushindi kwa kuvuruga daftari la wapiga kura na kuongeza idadi watu kwa miujiza, ikidai kuwa hiyo ndiyo silaha yao kubwa.

Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuzindua kampeni uchaguzi wa ubunge Mbeya Vijijini, naibu katibu mkuu wa CUF, Duni Haji alisema kuwa chama chao kinahitaji mabadiliko na kimekuwa na nafasi kubwa ya kushinda katika chaguzi mbalimbali, lakini tatizo kubwa ni mbinu chafu zinazotumiwa na CCM.

Duni alisema kuwa CCM huvuruga daftari na kuongeza idadi ya wapiga kura kimiujiza na mwisho wake huwa ni matokeo ya kura kuonyeha idadi kubwa tofauti na idadi ya waliojiandikisha.

Naibu katibu huyo alifafanua kuwa mbinu nyingine ni ile ya kumwaga polisi vijijini ili kuwajengea hofu wananchi.

"Mbinu zote hizo zinazotumiwa na CCM zina lengo la kuwaibia kura wapinzani huku wakijua mshindi anapotangazwa, wapinzani huenda mahakamani, lakini hurudi mikono mitupu kwa kuwa wao ndio serikali," alisema.

Alisema kuwa pamoja na CCM kutumia mbinu hizo chafu, bado CUF haitakata tama kudai haki na kuendelea kuwaelimisha wananchi juu ya kuacha tabia ya kuuza shahada zao.
 
Last edited by a moderator:
Kwa mujibu wa barua iliyotolewa na kusainiwa na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi jimboni hapo, juliana malange mgombea huyo wa chadema hataruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo ulioandaliwa kuziba pengo lililoachwa na mbunge richard nyaulawa aliyefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

vita sasa imehamia uwanja mpya baada ya tarime ccm kupigwa chini, hapa wameshikwa pabaya chadema lakini hii inaua demokrasia kwani dosari ndogo kama hizi msimamizi wa uchaguzi alisubiri watu waweke mapingamizi, nijuavyo fomu inaporejeshwa hukaguliwa na msimamizi na kuipokea iwapo ameridhika na kuomba ikamilishwe sasa alitulia akijua hilo litakuwa dili na kuwastua ccm na cuf waimalize chadema. Hapa bado sijaelewa bado naomba mnaoelewa mnisaidie ufafanuzi zaidi.
 
NInaomba kupewa tafsiri ya sheria ya Kiapo ya mwaka 1964 ili niweze kuona kama inaharamishwa na sheria ya uchaaguzi tafadhali.

Lunyungu asante sana kwa kuanzisha hii habari hapa. Tuwahakikishie wenzetu kuwa tutaendelea kuleta habari za yale yanayojiri kule Mbeya hapa jukwaani kwa ajili ya taarifa na mjadala.
 
NInaomba kupewa tafsiri ya sheria ya Kiapo ya mwaka 1964 ili niweze kuona kama inaharamishwa na sheria ya uchaaguzi tafadhali.

Lunyungu asante sana kwa kuanzisha hii habari hapa. Tuwahakikishie wenzetu kuwa tutaendelea kuleta habari za yale yanayojiri kule Mbeya hapa jukwaani kwa ajili ya taarifa na mjadala.

Tafadhali mwenye uelewa zaidi wa mambo haya ya sheria atusaidie. Siwezi kuamini kuwa CHADEMA ni mbumbu kiasi cha kufanya kosa kama hilo. Mbaya zaidi mgombea wao ni mwanasheria.

Hata hivyo napata taabu na mambo kama haya ambayo kweli yanooenekana ni upuuzi mtupu. Iweje CUF imwekee pingamizi mgombea wa CHADEMA wakati wao walilaani sana walipowekewa pingamizi na NCCR-Mageuzi huko Pemba?? Tunahitaji kufika mahala pa kutupa pumba tubakize mchele. Huwezi kuacha kuamini kwamba hapa kuna mchezo wa kutumiana!!
 
Good news...!
Lunyungu naona winter ya Moscow imekushinda na sasa upo MBY Vijijini!..Good
 
Wana-JF nielewesheni. Mbona kwa miaka mingi Makamishna wa Viapo hapa nchini ni Pamoja na Mawakili wa Kujitegemea na si Mahakimu pekee? Mbona nyaraka zilizoidhinishwa na mawakili hupokelewa na Serikali kama nyaraka halali? Vipi kwenye nyaraka za uchaguzi Mawakili si tena makamishna wa Viapo (commissioners of oaths)? Sheria ya uchaguzi inasemaje kuhusu viapo vya wagombea? Nielezeni tafadhali. Mbona CHADEMA wana viongozi wanasheria, wamejisahau kweli?
 
Good news...!
Lunyungu naona winter ya Moscow imekushinda na sasa upo MBY Vijijini!..Good

Kibungango unataka kuniambia kwamba watu wa Tanzania walio kuwa wanafuatilia uchaguzi wa Obama ama wengine wanavyo fuatilia habari za Gaza wako huko ? Kaka unaishiwa nini ?

Jamani CUF ina historia ya kuwekea Chadema mapingamizi .Hata kama Chadema wakishindwa kuweka mgombea bado CUF Mbeya wako very weak na watashindwa tu .Migogoro hii NCCR , TLP na CUF ndiyo wana iendekeza nadhani kwa rupia kupenya .Hapa ni baridi sana wandugu wacha nitafute kahawa nirudi ila nimesikitika sana .
 
Hata kama alikosea mahali pa kulia kiapo, bado naona ni dosari ambayo inatakiwa msimamizi wa uchaguzi amwambie akairekebishe na wananchi walio wengi waamue. Hizi sheria za uchaguzi zinatakiwa kuangaliwa upya. Hivi kukosea sehemu ya kulia kiapo ni kigezo kikubwa cha kumnyima mtu sifa za kuwa mgombea?
 
Kwa sasa viongozi wa CHADEMA ambao walikuwa wameshafika Mbeya tayari kwa ajili ya kuanza rasmi mabio ya kushinda uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijijini wako katika kikao kizito. Bidii za kujua nani anaongoza kikao hicho na ni nini kinajadiliwa zimegonga mwamba. Hata hivyo tuna habari kuwa Wakurugenzi John Mrema wa Bunge na Halmashauri, Singo Benson Kigaile wa Elimu na Sera. wapo ndani ya kikao hicho. Chanzo chetu kilichoko ndani ya kikao hicho kimetuhakikishia kuwa mara watakapotoka watatupa taarifa ya yale yaliazimiwa.

Stay tuned
 
chama chake kiliamua kumwekea pingamizi Shitambala kutokana na kuapa katika kampuni ya uwakili badala ya Mahakama ya Wilaya.

- Wakuu please msaada hapa on sheria, what the hell is this kuapa thing?
 
Jamani CUF ina historia ya kuwekea Chadema mapingamizi. Hata kama Chadema wakishindwa kuweka mgombea bado CUF Mbeya wako very weak na watashindwa tu. Migogoro hii NCCR, TLP na CUF ndiyo wana iendekeza nadhani kwa rupia kupenya.
Mkuu Lunyungu, unayoyasema yana ukweli tupu; it's frustrating to hear CUF ambao ni wakwanza kumwekea pingamizi mgombea wa CHADEMA wakidai kupitia kwa Juma Duni Haji kuwa vyama vingine ndio vinasababisha ushirikiano kuyumba. Haya ni ya Filauni kama ulishayaona ya Mussa!!!!!!!!!!

Chama cha Wananchi (CUF), kimesema ushirikiano wa vyama vinne vya upinzani, unayumba kutokana na viongozi wakuu wa vyama hivyo vya TLP, Chadema, NCCR-Mageuzi na chama hicho, kukacha mikutano ya pamoja.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Juma Duni Haji aliyasema hayo alipozungumzia kampeni za chama hicho zilizotarajia kuanza jana kuwania nafasi ya ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini pamoja na masuala mengine yahusuyo muungano wa vyama vya upinzani.

Duni alisema Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba mara kwa mara amekuwa akiwaita viongozi wa vyama vingine kwa simu na barua ili wakutane, lakini wamekuwa wakishindwa kuhudhuria mikutano bila sababu za msingi na kusababisha vyama hivyo kukosa mwelekeo.

Alisema bila ya vyama vya upinzani kuungana, kamwe hawawezi kukiangusha Chama Cha Mapinduzi. “Siafu na sisimizi ili waweze kumwangusha tembo ni lazima waungane, wakati sisimizi akiingia kwenye mkonga wa tembo siafu anauma tumboni hadi tembo ataanguka,” alisema Duni.

Aidha, Duni alipinga hoja ya Chadema iliyotaka wagombea wa vyama vilivyojitokeza katika uchaguzi huo wakutanishwe na kumpata anayekubalika kwa madai kuwa tamko la muungano wa vyama hivyo halisemi hivyo na kwamba wao walikiandikia barua chama hicho ili kiwaachie jimbo hilo.

Alisema CUF iliwaachia Chadema katika majimbo mbalimbali likiwamo Tarime mkoani Mara, lakini wanashangazwa na Chadema kutaka wakutane ili kumpata mgombea anayekubalika wakati wao hawakuwawekea masharti huko nyuma.

Katika hatua nyingine, Duni alisema wanaingia katika kinyang’anyiro cha kuwania ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini wakiwa hawana imani na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutokana na kuibiwa kura katika chaguzi zilizopita.

Alidai katika uchaguzi wa mwaka 2005, mgombea wao, Amina Ahmed alishinda lakini kutokana na wizi waliofanyiwa, marehemu Richard Nyaulawa alionekana kuibuka na ushindi na kumshinda mgombea wao. “Zanzibar tumeshinda mara tatu, lakini mara zote tumenyang’anywa na kila mtu anajua hilo, tutaendelea kupigania haki hadi mwisho,” alidai Duni.

Alidai licha ya kuibiwa kura katika chaguzi mbalimbali wataendelea kushiriki katika chaguzi zinazofanyika nchini kwa kuwa lengo la chama hicho ni kuwakomboa wananchi kutoka katika fikra za kikoloni alizodai zimepandikizwa na CCM.

Hata hivyo wakati CUF ikidai kuwa iliiandikia barua Chadema, Mkurugenzi wa Vijana Taifa wa Chadema, John Mnyika alisema CUF iliandika barua ya kuomba kuachiwa nafasi katika kinyang’anyiro hicho na hawakuomba mazungumzo. Akizungumzia suala la Tarime, alisema CUF yenyewe haikusimamisha mgombea na kwamba NCCR-Mageuzi haikuwaunga mkono.

Katika hatua nyingine, hatima ya wagombea wa CCM, Chadema na DP waliowekewa pingamizi kutokana na kukiuka taratibu mbalimbali kisheria katika ujazaji wa fomu za kuwania kuteuliwa kuwania ubunge, inatarajiwa kujulikana leo.

Hadi kufikia jana majira ya saa 10 alasiri, wagombea wa vyama vilivyokuwa vimewekewa pingamizi walikuwa tayari wamerudishiwa majibu ya pingamizi walizowekewa na wagombea wenzao. Hata hivyo, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Juliana Malange kupitia kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Damson Ntangu, aliwaeleza wanahabari saa 11:20 kuwa bado anapitia majibu yaliyotolewa na wagombea.

“Msimamizi amesema niwaambie kuwa bado anapitia maelezo ya wagombea, alitegemea atatoa maamuzi leo, lakini hatafanya hivyo na badala yake atawapa taarifa kesho saa tatu asubuhi,” alisema Nthangu na kuongeza kuwa waandishi wanaweza kupata majibu kwa njia mbili, moja kwa kuwasiliana na wagombea wenyewe au kusubiri hadi kesho asubuhi.

‘HabariLeo’ ilipata nakala ya majibu ya mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala aliyekuwa anajibu pingamizi alizowekewa na vyama vya CUF na CCM; la kwanza likihoji uhalali wake wa kugonga kuapa na kugonga muhuri wa wakili badala ya hakimu kama Sheria ya Uchaguzi inavyoelekeza.

Katika majibu yake, alisema Tume ya Uchaguzi ilitangaza kuchukua fomu ni Desemba 27 na kurudisha ni Desemba 27, huku ikitambua fika kuwa Desemba 25 na 26 ni siku za sikukuu na Desemba 27 ni Jumamosi ambayo mahakama hazifanyi kazi. Aidha, Shitambala amemweleza Msimamizi wa Uchaguzi kuwa Sheria ya Uchaguzi haisomwi na wala haipaswi kusomwa peke yake na pia kiini cha kuapishwa na hakimu kieleweke.

Alisema kimsingi hakimu anapata uwezo wa kuapisha kisheria kutokana na Sheria ya Viapo (Judicial Proceedings) and Statutory Declarations Act 1996) katika kifungu cha 11 ikisomwa pamoja na Sheria ya Notaries Public and Commissioner for Oaths kifungu cha 10 kinachotaja nani wanaruhusiwa kuapisha. Kadhalika ametupilia mbali madai kuwa alijiapisha mwenyewe ofisini kwake pamoja na kutojaza kipengele cha kama amewahi kushitakiwa au la kwa kile alichodai wawekaji pingamizi hawajasoma vizuri taratibu za ujazaji wa fomu hizo.
 
FM ni wazi kuwa sheria ya uchaguzi inahitaji overhaul. Tatizo is not oath alone!!!!
 
All this game tells of how coward CCM is and again the depth of CUF weakness. CUF is ready to sacrifice anything for MUAFAKA. I don't see a point that 's causing CUF's celebration in the saga facing CHADEMA.
 
Kama Chadema watakosa kabisa kusimama basi kila mtanzania atajua kwamba CUF si upinzani haswa maana hawatashinda kabisa .CUF bara haina uwezo wa kushinda ki hivyo labda itokee sehemu chache .CUF wamekuwa maeneo mengi sana wanashindwa ku comply na makubaliano yao .Kuna mifano mingi sana tunaweza kutoa hapa ambapo CUF walienda Kinyume achilia mbali kuweka pingamizi .Kaburi lao wanalichimba wenyewe wacha uone baada ya Mbeya watasema nini .CUF watabakia kuwa Visiwani lakini bara watabaki na udini wao .

Kampeni zinashindwa ama mgombea anapita kwa mambo mengi yakiwemo mvuto wa mtu anaye gombea .
 
Huwezi kujua nani mpinzani halisi mpaka mambo fulani yatokee. Kenya walitengana, lakini walipoamua kuunganisha nguvu na kuacha UMIMI/USISI wakaweza kuing'oa KANU madarakani. Kwa Tanzania bado, wananchi wako tayari kuunganisha nguvu, lakini Viongozi bado kila mmoja anataka kuongoza, mpaka wajue kuwa "Hawawezi kuongoza wote kwa wakati mmoja, bali wataongoza wote kwa nyakati tofauti", hapo ndipo wataamua kuungana na kuing'oa CCM madarakani. Kweli CCM watacheka miaka mingi ijayo kama washindani ndio hawa....
 
Ukweli ni kuwa CHADEMA wako sahihi kwa mtazamo wa sheria! Hilo ni kosa jingine CCM wamefanya! Sasa ni rasmi jimbo la Mbeya Vijijini linakwenda kunyakuliwa na CHADEMA!

Uzuri ni kuwa mabao ya kiufundi kama haya CCM na vyama vingine hawayajui wala hawaoni! Tayari CHADEMA imeibua hisia nzito miongoni mwa jamii kuwa inaonewa, hamasa imekuwa kubwa, CUF wanarudia kosa waliofanya Tarime kuungana na CCM kuishambulia CHADEMA, wamejimaliza sasa tusubiri wanamume wa shoka wamalize kazi, hako kamtego wanakachomoa kiulaani, lisu na mdee wanatatua hiyo ishu kirahisi kabisa na ni suaala lilio wazi kabisa kisheria.

Kitakachotokea ni kuwa CHADEMA inakwenda kushinda rufaa yake, CUF watasinyaa kwa aibu kama ilivyokuwa baada ya ushindi wa Tarime, leo wanajibalaguza kuwa waliunga mkono CHADEMA Tarime wakati ukweli ni kuwa CUF walikubaliana na TLP na NCCR kumuunga mkono mgombea wa NNCR mageuzi, na pia hatujasahau tamko la Lipumba, Mrema na Mbatia ambao kwa pamoja walijarinu kuwasaidia CCM katika kupandikiza hisia mbaya katika jamii kuwa CHADEMA inahusika na kifo cha wangwe na pia CUF ilisimamisha mgombea katika nafasi ya Udiwani, kama kweli walikuwa na nguvu Tarime tungeona mtetemeko wao katika kinyan'ganiro cha udiwani lakini wapi mgombea wao aliachwa mbali mno na Kamanda John Heche wa CHADEMA.

Kwa mtazamo mpana CCM wameisafishia njia CHADEMA na kuwapa mtazji mkubwa wa kisisasa mbeya vijijini.Maana kwa tafisri ya jumla ni kuwa CCM wanaiogopa CHADEMA! Sasa wasubiri goli la kisigino.

Hakuna ukiukwaji wowoete wa sheria hapo,ni umbumbumbu wa msimamizi wa uchaguzi wenye msukumo wa hofu na nia mbaya dhidi ya CHADEMA. Namshukuru mungu kwa kuendelea Kuifunga CMM kutoona haya yaliotabiriwa. Freeman, Zito, Slaa, Mnyika, Lisu, Arfi, Mdee na makamanda wengine wa Chama Mbadala tupeni watanzania zawadi ya mwaka mpya kwa kulinyakua jimbo la Mbeya Vijijini mnano Januari 25.
 
Last edited:
Kama Chadema watakosa kabisa kusimama basi kila mtanzania atajua kwamba CUF si upinzani haswa maana hawatashinda kabisa .CUF bara haina uwezo wa kushinda ki hivyo labda itokee sehemu chache .CUF wamekuwa maeneo mengi sana wanashindwa ku comply na makubaliano yao .Kuna mifano mingi sana tunaweza kutoa hapa ambapo CUF walienda Kinyume achilia mbali kuweka pingamizi .Kaburi lao wanalichimba wenyewe wacha uone baada ya Mbeya watasema nini .CUF watabakia kuwa Visiwani lakini bara watabaki na udini wao .

Kampeni zinashindwa ama mgombea anapita kwa mambo mengi yakiwemo mvuto wa mtu anaye gombea .


Kwanza nikupongeze kwa kauli nzito kama hii. Ni vizuri umelisemea hili la udini, maana nilidhani wanasingiziwa hawa jamaa. Kumbe hata ninyi wanasiasa mnakubaliana nalo huko kwenye vyama vyenu.

Pili, kama kweli kuna ukiukwaji wa sheria katika ujazaji wa hizo fomu, haijalishi ni nani anaweka pingamizi as long as amefuata taratibu zilizopo kisheria. Haya mambo ya kujifanyia mambo kiholela ndiyo yameifikisha hii nchi hapa mahali tulipo. Lazima tukubali kumeza machungu yatokanayo na kukurupuka kwetu bila kuangalia taratibu zikoje. Na kwa chama makini, linapotokea kosa la kiufundi kama hilo suluhu siyo kukimbilia kulaumu waliokuwekea pingamizi ama sheria iliyopo ila ni kujipanga upya ili kesho na keshokutwa haya yasijitokeze. CUF wana haki kabisa ya kuweka pingamizi kwa vile ni chama cha siasa cha upinzani dhidi ya vyama vingine vyote vyenye usajili hapa nchini. Haya mambo ya kujitengenezea sijui muungano wa vyama ni upumbavu tu, labda viamue kujiua na kuunda chama kimoja ndipo nitawaelewa.

Suala la tatu ni hivi: Hao wagombea wa vyama vingine waliapishwa na nani iwapo ilikuwa vigumu kwa mgombea wa Chadema kupata mahali halali (kwa sheria za uchaguzi) pa kwenda kuapa kwa kisingizio cha siyo siku ya kazi?

Na je, ni kwa nini hakuna aliyelalamikia kwamba fomu za wagombea zisingeweza kurudishwa siku hiyo kwa vile ingekuwa vigumu kwa wahusika kukamilisha matakwa ya kisheria ikiwemo ni pamoja na kuapa kwa mamlaka halali? Hii yote ni kwa sababu ya kukurupuka tu bila kuwa makini.
 
Du; Eric; umenigusa kidogo; mie mwenyewe ktk mambo yangu yote huwa naapa kwa Mwanasheria tu jengo la mbele akiweka mhuri basi OATH yangu imeisha; naamini sheria ni hiyo hiyo ya kula kiapo unless kuwepo na jingine zaidi; bado naamini kuna jambo kubwa litafanyika kwa Chadema kuchukua hilo jimbo kwa makosa madogo madogo kama haya; Chadema italichukua jimbo lile; maana rufaa itapita na watalichukua; Mie hakima wa wilaya simjui na nimefanya mambo mengi sana ya kimahakama; je yote ni batili?? Nijuzwe kidogo tusichoke
 
Back
Top Bottom