Mbeya vijijini: Kampeni, uchaguzi na yatokanayo

Kwanza nikupongeze kwa kauli nzito kama hii. Ni vizuri umelisemea hili la udini, maana nilidhani wanasingiziwa hawa jamaa. Kumbe hata ninyi wanasiasa mnakubaliana nalo huko kwenye vyama vyenu.

Pili, kama kweli kuna ukiukwaji wa sheria katika ujazaji wa hizo fomu, haijalishi ni nani anaweka pingamizi as long as amefuata taratibu zilizopo kisheria. Haya mambo ya kujifanyia mambo kiholela ndiyo yameifikisha hii nchi hapa mahali tulipo. Lazima tukubali kumeza machungu yatokanayo na kukurupuka kwetu bila kuangalia taratibu zikoje. Na kwa chama makini, linapotokea kosa la kiufundi kama hilo suluhu siyo kukimbilia kulaumu waliokuwekea pingamizi ama sheria iliyopo ila ni kujipanga upya ili kesho na keshokutwa haya yasijitokeze. CUF wana haki kabisa ya kuweka pingamizi kwa vile ni chama cha siasa cha upinzani dhidi ya vyama vingine vyote vyenye usajili hapa nchini. Haya mambo ya kujitengenezea sijui muungano wa vyama ni upumbavu tu, labda viamue kujiua na kuunda chama kimoja ndipo nitawaelewa.

Suala la tatu ni hivi: Hao wagombea wa vyama vingine waliapishwa na nani iwapo ilikuwa vigumu kwa mgombea wa Chadema kupata mahali halali (kwa sheria za uchaguzi) pa kwenda kuapa kwa kisingizio cha siyo siku ya kazi?

Na je, ni kwa nini hakuna aliyelalamikia kwamba fomu za wagombea zisingeweza kurudishwa siku hiyo kwa vile ingekuwa vigumu kwa wahusika kukamilisha matakwa ya kisheria ikiwemo ni pamoja na kuapa kwa mamlaka halali? Hii yote ni kwa sababu ya kukurupuka tu bila kuwa makini.

MKuu; viapo vyangu vya chuoni kusoma; kwenda nje; kiwanja; shamba; mkopo wangu vyote sikwenda kwa Hakimu wilaya- je ni batili- maanake mamlaka zote hizo zinafanya kazi kinyume? kiapoa cha uchaguzi kina sheria yake? mnijuze jamani sio ushabiki maana hapa ni sheria tu
 
Kuna sheria mbili (kuu) zinazohusiana na masuala ya viapo-kuna sheria ya Oaths (Judicial proceedings) na Statutory Decralation act-1966.
Sheria hizi zinampa hakimu na wakili mamlaka ya kutoa viapo.
lakini sheria ya uchaguzi inakipengele kinachosema kuwa mtu anayewania nafasi ya uongoni ni sharti ale kiapo kwa Hakimu tu.
kwa hiyo hapa ni suala la tafisir ya sheria. Chadema wanaweza kusimama katika sheria hizo mbili mama na kusema kuwa mgombea wao alikuwa sahihi kula kiapo kwa wakili. lakini wakati huo huo, Tume inaweza kusimama kwenye sheria ya uchaguzi ambayo inataka mgombea kula kiapo kwa hakimu
 
Sheria msumeno wakili Shitambala alitakiwa kulijua hili mwanzo, huwezi "kujiapisha" kwenye kampuni yako mwenyewe.

Mambo mengine tunalalamika for the sake of it tu.....
 
MKuu; viapo vyangu vya chuoni kusoma; kwenda nje; kiwanja; shamba; mkopo wangu vyote sikwenda kwa Hakimu wilaya- je ni batili- maanake mamlaka zote hizo zinafanya kazi kinyume? kiapoa cha uchaguzi kina sheria yake? mnijuze jamani sio ushabiki maana hapa ni sheria tu


Katika maelezo yako sijaona mahali popote uliposema uliapa kwa ajili ya kushiriki uchaguzi.

Vipo viapo vya aina nyingi tu; na taratibu zake ziko wazi. Mojawapo ni hivyo ulivyoapa wewe kwa taratibu zilizopo (na iwapo kuna sheria ilivunjwa wakati una kula kiapo, hilo ni kosa kama mengine).

Hata Rais wa nchi ana kiapo chake; waziri, katibu mkuu n.k. Na hao wote wanaapishwa na mamlaka zilizotajwa kisheria na kikatiba.
 
Kuna sheria mbili (kuu) zinazohusiana na masuala ya viapo-kuna sheria ya Oaths (Judicial proceedings) na Statutory Decralation act-1966.
Sheria hizi zinampa hakimu na wakili mamlaka ya kutoa viapo.
lakini sheria ya uchaguzi inakipengele kinachosema kuwa mtu anayewania nafasi ya uongoni ni sharti ale kiapo kwa Hakimu tu.
kwa hiyo hapa ni suala la tafisir ya sheria. Chadema wanaweza kusimama katika sheria hizo mbili mama na kusema kuwa mgombea wao alikuwa sahihi kula kiapo kwa wakili. lakini wakati huo huo, Tume inaweza kusimama kwenye sheria ya uchaguzi ambayo inataka mgombea kula kiapo kwa hakimu

Asanate sana Mpita Njia; walau umenitoa tongo tongo; SO for this sheria zinapingana? kila mtu anaweza kuchukua msimamo wake?; maana mie mbumbumbu wa sheria lakini at the end of the day lazima ipo sheria ambayo haiendi kinyume na Katiba na ambayo ndiyo itafuatwa;ebu tujuze zaidi mkuu au yeyote mwenye upenyo; this is technical sio ushabiki
 
Katika maelezo yako sijaona mahali popote uliposema uliapa kwa ajili ya kushiriki uchaguzi.

Vipo viapo vya aina nyingi tu; na taratibu zake ziko wazi. Mojawapo ni hivyo ulivyoapa wewe kwa taratibu zilizopo (na iwapo kuna sheria ilivunjwa wakati una kula kiapo, hilo ni kosa kama mengine).

Hata Rais wa nchi ana kiapo chake; waziri, katibu mkuu n.k. Na hao wote wanaapishwa na mamlaka zilizotajwa kisheria na kikatiba.


So kila kiapo na muapaji kutegemea na swala kuna tena sheria yake? (Mhh kwa watu wa computer this will be duplication of sherias)
Mie haikuhusu uchaguzi mkuu; kama nilivyoeleza; mie nataka ati the end of day sio Chadema tu; hata CCM au TLP au CUF wasije tena wakarudia kosa kwa kutokujua; na hii forum kumbuka hata mkulu anachungulia sana huku; so tujuze bila kuchoka; Ebu tupe sheria mama ( katiba inasemaje kuhusu kiapo)
 
Kaazi kweli kweli.
Hapo CCM mme haribu sana mmeamusha machungu ya watu kibao kama lengo lao lilikuwa kumnyamazisha na kuwadhoofisha CHADEMA basi wamelikologa jimbo hiloooooo wamesha lipoteza.Watu kila kitu tunaapa kwa mawakili wanao tambulika sasa sijui ni lini na ni wapi wamesema kuwa wakili haruhusiwi kuapisha watu.
Huyo mama katishiwa nyau ndo maana kaamua hivyo wakimkalia kohoni atasema ukweli nani kamwambie apoteshe uuma.Nawasi wasi anaweza akapindisha hata matokeo amesha onyesha wazi wazi kuwa ni dhaifu.
 
Kuna sheria mbili (kuu) zinazohusiana na masuala ya viapo-kuna sheria ya Oaths (Judicial proceedings) na Statutory Decralation act-1966.
Sheria hizi zinampa hakimu na wakili mamlaka ya kutoa viapo.
lakini sheria ya uchaguzi inakipengele kinachosema kuwa mtu anayewania nafasi ya uongoni ni sharti ale kiapo kwa Hakimu tu.
kwa hiyo hapa ni suala la tafisir ya sheria. Chadema wanaweza kusimama katika sheria hizo mbili mama na kusema kuwa mgombea wao alikuwa sahihi kula kiapo kwa wakili. lakini wakati huo huo, Tume inaweza kusimama kwenye sheria ya uchaguzi ambayo inataka mgombea kula kiapo kwa hakimu

CHADEMA kikiwa ni chama cha siasa chenye wanasheria waliobobea kuanzia kwa Tundu Lisu, Halima Mdee hadi kwa Shitambala mwenyewe, napata shida sana kuamini kama hawaijui sheria ya uchaguzi.Kama wameweza kuisoma sheria mama walishindwaje kuisoma hiyo sheria ya uchaguzi?
Au waliamua kwa makusudi kuleta mpambano wa kisheria?au hakimu wa wilaya aligoma kumwapisha shitambala kwahiyo akaamua kuapishwa na wakili? au walishindwa kumpata hakimu wa wilaya?maana hizi tarehe za sikukuu labda hakimu kaenda vijijini kula krismas!!Kwa kweli bado sijapata majibu ya hayo maswali, na sijui CHADEMA watawaeleza nini wapenzi na wanachama wao, na sijui watwezaje kuendelea kuwaaminisha watu/wananchi kuwa wao ni chama makini na mbadala wa ccm katika nchi yetu.
 
Asanate sana Mpita Njia; walau umenitoa tongo tongo; SO for this sheria zinapingana? kila mtu anaweza kuchukua msimamo wake?; maana mie mbumbumbu wa sheria lakini at the end of the day lazima ipo sheria ambayo haiendi kinyume na Katiba na ambayo ndiyo itafuatwa;ebu tujuze zaidi mkuu au yeyote mwenye upenyo; this is technical sio ushabiki

Katika legal technicalities, msimamizi wa uchaguzi anawekuwa sawa zaidi (haimaanishi kuwa mgombea wa chadema yuko wrong) wka sababu ameitumia sheria ya uchaguzi kwa sababu kinachoshughulikiwa hapa ni uchaguzi specifically. Hivyo, kwa sababu ipo sheria specifically inayohusu masuala ya uchaguzi, ndiyo inayopaswa kuangaliwa zaidi kuliko sheria nyingine. kama suala linalobinshaniwa lingekuwa halimo kwenye sheria ya uchaguzi, basi mgombea angekuwa na haki kutumia sheria nyingine ili kuhakikisha anapata haki yake. mathalani kama sheria ya uchaguzi ingekuwa haitoa specific condition kuwa mgombea anatakiwa kuapa wapi, basi wagombea wangekwua na hak ya kutumia zile sheria mbili kuapa. lakini kwa sababu sheria ya uchaguzi inatoa utaratibu wa kuapa, inapaswa kuheshimiwa hiyo katika masuala ya uchaguzi. Kama ikibainika kuwa sheria hiyo ya uchaguzi, au kipengele kinachobishaniwa kinapingana na katiba, hapo NEC ingekuwa matatizoni na sheria yake
 
Kuna sheria mbili (kuu) zinazohusiana na masuala ya viapo-kuna sheria ya Oaths (Judicial proceedings) na Statutory Decralation act-1966.
Sheria hizi zinampa hakimu na wakili mamlaka ya kutoa viapo.
lakini sheria ya uchaguzi inakipengele kinachosema kuwa mtu anayewania nafasi ya uongoni ni sharti ale kiapo kwa Hakimu tu.

Kaka kama una uhakika na hili.... well but kwa mfano sheria ya mazingira ya 2004 inasema wazi kuwa kama kuna sheria nyingine za mazingira e.g. forect Act, Regulations zinapinga nao basi hii ya Mazingira ngo last say. Je, kwenye sheria ya uchaguzi hii ipo? Je unaweza kuweka masharti bila kuwa na Principal Act?
 
Kwanza nikupongeze kwa kauli nzito kama hii. Ni vizuri umelisemea hili la udini, maana nilidhani wanasingiziwa hawa jamaa. Kumbe hata ninyi wanasiasa mnakubaliana nalo huko kwenye vyama vyenu.

Pili, kama kweli kuna ukiukwaji wa sheria katika ujazaji wa hizo fomu, haijalishi ni nani anaweka pingamizi as long as amefuata taratibu zilizopo kisheria. Haya mambo ya kujifanyia mambo kiholela ndiyo yameifikisha hii nchi hapa mahali tulipo. Lazima tukubali kumeza machungu yatokanayo na kukurupuka kwetu bila kuangalia taratibu zikoje. Na kwa chama makini, linapotokea kosa la kiufundi kama hilo suluhu siyo kukimbilia kulaumu waliokuwekea pingamizi ama sheria iliyopo ila ni kujipanga upya ili kesho na keshokutwa haya yasijitokeze. CUF wana haki kabisa ya kuweka pingamizi kwa vile ni chama cha siasa cha upinzani dhidi ya vyama vingine vyote vyenye usajili hapa nchini. Haya mambo ya kujitengenezea sijui muungano wa vyama ni upumbavu tu, labda viamue kujiua na kuunda chama kimoja ndipo nitawaelewa.

Suala la tatu ni hivi: Hao wagombea wa vyama vingine waliapishwa na nani iwapo ilikuwa vigumu kwa mgombea wa Chadema kupata mahali halali (kwa sheria za uchaguzi) pa kwenda kuapa kwa kisingizio cha siyo siku ya kazi?

Na je, ni kwa nini hakuna aliyelalamikia kwamba fomu za wagombea zisingeweza kurudishwa siku hiyo kwa vile ingekuwa vigumu kwa wahusika kukamilisha matakwa ya kisheria ikiwemo ni pamoja na kuapa kwa mamlaka halali? Hii yote ni kwa sababu ya kukurupuka tu bila kuwa makini.



Maneno yako yote nimeyakubali na hasa hali ya mtu na kuweka pingamizi.Nakukumbusha kwamba Chadema hawajaenda magazetini ila wataalam wake wako msituni na wataibuka punde kusema walicho kifanya .Nakuweka sawa tu uweke sawa record yako baadaye .Nani Chadema kaenda kwenye magazeti na kuanza kulalama ? Nitajie mmojawapo tafadhali .Kama hakuna basi ujue watu wako makini na wana endelea na taratibu za kisheria .CUF wana haki ya pingamizi kabisa .
 
Tatizo la Tanzania ni hizi sheria za kutegeana. Mahali pengine popote kunakuwa na muda wa kufanya marekebisho kama mtu amefanya makosa. Akishindwa kurekebisha basi ndio anachukuliwa hatua.

Ilitakiwa kuwe na wiki moja ya kuwakilisha forms ili hao tume wazipitie na wale wanaopinga jambo wafanye hivyo na kisha mhusika anapewa muda wa kurekebisha hizo kasoro. Akishindwa hapo ndipo ingekuwa sawa kutolewa.

Ila nao CHADEMA ilikuwaje wakashindwa kuiona na kuelewa maana ya sheria hiyo. Tatizo la Tanzania ni watu kujifanya wako juu ya sheria na mara nyingi kupenda mambo ya mkato mkato. Mwanasheria anashindwa kufuata sheria kisha anasingizia muda na sikukuu? Hao viongozi wa kitaifa nao hawakuliona hilo? Kwenye sheria lazima tuwe makini, hakuna kupindisha sheria. Kama haifai basi tuipinge ili ibadilishwe huko mbeleni.

Ukiwa chama cha upinzani, tena Afrika lazima uchukue extra care kuhakikisha unafanya mambo yote kwa mujibu wa sheria.

Tumekosa utamu wa mpambano kati ya CCM na CHADEMA.
 
Kuna mwanasheria amenipa hints labda tuzifanyie kazi;
- Hii sheria ya uchaguzi inasupersede sheria nyingine?
- Ipi sheria ya kwanza kutoka inakuwa affected na sheria nyingine kama katiba haikusema?
- Wakili na Hakimu katika sheria za kimahakama zinasemaje?

Ameniambia kuwa nikiweza kujibu haya basi nitapata mwanga maana sikutoa ahadi ya kumlipa.

asanteni
 
Kaka kama una uhakika na hili.... well but kwa mfano sheria ya mazingira ya 2004 inasema wazi kuwa kama kuna sheria nyingine za mazingira e.g. forect Act, Regulations zinapinga nao basi hii ya Mazingira ngo last say. Je, kwenye sheria ya uchaguzi hii ipo? Je unaweza kuweka masharti bila kuwa na Principal Act?

Mkuu, sheria ya mazingira ilitungwa huku watungaji wakujua kuwa kuna baadhi ya sheria ambazo zilikuwa zinapingana na baadhi ya makatazo waliyokuwa wameyaweka kwenye sheria hiyo, na ndio maana wakaweka angalizo hilo.
Kwa upande wa sheria hizi tatu, kwanza hakuna kati yazo yenye kipengele kama hicho. Na kimsingi, hakuna kipengele hicho kwa sababu sheria hizo zote hazipingani. Zile sheria za kuapiasha za awali, zinatoa mamlaka kwa hakimu na mawakili kuapisha. Sheria ua uchaguzi inasema atakayeapisha wagombea ni hakimu (ambaye ameshaidhinishwa kuapishwa kwenye ile sheria ya awali). Hivyo hakuna mgongano wa sheria hizi. Kinachogomba hapa ni tafsiri tu ya sheria hizi, wakati Tume inasimamia kwenye sheria ya uchaguzi, Mgombea wa chadema anasimamia kwenye sheria zile nyingine.
Lakini kwa sababu kinachofanyika ni uchaguzi, tukio ambalo lina specific piece of legislation, nadhani Tume wanaweza kwua sahihi zaidi wka sababu wanatumia specific legislation kuhusiana na tukio linalotokea. Mgomba wa chadema anaweza kuwa sahihi kuapa kwa wakili wka sababu sheria inaruhusu hivyo lakibni sheria ya uchaguzi haitaki hivyo na inatoa specific directives za namna ya kuapa
 
Tatizo la Tanzania ni hizi sheria za kutegeana. Mahali pengine popote kunakuwa na muda wa kufanya marekebisho kama mtu amefanya makosa. Akishindwa kurekebisha basi ndio anachukuliwa hatua.

Ilitakiwa kuwe na wiki moja ya kuwakilisha forms ili hao tume wazipitie na wale wanaopinga jambo wafanye hivyo na kisha mhusika anapewa muda wa kurekebisha hizo kasoro. Akishindwa hapo ndipo ingekuwa sawa kutolewa.

Ila nao CHADEMA ilikuwaje wakashindwa kuiona na kuelewa maana ya sheria hiyo. Tatizo la Tanzania ni watu kujifanya wako juu ya sheria na mara nyingi kupenda mambo ya mkato mkato. Mwanasheria anashindwa kufuata sheria kisha anasingizia muda na sikukuu? Hao viongozi wa kitaifa nao hawakuliona hilo? Kwenye sheria lazima tuwe makini, hakuna kupindisha sheria. Kama haifai basi tuipinge ili ibadilishwe huko mbeleni.

Ukiwa chama cha upinzani, tena Afrika lazima uchukue extra care kuhakikisha unafanya mambo yote kwa mujibu wa sheria.

Tumekosa utamu wa mpambano kati ya CCM na CHADEMA.


Mimi siku zote sitafungamana na mtu yeyeote aishindwa kuelewa hata kama ni rafiki yangu sana .Wewe Mtanzania tumekaa sote hapo UK u rafiki yangu sana kama ES lakini nakupinga hapa .

Sheria iko wazi na pia kuna kutegeana umesema vyema .Ila unaambiwa siku ya kula kiapo ilikuwa sikukuu Hakimu angalipatikana wapi ili kiapo kitolewe ? Sasa wakasema kwa kuwa sheria inaruhusu wote 2 kutoa kiapo then twende kwa aliyeko jirani maana yeye anapatikana .Sasa nani yuko juu ya sheria hapa wandugu ?
 
Naomba niungane na wenzangu kuomba msaada wa kisheria kuhusu masharti ya kiapo yaliyohitajika kwani katika hali ya kawaida hata kama sio graduate ni vigumu kukiuka sharti nyeti kama hilo.
 
Mkuu, sheria ya mazingira ilitungwa huku watungaji wakujua kuwa kuna baadhi ya sheria ambazo zilikuwa zinapingana na baadhi ya makatazo waliyokuwa wameyaweka kwenye sheria hiyo, na ndio maana wakaweka angalizo hilo.
Kwa upande wa sheria hizi tatu, kwanza hakuna kati yazo yenye kipengele kama hicho. Na kimsingi, hakuna kipengele hicho kwa sababu sheria hizo zote hazipingani. Zile sheria za kuapiasha za awali, zinatoa mamlaka kwa hakimu na mawakili kuapisha. Sheria ua uchaguzi inasema atakayeapisha wagombea ni hakimu (ambaye ameshaidhinishwa kuapishwa kwenye ile sheria ya awali). Hivyo hakuna mgongano wa sheria hizi. Kinachogomba hapa ni tafsiri tu ya sheria hizi, wakati Tume inasimamia kwenye sheria ya uchaguzi, Mgombea wa chadema anasimamia kwenye sheria zile nyingine.
Lakini kwa sababu kinachofanyika ni uchaguzi, tukio ambalo lina specific piece of legislation, nadhani Tume wanaweza kwua sahihi zaidi wka sababu wanatumia specific legislation kuhusiana na tukio linalotokea. Mgomba wa chadema anaweza kuwa sahihi kuapa kwa wakili wka sababu sheria inaruhusu hivyo lakibni sheria ya uchaguzi haitaki hivyo na inatoa specific directives za namna ya kuapa

Mpita Njia,

Hata mgombea mwenyewe kwenye utetezi wake alisingizia mahakama kufungwa shauri ya sikukuu. Hii ni dalili anajua sheria inasemaje ila sasa yametokea wataanza kulalamika kwamba wanaonewa. Wanasheria huwa wanaongoza kwa kuvunja sheria, ilitakiwa chama cha siasa kiwe na watu wa kuhakikisha kila kitu kiko OK kabla ya kupeleka hizo forms.

Sheria ni msumeno, mtu akilimwa kwa sheria halali kwa kweli hakuna cha kusikitika hapo.

Labda sasa tuseme hiyo sheria haifai. Ugomvi wangu mimi ni kutokuwa na nafasi ya kurekebisha makosa. Kwanini tunategea watu wafanya kosa hata dogo ili tuwatupe nje?

Lengo la uchaguzi ni kushirikisha watu wengi iwezekanavyo ili wananchi wachague wanayemtaka na sio watu kuondolewa na tume.
 
Hii sheria iliwahi kumuondoa Njelu Kasaka, Mbunge wa zamani wa CCM aliyehamia CUF baada ya kushindwa ktk kura ya maoni ndani ya CCM. Alienda apa kwa Wakili badala ya Hakimu na kusema ilikuwa ngumu kwake kuwahi mahakamani siku hiyo (mahakama ilikuwa mbali ama ilikuwa week end siku hiyo). Tume ya Uchaguzi waliligundua hilo na kumuondoa asigombee ubunge. Huyu jamaa karudi tena CCM.
 
Mimi siku zote sitafungamana na mtu yeyeote aishindwa kuelewa hata kama ni rafiki yangu sana .Wewe Mtanzania tumekaa sote hapo UK u rafiki yangu sana kama ES lakini nakupinga hapa .

Sheria iko wazi na pia kuna kutegeana umesema vyema .Ila unaambiwa siku ya kula kiapo ilikuwa sikukuu Hakimu angalipatikana wapi ili kiapo kitolewe ? Sasa wakasema kwa kuwa sheria inaruhusu wote 2 kutoa kiapo then twende kwa aliyeko jirani maana yeye anapatikana .Sasa nani yuko juu ya sheria hapa wandugu ?

Lunyungu,

Hao wagombea wa CCM na CUF walienda kuapa wapi? Tatizo hapo ni planning. Aliyekuwa anapanga uchaguzi wa CHADEMA alichemsha, ilitakiwa ajue ratiba nzima mpaka kurudisha forms.

Tatizo la Tanzania ni ubabaishaji mkubwa mpaka kwenye hivyo vyama. Inaelekea hata hawana watu ambao wanajua sheria zinasema nini.

Ukisoma maelezo ya Mpita Njia inaelekea sheria iko wazi na hata huyo mgombea alijua hicho. Lengo lake la kwanza lilikuwa kwenda mahakamani lakini baada ya kushindwa ndio akaamua kuapa kwa wakili.

Mimi sina huruma yoyote na mtu ambaye hafuati sheria ila pia niko concerned na hizi sheria za kutegeana.

Lunyungu, acha usanii, tumekaa wote UK wapi? kwi kwi kwi!!!
 
Kuna mwanasheria amenipa hints labda tuzifanyie kazi;
- Hii sheria ya uchaguzi inasupersede sheria nyingine?
- Ipi sheria ya kwanza kutoka inakuwa affected na sheria nyingine kama katiba haikusema?
- Wakili na Hakimu katika sheria za kimahakama zinasemaje?

Ameniambia kuwa nikiweza kujibu haya basi nitapata mwanga maana sikutoa ahadi ya kumlipa.

asanteni

Sheria ya uchaguzi inasupercede hizi nyingine wka sababu yenyewe i current zaidi. Moja kati ya zile mbili ilitunmgwa mwaka 1966 (nyingine sikumbuki lini) lakini nayo ni miaka ya zamani. Sheria ya uchgzui imekuja kutokana na kuejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, kwa hiyo yenyewe ni current zaidi.
Katika sheria za kimahakama, (specifically zile sheria mbili za masuala ya kuapishwa) wote wanapewa mamlaka ya kuapisha-tofauti nadhani ipo katika aina za viapo ambavyo wanaruhusiwa. Siwezi kuingia wka udnani katika hilo la aina za viapo kwa sababu sina uhakika nalo-mpaka nikachungulie
 
Back
Top Bottom