CHIPESI NAMISUKU
Member
- Oct 7, 2019
- 51
- 156
Leo DR Tulia ambaye Ni naibu Spika alikula Chakula Cha mchana kwa mamaNtilie Jijini Mb
eya. Kabla ya kuhitimisha vikao vya bunge alisema atagombea mwaka huu sisi HATUJUI ni Jimbo gani lakini niliwahi kuandika kuwa Sugu ASIMBEZE DR TULIA.... Niwakumbushe kidogo, bado msimamo wangu na analysis yangu katika Jimbo hili Kama watakutana Sugu na Dr Tulia unabaki vile vile.
Uchaguzi uliopita CCM tulitandikwa hapa kisawasawa mgombea wetu SAMBWEE Mwalyego Shitambala alipata kura 54,296 huku Mgombea wa Chadema Sugu akipata Mara mbili ya kura 108,566 karibia Mara mbili ya mgombea wa CCM.
Sugu 2015 alibebwa na vitu viwili vikubwa Moja uimara wa mgombea urais waliyekuwa naye Lowassa lakini cha pili Ni hulka ya majimbo ya mjini huwa yanatutesa Sana CCM.
2020
Vita ya kipindi hiki Ni ngumu kidogo kwa Sugu kutokana na aina ya Mgombea anayejipitisha pitisha jimboni. Dr Tulia uwezo wake Ni mkubwa na ana mvuto wa kisiasa kuliko mgombea wa CCM 2015. Mambo kadhaa yanayombeba Tulia Elimu yake, Kuna future mbele ya kuwa kiongozi mkubwa ukiachana na Ubunge anaweza kuukwaa uwaziri au hata Uspika kabisa hili Lina faida kwa wanambeya mnapopata mtoto wa kuingia kwenye Baraza la mawaziri si nafasi ya kuchezea, ground work kaifanya vizuri sana, kwa namna flan naye Ni mbishi kwenye Siasa sio mlaini Kama mgombea wetu wa 2015, Nguvu ingine ya Tulia Ni jinsia yake, Kama atacheza na mahitaji ya wanawake vizuri watambeba Sana kwenye uchaguzi.
Akiweza kuwaunganisha kundi hili atashinda kirahisi Sana mbeya. Mwisho kitakachombeba Ni Mgombea urais wetu Dr Magufuli, Dr Magufuli kwa Sasa kwa ukanda huu wa Afica mashariki amekuwa na Siasa za aina yake tutakuja kulichambua hili baadaye.
Kinachoweza kumwangusha kikubwa Ni kura za maoni hata Kama atapenya CCM Ina tabia ya kupasuka baada ya kura za maoni. Cha pili Ni Jimbo analogombea nimesema toka awali kuwa majimbo ya mjini sio Rafiki Sana kwa CCM.
Sugu yeye Ubora wake upo kwenye uanaharakati, tukumbuke huyu kiasili Ni mwanaharakati, Siasa za harakati zinapendwa Sana na Vijana. Kama vijana watajiandikisha wengi Mbeya CCM itapata wakati mgumu, Jambo la pili kwa sugu Ni kwamba yeye kizingiti cha Kura za maoni ameshakivuka huu Ni utaratibu wao kwenye chama, anaonekana hatashindanishwa na Mtu kutokana na maneno yake. Jambo la tatu Ni ulevi wa majimbo ya mjini katika Siasa za Upinzani hapa kutamnufaisha kuliko CCM.
UDHAIFU wake Ni ahadi alizotoa hajazikamilisha, yaani ukiacha maneno mengi anayoongea Sugu hakuna Mambo makubwa Sana aliyoyafanya atakayokumbukwa nayo. Pili Ni tabia ya vijana kutokupenda kupiga kura, anaweza kuwa nao wengi wa kumshabikia lakini siku ya kura wakakosa sifa ya kupiga kura, aina ya mgombea anayekutana naye mwaka huu Kama akipita Tulia ana nguvu kuliko yule aliyekutana naye 2015, kitu kingine ambacho atakutana nacho na kitamuathiri Ni Siasa za propaganda, Tukumbuke Sugu kwa Sasa kajiendeleza Sana kiuchumi ana vitega uchumi vingi mpaka hotel, maisha yake hayalingani na ya wamachinga wa pale Mbeya kwa Sasa hili CCM lazima walitumie na Tukumbuke hakuna urafiki Kati ya maskini na tajiri. Mwisho kabisa Ni nguvu aliyonayo Rais Magufuli kwenye Medan za kisiasa.
Sugu asichukulie Poa hili Jimbo la Mbeya litamponyoka Mambo sio marahisi Kama 2015. Ni tahira tu anayeweza kusema Sugu atashinda kwa asilimia au Tulia atashinda kwa asilimia. Kila mtu ana nafasi sawa ya kushinda hili Jimbo kwa Sasa (Equal chance).
Naelekea Mbeya....
eya. Kabla ya kuhitimisha vikao vya bunge alisema atagombea mwaka huu sisi HATUJUI ni Jimbo gani lakini niliwahi kuandika kuwa Sugu ASIMBEZE DR TULIA.... Niwakumbushe kidogo, bado msimamo wangu na analysis yangu katika Jimbo hili Kama watakutana Sugu na Dr Tulia unabaki vile vile.
Uchaguzi uliopita CCM tulitandikwa hapa kisawasawa mgombea wetu SAMBWEE Mwalyego Shitambala alipata kura 54,296 huku Mgombea wa Chadema Sugu akipata Mara mbili ya kura 108,566 karibia Mara mbili ya mgombea wa CCM.
Sugu 2015 alibebwa na vitu viwili vikubwa Moja uimara wa mgombea urais waliyekuwa naye Lowassa lakini cha pili Ni hulka ya majimbo ya mjini huwa yanatutesa Sana CCM.
2020
Vita ya kipindi hiki Ni ngumu kidogo kwa Sugu kutokana na aina ya Mgombea anayejipitisha pitisha jimboni. Dr Tulia uwezo wake Ni mkubwa na ana mvuto wa kisiasa kuliko mgombea wa CCM 2015. Mambo kadhaa yanayombeba Tulia Elimu yake, Kuna future mbele ya kuwa kiongozi mkubwa ukiachana na Ubunge anaweza kuukwaa uwaziri au hata Uspika kabisa hili Lina faida kwa wanambeya mnapopata mtoto wa kuingia kwenye Baraza la mawaziri si nafasi ya kuchezea, ground work kaifanya vizuri sana, kwa namna flan naye Ni mbishi kwenye Siasa sio mlaini Kama mgombea wetu wa 2015, Nguvu ingine ya Tulia Ni jinsia yake, Kama atacheza na mahitaji ya wanawake vizuri watambeba Sana kwenye uchaguzi.
Akiweza kuwaunganisha kundi hili atashinda kirahisi Sana mbeya. Mwisho kitakachombeba Ni Mgombea urais wetu Dr Magufuli, Dr Magufuli kwa Sasa kwa ukanda huu wa Afica mashariki amekuwa na Siasa za aina yake tutakuja kulichambua hili baadaye.
Kinachoweza kumwangusha kikubwa Ni kura za maoni hata Kama atapenya CCM Ina tabia ya kupasuka baada ya kura za maoni. Cha pili Ni Jimbo analogombea nimesema toka awali kuwa majimbo ya mjini sio Rafiki Sana kwa CCM.
Sugu yeye Ubora wake upo kwenye uanaharakati, tukumbuke huyu kiasili Ni mwanaharakati, Siasa za harakati zinapendwa Sana na Vijana. Kama vijana watajiandikisha wengi Mbeya CCM itapata wakati mgumu, Jambo la pili kwa sugu Ni kwamba yeye kizingiti cha Kura za maoni ameshakivuka huu Ni utaratibu wao kwenye chama, anaonekana hatashindanishwa na Mtu kutokana na maneno yake. Jambo la tatu Ni ulevi wa majimbo ya mjini katika Siasa za Upinzani hapa kutamnufaisha kuliko CCM.
UDHAIFU wake Ni ahadi alizotoa hajazikamilisha, yaani ukiacha maneno mengi anayoongea Sugu hakuna Mambo makubwa Sana aliyoyafanya atakayokumbukwa nayo. Pili Ni tabia ya vijana kutokupenda kupiga kura, anaweza kuwa nao wengi wa kumshabikia lakini siku ya kura wakakosa sifa ya kupiga kura, aina ya mgombea anayekutana naye mwaka huu Kama akipita Tulia ana nguvu kuliko yule aliyekutana naye 2015, kitu kingine ambacho atakutana nacho na kitamuathiri Ni Siasa za propaganda, Tukumbuke Sugu kwa Sasa kajiendeleza Sana kiuchumi ana vitega uchumi vingi mpaka hotel, maisha yake hayalingani na ya wamachinga wa pale Mbeya kwa Sasa hili CCM lazima walitumie na Tukumbuke hakuna urafiki Kati ya maskini na tajiri. Mwisho kabisa Ni nguvu aliyonayo Rais Magufuli kwenye Medan za kisiasa.
Sugu asichukulie Poa hili Jimbo la Mbeya litamponyoka Mambo sio marahisi Kama 2015. Ni tahira tu anayeweza kusema Sugu atashinda kwa asilimia au Tulia atashinda kwa asilimia. Kila mtu ana nafasi sawa ya kushinda hili Jimbo kwa Sasa (Equal chance).
Naelekea Mbeya....