Sugu asithubutu kuchukua fomu kushindana na Dkt. Tulia Mbeya mjini, hakuna mwenye akili timamu atakayempigia kura tena

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,301
9,727
Ndugu zangu Watanzania,

Huo ni ukweli mchungu ambao napenda umfikie Joseph mbilinyi au Sugu, kuwa nafasi aliyoipata siku za nyuma ya kuongoza jimbo la Mbeya mjini kwa miaka kumi haipo tena.

Haiwezi kurudi tena, hawezi kuipata tena na hakuna mwenye hamu wala wazo la kumpigia na kupoteza kura yake kumpa kura ya ndio Sugu.

Kwa kuwa katika miaka kumi jimbo la Mbeya mjini lilikuwa na Mbunge hewa, lilikuwa wazi,lilikosa wa kulisemea na kulipigania Bungeni, lilikosa mtetezi, lilikosa sauti yenye ushawishi, nguvu na kusikika masikioni mwa serikali.

Miaka yote ya Ubunge wake Sugu alifanya kazi ya kuzurula tu, kupigania maslahi yake binafsi na tumbo lake, alifanya kazi ya kutafuna posho na mshahara wa ubunge pasipo kuufanyia kazi.

Wananchi katika miaka yote ya Sugu walikosa mahali pa kukimbilia kupeleka shida, kero na changamoto zao kwa kuwa muda wote Sugu alikuwa bize na biashara zake, mambo yake, bize na Dar tu huku Mbeya akifanya kama kituo cha kugongea muhuri wa kwenda Bungeni kama mbunge.

Aliwafanya wana Mbeya kama wajinga, akajiona yeye ni mtoto pendwa na kwamba yeye ni yeye mwenye hati miliki na jimbo la Mbeya mjini na kwamba hayupo wa kuchukua nafasi hiyo isipokuwa yeye tu aliyemteule wa Mbeya mjini.

Wanambeya walipochoka na dharau zake na ubabaishaji wake pamoja na kushindwa kwake kutimiza majukumu yake ya kibunge, wakaamua kugeukia upande wa pili kulikokuwa na CCM ikiwakilishwa na wakili Nguli na msomi, walimu wa walimu wa sheria, Naibu Mwanasheria Mkuu Mstaafu na Naibu Speaker wa Bunge Dr. Tulia Acksoni Mwansasu kwa kumpa ushindi wa kishindo ulioitetemesha Mbeya nzima.

Dada msomi, msikivu wa hali ya juu, mkalimu, mcheshi, mchapakazi, mnyenyekevu, mpole, mwenye moyo wa huruma na upendo, mzalendo wa kweli na aliyebarikiwa na Mungu kipawa na Karama ya uongozi.

Mwenye kujuwa nini maana ya maisha, mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu na aliyekulia katika maisha ya kawaida na ya chini ya kipato cha kuuza mboga mboga huku akimtumainia na kumtegea Mungu wake katika kila hatua aliyopita.

Wana Mbeya wameshuhudia ndani ya muda mfupi wa Ubunge wa Dr. Tulia namna Mbeya ilivyobadilika, namna inavyochipua kwa miradi ya maendeleo, namna inavyoendelea kupokea mamilioni kwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Wana mbeya wanaona kwa mara ya kwanza chini ya Ubunge wa Dr. Tulia wanakwenda kupata barabara za lami njia nne kutoka Igawa Mbeya hadi Tunduma, zenye urefu wa KM 237.9 wana shuhudia namna ambavyo shule, vyumba vya madarasa, zahanati, vituo vya afya, barabara za mitaa zimekuwa zikijengwa wakati wote wa Dr. Tulia.

Wana Mbeya wameshuhudia namna wakati huu wa Dr. Tulia ambavyo viongozi wakuu wa serikali wamekuwa wakifika na kuitembelea Mbeya na kuahidi kuleta mamilioni kwa mabilioni ya pesa kwa ajili ya miradi mbalimbali.

Wana Mbeya wanaona namna jiji linavyoendelea kupangwa katika kulifanya liwe na sura halisi na hadhi ya jiji, na siyo kuwa jiji lenye mkusanyiko wa nyumba nyingi tu.

Ujio huo wa maendeleo na miradi ya maendeleo mfululizo ambayo wanambeya wameipata ndani ya muda mfupi imewafanya wajute na walaani sana kumpatia Sugu miaka kumi kuwa Mbunge wa Mbeya mjini.

Imewafanya wajipige vifua vyao na kuapa kuwa katu na kamwe hawatampa kura za ndio tena sugu kuwa mbunge wa Mbeya mjini. Wanasema walifanya makosa ambayo kamwe hawawezi kuyarudia kuyafanya.

Hawawezi kurudia mzaha huo wa kufanya majaribio ya maisha yao kwa kumpa mtu uongozi asiye jitambua wala kutambua thamani na heshima aliyokuwa amepewa.

Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Tulia inabidi akuangalie kimtindo

Unampigania sana

Ova
Mimi naongea ukweli kwa namna mambo yanavyokwenda na namna wanambeya wanavyozungumza kwa vinywa vyao Wenyewe .mbeya mjini inamtaka Dr Tulia na imeridhishwa na uchapa kazi wake na ndio chaguo lao tena uchaguzi ujao. Hawapo tayari kurudia makosa waliyofanya huko nyuma ya kumpa mtu ubunge asiye jitambua wala kutambua majukumu yake.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Huo ni ukweli mchungu ambao napenda umfikie Joseph mbilinyi au Sugu. kuwa Nafasi aliyoipata siku za nyuma ya kuongoza jimbo la Mbeya mjini kwa miaka kumi haipo tena ,haiwezi kurudi tena,hawezi kuipata tena na hakuna mwenye hamu wala wazo la kumpigia na kupoteza kura yake kumpa kura ya ndio Sugu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Ni kweli naunga mkono hoja
P
 
Ndugu zangu Watanzania,

Huo ni ukweli mchungu ambao napenda umfikie Joseph mbilinyi au Sugu. kuwa Nafasi aliyoipata siku za nyuma ya kuongoza jimbo la Mbeya mjini kwa miaka kumi haipo tena ,haiwezi kurudi tena,hawezi kuipata tena na hakuna mwenye hamu wala wazo la kumpigia na kupoteza kura yake kumpa kura ya ndio Sugu.

Kwa kuwa katika miaka kumi jimbo la Mbeya mjini lilikuwa na mbunge hewa,lilikuwa wazi,lilikosa wa kulisemea na kulipigania Bungeni,lilikosa mtetezi,lilikosa sauti yenye ushawishi ,nguvu na kusikika masikioni mwa serikali.miaka yote ya ubunge wake sugu alifanya kazi ya kuzurula tu, kupigania maslahi yake binafsi na tumbo lake,alifanya kazi ya kutafuna posho na mshahara wa ubunge pasipo kuufanyia kazi.

Wananchi katika miaka yote ya sugu walikosa mahali pa kukimbilia kupeleka shida,kero na changamoto zao.kwa kuwa muda wote sugu alikuwa Bize na biashara zake,Bize na mambo yake,Bize na Dar tu huku Mbeya akifanya kama kituo cha kugongea muhuri wa kwenda Bungeni kama mbunge.aliwafanya wana Mbeya kama wajinga,akajiona yeye ni mtoto pendwa na kwamba yeye ni yeye mwenye hati miliki na jimbo la Mbeya mjini na kwamba hayupo wa kuchukua nafasi hiyo isipokuwa yeye tu aliyemteule wa Mbeya mjini.

Wanambeya walipochoka na dharau zake na ubabaishaji wake pamoja na kushindwa kwake kutimiza majukumu yake ya kibunge.wakaamua kugeukia upande wa pili kulikokuwa na CCM ikiwakilishwa na wakili Nguli na msomi ,mwalimu wa walimu wa sheria ,naibu mwanasheria Mkuu mstaafu na naibu speaker wa bunge Dr Tulia Acksoni Mwansasu kwa kumpa ushindi wa kishindo ulioitetemesha Mbeya nzima.

Dada msomi,msikivu wa hali ya juu ,mkalimu, mcheshi, mchapa kazi, mnyenyekevu,mpole,mwenye moyo wa huruma na upendo, mzalendo wa kweli na aliyebarikiwa na Mungu kipawa na Karama ya uongozi,mwenye kujuwa nini maana ya Maisha,mcha Mungu na mwenye hofu ya Mungu na aliyekulia katika maisha ya kawaida na ya chini ya kipato cha kuuza mboga mboga huku akimtumainia na kumtegea Mungu wake katika kila hatua aliyopita.

Wana Mbeya wameshuhudia ndani ya muda mfupi wa ubunge wa Dr Tulia namna Mbeya ilivyobadilika,namna inavyochipua kwa miradi ya maendeleo,namna inavyoendelea kupokea mamilioni kwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.wanambeya wanaona kwa mara ya kwanza chini ya ubunge wa Dr Tulia wanakwenda kupata barabara za lami njia nne kutoka igawa Mbeya hadi Tunduma zenye urefu wa km 237.9%,wana shuhudia namna ambavyo shule, vyumba vya madarasa,zahanati,vituo vya afya, barabara za mitaa zimekuwa zikijengwa wakati wote wa Dr Tulia.

Wana Mbeya wameshuhudia namna wakati huu wa Dr Tulia ambavyo viongozi wakuu wa serikali wamekuwa wakifika na kuitembelea Mbeya na kuahidi kuleta mamilioni kwa mabilioni ya pesa kwa ajili ya miradi mbalimbali.wana Mbeya wanaona namna jiji linavyoendelea kupangwa katika kulifanya liwe na sura halisi na hadhi ya jiji ,na siyo kuwa jiji lenye mkusanyiko wa nyumba nyingi tu .

Ujio huo wa maendeleo na miradi ya maendeleo mfululizo ambayo wanambeya wameipata ndani ya muda mfupi imewafanya wajute na walaani sana kumpatia sugu miaka kumi kuwa mbunge wa Mbeya mjini,imewafanya wajipige vifua vyao na kuapa kuwa katu na kamwe hawatampa kura za ndio tena sugu kuwa mbunge wa Mbeya mjini. Wanasema walifanya makosa ambayo kamwe hawawezi kuyarudia kuyafanya ,hawawezi kurudia mzaha huo wa kufanya majaribio ya maisha yao kwa kumpa mtu uongozi asiye jitambua wala kutambua thamani na heshima aliyokuwa amepewa.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
sugu amesharidhika na ile hotel, na ameshazeeka. ameshasalenda kwa ccm wala hawezi kuleta upinzani. labda mwabukusi anaweza kumtikisa kidogo tulia. na mwabukusi hawezi kugombea jimbo la mbeya mjini kwasababu yeye anakogomea miaka yote ni Busokelo kwao. na hata akija mjini hana chama, manake NCCR mageuzi imeshamezwa na ccm, na chadema pale mjini wana mtu wao hivyo mwabukusi hawezi kugombea ubunge tena, ni kama hana chama kwa sasa.
 
HAKUNA MWENYE AKILI TIMAMU HIVI SASA MBEYA ANAEPOTEZA MUDA NA ALIEPO. MBEYA SIO KAMA WEWE,HAWADANGANYWI NA HIYO IPQ
Dr Tulia ndiye chaguo la wana Mbeya na ndiye anayekwenda kuchaguliwa tena uchaguzi ujao.kila mwanambeya anajivunia kuwa kura yake kwa Dr Tulia imetupatia heshima kama Taifa kutoa Rais wa umoja wa mabunge Duniani na mwanamkea wa kwanza kutoka Barani Afrika kushika nafasi hiyo.kwa hiyo hayupo aliye tayari wala kujaribu kumnyima kura ya ndio Dr Tulia uchaguzi ujao.
 
Kwani Hapo Mbeya wenye sifa za Ubunge ni Dr Tulia PhD na Sugu tu, hakunaga msafwa Mwenye uwezo hata yule kada maarufu Choicevariable 😂😂🔥🐼
CCM na Wana CCM Chaguo lao kuwakilisha jimbo la Mbeya mjini ni Dr Tulia ambaye ndiye anayehitajika na wana Mbeya wote.kwa hiyo wana CCM kazi yao ni kuwapelekea wana Mbeya chaguo lao ambaye ni Dr Tulia.
 
Back
Top Bottom