figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Moto mkubwa unawaka muda huu kijiji cha mwale Chimala mkoani Mbeya malori ya mafuta yanateketea na moto chanzo cha ajali bado hakijulikani. Malori ya mafuta yanawaka moto ni balaa
Ni pale hapo stendi mpya karibu na dukani kwa Mama Pipo.
=====
MOTO WATEKETEZA MAGARI 6 NA NYUMBA 4 MBEYA
Taarifa iliyothibitishwa na Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Ayoub Sanga, imeelezwa kuwa Magari 6, Pikipiki 2 na Nyumba 4 zimeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huko Chimala Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya
Diwani wa Kata hiyo, Charles Komba amesema moto huo ulianza majira ya saa nne usiku kutoka kwenye Lori lililokuwa limeegeshwa katika kituo maalumu cha magari maarufu kama Mama People
Zimamoto lilifika saa 6 usiku na kufanikiwa kuzima moto huyo ambao chanzo chake kimetajwa kuwa ni biashara holela ya mafuta ya Petroli na Dizeli iliyokuwa ikifanywa na madereva katika eneo hilo.
#JamiiForums #JFMatukio
Ni pale hapo stendi mpya karibu na dukani kwa Mama Pipo.
=====
MOTO WATEKETEZA MAGARI 6 NA NYUMBA 4 MBEYA
Taarifa iliyothibitishwa na Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Ayoub Sanga, imeelezwa kuwa Magari 6, Pikipiki 2 na Nyumba 4 zimeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo huko Chimala Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya
Diwani wa Kata hiyo, Charles Komba amesema moto huo ulianza majira ya saa nne usiku kutoka kwenye Lori lililokuwa limeegeshwa katika kituo maalumu cha magari maarufu kama Mama People
Zimamoto lilifika saa 6 usiku na kufanikiwa kuzima moto huyo ambao chanzo chake kimetajwa kuwa ni biashara holela ya mafuta ya Petroli na Dizeli iliyokuwa ikifanywa na madereva katika eneo hilo.
#JamiiForums #JFMatukio