Idimi
Platinum Member
- Mar 18, 2007
- 15,506
- 11,439
Haki ya kufanya biashara maeneo ambayo hayajatengwa kwa ajili hiyo?
Mkubwa, tatizo la Wamachinga wa Mbeya linatokana na kuunguliwa na masoko mfululizo, hawana pahala pa kuweka bidhaa zao baada ya masoko kama 7 hivi kuungua tangu mwaka 2006, na mpaka sasa hakuna soko hata moja ambalo limejengwa na kutumika, tangu yameungua (Mbalizi, Mwanjelwa, Uhindini, Sido n.k). Kandoro na watawala wenzake waliahidi kutafuta na kutenga mahali pa kufanyia baiashara kwa ajili ya Watanzania hawa, lakini mpaka jana ambayo ndo ilikuwa deadline hawajatekeleza chochote. Hayo ndo madhara ya kuingiza longolongo za kisiasa katika masuala ya kiutendaji. Ni makosa makubwa. Ikumbukwe kwamba Mbeya mjini wapinzani wana nguvu, si kama miaka ya nyuma. Hakuna haki inayopatikana bila kuifanyia kazi, ndo sababu unaona leo Watanzania wenzetu wanapodai haki yao wanapigwa mabomu. Yana mwisho haya.