Ndiyo maana Najuta kuikacha JWTZ. Hawa jamaa safi sana. Mungu awabariki kwa uzalendo na moyo wa utayari wa kuilinda Tanzania na Watanzania. Hongera sana JwTZ. Ninyi ndo tegemeo pekee.
Mkuu nikweli lakin ninamashaka na mambo yao.
Wangetusaidia basi nakuwaondoa hawa mafisadi endapo wanamoyo wa dhati kulinda taifa na watu wake.
Ufisadi unafanya maafa kama vita vingine vyovyote, maafa yakutisha
1. Mahospitalin wanakufa wengi sana kwa kukosa huduma bora
2. Mashulen, tunapata maafa yakutisha kwasababu huko tunapata wataalam feki
wahandisi-majumba,madaraja yanaporomoka...watu wanakufa wengi
Madakitari-operation za vichwa kuhamia miguun, madawa feki...watu wanakufa wengi.
Maajali barabaran watu wengi wanakufa, watawala wameshindwa kudhibiti achilia mbali mauwaji walemavu wa ngozi nk
Taifa linateketea, watu wanakufa lakin wazelendo hawa wajeshi hawashughuliki na mafisadi wanaoteketeza taifa.
Kwao uzalendo nikupambana na walalahoi ambao teyari wameshapigika vyakutosha na ufisadi.
Je uzalendo wao unaonekana kwa wananchi wakawaida tu au uzalendo wao upo kulinda maslahi ya watawala ambao ndio mafisadi?