Mbeya kuna nini leo? JWTZ watanda mji mzima

Mbeya kuna nini leo? JWTZ watanda mji mzima

Jana kuna sms ilisambazwa kwenye simu na chanzo kinachodaiwa kuwa ni jwtz kwamba kuna vitu kama mabomu vimerushwa kutoka malawi au rwanda. Huenda ni tahadhari inachukuliwa
 
Raia wanapataje hofu mkuu.ninavyojua kipindi kuelekea uchaguzi huwa kuna pilipilika nyingi na ndo mana kipindi hicho mpaka rais mpya anapoapishwa matukio mengi kama vile ujambazi huwa yanatokea kwa wingi najua hapo jeshi letu linajiweka sawa pia kwa kushirikiana na polisi ili mambo yaende sawa

Hebu tupe mfano ni lini kipindi cha uchaguzi kulikuwa na ujambazi na hayo matukio mengi mpaka jeshi likatumika
 
Hizo zinaitwa internal Force tatizo la nchi yetu TZ hatujazoea hizi mission mission za miltary mijini kuna amani soon tutazoea nchi zenye vita ni kawaida kupishana na vifaru mjini na ndege za kivita kutanda hewani
Na kwa upande wa wanajeshi wetu hawajazoea kupambana na waasi wa ndani hivyo wakipata afasi ya kuja mjini lazima waonyeshe ubabe na uwepo wao wewe angalia ck ya uhuru mbwembwe zao uwanjani za kuvunja tofali n.k
Sasa raia wema wakishawazoea itakuwa kama traffic barabarani na zile heshima za kijeshi zitaisha
 
Huu ni uzushi, mimi niko jijini Meya muda huu, hakuna kitu kama hicho. Nahofu kuingizwa kwenye mtego wa mambo ya uzushi kama ule wa mapambano kati ya TPDF na El Shababu kule mapango ya Amboni. Ebu leta ushahidi wa picha yenye tarehe kama una ukweli !!!

wapo mbona..mi nimewaona roundabt ya kwenda Ghana tena wamebeka bunduki zao ila wanatembea tu....weeee hahahaaa picha..ole wake ..atabalazwaaa,atakoma hahahaaa
 
Raia wanapataje hofu mkuu.ninavyojua kipindi kuelekea uchaguzi huwa kuna pilipilika nyingi na ndo mana kipindi hicho mpaka rais mpya anapoapishwa matukio mengi kama vile ujambazi huwa yanatokea kwa wingi najua hapo jeshi letu linajiweka sawa pia kwa kushirikiana na polisi ili mambo yaende sawa

Ningewashukuru sana kama wange watafuta wanunuzi wa viungo vya albino
 
Kitisho kinatoka wapi?

Niupumbavu, waende kongo nani kasema Mbeya hakuna au kunakitisho cha amani?

Wanatafuta namna ya kuingia kwenye usimamizi wa kuiba kura kwamba interigenssia ya geshi imeonyesha kutakuwa na fujo kipindi cha kupiga kura
 
Asubuhi nimetoka Tunduma kufika Songwe kuna magari zaid ya hamsini yamesimamishwa MP mmoja wa Jeshi akatuamuru tushuke huku mikono juu, tukapangwa mstari na kusachiwa unaambiwa kama unahela simu au pochi shika mikononi (wakati ikiwa juu)

Wanawake wanasachiwa na askari wa kike na wanaume kwa wanaume, huku unaulizwa maswali ya kizushi uraia wako kabila lako kitambulisho nak.

Tumetoka Songwe kufika Mbeya mjini mchezo ni uleule magari yote hasa ya abiria, abiria tumeshushwa kijeshi mikono juu na kusachiwa huku unaambiwa kimbia kwenda mbele kama mita miatano ndio unaenda kupanda gari lako.

Haijalishi wamama wazee au wenye watoto wote mchakamchaka, ukisema unaumwa wanakwambia wanaoumwa wako Hospitalini, ukileta utani unaambiwa ruka kichura kabla ya kuambiwa simama na kukimbia sana.

Licha ya nia ya mazoezi yao, ila kiasi kuna kuwajenga wananchi hofu isiyo ya lazima.

Nimegundua wananchi wanawaogopa sana Wanajeshi, kama wengekuwa polisi sidhani kama wananchi wangetii namna walivyowatii wao.

Na inasemekana zoezi ni la siku tatu usiku na mchana.
 
ayo ni mazoezi kwaajili ya kujiweka tayari na ni silibas ya kimataifa huwa yanafanyika katika maeneo mbalimbali kulingana na topic yenyew.yapo ya porin mf..jungle patrol base.n mjini ndo kama hayo FiBUA,RAID cloud d sparz.etc

Kujiweka tayari for what? kuna vita hapa? Au ndiyo kulinda raia huko?
 
Wanatafuta namna ya kuingia kwenye usimamizi wa kuiba kura kwamba interigenssia ya geshi imeonyesha kutakuwa na fujo kipindi cha kupiga kura


Nikweli mkuu.

Lakin wafaham kulazimisha ccm ibakie madarakan nikuchafuwa hali yahewa.


Waache sanduku la kura liamue tutabaki salama, tofauti na hapo tutashuhudia viongozi kuuwawa kwa kuviziwa, mali za serikali kuhujumiwa kwa siri nk

Kwanin tufike huko? Waache kura ziamue na atakayeshinda apewe kijiti hapo tutajenga taifa imara lenye afya na amani.


Huu sio uungwana hatakidogo.
 
dunia ya saiv imebadilika amna vita ya porin kama enz zile za uganda nwadyz maadui wanaweka ngome kwenye miji na sehemu za watu coz nia yao s kuua askari bali n raia.wakuu wa serekali.majengo muhimu etc

Kuna bomu lilirushwa kanisani Olasiti Arusha mbona sikuwaona hao wajeda, kuna bomu lilirushwa kwenye mkutano wa CDM kwenye viwanja vya soweto Arusha hao wajeda walikuja kukagua after tukio lkn sikuona any reaction au taarifa waliyotoa sasa hizo vita za mjini hapo Mbeya ni ipi?
 
Walishaleta barua kwenye ofisi nyeti tangu alhamisi kuwa kutakuwa na mazoezi ya pamoja na mengine kukamata magaidi.
Don't worry wana mbeya.
 
Nikweli mkuu.

Lakin wafaham kulazimisha ccm ibakie madarakan nikuchafuwa hali yahewa.


Waache sanduku la kura liamue tutabaki salama, tofauti na hapo tutashuhudia viongozi kuuwawa kwa kuviziwa, mali za serikali kuhujumiwa kwa siri nk

Kwanin tufike huko? Waache kura ziamue na atakayeshinda apewe kijiti hapo tutajenga taifa imara lenye afya na amani.


Huu sio uungwana hatakidogo.

Serikali imechoka, viongozi wamechoka.
Fikiria mtu tangia ana miaka 20 mpaka 70 yeye ni kiongozi unafikiria ataweza kuongoza nini leo zaidi ya kuwa mtawala tena wa mabavu.
At this time wanajiona uongozi ni KAZI yao ya milele not dhamana ya kuwatumikia wananchi
 
Back
Top Bottom